Gerson Msigwa: Tuko mbioni kuanzisha Televisheni ya Serikali itakayorusha Habari za Maendeleo tu

Ina maana TBC hairushi mambo ya msingi ya serikali? jamani hii sio sawa? au anamaanisha mkurugenzi hafai?
 
Kumbe TBC huwa inamwongozo wa kurusha mambo yasiyo ya Msingi pia...sasa tungojee hiyo Yenye mambo ya Msingi TU sasa...!!!
 
Hii nchi ni ngumu sana kuielewa!!yaani Tv ya taifa ipo na ndio mpiga debe mkuu wa serikali, kuna chaneli ten, mpiga debe wa chama, zote hizo hazitoshi?!!sasa kama ni hivyo kwanini wasiifanye TBC 2, ndio iwe na majukumu hayo?!!
wanatengeneza ajira kwa vijana wao!!
 
Mbona ccm na siri-kali yake tayari wanazo tv, yaani:
Tbc, channel 10, clouds, wasafi..
Nyingine ya nini tena?!!!
 
Serikali ya kijinga kabisa..
Wanalojua wao ni kuongeza kodi tu..
Hata muanzishe jambo gani haliwezi kufanikiwa kwa sababu hampo hapo kihalali, mpo hapo sababu ya wizi wa kura..
MMELAANIWA.
 
Maendeleo huwa yanaonyeshwa?
Mbona maendeleo huwa yanaonekama kwa macho,kwani sisi watanzania tunaishi hewani ili tusione kinacho onekana?
 
Hapana hii itaongeza matumizi kwa serikali badala yake TBC na channel 10 zitumike kwa kazi hiyo
 
TBC ni ya CCM au Binafsi [emoji1][emoji1] shikamoo serikali mkitoka apo mkaongeze tozo[emoji1][emoji1]
Tbc tu siiingalii ndio utakuwa huo upuuz mpya?!
Vp lile somo la historia ya tanzania ?
Wameanzisha tv ya Safari, haina ubunifu kila siku inaonyesha ile zoo ya Chato-Burigi.
Na hii inachoma kodi zetu si waiboreshe hata hiyo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…