Goli la Mama: Rais Samia kununua kila goli Tsh. Milioni 5 mechi za Simba, Yanga CAF

Goli la Mama: Rais Samia kununua kila goli Tsh. Milioni 5 mechi za Simba, Yanga CAF

Halafu watoto wetu wanakaa chini mashuleni.

Trump hakukosea kabisa kwa kauli yake kuhusu Africa..

Hizo pesa zinanunuwa madawati mangapi?

Sent from my 2201117SG using JamiiForums mobile app
Wewe umeshawahi kuchangia nini katika shule uliyosoma? Acheni unafiki, huwezi kumaliza shida wala kumaliza maskini. Wamaskini na shida zinaendelea kuwepo na bata lazima ziliwe
 
Niende kwenye mada, Rais Samia amekuwa akitoa zawadi ya milioni moja kwa kila goli itakalofunga Simba au Yanga kwenye michuano ya kimataifa

Hii sio sawa, japo wote wanacheza michuano ya kimataifa ila ni michuano ya viwango tofauti kabisa vya ubora, ni kama ligi kuu na ligi ya daraja la kwanza

Sasa kutokana na tofauti za ubora viwango vya zawadi pia vingetofautiana, labda Yanga apewe laki 5 kwa kila goli na Simba milioni 5 kwa kila goli

Sababu hata CAF wenyewe wanatoa viwango tofauti vya zawadi kwa washindi na washiriki wa mashindano hayo
Anayebeba Champions League anapewa fedha nyingi zaidi kuliko anayebeba Shirikisho

Hata mashindano kwenye mabara mengine mfano UEFA na EUROPA zawadi huwa ni tofauti kwa washiriki wake kutokana na ubora wa mashindano kutofautiana
 
Kama mtu aliyefeli na kushushwa daraja anapata zawadi sawa na yule aliyefanya vizuri, Kuna umuhimu gani wa kufanya vizuri?

Huyu aliyefanya vizuri atakuwa na motisha gani wa kuendelea kufanya vizuri?
 
Kama mtu aliyefeli na kushushwa daraja anapata zawadi sawa na yule aliyefanya vizuri, Kuna umuhimu gani wa kufanya vizuri?

Huyu aliyefanya vizuri atakuwa na motisha gani wa kuendelea kufanya vizuri?
Huwa unaanzusha mada ili watu wasome au tu ili upate comments? Wewe ni mtu mpumbavu, jf ukishaweka post hata kama hakuna aliyecomment jua imesomwa na watu wengi na maoni yako yamefika/yamesikika
 
Niende kwenye mada, Rais Samia amekuwa akitoa zawadi ya milioni moja kwa kila goli itakalofunga Simba au Yanga kwenye michuano ya kimataifa

Hii sio sawa, japo wote wanacheza michuano ya kimataifa ila ni michuano ya viwango tofauti kabisa vya ubora, ni kama ligi kuu na ligi ya daraja la kwanza

Sasa kutokana na tofauti za ubora viwango vya zawadi pia vingetofautiana, labda Yanga apewe laki 5 kwa kila goli na Simba milioni 5 kwa kila goli

Sababu hata CAF wenyewe wanatoa viwango tofauti vya zawadi kwa washindi na washiriki wa mashindano hayo
Anayebeba Champions League anapewa fedha nyingi zaidi kuliko anayebeba Shirikisho

Hata mashindano kwenye mabara mengine mfano UEFA na EUROPA zawadi huwa ni tofauti kwa washiriki wake kutokana na ubora wa mashindano kutofautiana
sako alipataje goli bora akiwa michuano gani?
 
Hili wazo ni baya na nitatoa sababu mbili tatu.

Kwanza, linaweza kuharibu mipango ya uchezaji wa timu. Siku hizi timu zinacheza kwa mipango siyo tu kufunga magoli. Tumeona juzi Watunisia baada ya kupata goli mbili wakatulia. Ukiahidi pesa ya magoli kuna timu au wachezaji wanaweza kuwaza kufunga badala ya kucheza kimbinu hasa kama timu tayari inaongoza.

Pili, kwa mazingira ya sasa Rais kuahidi tumilioni 5 kwa shughuli pevu kama ya weekend hii ni kushusha umuhimu wa magoli yenyewe.

Tatu, tuache kutafuta njia za mkato za mafanikio. Simba mwaka 1993 waliahidiwa kupewa basi kila mchezaji na bado wakashindwa kutoboa katika mechi moja tu uwanja wa nyumbani. Nchi iwekeze ipasavyo katika michezo na tuache kurukia pale tunapoona kuna upenyo wa kufaidika kisiasa, hizi njia nyingine tumezijaribu sana hazina mafanikio.
Kuna timu itafungwa 4-2 halafu itapewa hela nyingi kuliko ile iliyoshinda 1-0. Hili linaweza kutokea na sijui watajificha wapi kwa aibu hiyo.
 
Back
Top Bottom