GPA ya 5 - Anazurura mtaani; we are not serious!

GPA ya 5 - Anazurura mtaani; we are not serious!

Leo nilikua namwambia kijana wangu kwamba.

Shule itampa maarifa, lakini kusoma hakumpi guarantee ya kufanikiwa.

Lakini nilimwambia kwamba.

Akishaipata elimu, atakua namaarifa. Ili afanikiwe anapaswa kuwa mwenye bidii na nidhamu
Sure, that is what I always tell guys of mine
 
Mzee hii nchi kuna vichwa aisee labda kama hujakutana navyo tu, mimi sikuamini mpaka nilivyokutana na mwanafunzi ana A zote mwaka wa kwanza na wa pili!, (sasa hivi yupo mwaka wa tatu kozi ngumu tena sayansi!) asipoyumba mwaka huu wa mwisho lazima awe overall
Mrejesho tafadhali
 
Kosa kubwa sana la kiufundi,Hawa vijana wanaopasi kwa alama za juu,kuanzia secondary mpaka vyuoni,ilibidi wapewe nafasi kubwa walelewe kwenye vitengo kazi wanazozitaka,au kuwafaa,wapikwe mpaka waive ndani na nje ya nchi,then wapewe nafasi wafanye maajabu baada ya kuiva,sasa li inchi letu mtu katoka chuo bado amejaa nadharia tu na anaufaulu mkubwa wanataka ajiajiri,ushenzi mtupu
Hujui tu usomaji wa vijana wa leo.

Mtu anameza madesa kwa ajili ya kufanyia mtihani tu baada ya hapo hana analokimbuka ama kuelewa ukimleta kwenye field husika.

Kuna jamaa nilikuwa nasoma naye chuo fulani alikuwa anameza madesa hatari lakini hata kuandika field report anatafuta mtu amsaidie.
 
Namfahamu rafiki angu UDSM certificate alitoka with distinction about 4.7 ila hakuwa na connection angesoma degree direct. Akaenda OUT LLB akapiga GPA ya Tano na hakupewa tuzo ya mwanafunzi bora. Dizzle anatafuta pesa yupo mtaani since 2018,aende law school ila he is seriously and tallented
UDSM mwanafunzi wao yeyote aliyesoma pale Certificate akipata ufaulu wa distinction ana ofa ya kusoma degree moja kwa moja haihitaji connection.
 
Kwa mtazamo wangu tumechelewa kujua umuhimu wa pass za juu katika kupaisha Taifa kiuchumi nk

Hivi inakuwaje mwanafunzi amemaliza Chuo amepata GPA ya 4.8 au kwa wenzetu wa Arts wanapata hadi GPA 5 naye yupo mtaani hana ajira?
[emoji38][emoji38][emoji38] nyie danganyeni watu wakomae na izo GPA za 5 harafu tutakutana kiataani kinachofanya kazi so ufauru Wala usidanganywe na mtu soma Kwa step huku ukiandaa future Yako baada ya chuo .
 
Creativity and innovation matter most ,Elon musk kafika hapo alipo kwa kujiongeza computer hakufundishwa darasani na ndio imemfikisha alipo mm naamini kama uko serious GPA ni upuuzi tu kikubwa get right materials angalia upepo unaelekea wapi jitose ulingoni...
Unadhani kuna kina Elon wangapi tena wengine zaidi yake na wamekufa bila senti.., its more than being creative and innovative - kuna right idea at the right time, being at the right place at the right time n.k. A lot of things needs to fall in place....

Nadhani the bigger issue sio kushangaa nani ana nini na anasugua benchi mtaani cha kulalamika ni kwanini nchi inayohitaji yenye mahitaji lukuki kuna nguvu kazi haifanyi kazi - yaani wastage..., Hayo mengine unaweza ukawa sio mgunduzi wala creative ila una-copy na ku-paste au unachukua idea za watu na kuziwa mainstream
 
  • Thanks
Reactions: Sax
Kwa mtazamo wangu tumechelewa kujua umuhimu wa pass za juu katika kupaisha Taifa kiuchumi nk

Hivi inakuwaje mwanafunzi amemaliza Chuo amepata GPA ya 4.8 au kwa wenzetu wa Arts wanapata hadi GPA 5 naye yupo mtaani hana ajira?
GPA ya 2.7 ya Muhas ni bora zaidi ya GPA ya 5 ya vyuo vingine
 
GPA ya 2.7 ya Muhas ni bora zaidi ya GPA ya 5 ya vyuo vingine
kila mwaka napokea wanafunzi kutoka hivi vyuo vya afya nchini tanzania na nje ya nchi kwa taasisi fulani hapa nchini

Huwa naona uwezo wa wanafunzi hawa vizuri sana lakini huwa sioni utofauti kabisa unaozushwa kuwa wanafunzi wa muhas wanakuwa bora zaidi kuliko vyuo vingine(ni uongo mkubwa kabisa).
 
kila mwaka napokea wanafunzi kutoka hivi vyuo vya afya nchini tanzania na nje ya nchi kwa taasisi fulani hapa nchini

Huwa naona uwezo wa wanafunzi hawa vizuri sana lakini huwa sioni utofauti kabisa unaozushwa kuwa wanafunzi wa muhas wanakuwa bora zaidi kuliko vyuo vingine(ni uongo mkubwa kabisa).
Kwenye hiyo organization ww ni mtaalam wa nn?.
 
Back
Top Bottom