Gharama kufuru za matibabu hospitali za umma ni kwa uhalali upi?

Gharama kufuru za matibabu hospitali za umma ni kwa uhalali upi?

Imekuwa si nadra kusikia ankara za mamilioni ya pesa kwa ajili ya tiba kwenye hospitali za umma.

Nani anayepanga bei hIzi na kwa vigezo gani?

Je, ni bei kwa ugonjwa, dawa, ujuzi, vifaa au majengo?

Au ni yale ya Bashe na wakulima na bei zao za vyakula?

Kwamba kama bei ni kubwa basi kila mtu akaanzishe hospitali yake?

Kama taifa tunakoelekea yaweza kuwa siyo kwema sana.
Bei hizo hutokana na matibabu makubwa ya kibingwa ambayo gharama na teknolojia yake ni kubwa saana ,tena kwa hizi hospital za umma gharama hizo ni nafuu saana ililinganishwa na hospitali za binafsi au nje ya nchi ,ili kuweza kuendesha huduma hizo kwa wananchi kwa wakati wote Mwananchi anapaswa kuchangia gharama kidogo ,suluhu ya kudumu ya jambo hili ndio huu mpango wa Bima ya Afya kwa wote ambayo itamhakikishia Mwananchi wa hali yeyote kupata huduma za matibabu makubwa na madogo kwa nyakati zote ,BIMA YA AFYA KWA WOTE ITATUONDOLEA ADHA HIZI KWA KUTUHAKIKISHIA HUDUMA BORA KWA NYAKATI ZOTEEE ,bima ni muhimu saana .
 
Bajeti ya matibabu ya 10m/- kwa mwanafamilia kwenye nchi yenye tozo na kodi zote zilizopo nchini haiwezekani.

Hali kadhalika hakuna bima ya Afya itaacha kufilisika Kwa bei hizo.

Zingatia msingi wa hoja:

Bei ni kwa kigezo cha ugonjwa, ujuzi, dawa, vifaa au majengo?

Bila kusahau kuwa wawekezaji kwenye vyote hivyo ni sisi wananchi.
Ndio mana kuna ishu ya bima ya Afya ambayo malipo yake ni kidogo lakini ita cover haya mambo yote, leo mtu anapinga 340,000 km malipo ya bima ya Afya Kisha akipewa gharama halisi qnalalaika inakuwaje? Tujifunze
 
Mkuu unasomeka. Hawa si wa kuomba.

Kuna bajeti waizara ya afya, kuna tozo na kodi kwetu.

Hawa jamaa wanapanga hatch bei kama kuku anavyotaga mayai.

Hawa ni wa kuwavaa head on.

Family member mmoja anatibiwa kwenye viwango vya 10m halafu mkulima anaambiwa anatetewa naye anakenua.

Familia ipi itamudu gharama hewa kama hizo?
wanapanga bei kwa watu binafsi sio vya kwao...tunatakiwa kufanya kama watanzania ni kuiondoa ccm madarakani, ccm ina nguvu sana sasa ,wanafanya chochote kile hakuna wakuwafanya chochote, wenyewe wanasema hata hili litapita.....we unafikili pesa za uchaguzi wanatoa wapi?
 
Kwenye hospitali ya umma cost sharing haiwezi kuwa kuweka gharama zinazoendana na hospitali binafsi, kwani kodi za wananchi ndo zinazoendesha hospitali hizo ikiwemo kulipa mishahara ya wataalamu na wahudumu, kununua vifaa tiba na madawa nk. Huwezi kutoza kipimo cha kawaida cha makohozi elfu 80 kwenye hospitali ya umma kwa kisingizio cha cost sharing, ingekuwa elfu 5 ingeeleweka kwamba ni kuchangia gharama.
Tunajua kuwa amekaa hospitali kwa kipindi gani? Zimetumika gharama kiasi gani za ununuzi wa dawa na baadhi ya matibabu yamekwendaje? Yawezekana kwa kiasi hicho cha pesa angekwendq India ingekuwa zaidi ya milioni hamsini huko, lazima tulinganishe huduma na gharama za matibabu mana serikali ikiboresha huduma gharama nazo lazima ziongezeke hata kwa kiasi fulani
 
Imekuwa si nadra kusikia ankara za mamilioni ya pesa kwa ajili ya tiba kwenye hospitali za umma.

Nani anayepanga bei hIzi na kwa vigezo gani?

Je, ni bei kwa ugonjwa, dawa, ujuzi, vifaa au majengo?

Au ni yale ya Bashe na wakulima na bei zao za vyakula?

Kwamba kama bei ni kubwa basi kila mtu akaanzishe hospitali yake?

Kama taifa tunakoelekea yaweza kuwa siyo kwema sana.
Huduma siyo anasa. Hospitali inalipa umeme, maji, wataalamu ,matengenezo ,madawa na uchunguzi na vitu vingine vingi . Ni muhimu sana kuchangia matibabu ili kuwa na uhakika wa uendeleevu wa utoaji huduma katika vituo vyetu vya afya. Hili linawezekana tu pale kila mtu atakapokuwa na bima. Nguvu yetu iende huko ,tusipolipa kesho tutashindwa kutoa huduma kwa watanzania wengine .Bima inaweza onekana haina umuhimu ila ukikata bima inaweza kuokoa mamilioni ya fedha ,UGONJWA HAUPIGI HODI
 
Tupunguze Double standard tunapojadili mambo yenye maslahi kwa umma. Hospitali hazijiendeshi for free hivyo hizi charges zinazowekwa ambazo hata sio nyingi ni kwa ajili ya kugharamia mambo muhimu ili huduma zipatikane kiurahisi
 
Bei hizo hutokana na matibabu makubwa ya kibingwa ambayo gharama na teknolojia yake ni kubwa saana ,tena kwa hizi hospital za umma gharama hizo ni nafuu saana ililinganishwa na hospitali za binafsi au nje ya nchi ,ili kuweza kuendesha huduma hizo kwa wananchi kwa wakati wote Mwananchi anapaswa kuchangia gharama kidogo ,suluhu ya kudumu ya jambo hili ndio huu mpango wa Bima ya Afya kwa wote ambayo itamhakikishia Mwananchi wa hali yeyote kupata huduma za matibabu makubwa na madogo kwa nyakati zote ,BIMA YA AFYA KWA WOTE ITATUONDOLEA ADHA HIZI KWA KUTUHAKIKISHIA HUDUMA BORA KWA NYAKATI ZOTEEE ,bima ni muhimu saana .

Kwamba ni gharama za kibingwa? Hii si ni Ile ya Bashe na wakulima?

Hizi gharama za kibingwa zinafikiwa je? Majengo ya umma? Vifaa vya umma? Mabingwa wanesomeshwa na umma? Wanalipwa na umma? Nk nk.

Kwamba kama vipi Kila mtu akawe bingwa?

Kwa bei hIzi hakuna mfuko wa bima au mtu utaweza kumudu.

Si waseme tu kama nia yao ni pesa kama vipi watu tufanye maamuzi magumu?

Ninakazia:

Tunakoelekea siyo kwenyewe.
 
wanapanga bei kwa watu binafsi sio vya kwao...tunatakiwa kufanya kama watanzania ni kuiondoa ccm madarakani, ccm ina nguvu sana sasa ,wanafanya chochote kile hakuna wakuwafanya chochote, wenyewe wanasema hata hili litapita.....we unafikili pesa za uchaguzi wanatoa wapi?
Kuiondoa ccm madarakani sio solution. Solution hapa ni Mfumo wa Bima ya Afya kwa wote ambao utakua mfumo rfiki wa kuhakikisha Matibabu kwa wote yanakua sawa
 
Basi na serikali iache kutenga bajeti kwa wizara ya afya!
Ikiacha kutenga Bajeti Wananchi mtaweza kuchagia ili kulipa mishahara ya Madaktari na wahudumu wa afya? na kununua Vifaa Tiba? pamoja na kujenga Majengo ya kutolea Huduma?
 
Hayupo anayekataa cost sharing ila break down ya gharama ni vyema vikajulikana, nani anaweka bei na vigezo gani.

Vinginevyo hapa ni ujanja ujanja tu.
Umefuatilia breakdown ya gharama na ukakosa!?..juzi hapa nilisikia mjadala wa Bei ya kumuona daktari,uliufuatilia..au umebakiza lawama tu
 
Gharama kubwa hazitoki mbinguni. Kwa nini hatupeani vigezo vya bei hizo Ili tukubaliane sote kuwa dialysis Kwa mfano gharama yake ni 400,00/- kwa mpigo na hufanyika angalau mara 2 kwa wiki?

Tukajua gharama hizo zinatokana na:

1. Umeme kiasi kiasi gani?
2. Maji kiasi gani?
3. Ujuzi kiasi gani?
4. Chemicals kiasi gani?
5. Sindano kiasi gani?
6. Nk

Vivyo hivyo kwa MRI, CT scan, Ventilator, ICU, kulazwa, machela, nk?

Kwa bei hewa hIzi tunazoona haupo mfuko wa bima wala mtu atakayeweza ku survive.

Kimsingi lengo la serikali hapa litakuwa ni kufukarisha watu kwa kisingizio cha gharama kubwa zisizokuwapo.
Mkuu unajua dialyser moja ina cost kiasi gani?
Zile chemical je ? Ujuuzi na utaalamu wa wafanyakazi wa hospital husika, fee ya consultations?
Usiseme unapigwa , kimahesabu hospital nyingi bado zinarun kwa hasara

Sent from my 220333QAG using JamiiForums mobile app
 
Huduma siyo anasa. Hospitali inalipa umeme, maji, wataalamu ,matengenezo ,madawa na uchunguzi na vitu vingine vingi . Ni muhimu sana kuchangia matibabu ili kuwa na uhakika wa uendeleevu wa utoaji huduma katika vituo vyetu vya afya. Hili linawezekana tu pale kila mtu atakapokuwa na bima. Nguvu yetu iende huko ,tusipolipa kesho tutashindwa kutoa huduma kwa watanzania wengine .Bima inaweza onekana haina umuhimu ila ukikata bima inaweza kuokoa mamilioni ya fedha ,UGONJWA HAUPIGI HODI
Tarizo si kuchangia. Tatizo ni huyu mbuzi kwenye gunia.

Mgonjwa kafa anadaiwa 10m/- plus. Pesa hizi ni kwa kigezo kipi?

Ujuzi, umeme, machela, vifaa, dawa, maji, au majengo?

Mfuko gani utahimili malipo ya namna hii hospitali zinazopata bajeti tokea tunakokamuliwa sisi kodi na tozo zisizokuwa kifani?
 
Hayupo anayekataa cost sharing ila break down ya gharama ni vyema vikajulikana, nani anaweka bei na vigezo gani.

Vinginevyo hapa ni ujanja ujanja tu.
Kelele zote hizi ni kukosekana kwa Mfumo mzuri wa Bima ya Afya. tutakapoona umuhimu wa Bima ya afya kwa wote nadhani hizi ngonjera za kulilia gharma za matibabu hatutazisikia kwani Bima ya afya kwa wote inaenda kuwa mwarubaini wa changamoto hizi
 
Kwamba ni gharama za kibingwa? Hii si ni Ile ya Bashe na wakulima?

Hizi gharama za kibingwa zinafikiwa je? Majengo ya umma? Vifaa vya umma? Mabingwa wanesomeshwa na umma? Wanalipwa na umma? Nk nk.

Kwamba kama vipi Kila mtu akawe bingwa?

Kwa bei hIzi hakuna mfuko wa bima au mtu utaweza kumudu.

Si waseme tu kama nia yao ni pesa kama vipi watu tufanye maamuzi magumu?

Ninakazia:

Tunakoelekea siyo kwenyewe.
Bingwa gani kasomeshwa na umma ? Si tunalipa kodi? Vifaa kuwa vya umma havihalalishi kutolipiwa mkuu , Mwendokasi ni ya Umma ila tunalipa

Usilete siasa hapo mkuu

Sent from my 220333QAG using JamiiForums mobile app
 
Kwa sasa hv jitahd ukate BIMA ya Afya , bila BIMA ya Afya hutoboi labda uwe fisadi , hata level ya dispensary tuu bila BIMA ya Afya utapata taabu Sana
 
Huduma siyo anasa. Hospitali inalipa umeme, maji, wataalamu ,matengenezo ,madawa na uchunguzi na vitu vingine vingi . Ni muhimu sana kuchangia matibabu ili kuwa na uhakika wa uendeleevu wa utoaji huduma katika vituo vyetu vya afya. Hili linawezekana tu pale kila mtu atakapokuwa na bima. Nguvu yetu iende huko ,tusipolipa kesho tutashindwa kutoa huduma kwa watanzania wengine .Bima inaweza onekana haina umuhimu ila ukikata bima inaweza kuokoa mamilioni ya fedha ,UGONJWA HAUPIGI HODI
hapa tatizo sio bima, jamaa anauliza gharama za matibabu zinalinga na gharama za huduma?
Kwa mfano dawa x hospitali ya serikali ni sh mia ukienda famasi au binafsi ni sh 50, hii ni kwa nini ? Wakati majengo , madawa ,madocta nk vyote vina pata pesa kutoa kwa watanzania
 
Mtoa mada ungekuwa na bima ya afya usinge lalamika , kata bima ya afya

Serekali Ina tumia Kodi kujenga ,kulipa mishahara na huduma za Bure kama HIV , TB ,Watoto , RCH , maternity n.k

Running cost zote zinakuhusu ,

Siwezi kubali Kodi yangu itumike kukutibia badala wewe ufanye kazi ujitibu wewe na familia Yako , Kodi yangu itakusaidia Kuweka miundo mbinu na vitendea kazi

Serekali imemlipa mfanyalazi unataka na vifaa tiba ikulipie?
 
Mkuu unajua dialyser moja ina cost kiasi gani?
Zile chemical je ? Ujuuzi na utaalamu wa wafanyakazi wa hospital husika, fee ya consultations?
Usiseme unapigwa , kimahesabu hospital nyingi bado zinarun kwa hasara

Sent from my 220333QAG using JamiiForums mobile app
Kwamba ujuzi na utaalamu siyo? Namwona Bashe kazini akiwachuuza wakulima.

Hapa ilikuwa muafaka kila mtu akishika chake:

1. Mtaalamu ashike utaalamu na ujuzi wake.
2. Mkulima akamate chakula chake
3. Mwenye Kodi na tozo azing'ng'anie.
4. Mwanajeshi akamate makombora yake.
5. Kila mtu na lwake.

Hawa watu wapo kwenye majengo ya umma, dawa za umma, mashine za umma, wanalipwa na umma, nk nk.

Tunakijua kweli tunachokisema?

Kwani hata pesa hizi zinaishia wapi? Kwani wanalipwa wao?
 
Imekuwa si nadra kusikia ankara za mamilioni ya pesa kwa ajili ya tiba kwenye hospitali za umma.

Nani anayepanga bei hIzi na kwa vigezo gani?

Je, ni bei kwa ugonjwa, dawa, ujuzi, vifaa au majengo?

Au ni yale ya Bashe na wakulima na bei zao za vyakula?

Kwamba kama bei ni kubwa basi kila mtu akaanzishe hospitali yake?

Kama taifa tunakoelekea yaweza kuwa siyo kwema sana.
Ni mambo ya ubinafsi mtupu. Vigogo wanabinafsisha huduma serikali imewekeza. Wakichunguza watu waadilifu watakuta fedha nyingi wanajilipa watumishi kwa kupeana marupurupu makubwa au wizi wa moja kwa moja.
Ni jambo la kusikitisha kuona eti sera ya kuchangia matibabu imeishia kukandamizwa raia kwa gharama kubwa kiasi hiki.
 
Back
Top Bottom