Ta Muganyizi
R I P
- Oct 19, 2010
- 5,355
- 2,736
Aisee kweli haya ni makandokando.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Philip mpango ameweka bayana kwamba imewekwa kwenye mpango wa bajeti inayofuata. Let's hope bajeti itapitishwa accordinglymagufuli akiambiwa je ataweza kurudisha?
Kimeeleweka?Tutakutana October, lazima kieleweke!!!!
Inasikitisha mno kupeana ahadi za uongo as if sisi ni watoto, haipendezi, tuombwe radhi!Wananchi tulielezwa kwa uwazi kabisa enzi za Wahe. Kigoda (Marehemu), Mary Nagu waliokuwa Mawaziri wa Viwanda na Biashara enzi hizo kuwa Kiwanda cha General Tyre Arusha tayari Serikali inaimiliki kwa asilimia 100 na itafunguliwa katika mwaka wa fedha 2014/15 na kuanza kazi. Mpaka leo Kiwanda hakijafunguliwa na hakifanyi kazi. Tunaiomba Serikali itutake radhi kwa kutotimiza ahadi yake kama ilivyoahidi.
Kwa swala la viwanda kufa ni shida kubwa sana sidhani kama tungekua na tatizo kubwa la ajira kama ilivyo sasa
Naomba kama inawezekana tuweke thread inayo onesha viwanda vilivyo fungwa kwa makusudi na watawala wasio waaminifu kwa kila mkoa.
Mfano Kilimanjaro kuna Machine tools pale junction ya kwenda Machame na Kiwanda cha Magunia kule Kiboroloni.
Nimeona Itv wakitaarifu kuwa serikali itawekeza zaidi ya sh.biliioni 1 kwenye kiwanda cha kilimanjaro machine tools kilichopo nje kidogo ya mji wa moshi cha kutengeneza vipuri vya mashine ili kiongeze uzalishaji na kufanya kazi kwa ubora zaidi.
ni jambo la kufurahisha , ziara ya mh raisi aliyoifanya moshi imeleta matokeo mazuri.
uchumi wa nchi utakuwa kwa kupata fedha za kigeni na ajira za kazi ,tunaomba na general tyre ifufuliwe.
ningeshauri uwekezaji uongezwe hata kutoka kwa watu binafsi kwa hisa, serikali iwe na hisa nyingi 51% ili isamamie maamuzi muhimu .
kilimanjaro machine tools ni ya tatu barani afrika baada ya afrika kusini na misri kwa utengenezaji vipuri
Serikali imetoa takwimu ikielezea hali ya ukuaji uchumi katika kipindi cha mwaka 2016.
View attachment 521243
Waziri Dk. Philip Mpango
=> Kiwango cha ukuaji uchumi 2016/2017kimeendelea kukua kwa wastani wa asilimia saba ikiwa ni pungufu kidogo ya kile kilichotarajiwa awali. Makadirio ya awali yalionyesha kuwa uchumi huo ungekua kwa wastani wa asilimia 7.2.
=> Hali ya ukuaji uchumi imeendelea kushuhudiwa katika kiwango kilekile cha awali cha asilimia saba na hii imechangiwa na mambo mengi ikiwamo baadhi ya sekta kutofanya vizuri. Sababu hizo ni pamoja na kushuka wa sekta ya kilimo iliyotarajiwa kukua kwa asilimia 2.9, lakini malengo hayo hayakufikiwa na badala yake yalikuwa kwa asilimia 2.1.
=> Sekta ya biashara ilikuwa 6.7% hali ambayo ni tofauti na makadirio yaliyowekwa awali yaliyokuwa 7.8%
=> Eneo la chakula limechangia kufikia kwa malengo ya ukuaji uchumi. Makadirio yetu yalikuwa kwamba sekta ya chakula ingekua kwa 8%, lakini bahati mbaya ilishuka na kuwa 3.7%.
=> Kuna sekta zimefanya vizuri na kusaidia uchumi wa Taifa, sekta hizo ni pamoja na habari na mawasiliano, madini na kiashirio cha kuendelea kukua kwa sekta ya viwanda.
=> Kwa mwaka 2016/2017 Serikali ilipanga kutumia Shilingi Bilioni 11,820.5 kwa ajili ya bajeti ya mandeleo. Hadi April 2017 fedha zilizokuwa zimetolewa ni Shilingi Bilioni 4516.7 sawa na Asilimia "38" ya Bajeti nzima.
2017/2018
=> Serikali imetenga bajeti kwa mwaka wa fedha wa 2017/18 kwa ajili ya kufufua kiwanda cha matairi yaani General tyre.
=> Serikali inafanya utaratibu katika kuboresha maisha ya wananchi na watumishi wa umma kwa kuweka malengo na bajeti katika kutekeleza hayo.
Huwezi amini, hii ni 2018 na hakuna dalili..!Ombeni SEfue aliwai sema kiwanda kitafunguliwa kabla ya mwisho wa mwaka(that was sept/oct 2015 baada ya serikali kuwa na 100% shares) ndo imebaki kesho tuu watu wa Arusha tupeni updates pls kinafanya kazi?
Daah ni hatari..nani alietulaani jamani?kuna mchwa wameila nchi hii mpk imebaki skeletonSababu za kufa General Tyre ni kama ifuatavyo.
Mosi,Bodi ya wakurugenzi ilikuwa ya kisiasa zaidi badala ya kuzingatia utaalamu.
Wajumbe wengi wa bodi walikuwa ni wabunge wa JMT ambao walitakiwa kuyasimamia mashirika ya umma kupitia kamati kama PAC.Madudu yaliyokuwa yakifanywa na management yalikuwa yakipata baraka za bodi kupitia vikao na posho mbali mbali.Wabunge waliokuwa wakiisumbua serekali kupitia hoja mbali mbali walikuwa wakitupwa kwenye hizi bodi za ulaji bila pasipo uwajibikaji.Kamati za kusimamia mashirika ya umma mara nyingi zilijikuta zikishindwa kufanya kazi ipasavyo kwasababu ya kuwa wajumbe wa bodi za mashirika hayo na wakati huo huo wajumbe wa kamati za bunge.Hili Zitto kalisema sana lakini watawala wetu wametia pamba kwenye masikio.
Laiti wanyama pori wangekuwa wanazalishwa kama bidhaa nyingine mashirika kama TANAPA & Ngorongoro Conservation Area Authority yangeshafungwa siku nyingi.Mashirka kama NSSF,PPF.... tungeshayasahau kama yalishakuwepo.
Pili,Ikumbukwe General Tyre ilianzishwa na Mwl Nyerere ambaye alitembelea USA miaka ya sabini mwanzoni akakuta General Tyre Amerika wana modernise kiwanda chao so mitambo ya zamani haikuwa na kazi kwao wakati huo.Mwl Nyerere akawaomba General Tyre wailete mitambo ya zamani Tanzania jambo ambalo walilikubali.General Tyre USA wakapewa 26% na serekali ikamiliki 74%.Mwl Nyerere angekuwa mlaku kama wanasiasa wengine pengine 74% share zingekuwa zake na familia yake lakini hakufanya hivyo.Katika makubaliano hayo Tanzania ilikubaliwa kuunda bodi na baadhi ya manager hasa HRM na maeneo mengine hasa ya technical wakaachiwa wamarekani.Kwenye bodi aliingia Mkurugenzi mkuu,mkurugenz wa fedha na mkurugenzi wa uzalishaji wote hawa wamarekani watanzania badala ya kuingiza vichwa vya ukweli tukawapa ujumbe wa bodi akina Gullamal,Shellukindo na wabunge wengine wengi kwaajili ya kulipana posho.
Kwakuwa General Tyre ilianzishwa na technoligia ya zamani kama nilivyoonysha hapo juu.Kati ya mwaka 2003 - 2005 sikumbuki vizuri ilikubaliwa kununua mitambo mipya ya kisasa kwaajili ya kuendana na kasi kubwa ya maendeleo ya uzalishaji wa tyre.NSSF ikatoa mkopo wa dola 10 milion serekali ikiwa mdhamini wa mkopo huo.Badala ya kununua mitambo mipya mitambo ya zamani ikapakwa rangi na fedha zote zikatokomea.Utashangaa leo unaambiwa deni la taifa linazidi kuongezeka ukichunguza utakuta linaongezeka kwa mambo kama haya.
Hii fedha ya NSSF naambiwa ilitumika kujenga hotel ya waziri aliyepitisha udhamini wa serekali baada ya msukoko wa kuoneeana wivu akauza hiyo hotel kwa Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.