Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Tupo pamoja sana bampa 2 bampa
 
Pamoja sana mkuu blackstarline

Kitu ni kali mpaka ninatetemeka
 
SURA YA KUMI NA TANO

Baada ya mapigano kuisha, Bwana Henry na Bwana Good walichukuliwa na kuwekwa katika jumba la Twala, nami nilikwenda pamoja nao.

Wote walikuwa dhaifu kabisa kwa kuchoka na kwa kutokwa na damu, na hata mimi hali yangu ilikuwa hivyo hivyo.

Lakini mimi ni mwembamba kama uzi wa simu, yaani sichoki upesi: lakini usiku ule kwa kweli nilikuwa nimechoka kabisa.

Kwa hakika sote tulikuwa katika hali dhaifu, tukawa tukijifariji kwa kukumbuka kuwa tu hai wala si kama wale waliolala wakavu katika uwanda ule wa vita.

Kwa msaada wa Foulata aliyejifanya kuwa mtumishi wetu, tulizivua nguo zile za chuma ambazo kwa yakini zimetuokoa hivi leo. Lakini tulipozivua tuliona kama tumechubuka sana, maana ingawa zilitulinda tusichomwe na silaha hazikuzuia tusipate machubuko.

Foulata akaleta majani ya dawa yalionukia vizuri na ambayo yalipunguza maumivu yetu. Lakini maumivu yangu hayakuwa kama yale ya Bwana Henry na Bwana Good.

Bwana Good alikuwa amejeruhiwa mguuni maana mkuki ulipenya hata upande wa pili akatokwa na damu nyingi; na Bwana Henry alikuwa na majeraha mengi, na hasa moja kubwa usoni pale alipopigwa shoka na Twala.

Lakini kwa bahati Bwana Good alikuwa mganga wa kutosha akatuganga sote kwa dawa zilizokuwa katika kasha lake. Huku nyuma Foulata alitupikia mchuzi wa kututia nguvu, maana tulikuwa tumechoka hata hatukuweza kula.


Kisha baada ya kunywa mchuzi tukajitupa juu ya ngozi zilizokuwa katika jumba la Twala tukalala. Lakini ilikuwa vigumu kupata usingizi vizuri baada ya kazi za mchana, kwa sababu sauti za kuagana za wale wanaokufa, na vilio vya wale.

Waliofiwa zilizagaa kote. Kutoka kila upande tulisikia vilio vya wanawake waliofiwa na wanaume, wana na ndugu katika vile vita vikali.

Na kwa hakika walikuwa na haki ya kulia, maana katika jeshi la Wakukuana, karibu elfu kumi na mbili waliangamia katika vita vile.

Ilituathiri sana kusikia vilio vile vya huzuni walivyowalilia wale ambao hawarudi tena; vikanikumbusha sana kazi ya kutisha iliyotendeka siku ile kwa ajili ya kutekeleza tamaa za wanadamu.

Lakini ilipofika kiasi cha saa sita, vilio vilipungua, na baadaye kidogo ikawa kimya ila kwa sauti tuliyosikia ikitoka kwa nyuma ya jumba, tukafahamu baadaye kuwa alikuwa Gagula akimlilia mfalme Twala.



Baada ya saa sita nililala kidogo, lakini mara kwa mara nilishtuka nikafikiri kuwa nimo katika vita tena, na katika ndoto zangu nilipigana vita vyote tangu mwanzo.

Basi usiku ulipita, kukapambazuka; nikaona kuwa hata na wenzangu vile vile hawakulala vizuri.

Bwana Good alikuwa na homa kali sana, na akili zilimruka; pia akaanza kutema damu, maana nadhani Yule Mkukuana aliyejaribu kumchoma mkuki alimuumiza vibaya kwa ndani. Lakini Bwana Henry alipata nafuu ingawa alijimudu kwa shida bado kwa namna alivyokuwa ameumia.


Ilipofika kama saa mbili Infadus akaja kutuamkia, naye alikuwa kama hakuwamo katika vile vita vya jana, jinsi alivyokuwa mzima. Alifurahi sana kutuona tena, akatupa mikono na kututikisa kwa nguvu sana, lakini akamsikitikia sana Bwana Good.
 
Lakini niliona kuwa siha zake kwa Bwana Henry zilikithiri, baadaye tulikuja kujua kuwa askari hawakumfananisha Bwana Henry na mwanadamu wa kawaida.

Walisema kuwa hapana mwanadamu aliyeweza kupigana na Twala kama yeye alivyopigana naye, na hasa baada ya siku ya vita kama vile, maana Twala alisifiwa kuwa si mfalme tu lakini ni askari shujaa kupita wote.

Na pigo lile alilompiga hata kumkata kichwa likawa kama methali, yaani pigo lolote lililozidi nguvu likiitwa, Pigo la Ndovu.


Infadus akatuarifu kuwa askari wote wa Twala wamejiweka chini ya amri ya Ignosi, na wale waliokaa mbali wanafika sasa kujitoa. Kufa kwake Twala kwa mkono wa Bwana Henry kumemaliza kabisa vita katika nchi, maana Skraga aliyekua mrithi hata yeye amekufa.


Baadaye Ignosi akaja kutuamkia amevaa ile almasi ya kifalme juu ya kipaji cha uso. Nikamtazama alipokuwa akija, nikajaribu kumfananisha na Yule aliyekuja kwetu, akiomba tumpe kazi miezi michache nyuma.


Basi alipokaribia nikanyanyuka nikasema, ‘Hujambo, Ewe mfalme!’
Akajibu, ‘Sijambo, Makumazahn, mimi ni mfalme kwa nguvu za mikono yenu.’ Akatuarifu kuwa mambo yote yanaendelea vizuri, naye alitumaini kufanya karamu baada ya juma mbili apate kuonekana mbele ya watu wake.


Nikamuuliza atamfanya nini Yule Gagula, akajibu, ‘Yeye ni kama waziri mwovu katika nchi, na lazima nimuue, pamoja na wachawi wote.


Ameishi sana duniani, hata hapana anayejua miaka mingapi, naye ndiye aliyewafundisha wachawi wote na kufanya nchi iwe mbaya mbele ya Mungu.’
Nikajibu, ‘Kweli, lakini anayo maarifa mengi, na ni rahisi kuharibu maarifa kuliko ‘kuyapata!’


Akajibu, ‘Kweli, ni yeye peke yake ajuaye siri ya Wale Watatu Walio Kimya, na palipozikwa wafalme.’ Nikasema, ‘Ndiyo, na usisahau kuwa almasi zipo. Usisahau, Ignosi, yale uliyoahidi kuwa utatuongoza mpaka mashimo ya almasi, hata kama itakulazimu umwache Gagula aishi.’ Akajibu, ‘Mimi siwezi kusahau, Makumazahn, nami nita yafikiri maneno uliyosema.’


Ignosi alipoondoka nilikwenda kumtazama Bwana Good, nikamkuta ameshikwa na homa kali sana. Kwa siku mbili tulifikiri kuwa lazima atakufa, tukawa na mioyo mizito sana, lakini Foulata hakukubali, akasema kuwa lazima atapona.


Usiku wa tano wa ugonjwa wake nilikwenda kumtazama usiku kabla ya kwenda kulala, nikaingia chumbani pole pole sana, na kwa mwangaza wa taa nilimwona Bwana Good, lakini hakuwa akigaagaa kama siku zote, alilala kimya kabisa. Basi nilifikiri huu ndio mwisho, na nilikaribia kulia kwa uchungu.


Mara nilisikia sauti, ‘Sh! Sh!’ Nikatambua nikaenda karibu nikaona kuwa amelala usingizi wala hakufa, Alilala hivyo kwa muda wa saa kumi na nane, na wakati huo wote ameshika mkono wa Foulata, naye hakuweza kuondoka kwa sababu aliogopa atamwamsha.

Akakaa hivi bila kujinyosha na bila kula; lakini kwa kweli alipoamka ikawa lazima kumchukua, maana hakuweza kwenda kwa sababu viungo vyake vilikufa ganzi.
 
Baada ya hivi, hakukawia kupona, lakini Bwana Henry hakumwambia habari za vitendo vya Foulata mpaka alipokuwa karibu ya kupona. Bwana Good akasema, ‘Mwambie kuwa ameniokoa, nami sitasahau kabisa wema wake.’


Nikamwambia Foulata maneno aliyosema Bwana Good na Foulata akafurahi sana, akamtazama kwa macho ya mapenzi akasema, ‘Sivyo, bwana, labda bwana wangu amesahau kuwa yeye ndiye aliyeokoa maisha yangu, na mimi ni kijakazi wa Bwana.’


Baada ya siku chache Ignosi akafanya baraza kuu akakubaliwa na wakubwa wote wa nchi. Ikawa sherehe kubwa sana, na askari wale waliobaki katika jeshi lile la Wajivu waliwekwa mbele wakapewa shukrani za mfalme kwa kazi nzuri na ushujaa waliofanya katika vita.

Kila mtu alipewa zawadi ya ng’ombe na wote wakapandishwa kuwa wakubwa katika jeshi jipya ambalo vile vile liliitwa kwa jina la Wajivu.


Tena Ignosi alithibitisha maneno yale aliyotuahidi, mbele ya watu wote, yaani, watu hawatauawa tena bila ya kuhukumiwa, naya kuwa desturi ile ya kuwafichua wachawi itakoma mara moja.


Baraza ilipovunjika tulimsuburi Ignosi tukamwambia kuwa sasa tuna hamu ya kuzifichua siri zile za Mashimo yale ya Sulemani ambayo yalikuwepo mwisho wa Njia Kuu ya Sulemani; tukamuuliza kama amekwisha pata habari yoyote, akajibu, ‘Rafiki zangu, nimepata habari kuwa ni pale wanapokaa Wale Watatu Walio Kimya, ambao Twala alitaka kumuua Foulata awe ndiye mhanga wao.


Tena ni pale katika shimo kubwa wafalme wanapozikwa; ndipo mtakapoona maiti ya Twala amekaa pamoja na wale waliomtangulia. Na hapo lipo shimo lililokwenda chini sana lililochimbuliwa na watu wa zamani sana, labda kwa makusudio ya kutafuta mawe ya thamani uliyotaja.


Hapo ndipo Mahali pa Mauti, na humo kuna chumba ambacho hakijulikani. Ila na mfalme na Gagula. Twala alikijua lakini sasa amekufa, nami sikijui, wala sijui nini kilichomo.

Lakini imesimuliwa kuwa zamani mtu mweupe alivuka milima, akaongozwa na mwanamke mmoja, akaonyeshwa chumba kile cha siri, akaonyeshwa hazina.


Lakini kabla hawajaweza kuzichukua, akampitia kinyume na kuwaambia adui zake, akafukuzwa na mfalme wa wakati ule, na tangu siku ile hapana mtu aliyeingia katika mahali hapo.’


Nikasema, ‘Hadithi hiyo ni ya kweli Ignosi, maana tuliona maiti ya huyo mtu katika milima.’ Akajibu, ‘Ndiyo, tulimwona, na sasa nimeahidi kuwa kama mnaweza kukifikia chumba hicho, mna ruhusa kuchukua mawe yale ikiwa yapo.’

Nikasema, ‘Hicho kito unachovaa juu ya kipaji cha uso kila siku chathibitisa kuwa yapo.’ Akasema, ‘Labda, kama yapo mnayo ruhusa kuchukua kadiri mnayotaka, yaani ikiwa ni lazima mniache, ndugu zangu.

’Nikasema, ‘Lazima, lazima tukitafute hicho chumba .’ Akajibu, ‘Yupo mtu mmoja tu anayeweza kutuonyesha, naye ni Gagula.’

Nikasema, ‘Na kama hatakubali kutuonyesha itakuwaje?’
Akasema, ‘Basi atakufa. Nimemwacha hai kwa kusudio hilo tu. Tumwite tuone kama atakubali.’

Akatuma mtu kumwita. Baada ya kitambo akaletwa na askari huku akiwatukana. Mfalme akamwambia askari wamwache, na mara alipoachiliwa akakaa chini, na macho yake yakang’aa kama kito, akasema, ‘Wataka nini kwangu, Ignosi? Huthubutu kunigusa, ukinigusa nitakuua papo hapo ulipokaa. Jihadhari na uchawi wangu.’

Ignosi akajibu, ‘We mbwa jike, uchawi wako haukumwokoa Twala, wala hauwezi kunidhuru mimi.

Sikiliza, nataka utwambie habari za siri za mawe yale yanayong’aa’.
Gagula akacheka, akasema, ‘Ha!Ha! Hapana ajuaye ila mimi nijuaye siri hizo, nami sitakwambia kamwe.

Mashetani weupe hawa watakwenda zao mikono mitupu.’
Ignosi akasema, ‘Lazima utaniambia. Nitakushurutisha.’ Akajibu, ‘Kwa namna gani, Ewe mfalme? Wewe kweli ni mkubwa mwenye nguvu lakini nguvu zako zinawezaje kuukamua ukweli kutoka kwa mwanamke?’


Ignosi akajibu, ‘Najua ni vigumu, lakini nitafanya.’ Gagula akasema, ‘Ndiyo, lakini kwa namna gani?’ Ignosi akasema, ‘Hivi, ikiwa huniambii, utakufa kwa mateso ya pole pole.’
Gagula akalia, akasema, ‘Kufa? Hutothubutu kunigusa; wewe hujui mimi ni nani.


Umri wangu wadhani ni miaka mingapi? Mimi niliwajua baba za baba za baba zako. Nchi ilipokuwa mpya, mimi nilikuwapo; nchi itakapokuwa imechakaa mimi nitakuwapo. Siwezi kufa ila kuuawa kwa ajali, maana hapana anayethubutu kuniua.’


Ignosi akajibu, ‘Ndiyo, lakini nakwambia kuwa mimi nitakuua.’ Akashika mkuki wake akamsimamia juu tayari. Yule kizee akasema, ‘Sitakuonyesha kabisa; huwezi kuthubutu kuniua, huwezi kabisa. Atakayeniua mimi atalaaniwa milele.’


Pole pole Ignosi akashusha mkuki hata ncha yake ilimchoma kidogo, na mara Gagula akaruka juu kwa sauti kali, kisha akaanguka chini akagaagaa, huku akisema, ‘Basi, basi, niachilie niishi nami nitakuonyesha.’


Ignosi akasema, ‘Vema. Nilihisi’ kuwa nitapata njia ya kukufanya ukubali. Kesho utafuatana na Infadus na ndugu zangu weupe, kuwaonyesha hapo mahali, na uangalie sana usifanye makosa, maana usipowaonyesha, hakika utakufa.’


Yule kizee akajibu, ‘Sitakosa, Ignosi. Ni desturi yangu kutimiza niliyoahidi. Ha!Ha!Ha! Zamani mwanamke mmoja alimwonyesha mtu mweupe kile chumba na tazama! Alipatikana na maovu. Jina lake lilikuwa Gagula vile vile.


Labda mimi na huyo mwanamke ni mmoja.’ Na mcho yake maovu yalizidi kung’aa.
Nikasema, ‘Mwongo, hayo yalitokea zamani vizazi kumi nyuma.’


Akasema, ‘Labda, labda; mtu akiishi miaka mingi pengine husahau. Labda lilikuwa jina la mama yangu nayeye aliniambia, kwa hakika jina lake lilikuwa Gagula vie vile. Lakini, angalieni, nawaambia ya kuwa katika chumba kile yalipo hayo mawe, mtaona kifuko cha ngozi kimejaa mawe meupe.


Huyo mtu alijaza kifuko hicho, lakini hakuwahi kukichukua. Alipatikana na maovu , nasema alipatikana na maovu! Labda aliyeniambia alikuwa mama wa mama yangu! Itakuwa safari ya furaha.


Tutapita katika mahali walipopigana askari juzi, tutaona maiti waliokufa katika vita. Macho yao yatakuwa yamekwisha pofuka sasa, na mbavu zao zitakuwa zimekwisha bonyeka. Ha! Ha!Ha!’
 
Pamoja sana mkuu
 
mzee baba ...imeishiaa patamuu daa ..fanya mambo yako basiii ..ovaa tunafuatiliaa tamthiliaa za startv ......
 
Leo Mkuu umetuweka sana shusha mzigo tunausubiri Kwa hamu sanaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…