GPA ya 5 - Anazurura mtaani; we are not serious!

GPA ya 5 - Anazurura mtaani; we are not serious!

Kupata A no kawaida ndugu,, hata Mimi nilipata pia. Lakini GPA ya 5? Do you know what it means?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Yes, upate A kwenye masomo yako yote, na sio kama haiwezekani sema hutokea kwa baadhi kuyumba kwenye baadhi ya masomo na ndio inapelekea mtu kupata B+ kadhaa anajikuta ana 4.8
 
Mtoa mada buana!mtaani na maofisin hatuishi kwa GPA,Mimi Nina GPA ya 2.1 lakini pengo langu hakuna wa kuliziba ofisini kwetu ingawa wapo wenye hizo GPA za 4s.
Duh, hahahaha kama naziona karai zilivyopamba cheti chako hahahaha

Ilikua kidogo ulingane na JK [emoji12]
 
Kwenye hivyo vyuo vya hovyo tu. Niliwahi ona tangazo la kazi likisema wote wenye sifa wanaweza kuomba kazi hiyo isipokuwa wahitimu wa UDOM!

Nilitafakari sana

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Unaweza kutuwekea tangazo ili nasi tukajifunze kitu na wakati mwingine itusaidie kwenye kuchagua vyuo ambavyo ni bora,otherwise utakuwa ni uchochezi either ulidisco kwenye hiko chuo ama ulikosa kazi
 
Yes, upate A kwenye masomo yako yote, na sio kama haiwezekani sema hutokea kwa baadhi kuyumba kwenye baadhi ya masomo na ndio inapelekea mtu kupata B+ kadhaa anajikuta ana 4.8

Hata ukipata A zote hupati Gpa ya 5. Maana A zinapishana maksi. A ya 81 sio sawa na A ya 90 ama A ya 100 kwenye gpa
 
Kifupi mleta mada mumbeya tu hajaitaja hiyo GPA ni ya course gani na chuo gani

Nafikiriataluwa wale mafailure vyuoni wenye GPA ya chini akijifariji

Kwenye maisha penda ku perform vizuri popote unapokuwa iwe shuleni chuoni,kazini ,nyumbani nk kama uwezo unao

Kupata GPA ya chini sio sifa .Unatakiwa kila unapopita uache mark ya highest performance
Tatizo Kuna misemo ya kumotivate watu Ujinga kule kwenye mtandao wa majiniaz

Sent from my VTR-L29 using JamiiForums mobile app
 
GPA na kuyamudu maisha kitaa ni vitu viwili tofauti,Std seven anayamudu maisha,anakula vizuri,analala pazuri na hana GPA,maisha hayana formula
Uhusiano upo. Chukua Std Seven wa sasa na Graduate wa sasa
 
Mzee hii nchi kuna vichwa aisee labda kama hujakutana navyo tu, mimi sikuamini mpaka nilivyokutana na mwanafunzi ana A zote mwaka wa kwanza na wa pili!, (sasa hivi yupo mwaka wa tatu kozi ngumu tena sayansi!) asipoyumba mwaka huu wa mwisho lazima awe overall
Yupo Chuo gani??.
 
SUA Mwenye , 75 au na 80 hawa ni watu wawili tofauti japokuwa inaonekana kam ni A lakini cheki GPA utastuka . Inaweza mwengine akawa na plus nyingi akaingizaA mbili za maana ww mwenye A nyingi lakin ndogo unapitwa[emoji23] unaweza dhani wamempendelea ila sio
Upo sahihi Mkuu
 
Umepita hapo SUA? Mbona mnaongea vitu havipo? Ni kweli BVM Iko unclassified, lakini waliobaki GPA inatafutwa Kwa raw marks siyo Mambo ya kuangalia A ngapi, B ngapi and so on!

Uko na A za 80, Mimi Niko na A za 81 GPA lazima itofautiane! Ndiyo maana tunahoji GPA ya 5 mnazipataje huko kwenu?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Mchango ule ulisema "sua ni marks tu". Hivi kwenye matokeo na transcript wanatoa marks? Naamini wanatoa grade. Kwenye Gpa calculatiòn ndio wanatumia formular ambayo inaendana
na grade yako. Hivyo mwenýe A na mwenye B wana formular tofauti. Marks ndio zinakuwa fed kwenye formular husika
Sasa kama degree inakuwa unclassified, wataangalia merits zipi mtu akitaka kwenda elimu ya juu?
Kwa SUA wanatumia vitu viwili your average score raw marks and your grade in the course or courses unayotaka kusoma.
 
[emoji23][emoji23][emoji23]umenikumbusha mbali kipindi na mimi nimemaliza chuo nahustle hakuna aliekua na time na mimi,wote wenye uwezo wananicheki tu waone nitaishia wapi,wengine wananisikitikia eti kasoma lakini hana kazi,anadhurura mtaani,elimu haijamsaidia

Nimekuja kulamba shavu kwa juhudi zangu,mambo safi sasa naanza ona simu simu,mara naitwa kijana wetu,mara kaka.

Walikua na vijigari vyao,wamejenga vijumba wanajidai dai,nimewalipa mara mbili.

Binadamu ni wanafiki,nimechinjia wote baharini,wanabaki wanasema tu.ooh eti ninadharau [emoji23]

Ulikua huna time na mimi,na mimi sina time na wewe

Sitakagi ujinga
Una roho mbaya mno. Samehe!
 
We sisi 2009-2012 tulisoma na mdada flani uchumi alikuwa ni kichwa balaa.
Kuna tutorial flani hadi alipokuwa akiingia darasani anakuwa hayuko na confidence maana dada alikuwa akitufundisha anamlima maswali sometimes kama anamsahisha.
Dada yani alikuwa pointed out na taasisi kubwa ya serikali hata kabla hatujamaliza.
Kuna jamaa mwingine naye alikuwa anapata alama za juu alichukuliwa na TBL mapema sana, sema jamaa kwenye presentation na kumwaga english ya kuzungumza alikuwa 0 kabisa.
Ila kwenye makaratasi alikuwa anatukimbiza balaa.
Hao wote walisoma kozi gani? Law? Nina maana kubwa, nijibu nakusihi.
 
Back
Top Bottom