Gharama za umeme: Rais Samia muwajibishe Waziri Kalemani na uongozi wote wa TANESCO

Mkuu,Naomba nikubaliane na Waziri
 
WATU mna roho mbaya Sana ,huyu tajiri unaemzungumzia , ni mtanzania na kwenye miradi yake analipa kodi za kutosha, kuwa tajiri Sio dhambi ili hali ni mtanzania so favour za serikali lazima hazipate Kama mtanzania yeyote ,
 
Waziri sio mjinga mkuu,aliyosema ni maagizo kutoka juu,this is obvious,hawezi kukurupuka tu na kutoa maamuzi mazito namna hii.Si ulimsikia akisema ni maagizo?Kalemani ana akili mkuu,si mjinga kama unavyo dhani.

Na hizi akili za kutaka matajiri walipe zaidi eti kwa kuwa wanazo, ni akili za kimaskini sana,mbona hakuna mtu anayekatazwa kuwa tajiri?Hela za tajiri ni zake,kwa hiyo aachwe atoe zaidi kwa kupenda through philanthropy kwa mfano,sio kwa kulazimishwa kwa kutumia hila.Naomba ikumbukwe kwamba tajiri naye ana haki ya kufaidi huduma zitolewazo na serikali.Kama serikali kwa mfano imetoa nguzo bure kwa nini tajiri achangie.Na wewe chakarika uwe tajiri mkuu,acha wivu.
 
Kuna mambo yanashangaza mzee na yataleta ugumu mbelenj kuyarudisha kama mwanzo mana ndio Uhalisia, Nachelea kusema tupo too too theoretically, Angalia mfano wa swala la wamachinga unawatoaje barabarani
 
Kuna watu huwa wengine mnasababisha hata mishahara ipandishwe kimya kimya , yani ukisikia tu mtu kapata hela unataka na bei ipande.
Hizi roho ndo zile ambazo manabii walitumwa kuja kuzifuatilia
 
Umeambiwa hii 27,000 ni kuunga single phase.
Less than 10% ya watanzania ndio wanajenga apartments, huoni hoja yako inataka kukatili asilimia zaidi ya 90 ya watanzania?
mimi sijui kuhusu umeme nileweshe hapo tofauti ya single phase na nyingine kwa gharama na hata nguvu ya umeme natanguliza shukrani
 
Nahisi hilo swala wangeliangalia kwa mtizamo wa tofauti kidogo, hii ya kuunganishiwa umeme kwa 27 ingebaki kwenye REA pekee, na kwingineko nzingebaki zile gharama za kawaida, mwisho wa siku shirika lilikosa ruzuku litayumba.
 
Mkuu Maji ,umeme ,barabara ni huduma za jamii ,hizo kwa nchi ambazo zinajielewa ilitakiwa zitolewe bure (maji+umeme kwenye kuunganisha) iwe inalipiwa kwenye matumizi tu.

Sikubaliani na wewe kwa 100% , Serikali inakusanya kodi nyingi sana sema zinatumika ndivyo sivyo,nyingi zinaishia kwa wala rushwa serikalini ,unamnunuliaje RC/DED/DAS.RAS etc Ma Viete ya milioni 400 wakati wanafunzi wanasoma chini ya miti?

Mimi napendekeza kabisa tena zifutwe kabisa hata hiyo 27k waunganishe bure,Maji siku hizi wanaunganisha kwa mkopo ,mkuu hiyo laki 3 au laki 5 gharama sio wote wanaweza mkuu ,hata kama wewe una kipato kizuri huko marekani ,jaribu kufikiria hawa wanaijibanabana kujenga vyuma vya polisi post waweze kujistiri.

Kama ni kweli wameweka flat rate kwa watu wa single phase kuunganishwa kwa 27k basi nampongeza sana waziri,tambua kwamba hao wa vijijini wanaounganishwa kwa elfu 27 nao wana mafremu na maghorofa vile vile na vile vile hapa town kuna watu wana vyumba viwili vya paa moja lakini wanaounganishwa kwa laki 3 ,sioni mantiki yako!!

Pia tambua REA watu wote wanachangia pindi ukinunua umeme na kwanini wabague wa mjini wakati tunachangia wote? Halafu vijiji karibia vyote viashaunganishwa na umeme(Vimebaki vijiji vichache) ,je unataka kutuambia kwamba sasa tusichangie tena REA? Hizo fedha za REA ndio zinapunguza unafuu kwa watu wote.
 
Duh ampeleke porini huko mpaka akili imkae sawa 😂😂😂😂😂
 
Wewe akili yako itakuwa na matatizo sio bure, wanaojenga magorofa na mafremu wako wangapi nchi nzima, hata tukihesabu unadhani unaweza fikisha 1000. Vilevile uelewe kuwa waziri anachotangaza kinakuwa kilishapitishwa na baraza la mawaziri yeye ni mtekelezaji/msimamizi tu, waziri ubavu wa kujiamulia mambo makubwa kama hayo anayatoa wapi? . Tatizo la tanesco naona liko hapa, waziri anatangaza hiyo gharama lkn ukienda Tanesco gharama ziko palepale kama unahitaji nguzo sio chini ya laki 5 nafikiria kuwafikisha mahakamani, haiwezekani waziri anasema yake lkn ukienda kwa watendaji wa chini nao wanasema yao, huu ni uhuni.
 
AMINI KWAMBA UMEANDIKA HAYA KWA KUTOKUJUA DIRA NA UELEKEO WA SERIKALI
 
Umeme wa REA vijijini umepita barabara kuu tuu. kama kufka kwako unahitaji nguzo 3 toka barabara kuu haupati umeme.
 
Namba ya wateja itaongezeka. Je, amejipangaje kuwapa umeme wa uhakika? Maana sa ivi umeme unakata kwa siku hata mara 10 coz ya upungufu wa wafanyakazi hivyo maintenance haifanyiki kwa wakati.
 
Umeme wa REA vijijini umepita barabara kuu tuu. kama kufka kwako unahitaji nguzo 3 toka barabara kuu haupati umeme.

Si kweli mkuu ,umeme wa REA naujua , hata hapa mjini kama unataka umeme na kuna nguzo zaidi ya mbili zinahitajika na ume apply peke yako haupelekewi hata kama utalipa 620k.

Umeme wa REA vijijini navyo ni hivyo hivyo kama nguzo zaidi ya mbili na unataka umeme peke yako haupati,umeme wa REA unapita barabara kuu kisha wanaingiza nguzo mbili ndani basi lakini gharama ni 27k flat.

Kuna mama ana chumba kimoja naye kwakuwa yupo mjini analipa laki 3 na 20 huu ni wizi wa mchana kweupe.

Dawasa wamejiongeza maji kuweka ni bure ila unalipa kwa awamu mpaka deni liishe...nao tanesco inabidi wajiongeza ,elfu 27 kuunganishwa kwa TZ nzima waziri amefanya jambo jema sana na tunampongeza.
 
Kwa hiyo matajiri wanaolipa huduma za maji sawa na masikini waongezewe bei?

Yaani mtoa mada ndio anataka iwe hivyo......Hata buku 1 kwa Unit 2.9 au 2.8 inabidi matajiri waongezewe wasiuziwe bei moja na sie wala vumbi.
 
Acha mawazo ya kijinga wanataka watu wengi wapate umeme na ni Moja ya Ahadi za ccm 2020
 
Kipindi cha nyuma makampuni ya simu alikuwa yanauza sim card kwa Tsh. 50,000/@1 Baadae wakapunguza mpaka Tsh. 10,000 na sasa ni Tsh. 1,000/ hadi 500/.
Walifanya hivyo ili kuwa na wateja wengi ili kuwakamua kwenye vocha/airtime.

Kama nguzo ya umeme na hiyo mita ni Mali ya tanesko ni kwanini umuuzie mteja?
Leo hii nikilipishwa nguzo Kesho ikishawekwa mteja mwingine anakuja kuitumia bure pasipo kunichangia gharama nilizozitumia awali! Do you think that is fair?
 
Ukiunganisha wengi utapata mapato.

Tanesko itakufa kwa kutegemea mapato ya kuunganisha umeme.

Kinachotakiwa wateja waunganishiwe haraka ili walipie bili na kutumia(hapa ndipo mapato yalipo)

by the way umeme huo wa 27000 ni single phase
Mwelekeze huyo naona anaongea vitu haelewi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…