Godbless Lema: Hatupingi Uwekezaji Bandarini, ila Serikali irekebishe yanayopigiwa kelele na wananchi

Godbless Lema: Hatupingi Uwekezaji Bandarini, ila Serikali irekebishe yanayopigiwa kelele na wananchi

chiembe

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2015
Posts
16,859
Reaction score
28,112
SERIKALI ya Tanzania, imeshauriwa kurekebisha baadhi ya vifungu vinavyolalamikiwa na wananchi katika mkataba wa ushirikiano wa kuendesha bandari ya Dar es Salaam, kati yake na Kampuni ya Dubai Port World (DP World).

Ushauri huo umetolewa leo tarehe 19 Juni 2023, katika mjadala wa kulinda na kuendeleza umoja wa kitaifa wakati wa mageuzi ya kisiasa na kiuchumi, uliofanyika jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika mjadala ulioandaliwa na Kampuni ya Media Brains, Mjumbe wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Godbless Lema, amesema nchi inahitaji uwekezaji lakini Serikali inapaswa irekebishe vifungu hivyo, kisha itoke kwa wananchi kueleza maboresho yaliyofanyika.

“Si dhambi kuleta mwekezaji, katika nchi huwezi kukwepa suala la uwekezaji. Dunia yote inafanya kazi kwa ushirikiano. Nchi inahitaji mwekezaji zaidi ya bandarini, kimsingi uwekezaji hakuna mtu anaukataa na hakuna namna Tanzania inaweza kuishi bila nchi nyingine,” amesema Lema na kuongeza:

“Kwenye ibara ya 4(2) ya makubaliano hayo imeeleza vizuri kwamba Tanzania ikitaka ku-adress jambo lolote la uwekezaji kuhusu bandari hawatamwambia mtu yeyote kwanza isipokuwa Dubai. Sasa mkirekebisha haya mambo halafu mkaja mkawaelewesha watu, mkaondoa vitu vyenye mashaka na watu wa kuwaambia wananchi ni wale wenye uweledi…msitume wale wanaocheza sarakasi bungeni watawaharibia,” amesema.
 
Anayepinga ni nani?

Hivi nyinyi maccm mnakichaa?

Tunachopinga ni mkataba usio na huruma na wananchi wa nchi ya Tanganyika ukiwapo na wewe!

Bandari zote nchini? Tena hakuna ukomo?

Hicho ndo wananchi tunapinga!

Hama ccm upate akili
 
Watanzania hawapingi uwrpo wa Wawekezaji wa kigeni hapa nchini, wanachopinga ni uwepo wa masharti/vipengele vibovu visivyofaa vya kuuza nchi vilivyopo ndani ya Mkataba wa uwekezaji. Wafuasi wa vyama vya siasa msipotoshe Jambo hili. tafadhali sana.
Watu wanahamisha magoli. Shida sio DP world kuwekeza bandarini, shida ni vipengele vya mkataba. Hata wangekuja wamarekani, waingereza au wafaransa kwa mkataba ule bado kelele zingepigwa.
 
Kama mwekezaji ni mwarabu kwangu ni Big No;
"Tuliwapinga Makaburu si kwa sababu ya rangi ya ngozi yao, Bali tuliwapinga kwa sababu ya matendo yao".
By Mwalimu J. K.Nyerere.

Hivyo basi, tunatakiwa kuwapinga Waarabu kutokana na matendo yao lakini siyo kwa sababu ya rangi ya ngozi yao au kutokana na wao kuwa Waarabu.
 
Anayepinga ni nani????

Hivi nyinyi maccm mnakichaa?

Tunachopinga ni mkataba usio na huruma na wananchi wa nchi ya Tanganyika ukiwapo na wewe!

Bandari zote nchini? Tena hakuna ukomo???

Hicho ndo wananchi tunapinga!

Hama ccm upate akili
Tupe huo mkataba kama unao hapo. Kama hauna kaa kimya na msubiri mumeo tu.
 
Exactly,kanisa ndo chanzo cha chokochoko zote
Kanisa lina wanasheria wengi sana asilimia kubwa ya mapadre husomea sheria sio mapopoma kama upande wa wavaa kubazi wao wakisha kariri Quraan baasi wamemaliza.
Na itoshe tu kuwapima uelewa wa mambo hasa ukilinganisha kauli zao kati ya Kitima na Sheikh mkuu wa Bakwata
 
Tatizo ni kanisa katoliki kuhamasisha chuki za kidini sio jingine.
Tunapopinga ubaya wa mikataba ya hovyo, hatusemi dini ya mtu kuwa ndiyo sababu ya ubaya huo

Tunapinga kiongozi yeyote kuingia mikataba ya hovyo bila kujali dini yake madamu tu ni mtanzania

Dini ya mtu haina uhusika wowote na kuingia mikataba mibovu

Kazi kwako sasa wewe mdini, na watu wadini siku zote huwa wajinga sana hawawezi kujiamini zaidi ya kujishuku labda dini yake ndiyo shida!

Wananchi tunakuhakikishia kuwa, Dini ni nzuri na haina shida, shida ni wewe kukubali kuwa mdini kwenye mambo yasiyo na uhusiano na dini
 
Back
Top Bottom