Gerson Msigwa: Huwezi kukurupuka kumfukuza mtu, pengine hata wakaguzi wa CAG nao ukaguzi wao una dosari

Nilipokaa muda huu Niko na DED aliyetajwa na CAG kuwa ni mwizi ana warembo wanne wanakula bata haijawahi kutokea. Ikitoka 10,000 ya bia moja hataki chenchi. Ana wapambe kama wote japo yeye amelala tu kwenye kiti udenda unamtoka.
 
Acha chuki mkuu 🤣🤣🤣
 
It was an analogy, nikilinganisha mfumo wa utoaji haki nchini na mfumo wa ukaguzi.

PCCB na polisi ni vyombo vya serikali, ripoti ya CAG sio kwa ajili yao ni kwa ajili ya kufanyiwa kazi na Bunge.

Serikali itapewa maazimio na Bunge wakishamaliza kuifanyia kazi ripoti, hatua zitachukuliwa.

Hakuna mtu anatetea ufisadi, ninachokisema ni utaratibu ufuatwe, ukiwa na tabia ya kupuuza sheria za nchi mwisho wake ndio yaleyale ya mtu katumbuliwa leo kesho anarudishwa baada ya kuonekana hana makosa.

Kuna watu wanaweza hata kupoteza maisha kwa presha za kutumbuliwa bila kuwa na makosa, unamkumbuka yule mkurugenzi wa jiji la Dar aliyetumbuliwa hadharani??
 
Msigwa ana hara na kutapika
 
Msemaji wa serikali anapaswa kutoa matamko yenye kuzingatia utaalamu na weledi wa fani husika. Kwa kuwa anachokisema huakisi uelewa wa mambo mbalimbali wa watawala. Ni lazima ajitofautishe anapochangia jambo lolote lile akiwa kama mtu binafsi, na pale anapoiwakilisha serikali. Siyo sahihi kwake kusema kuwa ripoti ya ukaguzi wa mahesabu imekosewa, isipokuwa angetoa maelezo kuwa pengine kuna kasoro zilizoainishwa zilitokana na kukosekana kwa ushahidi wa kinyaraka kwa wakati. Wakaguzi hawakurupuki, wala zoezi la ukaguzi haliendeshwi kwa usiri kiasi kwamba wahusika waseme kuwa hawakuwa na taarifa kuhusu mapungufu yaliyotolewa katika ripoti.

Wahusika hushirikishwa katika kila hatua ya ukaguzi, na hutakiwa kuleta ushahidi wa kinyaraka katika maeneo yanayokaguliwa. Siyo kosa la mkaguzi endapo zitatokea "audit queries" ambazo hazitolewi maelezo ya kuridhisha kuendana na kanuni na miongozo iliyowekwa, ama kutokana na mapungufu ya ushahidi wa kinyaraka.

"Audit queries" zinapotolewa maelezo ya kutosha basi huondolewa, la sivyo hubakia na kuripotiwa kuwa ni makosa, na aina ya kosa huangaliwa kuendana na athari yake kama ni kubwa, ya kati, ama ndogo ili hatua stahiki za kiutawala na kisheria zichukuliwe dhidi ya muhusika.

Msemaji wa serikali anapaswa kutambua ripoti ya CAG inatoa "fair view" kuhusu matumizi ya fedha za umma kwa mwaka uliopita wa serikali. Ni lazima pia atachague maneno sahihi pale anapozungumzia masula ya kitaalamu na kiuweledi kutokana na hadhi ya fani husika.
 
  • ni lini serikali iliwapeleka mahakamani watuhumiwa wa ufisadi utokanao na Ripoti ya CAG?
  • Serikali imekuwa ikifanyia Kazi mapendekezo ya Bunge Kwa kiwango kidogo Sana,
  • sheria gani ya nchi imepuuzwa hebu tutajie tukaisome.
 
Huyo pimbi naye mpuuzi tu
 
Msigwa Hana taaluma ya uhasibu. Ni vema akaongelea Mambo ya Yanga na Simba kupewa vitita vya milioni tano wakifuzu.
Nusu fainali imeongezeka, sasa kila goli mil 10
 

Kwa hapo nimekuelewa, ingawa position yangu ni kwamba, mtu anapotuhumiwa asimamishwe kazi kwa muda kupisha uchunguzi kuliko sasa unatuhumiwa halafu wewe ndio unaombwa utoe ufafanizi mbele ya kamati ya bunge.
 
Uyu Mshamba atafutiwe kazi nyingine!
 
Ni kutaka kutengeneza mianya ya kujisafisha...
Pia ni kutaka kumpa kagi mchuzi kidogo awatakatishe.
Aibu
 
  • ni lini serikali iliwapeleka mahakamani watuhumiwa wa ufisadi utokanao na Ripoti ya CAG?
  • Serikali imekuwa ikifanyia Kazi mapendekezo ya Bunge Kwa kiwango kidogo Sana,
  • sheria gani ya nchi imepuuzwa hebu tutajie tukaisome.
Some sheria ya ukaguzi wa umma kuanzia kifungu cha 37 mpaka 40, utaona kuwa ripoti hiyo ni kwa ajili ya Bunge kufanyia kazi, Bunge ndio linatoa mapendekezo serikalini ya hatua gani zichukuliwe.

Lakini pia, kama sehemu kuna wizi unaofanyika, haijalishi kama CAG amendika au la, vyombo husika kama PCCB wanapaswa kuchukua hatua. Kwani yote ambayo PCCB wanafanya CAG huwa anayaona?
 
Kwani wewe ni lini uliona watumishi wenzako wamechukuliwa hatua kutokana na ripoti ya CAG!
Acha usanii,hiyo ofisi ya CAG si ndiyo huwa inapewa kazi mpaka na taasisi za kimataifa kufanya ukaguzi?sasa leo unatuambiaje kuwa ripoti imekosewa?mbona kimataifa ofisi ya CAG inasifiwa kwa kazi nzuri!
 
Uyo Kilaza atakuwa na yeye katajwa ndiyo maana anatetea upuuzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…