Angel Nylon
JF-Expert Member
- Jul 26, 2011
- 9,164
- 18,402
Zaidi ya kazi.Majukum.ya ndoa yanakuzid sijakuon mda
Ila sivundi humu napita pita japo mara moja moja
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Zaidi ya kazi.Majukum.ya ndoa yanakuzid sijakuon mda
WellKESI YA MZEE MNYOKA 16
SAA 9:14 usiku
Oscar akiwa pale juu alimuona Askofu Majimbi na Tito Kimbikile, ilikua Ni ngumu kuendelea kushikilia pale juu, na hivyo aliomba waondoke Haraka pale chini ili aweze kuondoka, aliendelea kushikilia pale huku akiomba Mungu Mlinzi yoyote asipige jicho pale juu,
"Nilishauri tuweke kamera huku chini mkanipinga, oneni Sasa tunavyotolewa jasho"
Alisema Majimbi,
"Acha ubishi Askofu, kumbuka kamera zinatumia mfumo wa komputa kujiendesha, na kama ujuavyo kutokana na teknolojia Sasa hivi mtu anaweza kuingilia mfumo huu na kuona kila kitu, believe me tungekuwa na camera huku chini tusingefik.......
"
Tito alikatishwa maongezi ghafla,
"Mkuu tuondokeni Sasa juu kuko clear"
Alisema Sasa jamaa mwingine ambapo walianza kupanda ngazi kurudi juu huku Tito akisisitiza Bili afanye kazi ya kumkamata huyo mtu kabla ya usiku kwisha,
Oscar Sasa alitambaa taratibu kupanda akiacha hatua kadhaa baina yao,.
Alipita kwenye njia yake ya mwanzo na kutokea kule store Kisha akatoka nje ,
Kwa tahadhari kubwa alitambaa chini kwa chini, huku akizidi kuliacha jengo, na baadae akasimama na kupotelea msituni....
Alifika mafichoni mwake na kuchukua vifaa vyake vyote Kisha akapotea,
"Imeisha hii!"
Oscar alijisemea huku akikiacha Kijiji cha Kinjeki, alifurahi kuona amemaliza kazi yake salama kabisa.
***************
Dokta Kimei alimueleza mama Monica kuwa Mzee Mnyoka alipata mstuko mfadhaiko na akajikuta ametoka nje ya hospitali Ila yupo mahali salama, Mama Monica alilazimisha kumuona mumuwe usiku ule ule, dokta Kimei hakuwa na kipingamizi alienda nae
*************
Dar es salaam
Oscar alifika kwa bosi wake Mr Allan, ambapo alitoa taarifa zote ikiwemo wahusikia aliofanikiwa kuwaona pamoja na ramani ya pale,
"Kazi nzuri Oscar, hatukutegemea ungefanya kwa wepesi kiasi hiki,..
Kwasasa unaweza kwenda kupumzika na wakati wowote kutoka Sasa hivi utakwenda rasmi kwa ajili ya kazi,..
Tunasubiri activation kutoka kwa mkuu, akitoka kwenye mkutano, kwasasa tutakuwa tunaangalia nyendo za Tito, na Majimbi kwa karibu,...
Tunaamini hawawezi kufanya chochote ndani ya muda mfupi, hivyo mheshimiwa akitoka tu kazi itaanza ndani ya siku tatu au nne zijazo,.
Sasa unaweza kwenda"
Mr Allan alimalizia huku akimpa mkono Oscar,
************
Dar es salaam saa 9 alasiri
Oscar alikua nyumbani kwake amejipumzisha wakati alipopigiwa simu hii
"Ndio, nimekuelewa"
Alisema baada ya kuongea kwa dakika kadhaa na upande wa pili ,
Sasa baada ya simu hii alijisikia kuchangamka, mwenyewe alishachoka kukaa kaa tu Bila kazi,
Simu hii aliitegemea , ingawa ni Kama iliwahi hivi, hata hivyo tofauti na matarajio yake mpango kidogo ulibadilika, na Sasa alitakiwa kukutana na Mr Allan, jioni Ile saa moja ili apewe mpango mzima,
Na hatimaye safari hii aliambiwa atafute mwenza katika kazi hii, hivyo alijishauri, na hatimaye akaona amchukue jamaa yake wa siku zote,
Baada ya kuweka vitu vyake sawa Oscar alitoka nje ya nyumba yake Kisha akachukua boda boda,
"Twende mpaka Banana"
Oscar alisema huku akiweka sawa jacket lake...
**********
Kijijini Kinjeki siku hiyo hiyo
Frank aliegesha Gari lake huku akivuta pumzi ndefu,
Hakujua amuambie Nini Mr Bill,
Ni kweli alijitahidi kumuua Mzee Mnyoka Ila Sasa Mzee Alitoweka hospitali, pamoja na kufanya jitihada zake kwa siku mbili hakufanikiwa kumuona,
"Asipoelewa Basi"
Alipiga usukani wa Gari yake Kisha akafungua mlango na kutoka nje,
Alipita vibarua wakiendelea na kazi zao moja kwa moja Hadi kwa Bosi wake,
"Sema, naona unakodoa macho tuu"
Mr Bill aliongea huku akipanga mafaili yake mezani,
"Mkuu, nimemkosa yule Mzee"
Frank aliongea,
"Kwahiyo unataka Sasa nikupigie makofi nikupongeze kwa kumkosa au?"
Mr Bill aliongea kwa jazba,
"Sikiliza nashindwa kuwavumilia, juzi mpuuzi mmoja katuvamia hapa, Tena mbele ya wageni, na ameua Mlinzi mmoja na hajakamatwa, wewe nawe kwenda kumaliza kazi ya dakika mbili tu unanijia hapa baada ya siku 4 Tena ukiwa umeshindwa, task ndogo tu, una akili kweli? Hebu toka mbele yangu,..
Mfuate mpuuzi mwenzako huko mkaendelee kujaza vifua vyenu"
Mr Bill aliongea,
Frank alitoka zake na kurudi juu,
Alienda moja kwa moja kwa Tony ambaye alikua anapanga mizigo,
"Oya man vip"
Oscar alimstua Tony,
"Dah we boya umenistua kinyama"
Tony aliongea Sasa akisalimiana na swahiba wake huyo,
Baada ya story mbili tatu, Frank alimueleza kuhusu kushindwa kwa zoezi zima la kummaliza Mzee Mnyoka,
"Pole jamaa yangu, Ni Kama mkosi juu ya mkosi juzi Kuna boya katuvamia hapa Basi ndio Kama ulivyoona Carlos haelewi chochote humu ndani, "
Tony aliongea...
Huyu anamaliza Hana shidaHadithi za JF hazifikagi mwisho
Asante kipenzi
rasmi sasa nimetuliza komwe langu hapaHamuwezi Jutia kusoma hii story wanangu wa faida. Waswahili wanaita Bonge la story na mwandishi anamaliza hajawahi zingua. .
Analyse Half american Watu8 Numbisa Amehlo Depal wao ni wao Shunie Kalpana Dejane leadermoe Antonnia Lovelovie Depal Darlin Nuzulati Synod Binadamu Mtakatifu Johnnie Walker Glenn Mamaya Dahan moneytalk Cee Omar B Salum Dr Restart Numbisa Mo mp5 Santos06 Angel Nylon baby zu shikamkono01
Warry out bro, number coppiedGuys tusameheane hadithi hii ndio ya kwanza kuandika! Nikirefer kisa Cha kweli ambacho kilinitokea mwenyewe nikaongeza chumvi kwa kutumia fasihi,
Hadithi hii sikuihariri! Hivyo Kuna marudio mengi ya baadhi ya maneno kama vile "Sasa" na baadhi ya wahusika kujichanganya!
Bado Mimi ni mtunzi chipukizi kwa yeyote anataka kunipa support ikiwemo kunidhamini kutoa kitabu basi nitashukuru!!
Wengine wanaweza kuungana na mkuu Gily kuniwezesha bando!
Nawapenda sana!
Namba yangu ni 0746 mia mbili sitini na sita , mia mbili sitini na Saba!
Support tutaendelea kukup usijali kabisa. .Guys tusameheane hadithi hii ndio ya kwanza kuandika! Nikirefer kisa Cha kweli ambacho kilinitokea mwenyewe nikaongeza chumvi kwa kutumia fasihi,
Hadithi hii sikuihariri! Hivyo Kuna marudio mengi ya baadhi ya maneno kama vile "Sasa" na baadhi ya wahusika kujichanganya!
Bado Mimi ni mtunzi chipukizi kwa yeyote anataka kunipa support ikiwemo kunidhamini kutoa kitabu basi nitashukuru!!
Wengine wanaweza kuungana na mkuu Gily kuniwezesha bando!
Nawapenda sana!
Namba yangu ni 0746 mia mbili sitini na sita , mia mbili sitini na Saba!
Ukimaliza uje nikupe true story uwafikishie watanzania maana uko vizuri katika uandishi ndugu .KESI YA MZEE MNYOKA 20
"Oscar Kama ujuavyo kutokana na kazi zetu hizi tunakumbana na ghiliba nyingi, lakini kwakweli Jana umenifurahisha Sana, na zaidi ya yote ulinisaidia Sana, kwakweli, hata hivyo nikaona ili kutoa shukran zangu kwako nimeona nikupe kazi! Sijui unalionaje Hilo?"
Tito Sasa aliongea kwa hamasa!
"Kwakweli Mzee itapendeza Sana, lakini Sasa mpaka nijue kazi yenyewe maana unajua Mzee Mimi Elimu yangu Ni ya kidato cha nne tu, na sikua na matokeo mazuri Sana, "
Oscar alisema,
"Hata usijali, maisha Ni zaidi ya kusoma Oscar, wangapi Wana PhD zao lakini wako mtaani tuu, usiogope,
Unajua sisi mawaziri tuna kazi nyingi, Kuna mahali naweza kuhitajika wakati mwingine hata kufuata hata nyaraka tu! Sasa nikiwa na mtu Kama wewe unaweza kunisaidia zile kazi ndogo ndogo Kama hizo, kwa maana fupi nataka uwe msaidizi, wangu"
Tito alisema
"Na itakuwaje yaani utaratibu mzima wa kazi"
Oscar aliongea Sasa,
"Kazi kubwa Ni kuzunguuka na Mimi utakuwa Kama mlinzi wangu wa pili Ila Sasa wewe utakua unaniwakilisha kwenye zile shughuli zangu za nje ya ofisi, mfano Nina mashamba yangu kule kiluvya, Nina Ranchi moja kule mlandizi n.k, Sasa Mimi siwezi kufuatilia kila kitu kwahiyo wakati mwingine nitakua nakutuma wewe tu na mambo mengine tutazidi kuwasiliana, na sitakua nakulipa mshahara, Bali kila kazi utakayokua unafanya nitakulipa, na wakati mwingine utakua free na Mambo yako"
Tito aliongea
"Basi Hakuna shida Mzee, niseme kwamba Mimi nimekubali na tunaweza kuanza kazi!"
Alisema Oscar
************
Mzee Mnyoka aliwaza na kuwazua Sasa alikosa majibu,
Na hatimaye shule zilifungwa na mtoto wake James akarudi nyumbani kwa ajili ya likizo,
Mdogo wake Mary alimueleza kila kitu Kaka yake kuhusiana na kesi na "majanga" yote yaliyomkuta Mzee wao,
"Ndio Ni kweli tuko na Hali ngumu kwasasa Ila Mambo yatakaa sawa tu utarudi shule bila shida"
Mzee Mnyoka alikua akimtoa hofu mwanae, aliamini Kuna "namna" ya kuondokana na haya maseke seke,
Ingawa hakujua Ni kwa namna gani,
"Maisha hayawezi kusimama kwa ajili ya Jambo Hili"
Mzee Mnyoka aliwaza ,
*************
Baada ya wiki moja
Oscar Sasa alikua karibu na familia nzima ya Tito,
Na Kuna siku nyingine alichelewa Sana na "majukumu" yake akiwa na Tito hivyo alipewa sehemu ya kulala,
Kwa ufupi familia nzima ya Tito ilimuamini,
Siku hii ya leo, Oscar alipewa kazi ya kutuma baadhi ya taarifa kwa njia ya barua Pepe,
Zilikua Ni nyaraka mbili,
Oscar alizipeleka tu kwenye sehemu ya kutolea huduma za mtandao "internet cafe"
Ambapo alitakiwa tu kumuuliza Bwana ima,
Kisha angempa zile nyaraka,
Oscar aliamua kujiongeza na kununua bahasha nyingine ya kaki, Kama Ile Ile Kisha akachana na kusoma
"UreFact
The products may 2016"
Kilikua Ni kichwa Cha habari,
Oscar aliamua kuzipiga picha Kisha akaweka kwenye bahasha nyingine na Ile akaitupa mbali,
Alifika sinza kumekucha kisha akapaki Gari na kuingia kuelekea kwenye jengo moja lililokua na milango miwili ya vioo
"IMA INTERNET CAFE"
maandishi yalisomeka,
Baada ya salamu Oscar alimuuliza Kisha akampa Ile bahasha na kumnong'oneza
"Imetoka kwa Tito"
"Okay poa, naituma chap"
Alisema Ima Kisha akachukua Ile bahasha na kuingalia kidogo,
"Sikiliza jomba,
Hii bahasha sio, na usirudie Tena kufungua bahasha za watu"
Ima alimwambia Oscar kwa sauti ya chini
"Mhhh jamaa amejuaje? Na bahasha ziko sawa hizi?"
Oscar aliwaza huku akitafuta jibu la kumpa..