Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sasa kama haiwezi kuonekana mapema wewe umeiona wapi? Yaani maji yatuame kwenye bati lenye slope ya degree 10? Labda hilo bati liwe limebonyea.Shida kubwa ya contemporary House ni bati kuharibika mapema, Kwa maana bati Lina slope ndogo then linakaa na maji muda mrefu na kulifanya lioze haraka.
Shida hii haiwez onekana angalau after 6-13 yrs, Ila nawashauri wenye nyumba hizi wajipange sana
Mkuu niko na project ya contemporary na kuezeka ni mwezi wa 3 mwanzoni. Kelele za vitisho ninazopigiwa (kuhusu kuvuja) hadi nalala na hofu ama niahirishe. Lakini moyo wangu unazipenda sana hizi nyumba ni heri inifie mbeleni huko ila sio ya kuikosa katika umri huu.Sasa kama haiwezi kuonekana mapema wewe umeiona wapi? Yaani maji yatuame kwenye bati lenye slope ya degree 10? Labda hilo bati liwe limebonyea.
Wapo wengi,kikubwa awe mtaalamu na usimbanie bei.Mkuu niko na project ya contemporary na kuezeka ni mwezi wa 3 mwanzoni. Kelele za vitisho ninazopigiwa (kuhusu kuvuja) hadi nalala na hofu ama niahirishe. Lakini moyo wangu unazipenda sana hizi nyumba ni heri inifie mbeleni huko ila sio ya kuikosa katika umri huu.
Kama kuna mtu ana utaalamu wa hii kazi anicheki PM nimpe kazi ya kupaua.
Niunganishe naye,mradi uko Mkuranga kisemvule.Wapo wengi,kikubwa awe mtaalamu na usimbanie bei.
Hizo nyumba sio za njaa njaa
Naogopa lawama mtafute mwenyewe,kwanza Niko mkoaniNiunganishe naye,mradi uko Mkuranga kisemvule.
Kama nimeelewa vizuri, Cost ya Nyumba aina ya Contemporary, ikijengwa kitaalamu n bei yake inaweza kufanana na traditionnal roofing ?...Kuna kitu kinachoongezeka kwenye nyumba za contemporary ambacho ni ‘concrete Gutter’ (mitaro ya kukusanya maji). Ambacho kwa mtazamo wangu nili commet kuwa ndio hasa kinaweza kufanya unafuu wa contempoary uliotokana na roofing ukaja kujilipa (kwa kukalibia au hata kuzidi) kulingana na idadi na namna mitaro ya maji ilivyowekwa kwenye nyumba amabyo kwa namna flani inatokana na ‘spatial arrangement’ ya ndani na namna flani za kuboresha mvuto wa jengo (Contemporary house zinaongezeka mvuto with complexity).
Umenikumbusha kuna mtu kaniambia juzi huko mkoani kwetu viwanja vinauzwa bei kubwa kuliko hata dar. Nikamuuliza shida nini huko mpaka ardhi ifikw thamani kubwa hivyo? Akasema hawa wenzetu maisha yamewapiga sana sasa ukitaka kununua ardhi anataka matatizo yake yoote ayamalize🤣🤣🤣Tatizo lipo kwa mafundi wenyewe! Mnatoa bei za kukomoana! Nani alikuambia ww kunijengea nyumba yangu ndio unaponea kutatua matatizo yako yote? Muwe reasonable bana mfyuuuuu 😡!
Nyumba bwana ikichorwa hivi inapendeza mno.Habarini wakuu,
Kuna mjadala uliletwa humu kuhusu ni nyumba zipi zina gharama nafuu kwenye ujenzi kati ya hizi za kisasa za kuficha bati (‘contempoarary) na zile za kawaida. Ambapo kwa uzoefu wangu nilijaribu kuelezea kuwa kwa kawaida tunatarajia nyumba za paa la kuficha zitatumia tofali nyingi huku bati na mbao zikitumika kidogo sana (maranyingi haizidi nusu) wakati hizi za paa la kawaida zinatumia tofali chache huku zikitumia bati na mbao nyingi zaidi.
Lakini kuna mambo ya kuzingatia
1. Ongezeko la tofali kwenye contemporary house si kubwa sana kulinganisha na utofauti wa mahitaji ya mbao na bati za kupaulia baina ya aina hizi mbili za upauaji wa nyumba.
2. Gharama za mbao na bati kwa ujumla wake zinakupa ongezeko kubwa la gharama kwa nyumba za kawaida kulinganisha na contemporary house.
3. Kuna kitu kinachoongezeka kwenye nyumba za contemporary ambacho ni ‘concrete Gutter’ (mitaro ya kukusanya maji). Ambacho kwa mtazamo wangu nili commet kuwa ndio hasa kinaweza kufanya unafuu wa contempoary uliotokana na roofing ukaja kujilipa (kwa kukalibia au hata kuzidi) kulingana na idadi na namna mitaro ya maji ilivyowekwa kwenye nyumba amabyo kwa namna flani inatokana na ‘spatial arrangement’ ya ndani na namna flani za kuboresha mvuto wa jengo (Contemporary house zinaongezeka mvuto with complexity).
Hivyo basi pendekezo langu lilikuwa ni kwamba kama unataka kujenga kwa kuficha bati na huku pia ukitaka kupunguza gharama ni muhimu kuzingatia mpangilo wa nyumba utakao kufanya uepuke kujenga mitaro mingi kwenye nyumba.
Au unaweza kuepuka kabisa ujenzi wa mitaro kwa kuacha wazi upande wa nyuma ambao ndio maji yataelekezwa huko, na hii ni nzuiri zaidi maana pia itakupunguzia idadi ya tofali ambazo zingehitajika upande wa nyuma huku pia ukiepuka materials kwaajili ya ujenzi wa gutter ambalo lingehitaji zege la nondo.
Na kwakuongeza tu namna hii ya kuacha wazi upande wa nyuma iatakusaidia kupunguza risk ya nyumba kuvuja endapo hukutumia fundi mwenye uzoefu/ujuzi wa nyumba hizi, so risk ya kuvuja itabaki kuwa kwenye maungio ya bati na ukuta (kama fundi ni kimeo).
Kwa maelekezo zaidi juu ya masuala yote yahusuyo ujenzi unaweza kutucheki whatsapp 0717682856.
Unaweza kuona mfano wa hako ka ramani hapo chini (kalichorwa kwa lengo la kusave space na gharama). Kana vyumba vitatu (1master), kiStudy room kidogo, kitchen, dining na public toilet.
View attachment 1745814
View attachment 1745815
View attachment 1745816
Sure kwa sehemu za mabonde nyumba za namna hii labda ijengwe eneo la juu lakini ikijengwa bondeni haipendezi maana roofing yake inakua inaonekaNyumba bwana ikichorwa hivi inapendeza mno.
Jenga sasa mpaka uifikishe mwonekano huo utachina.
Viwanja vyenyewe vya Mbezi Makabe huku Contemporary haikai🤣
Kama anauzoefu wa nyumba za kawaida ndio anaweza vizuri tu boss. Lakini ni vizuri ukawa na ramani (au muhimu ijulikane ‘gutter’ litapita kwenye ukuta upi wa jengo) vinginevyo inaweza kuja kusumbua kuamua sehemu ya kujengea concrete gutter au ikalazimu kuweka mengi kitu ambacho kinaongeza gharamaNaomba kuliza, fundi amabaye hajawahi kujenga Contemporary style anaweza kujenga foundation hari lenta?
Muhimu ni ikisanifiwa (design) vizuri, kwamaana ya kwamba ikiwezekana mtaro wa maji uwe mmoja tu, au kama lengo hasa ni kupunga gharama basi usiweke kabisa mtaro (upande w nyuma uwe wazi) hapo uta save sana kuliko traditional roofingKama nimeelewa vizuri, Cost ya Nyumba aina ya Contemporary, ikijengwa kitaalamu n bei yake inaweza kufanana na traditionnal roofing ?...
Hili wazo zuri, nitalifanyia utafitiNadhani ili kuepuka kuvujiwa nikuacha nyuma wazi ili maji yatiririke bila tatizo
Unamaanisha hivi?Contemporary ndio nini? Kama hautaki bati lionekane kwa nini usimwage zege kabisa? Shida ya mapaa haya sio slope au ujuzi wa fundi. Shida ni mtu aliyechora. Matatizo mengi yanatokea pale ambapo bati linakutana na ukuta. Wengi wanachimbia kwenye ukuta. Hilo ni kosa kwa sababu bati na simenti na maji sio rafiki. Kinachotakiwa kufanyika ni kuchukua kipande kingine cha bati ambacho kitakunjwa kufunika hiyo joint na kuendelea juu na ukuta kama inchi 6 hafafu unaikunja tena kuiingiza kwenye ukuta. Bati hapo haliathiriki kwa sababu maji hayalifikii linaooingia kwenye ukuta. Kwa lugha ya kitaalamu kipande hiki çha bati kinaitwa "flashing".
Amandla....
Mkuu wewe ni fundi? kama Yes naomba namba yako PM au kama unaye fundi wako ni PM.Contemporary ndio nini? Kama hautaki bati lionekane kwa nini usimwage zege kabisa? Shida ya mapaa haya sio slope au ujuzi wa fundi. Shida ni mtu aliyechora. Matatizo mengi yanatokea pale ambapo bati linakutana na ukuta. Wengi wanachimbia kwenye ukuta. Hilo ni kosa kwa sababu bati na simenti na maji sio rafiki. Kinachotakiwa kufanyika ni kuchukua kipande kingine cha bati ambacho kitakunjwa kufunika hiyo joint na kuendelea juu na ukuta kama inchi 6 hafafu unaikunja tena kuiingiza kwenye ukuta. Bati hapo haliathiriki kwa sababu maji hayalifikii linaooingia kwenye ukuta. Kwa lugha ya kitaalamu kipande hiki çha bati kinaitwa "flashing".
Amandla....
Picha haionyeshi vizuri. Kuna shadow sana. Ila inafanana. Kitu muhimu ni ipande ukutani na ikunjwe ili iingie ndani ya ukuta ili kuzuia maji yatakayosuka na ukuta upita nyuma yake.Unamaanisha hivi? View attachment 2260036
Ni Fundi. Lakini sio mjenzi.Mkuu wewe ni fundi? kama Yes naomba namba yako PM au kama unaye fundi wako ni PM.
Vp tunaweza fanya kazi ya paa kuweka hizo kitu mkuu! tumeipenda hiyo design...maana kuna nyumba ya familia inaleta shida...na fundi wa kitaaa anasema itawekwa cement haitavuja. Tunataka tumkatae, mafundi wanatofautiana na technology pia.Ni Fundi. Lakini sio mjenzi.
Amandla...