GPA ya 5 - Anazurura mtaani; we are not serious!

GPA ya 5 - Anazurura mtaani; we are not serious!

Kifupi mleta mada mumbeya tu hajaitaja hiyo GPA ni ya course gani na chuo gani

Nafikiriataluwa wale mafailure vyuoni wenye GPA ya chini akijifariji

Kwenye maisha penda ku perform vizuri popote unapokuwa iwe shuleni chuoni,kazini ,nyumbani nk kama uwezo unao

Kupata GPA ya chini sio sifa .Unatakiwa kila unapopita uache mark ya highest performance
Wewe ulipata GPA ya ngapi, mwaka gani, kwa kozi ipi, na kwa chuo kipi?!
 
Mzee hii nchi kuna vichwa aisee labda kama hujakutana navyo tu, mimi sikuamini mpaka nilivyokutana na mwanafunzi ana A zote mwaka wa kwanza na wa pili!, (sasa hivi yupo mwaka wa tatu kozi ngumu tena sayansi!) asipoyumba mwaka huu wa mwisho lazima awe overall
Anasoma kozi ipi na chuo gani?
 
[emoji23][emoji23][emoji23]umenikumbusha mbali kipindi na mimi nimemaliza chuo nahustle hakuna aliekua na time na mimi,wote wenye uwezo wananicheki tu waone nitaishia wapi,wengine wananisikitikia eti kasoma lakini hana kazi,anadhurura mtaani,elimu haijamsaidia

Nimekuja kulamba shavu kwa juhudi zangu,mambo safi sasa naanza ona simu simu,mara naitwa kijana wetu,mara kaka.

Walikua na vijigari vyao,wamejenga vijumba wanajidai dai,nimewalipa mara mbili.

Binadamu ni wanafiki,nimechinjia wote baharini,wanabaki wanasema tu.ooh eti ninadharau [emoji23]

Ulikua huna time na mimi,na mimi sina time na wewe

Sitakagi ujinga
Aisee action uliyoichukua imeni inspire sana. Yaani watu wana nafasi za kukusaidia, na huku wanakuona unavyosota.
Mbaya zaidi wanakusanifu na kukukejeli tu wakikuita majina ya dhihaka. Inauma mno, nayajua maumivu yake, usiombe!

Sikushauri uwasamehe, hata hicho unachowafanyia sasa ni chema tu. Ila usilipize kwa watu wengine wasiohusika katika kukudharau na kukufungia vioo ulipokuwa unasota!
 
Kwa mtazamo wangu tumechelewa kujua umuhimu wa pass za juu katika kupaisha Taifa kiuchumi nk

Hivi inakuwaje mwanafunzi amemaliza Chuo amepata GPA ya 4.8 au kwa wenzetu wa Arts wanapata hadi GPA 5 naye yupo mtaani hana ajira?
GPA sio kipimo halali cha kupima skills au uwezo wa muhitimu wa chuo, siku hizi wanakariri vitini hvyo skills ya kufanya mambo makubwa hawana... vyeti vimebaki serikalini, huku mashirika binafsi skills katika fani flani ndio kila kitu.
 
Nafahamu!
But GPA ya 5! Yaani kwamba tangu anaanza mwaka wa Kwanza Hadi anamaliza chuo mwaka wa tatu au wa nne, alikuwa akipata [emoji817]% Kwa masomo yake yote?

Au ni wale ukipata "A" iwe ya 80 au 90 basi hiyo ni GPA ya Tano?

I wonder!
Unadhani chuo chetu pale Msamvu wana nongwa?
 
Hapana Economics and statistics na pure economics isiyo na statistics
Yaani hata kuajiriwa kama tutorial assistants kwenye vyuo walivyotoka imeshindikana!?!
B.o.T na Big 4, Delloitte, PwC, E&Y, KPMG hawajawachukua Sawa. Ila vyuo walivyotoka wamewakataa!?

Kutakuwa na attitude issue. Ama wanachagua kazi ama wana gundu!
 
Aisee action uliyoichukua imeni inspire sana. Yaani watu wana nafasi za kukusaidia, na huku wanakuona unavyosota.
Mbaya zaidi wanakusanifu na kukukejeli tu wakikuita majina ya dhihaka. Inauma mno, nayajua maumivu yake, usiombe!

Sikushauri uwasamehe, hata hicho unachowafanyia sasa ni chema tu. Ila usilipize kwa watu wengine wasiohusika katika kukudharau na kukufungia vioo ulipokuwa unasota!
Maumivu yalikua makali, usipime 😆😃😀
 
Tulichelew kujua kwamba elimu ya darasani imekuwa Haina msaada nje ya kuta nne za darasa Mana wengi tulikuwa pale kupigania alama ili zitulinde kupata kazi.
Maisha yanatupa jaribio then mafunzo hufuata ila shule ikageuza nakutupa funzo jaribio baadae.

Scholastic education imefunga akili za wengi kwa kuish "Soma uajiliwe"
 
Kwa mtazamo wangu tumechelewa kujua umuhimu wa pass za juu katika kupaisha Taifa kiuchumi nk

Hivi inakuwaje mwanafunzi amemaliza Chuo amepata GPA ya 4.8 au kwa wenzetu wa Arts wanapata hadi GPA 5 naye yupo mtaani hana ajira?
GPA ya 5 kutoka chuo gani? Isije kuwa kama wale wa St. Joseph walikuja na GPA za 4.5-5 kufika SUA hata 3.5 ikawa mbinde.
 
Mtoa mada buana!mtaani na maofisin hatuishi kwa GPA,Mimi Nina GPA ya 2.1 lakini pengo langu hakuna wa kuliziba ofisini kwetu ingawa wapo wenye hizo GPA za 4s.
Kufa uone. Pengo lako huwezi kuona km hakuna w kuliziba kisa upo, toka uje uone litakavozibika.
 
Hizi elimu zetu zinatuandaa kuwa wafanya kazi tu. Na si vinginevyo.
In this era University Education is a scam
 
Back
Top Bottom