Gharama za kuwapeleka watoto JKT ni mzigo mkubwa kwa wazazi

Gharama za kuwapeleka watoto JKT ni mzigo mkubwa kwa wazazi

Wapo ambao hawakwenda na sijawahi kuona wamepata hasara Gani na hakuna aliyewahi kuwauliza kwanini hawakwenda.
Napendekeza ukiona humudu gharama hauendi.
 
Mkuu nisamehe sana kukuita wewe ni "faller"

Sio kusudio langu lakini umesababisha mwenyewe.

1. Je maskini hastahili kuzaa?
2. Hujui mwenye nacho hufikisika?
3. Ukose pesa na watoto?
Tafakari
Mshana Jr
Na wewe acha ufala mkuu. masikini unazaa ili iweje. fuata ushauri wa hapo juu
 
Mkuu, upo sahihi! Mwaka juzi, mtoto wangu alichaguliwa kwenda Mafinga JKT, nami nipo Mwanza. Kwa upande wangu, ilikuwa nafuu, kwani kuna wengine walichaguliwa kwenda Songea.

Nikatumia nauli, pamoja na baadhi ya vifaa. Kufika huko, ikabidi arudi ili aje achague vyuo, hivyo ikanibifi nimtumie nauli. Baada ya hapo, nikamrudisha huko Mafinga. Baada ya kumaliza, ikabidi nigharamie nauli.

Ile kufika tu Mwanza, akaugua na kupelekea kulazwa hospitali wiki nzima!

Kwa kweli, binafsi sioni faida yoyote ya kupeleka watoto wetu huko. Mwenda zake, alikuwa anataka kuonyesha kuwa kila kilichowashinda/kuacha wenzie, yeye alikiweza!
Mwendazake siye aliyerudisha huu utaratibu. Utaratibu huu umerudi awamu ya nne.
 
Haina haja hata ya kumpeleka mwanao kwenye hayo mateso yasiyo kuwa na faida..Wadogo zangu wawili walichaguliwa na hatukuwapeleka.Mmoja alimaliza shule kaajiriwa huko huko serikalini na mambo yake yanamnyookea tu.
 
Kama mzazi ni masikini kwa nini alizaa watoto. Ukijiona masikini usiache kiumbe duniani ishi mwenyewe ujitafutie mwenyewe chakula basi.
dasikuwahi kufikiri kama kuna watu wa dizaini ya hiki kiumbe kilichoharisha hapa
 
JKT ipo kabla ya hilo unaloliita Jiwe, itoshe tu kusema umenajisi hoja yako.

Faida za JKT kwa ex-form SIX, ni pamoja na kukoma kwa migomo ya Vyuo Vikuu nchini TZ.
We pimbi, je mfumo wa zamani wa JKT ni sawa na wa sasa? Zamani wazazi walikuwa wana gharamikia?acha kutumia kamasi kuwaza
 
Ni kweli kabisa, watoto wanaenda jeshi, mzazi unanunua vifaa, katikati ya jeshi wanatakiwa kurudi majumbani kujaza makabrasha ya chuo, nauli za nenda rudi mzazi uwe nazo.

Gharama zake ni kubwa kwa serikali na wazazi, na jeshi lenyewe ni muda mfupi tu.

Everyday is Saturday............................... 😎
 
Mkuu nisamehe sana kukuita wewe ni "faller"

Sio kusudio langu lakini umesababisha mwenyewe.

1. Je maskini hastahili kuzaa?
2. Hujui mwenye nacho hufikisika?
3. Ukose pesa na watoto?
Tafakari
Mshana Jr
Unamuomba msamaha wa nini huyu ni fala nyangema tu, kwani kuna mtu ana penda kuwa masikini..? [emoji35][emoji706]
 
Haina tija, JKT ilikuwa zamani bana, enzi hizo unapewa kila kitu kuanzia PT short, raba etc, sasa siku hizi gharama hizi anapewa mzazi. Bora ifutwe tu
Hadi nauli mkuu enzi zile unapewa kabisa na ela ya chakula njiani, achana na ivyi vifaa vingine ambayo tulikua tunagaiwa bure
 
Upumbavu!

Jiwe ndo alianzisha JKT?
Utaratibu wa JKT ya zamani ilikuwa mtoto akienda anahudumiwa kila kitu, nauli anayotumia kwendea kambini urejeshewa baada ya kuwasilisha tiketi aliyokujia na kupatiwa nauli baada ya mafunzo. kwenye malazi walipewa vifaa vyote kuanzia nguo za mazoezi, viatu, shuka na mataulo. Ila baada ya kuja mzee baba na sera yake ya kubana matumizi hivyo vitu viliondolewa JKT ikabidi gharama hizo zibebwe na wazazi.
 
Nimetafakari gharama wanazoziingia wazazi kuwapeleka watoto ex form six JKT. Ni kubwa na mzigo usio na sababu ya msingi kwa wazazi masikini. Si chini ya laki mbili (200,000 Ths) kwa uchache. Hizi ni hela nyingi kwa mzazi wa vipato vya chini huko vijijini anaye-strugle kupata ada ya shule za Kata.

Najiuliza taabu yote hii ya nini kwa wazazi? Kwani JKT ina umuhimu gani WA LAZIMA kwa maisha binafsi ya mtoto na mzazi?

Kama serikali haina hela ya kuwagharamia watoto, mzazi anazipata wapi?

Kama serikali haina hela za kuwaweka watoto makambini waache mpango huo wa kuwapeleka JKT. Wasiumize watoto na wazazi kwa mambo ambayo si lazima sana katika maisha yao.

Bado kuna watoto wanahitaji hiyo JKT, wawaache hao waende maana wana uhitaji na hiyo JKT
NGOJA MIKUTUMIE NAMBA UWAAMBIE WENYEWE.. 😛
 
Hata Mimi nilitaka kumuuliza.
Nakumbuka MWAKA 2014 Kuna mzazi Kijiji Fulani aliuza shamba ili kijana wake aende jkt.
Sasa sijui MWAKA huu jiwe alikuwa madarakani!!!
Kipindi cha JK hakukuwa na mambo hayo, huyo mzee kama aliuza alifanya hivyo kwa hiari yake tuu
 
Kama mzazi ni masikini kwa nini alizaa watoto. Ukijiona masikini usiache kiumbe duniani ishi mwenyewe ujitafutie mwenyewe chakula basi.
Bangi ni mbaya sana hasa ukiwa huna pesa,, unajikuta unaongea utopolo hadharani.
 
Wakati wa kikwetr gharama zilikuwa chini ya serikali na vijana wengi waliosoma sayansi walipata ajira jwtz now ni maafisa jeshini.
Elimu huwa ni gharama. Vya bure mara nyingi hupuuzwa.
Maarifa wanayopewa yatakuwa na maana sana katika kipindi kisichotarajiwa. Ni kama boya katika chombo cha majini ambapo hufanya kazi tu wakati wa kutapatapa kujikwamua ili maisha yaendelee.
 
Back
Top Bottom