Green Card kumbe ni kweli aisee tucheze hii kitu

Be careful na hiyo link yako, isije mbele ya safari wakakutaka pesa ya hiki wanachosema "use our service if you need any help with the application process." Hapo wanatafuta kupiga watu tu kwa sababu Link sahihi ni ; kama unavyoona hapo, ina kikoi cha .gov kwa sababu inaendeshwa na serikali. Na kwa mwaka huu bado haijaanza, ingawaje link uliyotoa inasema deadline ni October 15. Kwa kawaida, hii lottery huwa inaanza October na kufungwa November. Na kujaza ni rahisi sana, wala mtu hana sababu ya kutaka msaada ili mradi ana picha inayokidhi vigezo vyao!
 
Ahsante
 
Kabla ya kupiga marufuku tujiulize je hzo bidhaa zna ubora kama hzo za China?? Na vp kuhusu bei? Afu unawezaje kumpiga stop boss wako assiingize mzigo akat unamtegemea yy akukopeshe hela, akuletee technology,,n.k
Ndio tuumize vichwa, cha msingi furniture za China zipigwe kodi nzito hadi waione hii nchi chungu, angalau mafundi seremali mitaani watapata nafuu, hali si hali, waChina wanaua kila kitu huku mtaani, si mafundi seremala si nani...
 
Kama suala ni ajira, ni simple tu, piga marufuku bidhaa za China zinazoweza kuzalishwa Tanzania, mfano furniture, hicho kipengele kimoja tu, kitazalisha ajira kwa maelfu kwa maelfu ya vijana

Sasa mkuu hapo umetaja ajira kwa kada za ufundi/mafundi, lakini mathalani kwa watu ambao ni madaktari, wauguzi, wahandisi au hata wasanii n.k...

Ukipata shavu zuri U.S, umasikini ndio kwaheri hivyo (kuna sababu kwa nini imekuwa ikijulikana kama ni the land of opportunity a.k.a american dream)
 
NI mwehu ndie ataenda na familia kwa mara ya kwanza!!! Hiyo Dar es salaam yenyewe tunaona watu wanatoka mkoa wanaingia Dar wakiwa peke yao, na mambo yakiwaendea vizuri ndipo wanafuata familia!!
nakubaliana..
 
Umekurupuka na uzi wako utafikiri watanzania wote milioni 50 wanaijua hiyo green kadi yako.Ni kitu gani hicho?,kadi ya uanachama wa ccm?
 
Kabla ya kupiga marufuku tujiulize je hzo bidhaa zna ubora kama hzo za China?? Na vp kuhusu bei? Afu unawezaje kumpiga stop boss wako assiingize mzigo akat unamtegemea yy akukopeshe hela, akuletee technology,,n.k

Huyo jamaa labda anataka tuishi kama korea ya kaskazini
 
Mbona naambia information entered is invalid,,,Kwan initial stage ni ipi!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…