God's Conscience vs Free Will: Je, Mungu anajua hatima ya wanadamu itakuwaje?

God's Conscience vs Free Will: Je, Mungu anajua hatima ya wanadamu itakuwaje?

Abracadabra tupu.

Anaeleza jinsi unavyomjua Mungu kwa maarifa, lakini haelezi kivipi unajua Mungu yupo.

Thibitisha step by step unavyojua Mungu yupo.
Nimecheka sana, soma tena umuelewe. Mwanachuoni huyo amemaliza kila kitu hapo.

Hujaona alovyo onyesha suala la maarifa ni mchakato ?

Kisha akamilizia kwa kusema ufunuo ambao nimeutaja huko juu unakamilisha uthibitisho. Ndiyo maana huwa nathibitisha hilo kwa kuweka ile aya ambayo ni sababu ya sisi kufikia hapa.

Hili kwangu rahisi sana, na kila siku nathibitisha ya kuwa Mola yupo.
 
Nimecheka sana, soma tena umuelewe. Mwanachuoni huyo amemaliza kila kitu hapo.

Hujaona alovyo onyesha suala la maarifa ni mchakato ?
Swali: Unajuaje kwamba kuna pembetatu duara katika planes za Euclidean geometry na habari ya kuwepo pembetatu duara si habari za uongo tu?

Jibu: Utajua pembetatu duara ipo kwa kutumia akili, maarifa na mchakato, utaielewa na kuiona pembetatu duara, utaona kivuli chake, kila duara na kila pembetatu zinatokana na pembetatu duara, bila ya pembetatu duara kuwepo huwezi kuwa na pembetatu wala duara, utaijua pembetatu duara kwa fikra na uchambuzi wa utambuzi wa kina pima pomoni na ushahidi wa uthibitisho na kutafsiri maono ya dunia na mengine yatajidhihirisha zaidi tukivumbua vitu zaidi.

Hapo nimethibitisha kwamba kuna pembetatu duara?
 
Unajuaje ukuu wa Mungu uko beyond human imagination, na kwamba hiyo si hadithi ya uongo uliyohadithiwa tu?

Vipi ikiwa Mungu hayupo, na watu wamejitungia tu hadithi ya uongo kwamba Mungu yupo na kapita uelewa wa watu?

Hapo ukiamini uongo huu, bila kuhoji kimantiki, utajuaje ukweli kwamba Mungu hayupo na habari za kuwepo kwake ni hadithi za uongo zilizotungwa na watu tu?
Wewe tu namna ulivyo inathibitisha uwepo wa Mungu hata bila kuambiwa na mtu yoyote.......ujuaji usio na maana hausaidii, ni kujitafutia tu maangamizi ya milele.
 
Swali: Unajuaje kwamba kuna pembetatu duara katika planes za Euclidean geometry na habari ya kuwepo pembetatu duara si habari za uongo tu?

Jibu: Utajua pembetatu duara ipo kwa kutumia akili, maarifa na mchakato, utaielewa na kuiona pembetatu duara, utaona kivuli chake, kila duara na kila pembetatu zinatokana na pembetatu duara, bila ya pembetatu duara kuwepo huwezi kuwa na pembetatu wala duara, utaijua pembetatu duara kwa fikra na uchambuzi wa utambuzi wa kina pima pomoni na ushahidi wa uthibitisho na kutafsiri maono ya dunia na mengine yatajidhihirisha zaidi tukivumbua vitu zaidi.

Hapo nimethibitisha kwamba kuna pembetatu duara?
Mfano wako si sahihi.
 
Wewe tu namna ulivyo inathibitisha uwepo wa Mungu hata bila kuambiwa na mtu yoyote.......ujuaji usio na maana hausaidii, ni kujitafutia tu maangamizi ya milele.
Hujanieleza mimi nilivyo inathibitishaje uwepo wa Mungu.

Hujanieleza ni vipi nina ujuaji usio na maana, hujaeleza ujuaji ulio na maana ni upi na usio na maana ni upi.

Hujanieleza maangamizi ya milele yanatafutwaje.

Yani kama hivi ndivyo unavyomtetea huyo Mungu, na yeye yupo anakuangalia, sasa hivi atakuwa anatingisha kichwa kusikitika jinsi ambavyo hujamtendea haki kutetea uwepo wake.
 
Mjenzi ni mtu au siyo mtu ? Hata mwenye nyumba husemwa amejenga, japo ni mmoja kwa maana ya umiliki. Kwahiyo usighurike na wingi ila tunarudi kwenye mjenzi.

Kukubali ya kuwa nyumba imejengwa na watu hiyo ni self evident truth tayari. Sasa kumjua ni nani hilo ni jambo lingine. Nikajua unajua maana ya "self evident truth" kumbe hujui.

Sahihi kabisa huo ndiyo uhalisia na hiyo ndiyo self evident truth.

Sasa hiyo ndiyo maana ya self evident truth, yaani unapoiona tu nyumba kuna haya yafuatayo yanadhihirika :

1. Yupo msanifu wa nyumba husika
2. Mwenye akili na maarifa
3. Mwenye malengo na makusudio ya kujenga nyumba hiyo

Sasa ndiyo umatakiwa uonyeshe ya kuwa ulimwengu haujaumbwa na utuambie imekuwaje ukawepo.

Huu utoto mwingine, tamko "kuumbwa au kuumba" kwa lugja yetu ya Kiswahili ni tamko haswa, halitumiki nje ta Mola muumba. Tafuta lugha nyingine.

Kingine umehoji kitoto sana, ina maana wewe kuwepo kwako ni matokeo ya kuwepo kampuni fulani iliyo tekeleza kuwepo kwako ?

Kwanini umeingiza suala la kampuni na ukatumia tamko "kuumbia" vibaya ?

Swali zuri sana, haya sasa ndiyo maswali ya kikubwa. Hakuna aliye shuhudia hayo ila haya yameelezwa kwenye vitabu vitakatifu.

Nani amethibitisha ya kuwa Nyumba imejengwa ? Self evident truth ni kitu kuonyesha uwepo wa kitu kingine kwa chenyewe. Kama unavyoona nyumba kuwepo kwa nyumba kunaonyesha uwepo wa msanifu, mjenzi mwenye sifa anuai. Hili unatakiwa uelewe. Ulimwengu kuwepo kwake unaonyesha ya kuwa yupo aliye sanifu jambo hili, mwenye uwezo, mwenye kujua ambaye hakuwahi kutanguliwa na kutokujua, mwenye maarifa, mwenye hekima na malengo.

Ulimwengu wenyewe kuwepo kwake wenyewe unajithibitisha ya kuwa umeumbwa, hii ndiyo maana ya self evident truth.

Historia ya ulimwengu ipo ni wewe ndiyo huijui. Vitabu vimeelezea hili na vipo vitabu vingi, soma kitabu kiitwacho "al-Bidayat wa al Nihaya (Mwanzo na Mwisho)".
Niambie kampuni lililohusika kuumba ulimwengu

Nithibitishie ni nani aliumba ulimwengu
 
Na ndio maana imeitwa illusion yani una exprience kitu ambacho hakina uhalisia ukidhani kuwa ni reality
Kitu gani kinafanya free will iwe ni illusion wakati tunaexperience hiyo free will ?
 
Kitu gani kinafanya free will iwe ni illusion wakati tunaexperience hiyo free will ?
kwasababu kila jambo lilisha setiwa, haukuweza kwenda vinginevyo kwasababu choice ishakuwa fixed
 
Mfano wako si sahihi.
Hujaeleza kwa nini mfano wangu si sahihi, hivyo ukosoaji wa mfano wangu, kwamba mfano wangu si sahihi, ndiyo kitu kisicho sahihi hapa.

Ukosoaji wako wa mfano wangu si sahihi, kwa sababu hujaeleza mfano wangu si sahihi kwa sababu gani.

Mimi si mzembe kama wewe. Nitakueleza kwa nini mfano wangu ni sahihi.

Mfano wangu na habari uLizotuma kuelezea Mungu ni sawasawa.

Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote anakuwa contradicted na ulimwengu huu unaoruhusu mabaya.

Pembetagu duara inakuwa contradicted na Euclidean gemetry.

Same thing.

Ukiamini Mungu huyu yupo, umeamini contradiction.

Pembetatu duara nayo ni contradiction.

Kwa nini usiamini pembetatu duara nayo ipo?
 
kwasababu kila jambo lilisha setiwa, haukuweza kwenda vinginevyo kwasababu choice ishakuwa fixed
Umejuaje kama kila jambo limesetiwa ilhali hatuoni athari ya kusetiwa kwa mambo hayo badala yake tuna experience free will ?
 
Hujaeleza kwa nini mfano wangu si sahihi, hivyo ukosoaji wa mfano wangu, kwamba mfano wangu si sahihi, ndiyo kitu kisicho sahihi hapa.
Mfano wako ndiyo huu huu wa kila siku unaotoa, na nimeshaukosoa zaidi ya mara moja.

Mfano wako si sahihi kwa sababu ni jambo la makubaliano na halikidhi haja.
Ukosoaji wako wa mfano wangu si sahihi, kwa sababu hujaeleza mfano wangu si sahihi kwa sababu gani.
Mfano wako si sahihi kwa kile unachokilinganisha kwacho. Unachokilinganisha kwacho ni "Necessary Neing" yaani kuwepo kwake ni lazima na hakijawahi kuwepo, kuhusu duara ni makubaliano ya kimahesabu tu.
Mimi si mzembe kama wewe. Nitakueleza kwa nini mfano wangu ni sahihi.
Usingekuwa unakimbia maswali yangu, katika mtu ninaye jibu maswali ni mimi na katika watu wasio jibu maswali ni nyinyi, uzembe unaonekana kwenu sababu si mahodari wa kujenga hoja na kujibu maswali.

Mfano wangu na habari uLizotuma kuelezea Mungu ni
Onyesha hilo.
Mungu mjuzi wa yote, mwenye uwezo wote na upendo wote anakuwa contradicted na ulimwengu huu unaoruhusu mabaya.
Ndiyo maana nikasema mfano wako haukidhi haja. Huwezi kuonyesha "contradiction" na kwa Mola muweza wa yote, yaani anachofanya ni kile anachotaka wala hapangiwi.

Swali la msingi, cotradiction inatokana wapi wakati yeye ndiyo ameruhusu hayo yatokee kwa kutaka. Siyo kila jambo unalo ona au kuhisi lina contradiction basi kweli lina utata, bali elimu yako ni ndogo na akili yako changa, ndiyo maana nakuonyesha hapa.
Pembetagu duara inakuwa contradicted na Euclidean gemetry.
Bado hujaonyesha contradiction, na nilijua tu kwamba hili huliwezi na hujawahi kuweza.
Same thing.
Hujaonyesha huo usawa.

Ukiamini Mungu huyu yupo, umeamini contradiction
Contradiction iko wapi ?
Pembetatu duara nayo ni contradiction.
Hujaonyesha contradiction kwa Mola muumba.
Kwa nini usiamini pembetatu duara nayo ipo?
Si halisi.
 
Mfano wako ndiyo huu huu wa kila siku unaotoa, na nimeshaukosoa zaidi ya mara moja.

Mfano wako si sahihi kwa sababu ni jambo la makubaliano na halikidhi haja.

Mfano wako si sahihi kwa kile unachokilinganisha kwacho. Unachokilinganisha kwacho ni "Necessary Neing" yaani kuwepo kwake ni lazima na hakijawahi kuwepo, kuhusu duara ni makubaliano ya kimahesabu tu.

Usingekuwa unakimbia maswali yangu, katika mtu ninaye jibu maswali ni mimi na katika watu wasio jibu maswali ni nyinyi, uzembe unaonekana kwenu sababu si mahodari wa kujenga hoja na kujibu maswali.


Onyesha hilo.

Ndiyo maana nikasema mfano wako haukidhi haja. Huwezi kuonyesha "contradiction" na kwa Mola muweza wa yote, yaani anachofanya ni kile anachotaka wala hapangiwi.

Swali la msingi, cotradiction inatokana wapi wakati yeye ndiyo ameruhusu hayo yatokee kwa kutaka. Siyo kila jambo unalo ona au kuhisi lina contradiction basi kweli lina utata, bali elimu yako ni ndogo na akili yako changa, ndiyo maana nakuonyesha hapa.

Bado hujaonyesha contradiction, na nilijua tu kwamba hili huliwezi na hujawahi kuweza.

Hujaonyesha huo usawa.


Contradiction iko wapi ?

Hujaonyesha contradiction kwa Mola muumba.

Si halisi.
Kwa nini Mungu ni necessary being?
 
Back
Top Bottom