Gwajima: Taifa tumekosa maono, inakuwaje kujenga reli kabla ya kuchimba chuma? Waziri Mwigulu ampinga

Gwajima: Taifa tumekosa maono, inakuwaje kujenga reli kabla ya kuchimba chuma? Waziri Mwigulu ampinga

Gwajima yupo sahihi. Ni kazi sana kwa nchi kuendelea bila chuma. Ukiwa na chuma utajenga reli kwa bei rahisi, utajenga nyingi, utajenga mabehewa. Na itakuwa rahisi kwako kurekebisha. Hao wakina Mwigulu wamekalia porojo za LNG utafikiri ni mtambo wetu!!
Bidhaa nyingi zinazozalishwa nchini sasa hivi ziko out of reach or means kwa wananchi wenzetu because of prices? ukiwauliza manufacturers wanalalmika taxes?
hizo chuma zingetolewa bure?
 
Bidhaa nyingi zinazozalishwa nchini sasa hivi ziko out of reach or means kwa wananchi wenzetu because of prices? ukiwauliza manufacturers wanalalmika taxes?
hizo chuma zingetolewa bure?
Sasa kama mashine zote na spares zote zinatoka nje unategemea nini kwa bidhaa zake. Na kwanini hatuzalishi hizo mashine humu? Hatuna chuma. Hakuna aliyesema kitatolewa bure.
 
Wewe ni mshamba ndio maana hujaona logic ya Gwajima. Ni sawa na kutoa tenda ya kusambaza vyakula mashuleni ila kampuni hiyo ikawa inanunua mahindi Kenya wakati hapa nchini yapo tungekuwa na mashine tungesaga.

Hivyo vyuma kama sikosei wanachukua zaidi Urusi kuja kujengea reli. Kuna ugumu gani kwenye teknolojia ya steel mpaka tuagize nje kwa kutumia billions of money? Tungekuwa na uzalishaji wa kujitosheleza tungetumia chuma chetu kutoka Mchuchuma & Liganga na kuzalisha ajira, kupunguza importation, kuongeza capacity ya uzalishaji na hatimaye kuuza nje, na huo mradi wa chuma ungerahisisha ujenzi wa viwanda.

Yani vyuma tumevilalia ardhini alafu unakuja na hoja za kishamba eti "comparative advantage". Hakuna nchi inaweza endelea bila kuwa na chuma, ambao hawana iron ore kama South Korea na Japan wanazalisha ila sisi tumelala na wala sio teknolojia ya nishati wala kompyuta kusema ni ngumu
Ok tuseme ana hoja kwanini iwe chuma tu? Pamba, dhahabu, almasi, Tanzanite, korosho na mengine mengi tu kwanini tusiwe na viwanda vyetu tuuze product sio raw materials. Kwani ukiwa na chuma ndio utajenda reli. Hapa tuna mbao kibao lakini furniture tunanunua toka nje kwanini? Kuuza raw materials haikufanyi kuuza bidhaa bora hatuna uwezo huo vibiriti vyetu mpaka kiwake umemaliza njiti 30. Nakubaliana na yeye kama nchi ni lazima tuwe na vision, tunataka kuwa nini wauzaji au watengenezaji.
 
Sasa kama mashine zote na spares zote zinatoka nje unategemea nini kwa bidhaa zake. Na kwanini hatuzalishi hizo mashine humu? Hatuna chuma. Hakuna aliyesema kitatolewa bure.
na wale watakao zalisha hizo machine au parts watapunguza bei zakuuza? logic here ni the tax structures are to high??
 
Mbunge wa Kawe akiwa bungeni, Joseph Gwajima amesema kwa miaka mitano Taifa limelipa fedha za kigeni dola za kimarekani bilioni 2.2, Gwajima amesema kwa mtu yoyote mwenye akili na anajua kuzitumia jambo hili hawezi kuruhusu kufanyika.

Gwajima amesema nchi imeanza na reli ambayo hayupo kinyume nayo lakini ameshangaa kuanza na reli ambayo 'component' kubwa ni chuma kwa kukiagiza nje ya nchi badala ya kuchimba chuma kisha kujenga reli.

Gwajima amesema kinachosumbua ni kukosa maono ya Taifa, mipango ya Taifa na dira.

Gwajima amesema Taifa linahitaji maono ya pamoja na hakuna nchi duniani iliyoendelea kwa miaka mitano au kumi.

Kingu-Taarifa
Kingu akichangia kupitia taarifa, amesema hadi tume ya kutengeneza mipango ya muda mrefu imefutwa. Amesema Taifa halina tume ya mipango kuanzia miaka 50.

Mwigulu akanusha
Waziri wa fedha, Mwigulu Nchemba amekanusha na kusema Taifa lina mipango ya muda mrefu na tangu uhuru limeongozwa na viongozi wenye maono na ndio maana kuna dira ya 2025 kutoka kwa Mkapa.

Mwigulu amesema nchi imeongozwa kwa maono ndio maana ipo ilipo. Mwigulu amemaliza kwa kusema Rais ameshaweka utekelezaji wa miradi mikubwa, yote inaenda kutekelezwa ya Liganga, LNG.
Sasa Mwigulu hiyo vision 2025 ndio mpango wa muda mrefu? Unajua tofauti ya short na long term Plans? Miaka 25 huwezi kuita long term ni makosa! Projections za miaka angalau 50 ijayo would suffice. Inakupa maono ya jinsi mnavyotegemea nchi iwe!
 
na wale watakao zalisha hizo machine au parts watapunguza bei zakuuza? logic here ni the tax structures are to high??
Hujui kuwa kitu kinachoagizwa na kinachozalishwa ndani kodi zao ni tofautu kabisa?
 
Watu wanamjibu Gwaji boy personal,,, ila hawajibu hoja zake...

But Gwajima ana point nzuri sana,, ni kukaa na kuiweka sawa tu... na Viongozi hawaipendi kwasababu wanaona itawabana...
 
Kama chuma kinapatikana, uzalishaji unaanza halafu kwenye tenda kunawekwa kipengele cha kutumia chuma kutoka ndani ya nchi.
Kwa maneno mengine gharama inapungua, pia biashara na ajira vinaongezeka.
Mbona sukari ya ndani ina bei kuliko na nje? hatujiulizi kwanini? nchi hii inashida kwenye mifumo ya tax sio attractive nchi inatoza kodi kubwa sana haivutii ni rahisi kuwa na kiwanda china kuliko hapa ndio maana unakuta bidhaa za ndani zinabei kuliko za nje pamoja na ushuru. Nchi ina cheap labour lakini kwanini viwanda vinashindwa kushindana mp
 
Wewe ni mshamba ndio maana hujaona logic ya Gwajima. Ni sawa na kutoa tenda ya kusambaza vyakula mashuleni ila kampuni hiyo ikawa inanunua mahindi Kenya wakati hapa nchini yapo tungekuwa na mashine tungesaga.

Hivyo vyuma kama sikosei wanachukua zaidi Urusi kuja kujengea reli. Kuna ugumu gani kwenye teknolojia ya steel mpaka tuagize nje kwa kutumia billions of money? Tungekuwa na uzalishaji wa kujitosheleza tungetumia chuma chetu kutoka Mchuchuma & Liganga na kuzalisha ajira, kupunguza importation, kuongeza capacity ya uzalishaji na hatimaye kuuza nje, na huo mradi wa chuma ungerahisisha ujenzi wa viwanda.

Yani vyuma tumevilalia ardhini alafu unakuja na hoja za kishamba eti "comparative advantage". Hakuna nchi inaweza endelea bila kuwa na chuma, ambao hawana iron ore kama South Korea na Japan wanazalisha ila sisi tumelala na wala sio teknolojia ya nishati wala kompyuta kusema ni ngumu

Kuna mambo ni magumu kufanyia uamuzi bila ku-dig deeper..., na katika hili suala tuakiacha Siasa kuna ingredients mbili za muhimu za kufahamu...

Je Production cost ya Tani moja ya Chuma mpaka inakuwa tayari ni kiasi gani ?
Je Tani hio ikinunuliwa inaponunuliwa mpaka kuletwa hapa ni kiasi gani ?
Je uchimbaji na utayarishaji wa hicho chuma hapa mpaka kinaenda sokoni kitaleta faida ya kiasi gani kama tukiuza bei sawa na washindani wetu ?

Hapo ndio naweza kuchangia vizuri nini kifanyike nikipata hizo data....

Nadhani ni vema kumalizia na Msemo wa Adam Smith

It is the maxim of a every prudent master of a family, never to attempt to make at home what it will cost him more to make than to buy.
 
Gwajima yupo sahihi. Ni kazi sana kwa nchi kuendelea bila chuma. Ukiwa na chuma utajenga reli kwa bei rahisi, utajenga nyingi, utajenga mabehewa. Na itakuwa rahisi kwako kurekebisha. Hao wakina Mwigulu wamekalia porojo za LNG utafikiri ni mtambo wetu!!
Hayuko sahihi. Nikueleze kwa kirefu kidogo. Kwanza nchi kuwa na madini ya chuma ni kitu kimoja na kuyachimba na,kuyabadilisha kuwa aina,kadhaa za chuma ni suala,lingine linalotegemea kiwango cha teknolojia nchi ilichonacho. Hicho kinachoitwa chuma kitaslam kinaitwa iron ore, ambapo ukishachimba unayeyusha na kupata pig iron, baada ya hapo kama una teknolojia unaweza kutengeneza aina kadhaa za steel na alloys zake. Sio kuwa maadam ni chuma basi unajengea tu reli au na mabehewa. Pili bidhaa kuzalishwa ndani ya nchi sio factor ya kufanya bidhaa hiyo iwe cheap; kuna bidhaa zinatoka Kenya kuletwa Tanzania lakini zinauzwa rahisi kuliko bidhaa hizo hizo zinazozalishwa Tanzania.

Nchi kama Korea na Japan ni watengenezaji wakubwa duniani wa meli, mabehewa na bidhaa zingine za vyuma lakini kwao hakichimbwi chuma. Switzerland wanatengeneza best chocolate lakini hawalimi cocoa. Ili nchi izalishe bidhaa bora lazima iwe na teknolojia yake sio kuzalisha kitu under licence au kujenga kiwanda cha kuunganisha bidhaa mfano magari au mgeni toka nje anajenga kiwanda ambacho kinazalisha hatua fulani ya bidhaa kisha nchi inatamba kuwa ina viwanda. Huwa nawauliza watu kuwa kuna,mtu mweusi anajua kugeuza,mchanga/udongo kuwa machine?
Pia nchi inaweza kuzalisha bidhaa lakini isiwe na comparative advantage hivyo bidhaa hiyo inaweza isiweze kushindana hata katika soko lake la ndani na bidhaa toka nje.

Sio lazima materials yatoke ndani ya nchi, mradi unapofanywa kuna manufaa ya,moja kwa moja kama vibarua na yasio ya,moja kwa moja kama supply ya vyakula na vitu vingine hivyo kuchochea ukuaji wa shughuli za,kiuchumi kutokana,na mradi huo mmoja tu.

Hicho chuma hata kikichimbwa bado ni iron ore tu inaweza kuwa aina ya chuma kinachohitajija kwa ujenzi wa reli ni lazima kiwe kimetengenezwa hatua kadhaa za process eg stainless steel, cast iron nk.kila mkataba unapofungwa kinachotakiwa ni quality output hivyo huwezi kulazimisha materials ya kazi yatoke nchini kwako, na hata yakitoka nchini kwako materials hayo yanauzwa kwa,bei ya soko hayatolewi bure kwa sababu kampuni inayozalisha hicho chuma inauza kwa faida na bei yake inaweza ikawa iko juu na kampuni inayojenga reli ni nyingine hivyo hizi ni kampuni mbili tofauti hivyo hazina uhusiano wa baba na mtoto.

Uchumi uko complex sio kama baadhi ya watu waanavyodhani.
 
Mawazo ya Gwajima ni potofu na ya unafiki. Kiuchumi sio lazima nchi iwe na chuma ndio ijenge reli wala hata kama ina chuma sio lazima kwanza kuchimba chuma ndipo nchi ijenge reli. Kila ntu sasa anajifanya mchumi!.
Ziko nchi nyingi tu zimejenga reli na hazina hicho chuma.

Unapotaka kujenga reli unatangaza tenda baada ya kuwa umefanya tathmini reli itajengwa vipi na costs ni kiasi gani. Mkandarasi akishapatikana ndiye anajua vyuma atanunua wapi na kwa bei gani; sisi tunachotaka tukabidhiwe reli iliyojengwa kwa viwango na kwa wakati.

Hicho chuma ikitokea kimechimbwa siku moja kitauzwa kwa wateja wanaohitaji wa nje na ndani ya nchi na kitaingiza mapato ya fexha za kigeni na pia shilingi.

Hakuna nchi inazalisha kila kitu yenyewe na sio lazima kiuchumi tuzalishe kila kitu, vingine tutaagiza tupende tusipende; ndio maana kuna kitu kinaitwa comparative advantage katika biashara ya kimataifa sio suala la kuzalisha tu
Upo off point na Mbunge, either hujamwelewa kabisa!! Yeye anachojaribu kusema ni kuwa shambani kwetu tayari Kuna nyanya na zinaweza kuvunwa na kuivishwa, hivyo katika kupika chakula inatakiwa ujitahidi utumie nyanya zako ulizovuna shambani!! Sasa swali lake ni iweje tukimbilie kununua nyanya Kwa jirani ilihali za kwetu zingeiva na kutumika kupunguza hasara hii kubwa ya manunuzi!? Tena Kwa Dola kutoka nje!!
 
Mbunge wa Kawe akiwa bungeni, Joseph Gwajima amesema kwa miaka mitano Taifa limelipa fedha za kigeni dola za kimarekani bilioni 2.2, Gwajima amesema kwa mtu yoyote mwenye akili na anajua kuzitumia jambo hili hawezi kuruhusu kufanyika.

Gwajima amesema nchi imeanza na reli ambayo hayupo kinyume nayo lakini ameshangaa kuanza na reli ambayo 'component' kubwa ni chuma kwa kukiagiza nje ya nchi badala ya kuchimba chuma kisha kujenga reli.

Gwajima amesema kinachosumbua ni kukosa maono ya Taifa, mipango ya Taifa na dira.

Gwajima amesema Taifa linahitaji maono ya pamoja na hakuna nchi duniani iliyoendelea kwa miaka mitano au kumi.

Kingu-Taarifa
Kingu akichangia kupitia taarifa, amesema hadi tume ya kutengeneza mipango ya muda mrefu imefutwa. Amesema Taifa halina tume ya mipango kuanzia miaka 50.

Mwigulu akanusha
Waziri wa fedha, Mwigulu Nchemba amekanusha na kusema Taifa lina mipango ya muda mrefu na tangu uhuru limeongozwa na viongozi wenye maono na ndio maana kuna dira ya 2025 kutoka kwa Mkapa.

Mwigulu amesema nchi imeongozwa kwa maono ndio maana ipo ilipo. Mwigulu amemaliza kwa kusema Rais ameshaweka utekelezaji wa miradi mikubwa, yote inaenda kutekelezwa ya Liganga, LNG.
Hili suala amewahi kuongea ZZK kitambo kidogo. Sijui kama kuna watu walimueleawa. Yaani chuma kwanza, reli ndo ifuate.
 
Mimi nimejibu kama mchumi tena professsional yeye amezungumza kama layman asiyeelewa abc za uchumi
Upo off point na Mbunge, either hujamwelewa kabisa!! Yeye anachojaribu kusema ni kuwa shambani kwetu tayari Kuna nyanya na zinaweza kuvunwa na kuivishwa, hivyo katika kupika chakula inatakiwa ujitahidi utumie nyanya zako ulizovuna shambani!! Sasa swali lake ni iweje tukimbilie kununua nyanya Kwa jirani ilihali za kwetu zingeiva na kutumika kupunguza hasara hii kubwa ya manunuzi!? Tena Kwa Dola kutoka nje!!

Upo off point na Mbunge, either hujamwelewa kabisa!! Yeye anachojaribu kusema ni kuwa shambani kwetu tayari Kuna nyanya na zinaweza kuvunwa na kuivishwa, hivyo katika kupika chakula inatakiwa ujitahidi utumie nyanya zako ulizovuna shambani!! Sasa swali lake ni iweje tukimbilie kununua nyanya Kwa jirani ilihali za kwetu zingeiva na kutumika kupunguza hasara hii kubwa ya manunuzi!? Tena Kwa Dola kutoka nje!!
Mimi nimechangia kama,mchumi yeye amazungumza kama layman .
 
Hayuko sahihi. Nikueleze kwa kirefu kidogo. Kwanza nchi kuwa na madini ya chuma ni kitu kimoja na kuyachimba na,kuyabadilisha kuwa aina,kadhaa za chuma ni suala,lingine linalotegemea kiwango cha teknolojia nchi ilichonacho. Hicho kinachoitwa chuma kitaslam kinaitwa iron ore, ambapo ukishachimba unayeyusha na kupata pig iron, baada ya hapo kama una teknolojia unaweza kutengeneza aina kadhaa za steel na alloys zake. Sio kuwa maadam ni chuma basi unajengea tu reli au na mabehewa. Pili bidhaa kuzalishwa ndani ya nchi sio factor ya kufanya bidhaa hiyo iwe cheap; kuna bidhaa zinatoka Kenya kuletwa Tanzania lakini zinauzwa rahisi kuliko bidhaa hizo hizo zinazozalishwa Tanzania.

Nchi kama Korea na Japan ni watengenezaji wakubwa duniani wa meli, mabehewa na bidhaa zingine za vyuma lakini kwao hakichimbwi chuma. Switzerland wanatengeneza best chocolate lakini hawalimi cocoa. Ili nchi izalishe bidhaa bora lazima iwe na teknolojia yake sio kuzalisha kitu under licence au kujenga kiwanda cha kuunganisha bidhaa mfano magari au mgeni toka nje anajenga kiwanda ambacho kinazalisha hatua fulani ya bidhaa kisha nchi inatamba kuwa ina viwanda. Huwa nawauliza watu kuwa kuna,mtu mweusi anajua kugeuza,mchanga/udongo kuwa machine?
Pia nchi inaweza kuzalisha bidhaa lakini isiwe na comparative advantage hivyo bidhaa hiyo inaweza isiweze kushindana hata katika soko lake la ndani na bidhaa toka nje.

Sio lazima materials yatoke ndani ya nchi, mradi unapofanywa kuna manufaa ya,moja kwa moja kama vibarua na yasio ya,moja kwa moja kama supply ya vyakula na vitu vingine hivyo kuchochea ukuaji wa shughuli za,kiuchumi kutokana,na mradi huo mmoja tu.

Hicho chuma hata kikichimbwa bado ni iron ore tu inaweza kuwa aina ya chuma kinachohitajija kwa ujenzi wa reli ni lazima kiwe kimetengenezwa hatua kadhaa za process eg stainless steel, cast iron nk.kila mkataba unapofungwa kinachotakiwa ni quality output hivyo huwezi kulazimisha materials ya kazi yatoke nchini kwako, na hata yakitoka nchini kwako materials hayo yanauzwa kwa,bei ya soko hayatolewi bure kwa sababu kampuni inayozalisha hicho chuma inauza kwa faida na bei yake inaweza ikawa iko juu na kampuni inayojenga reli ni nyingine hivyo hizi ni kampuni mbili tofauti hivyo hazina uhusiano wa baba na mtoto.

Uchumi uko complex sio kama baadhi ya watu waanavyodhani.
Hii habari ya comparative advantage ipo kumfanya mzalisha raw materials aendelee hivyo maisha yote, na anaetumia materal hayo kuzalisha bidhaa ghali aendelee hivyo. Ina usanii ndani yake. Ghana wamekuwa na mpango wa kuzalisha chokleti nchini mwao. Viwanda kadhaa vimeshaanzishwa na vinafanya kazi. Leo kwa kiasi Tz tunaweza safisha dhahabu, zamani walisema, kama wewe, "Mtu mweusi hawezi." Hao unasema hawachimbi chuma ila wanazalisha meli unawaangalia leo, huko nyuma walinunua iron ore kila kona na kufua chuma. Chuma ndiyo msingi wa viwanda.

Ukiweka factor za uzalishaji sawa, bidhaa za ndani zinakuwa na bei ya chini kuliko za nje. Na wenzetu wakati wanakua walizilinda bidhaa zao za ndani hata dhidi ya za bei ya chini kutoka nje.
Ipo hivi, ingefaa sana tujitosheleze kwa chuma. Ingefaa sana reli yetu tungejenga kwa chuma chetu.
 
Hayuko sahihi. Nikueleze kwa kirefu kidogo. Kwanza nchi kuwa na madini ya chuma ni kitu kimoja na kuyachimba na,kuyabadilisha kuwa aina,kadhaa za chuma ni suala,lingine linalotegemea kiwango cha teknolojia nchi ilichonacho. Hicho kinachoitwa chuma kitaslam kinaitwa iron ore, ambapo ukishachimba unayeyusha na kupata pig iron, baada ya hapo kama una teknolojia unaweza kutengeneza aina kadhaa za steel na alloys zake. Sio kuwa maadam ni chuma basi unajengea tu reli au na mabehewa. Pili bidhaa kuzalishwa ndani ya nchi sio factor ya kufanya bidhaa hiyo iwe cheap; kuna bidhaa zinatoka Kenya kuletwa Tanzania lakini zinauzwa rahisi kuliko bidhaa hizo hizo zinazozalishwa Tanzania.

Nchi kama Korea na Japan ni watengenezaji wakubwa duniani wa meli, mabehewa na bidhaa zingine za vyuma lakini kwao hakichimbwi chuma. Switzerland wanatengeneza best chocolate lakini hawalimi cocoa. Ili nchi izalishe bidhaa bora lazima iwe na teknolojia yake sio kuzalisha kitu under licence au kujenga kiwanda cha kuunganisha bidhaa mfano magari au mgeni toka nje anajenga kiwanda ambacho kinazalisha hatua fulani ya bidhaa kisha nchi inatamba kuwa ina viwanda. Huwa nawauliza watu kuwa kuna,mtu mweusi anajua kugeuza,mchanga/udongo kuwa machine?
Pia nchi inaweza kuzalisha bidhaa lakini isiwe na comparative advantage hivyo bidhaa hiyo inaweza isiweze kushindana hata katika soko lake la ndani na bidhaa toka nje.

Sio lazima materials yatoke ndani ya nchi, mradi unapofanywa kuna manufaa ya,moja kwa moja kama vibarua na yasio ya,moja kwa moja kama supply ya vyakula na vitu vingine hivyo kuchochea ukuaji wa shughuli za,kiuchumi kutokana,na mradi huo mmoja tu.

Hicho chuma hata kikichimbwa bado ni iron ore tu inaweza kuwa aina ya chuma kinachohitajija kwa ujenzi wa reli ni lazima kiwe kimetengenezwa hatua kadhaa za process eg stainless steel, cast iron nk.kila mkataba unapofungwa kinachotakiwa ni quality output hivyo huwezi kulazimisha materials ya kazi yatoke nchini kwako, na hata yakitoka nchini kwako materials hayo yanauzwa kwa,bei ya soko hayatolewi bure kwa sababu kampuni inayozalisha hicho chuma inauza kwa faida na bei yake inaweza ikawa iko juu na kampuni inayojenga reli ni nyingine hivyo hizi ni kampuni mbili tofauti hivyo hazina uhusiano wa baba na mtoto.

Uchumi uko complex sio kama baadhi ya watu waanavyodhani.
Unapoandika mambo mengi, inaonyesha fika umeelimika, je huoni umuhimu wa wewe kushauri kuendeleza raw material ya ndani uliyonayo na kuzalisha ajira ya kiwanda huku ukiwa tayari na soko la kujiuzia chuma!? Fikiria reli ya tazara, kulikuwa na viwanda kama Mang'ula kule ifakara, huona saving ilikuwa kubwa!! Tunapochambua hoja tuweke na uzalendo Sio story TU!!
 
Back
Top Bottom