Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Hadithi ya mashimo ya mfalme Sulemani

Bwana Henry akafadhaika akasema, ‘Nafikiri amejeruhiwa.’

Na hapo aliposema hayo, Yule tuliyefikiri kuwa ni maiti Mkukuana akaruka akampiga Bwana Good kichwani akamwangusha chini, akaanza kumchoma mikuki, Tulimkimbilia Bwana Good, na tulipomkaribia tulimwona Yule Mkukuana anampiga na kumpiga tena kwa mkuki, na kila alipopiga mikono na miguu ya Bwana Good ikaruka juu.


Yule Mkukuana alipotuona tunakuja, akazidi kumpiga kwa nguvu, akapiga kelele, ‘Haya, wewe mchawi nimekuua.’ Akakimbia. Bwana Good akalala kimya wala hakuweza kujimudu hata kidogo, tukafikiri kuwa rafiki yetu tayari amekufa.


Tulimkaribia kwa huzuni, tukashangaa tulipoona anacheka ingawa amegeuka rangi kwa maumivu, akacheka na miwani bado ipo katika jicho lake, akasema, ‘Hizi nguo za chuma ni nzuri sana, naona kuwa Yule Mkukuana amestaajabu.’

Na mara akazimia. Tulipomtazama tuliona kuwa amejeruhiwa vibaya mguu mmoja kwa pigo la kisu kikubwa, lakini nguo zile za chuma zimemlinda asiumizwe zaidi na Yule Mkukuana. Ikawa ameokoka kwa rehema ya Mungu.

Hatukuweza kumtibu wakati ule basi tukamweka juu ya ngao akachukuliwa pamoja nasi. Tulipofika penye lango la Loo tukaona kikosi cha askari wa upande wetu wamesimama kulinda zamu kwa amri za Ignosi.

Vikosi vingine viliwekwa penye milango mingine ya mji.
Yule mkubwa wa kikosi alipomwona Ignosi, alimwamkia kwa amkio la kifalme, akamwambia kuwa askari wa Twala wamejificha katika mji, na Twala mwenyewe vile vile yumo mjini, lakini alifikiri kuwa watu watajitoa, maana wame fadhaika kabisa.


Basi aliposikia hayo Ignosi alituma tarishi kwa kila mlango wa mji kuwaamuru walio ndani wafungue milango, naye aliahidi kuwa wote watakaojitoa na kutoa silaha zao watapata msamaha.

Basi habari hii ikapokewa, na mara tulisikia makelele na milango ikafunguliwa. Tukaingia katika mji, lakini tuliangalia sana tusije tukaghafilika.

Katika njia zote tulikuta askari wamesimama na vichwa kuinamia chini, na silala na ngao zao zimewekwa chini miguuni pao, na Ignosi alipokuwa akipita walimwamkia kwa amkio la kifalme.

Tukaenda mbele mpaka jumba la Twala, Tulipofika kwenye kiwanja kile tulichokwenda juzi juzi kutazama ngoma, tulikiona kipo wazi kabisa, lakini si wazi, maana pale mbele ya mlango wa jumba lake, Twala mwenyewe alikaa, pamoja na mtu mmoja tu, naye alikuwa Gagula.

Ilisikitisha kumwona vile alivyokaa, na shoka lake na ngao yake vimewekwa chini ubavuni pake, na kichwa chake kainamisha kifuani, na mtu mmoja tu amekaa kumfariji.


Na ingawa tulikumbuka ukatili wake, hatukuweza kujizuia kuto kumsikitikia.

Hapana hata askari mmoja katika maelfu ya askari wake; hapana hata mfuasi mmoja katika wale wengi walionyenyekea mbele yake, hapana hata mke mmoja aliyesalia kumfariji katika uchungu wa yaliyomfika. Masikini!

Tulipita mlango wa kiwanja tukaenda mpaka mbele ya Twala, na huku Gagula anatutukana vibaya.

Tulipokaribia, Twala akafanya kutuona, akainua kichwa chake kilichovikwa manyoya marefu, akamtazama Ignosi kwa jicho moja lake, likang’aa kama ile almasi iliyofungwa katika kipaji chake cha uso, akasema kwa sauti yenye uchungu na dharau, ‘Hujambo, Ewe mfalme, wewe uliyekula chakula changu, na sasa kwa msaada wa uchawi wa watu weupe umewashawishi askari wangu kuniasi!

Niambie, ajali yangu ni nini, Ewe mfalme?’

Ignosi akajibu kwa ukali, ‘Ajali yako ni ile ile uliyompa baba yangu, ambaye kiti chake umekikalia kwa miaka hii yote.’ Twala akasema, ‘Vema, nimekubali. Nitakuonyesha njia ya kufia, ili nawe ukumbuke wakati wako utakapowadia.

Tazama, jua linazama, ni vizuri na jua langu lizame pamoja nalo. Na sasa, ewe mfalme, mimi tayari kufa, lakini nataka haki ya mfalme wa Wakukuana, yaani nife nikipigana. Huwezi kunikatalia; ukikataa hata wale waoga waliokimbia leo, hata na wao watakwita mwoga.’

Ignosi akajibu , ‘Nimekubali. Chagua, utapigana na nani? Mimi mwenyewe siwezi kupigana nawe, maana mfalme hupigana katika vita tu.’


Jicho la Twala likatutazama, na kwa dakika moja nilimwona ananitaza mimi tu, na baadaye akasema, ‘Ndovu, wasemaje, tumalize yale tuliyoanza leo, au nikwite kwa jina la mwoga?’

Ignosi akasema kwa haraka, ‘La, huna ruhusa kupigana na Ndovu.’ Twala akajibu, ‘Vema, kama anaogopa, sipigani naye.’ Basi Bwana Henry alifahamu maneno hayo, na uso ulimwiiva akasema, ‘Nitapigana naye, naye ataona kuwa siogopi.’


Nikamsihi, ‘Nakuomba usipigane naye, usijitie katika hatari ya bure, maana huyu anajua lazima afe. Kila mtu aliyekuona leo anajua kuwa wewe ni shujaa, si muoga.’

Akajibu, ‘Lazima nipigane naye. Hapana mtu atakayeniita muoga na kuishi. Sasa mimi ni tayari.’ Akashika shoka lake akasimama mbele. Nilipoona kuwa amekwisha azimia, wasiwasi uliniingia, lakini sikuweza kumzuia asipigane.

Ignosi akaweka mkono juu ya bega lake kwa upole, akamwambia, ‘Rafiki, ndugu yangu mweupe, usipigane naye. Vita uliyopigana leo inatosha kabisa, na ukidhurika, moyo wangu utakuwa mzito sana.’

Bwana Henry akasema, ‘Ignosi, lazima nitapigana naye .’ Akaijibu, ‘vema, Ndovu, wewe ni shujaa kweli kweli. Tazama, Twala, Ndovu yu tayari kupigana nawe.’

Twala akacheka kicheko kikubwa, akasimama akamtazama Bwana Henry. Kwa muda kidogo wakasimama hivi na mwangaza wa jua lililokuwa likishuka ukawaangaza ukaonyesha maungo yao namna yalivyokuwa mazuri.

Kisha wakaangaza kuzungukiana, na mashoka yao juu.

Mara Bwana Henry akaruka mbele akajaribu kumpiga Twala kwa nguvu zake zote, lakini Twala aliepa.

Nguvu za pigo zilikuwa nyingi hata alitaka kuanguka, basi adui yake akawa tayari akapungu shoka lake kichwani, akapiga kwa nguvu nyingi kabisa. Moyo wangu ulisita, nikafikiri kuwa yamekwisha. Lakini sivyo;

Bwana Henry akaweka mkono wake juu kwa upesi akalikinga shoka. Mara Bwana Henry akapata nafasi kupiga mara ya pili, lakini Twala akakinga kwa ngao yake.

Basi ikaendelea hivyo, pigo kwa pigo, na kila pigo lilikingwa. Sasa watu wote waliokuwako wakaanza kusongana katika mshangao wao, wakapiga kelele au kuguna kwa kila pigo.

Hapo Bwana Good aliye kuwa amezimia, akapata fahamu tena, na mara akasimama akaanza kurukaruka huku akimtia moyo Bwana Henry.

Basi hivyo hivyo wakapigana, hata kwa bahati mbaya Twala akapata nafasi ya kulipiga shoga la Bwana Henry likamtoka mkononi, likaanguka chini.

Sasa wote waliugua kwa mashaka na huzuni, na Twala akainua shoka lake juu akamrukia huku akipiga kelele. Nikafumba macho.

Nilipofumbua macho tena, niliona ngao ya Bwana Henry imelala chini, naye amemkumbatia Twala kiunoni.

Huku na huku waliminyana, huku wamekamatana kwa nguvu zao zote. Twala akajitahidi sana, akamwinua Bwana Henry juu, wakaanguka chini wote pamoja, na Twala alijaribu kumpiga shoka la kichwa, na Bwana Henry akajaribu kumpiga Twala kisu.


Ikawa shindano kuu kabisa, na hapo Bwana Good alipiga ukulele, ‘Shika shoka lake!’ Na labda Bwana Henry alisikia, maana alitupa kisu chake akashika shoka la Twala wakaanza kupinduana chini wakipigana kama paka wa mwitu wanavyopigana, huku wakitweta kwa nguvu.

Mara tuliona kuwa ngozi iliyofungiwa shoka kwenye mkono wa Twala imekatika, na Bwana Henry ametengwa naye na amepata shoka hilo. Mara akaruka juu, na damu inamtoka usoni pale alipojeruhiwa na Twala, na mara ile Twala naye akaruka juu.


Basi sasa ikawa kupigana tena, mpaka Bwana Henry akajitahidi akapiga shoka kwa nguvu zote, akampiga la shingo.

Hapo watu waliokuwapo waliguna kwa pamoja maana kichwa cha Twala kikaanguka kikabiringika mpaka kikafika kwenye mguu wa Ignosi kikasita.


Kwa dakika hivi kiwiliwili chake kilisimama wima, kisha kikaanguka kwa kishindo, na pale pale Bwana Henry alizimia, naye akaanguka juu ya maiti ya Twala.


Basi tulimwinua tukammwagia maji akafumbua macho yake. Hakufa, nami, jua lilipokuwa likishuka, nikasimama mbele, nikafungua ile almasi iliyofungwa juu ya kipaji cha uso wa Twala, nikampa Ignosi, nikasema, ‘Itwae Ignosi, mfalme wa haki wa Wakukuana, mfalme kwa ‘kuzaliwa, na mfalme kwa kushinda.’

Ignosi akaifunga juu ya kipaji chake, akaja mbele akaweka mguu wake juu ya kiwiliwili cha Twala, akaanza kuimba wimbo wa ushindi, hivi:

Sasa uasi wetu umemezwa katika ushindi, na vitendo vyetu viovu vimegeuka kuwa haki kwa nguvu. Asubuhi wadhalimu waliamka wakajitikisa; walijifungia manyoya wakajiweka tayari kwa vita. Waliamka wakashika mikuki yao: askari waliwaita wakubwa wao, ‘Njooni mtuongoze.’

Na wakubwa walimwita mfalme, ‘Utuongoze vitani.’ Wakaondoka na kiburi chao, watu ishirini elfu na tena ishirini elfu.

Manyoya yao yalifunika nchi kama manyoya ya ndege yanavyofunika tundu lake; walitikisa mikuki yao kwa vigelegele.

Ndiyo, walirusha mikuki yao katika mwangaza wa jua; wakatamani vita wakafurahi.
Wakanishambulia; wenye nguvu wao eakanijia mbio waniue, wakipiga kelele,’ Hal Ha! Ni kama aliyekwisha kufa.’ Ndipo nilipovuma juu yao, na pumzi zangu zikawa kama upepo wa tufani, na tazama! Wakatawanyika .



Umeme wangu uliwachoma; nililamba nguvu zao kwa umeme wa mikuki yangu; niliwapeperusha kwa ngurumo ya kulia kwangu.

Walivunjika, walitawanyika, walitoweka kama ukungu wa asubuhi.
Sasa wamekuwa chakula cha kunguru na fisi, na mahali pa vita pamenona kwa damu yao.


Wa wapi wale walioamka asubuhi na nguvu zao?
Wa wapi wale wenye kiburi waliotikisa manyoya yao wakasema ‘Ni kama aliyekwisha kufa:’


Wameinamisha vichwa lakini si katika kusinzia; wamejinyosha, lakini si katika usingizi.
Wamesahauliwa; wametoweka gizani nao hawatarudi; ndiyo, watu wengine watawachukua wake zao, na watoto wao hawatawakumbuka tena.



Na mimi, mimi? Mimi ni mfalme. Kama tai nimeona tundu langu.

Tazama! Nilitembea mbali wakati wa usiku, lakini nimewarudika makinda yangu wakati wa mapambazuko.

Ingieni nyinyi kwenye kivuli cha mabawa yangu, ee nyinyi watu, nami nitawafariji, nanyi hamtafadhaika tena.

Huu ndiyo wakati wa neema, huu ndio wakati wa kuteka. Ng’ombe walio bondeni ni wangu, wanawali pia walio mjumbani ni wangu.

Taabu imepita, neema imefika. Sasa uovo utafunikwa uso wake, na Huruma na Furaha watakaa katika nchi.

Furahini, furahini, watu wangu!

Dunia yote ifurahi kwa kuwa jeuri imekanyagwa, na mimi ndiye mfalme.

Ignosi akanyamaza, na kutoka katika giza lililokuwa limeingia, jibu likaja kama ngurumo kutoka milimani, ‘Wewe ndiye mfalme!’

Hivyo yale niliyombashiria Yule tarishi yalitimia, na katika muda wa saa arubaini na nane, kiwiliwili cha Twala kimelala kikavu mbele ya mlango wa jumba lake.
Tupo pamoja sana bampa 2 bampa
 
Bwana Henry akafadhaika akasema, ‘Nafikiri amejeruhiwa.’

Na hapo aliposema hayo, Yule tuliyefikiri kuwa ni maiti Mkukuana akaruka akampiga Bwana Good kichwani akamwangusha chini, akaanza kumchoma mikuki, Tulimkimbilia Bwana Good, na tulipomkaribia tulimwona Yule Mkukuana anampiga na kumpiga tena kwa mkuki, na kila alipopiga mikono na miguu ya Bwana Good ikaruka juu.


Yule Mkukuana alipotuona tunakuja, akazidi kumpiga kwa nguvu, akapiga kelele, ‘Haya, wewe mchawi nimekuua.’ Akakimbia. Bwana Good akalala kimya wala hakuweza kujimudu hata kidogo, tukafikiri kuwa rafiki yetu tayari amekufa.


Tulimkaribia kwa huzuni, tukashangaa tulipoona anacheka ingawa amegeuka rangi kwa maumivu, akacheka na miwani bado ipo katika jicho lake, akasema, ‘Hizi nguo za chuma ni nzuri sana, naona kuwa Yule Mkukuana amestaajabu.’

Na mara akazimia. Tulipomtazama tuliona kuwa amejeruhiwa vibaya mguu mmoja kwa pigo la kisu kikubwa, lakini nguo zile za chuma zimemlinda asiumizwe zaidi na Yule Mkukuana. Ikawa ameokoka kwa rehema ya Mungu.

Hatukuweza kumtibu wakati ule basi tukamweka juu ya ngao akachukuliwa pamoja nasi. Tulipofika penye lango la Loo tukaona kikosi cha askari wa upande wetu wamesimama kulinda zamu kwa amri za Ignosi.

Vikosi vingine viliwekwa penye milango mingine ya mji.
Yule mkubwa wa kikosi alipomwona Ignosi, alimwamkia kwa amkio la kifalme, akamwambia kuwa askari wa Twala wamejificha katika mji, na Twala mwenyewe vile vile yumo mjini, lakini alifikiri kuwa watu watajitoa, maana wame fadhaika kabisa.


Basi aliposikia hayo Ignosi alituma tarishi kwa kila mlango wa mji kuwaamuru walio ndani wafungue milango, naye aliahidi kuwa wote watakaojitoa na kutoa silaha zao watapata msamaha.

Basi habari hii ikapokewa, na mara tulisikia makelele na milango ikafunguliwa. Tukaingia katika mji, lakini tuliangalia sana tusije tukaghafilika.

Katika njia zote tulikuta askari wamesimama na vichwa kuinamia chini, na silala na ngao zao zimewekwa chini miguuni pao, na Ignosi alipokuwa akipita walimwamkia kwa amkio la kifalme.

Tukaenda mbele mpaka jumba la Twala, Tulipofika kwenye kiwanja kile tulichokwenda juzi juzi kutazama ngoma, tulikiona kipo wazi kabisa, lakini si wazi, maana pale mbele ya mlango wa jumba lake, Twala mwenyewe alikaa, pamoja na mtu mmoja tu, naye alikuwa Gagula.

Ilisikitisha kumwona vile alivyokaa, na shoka lake na ngao yake vimewekwa chini ubavuni pake, na kichwa chake kainamisha kifuani, na mtu mmoja tu amekaa kumfariji.


Na ingawa tulikumbuka ukatili wake, hatukuweza kujizuia kuto kumsikitikia.

Hapana hata askari mmoja katika maelfu ya askari wake; hapana hata mfuasi mmoja katika wale wengi walionyenyekea mbele yake, hapana hata mke mmoja aliyesalia kumfariji katika uchungu wa yaliyomfika. Masikini!

Tulipita mlango wa kiwanja tukaenda mpaka mbele ya Twala, na huku Gagula anatutukana vibaya.

Tulipokaribia, Twala akafanya kutuona, akainua kichwa chake kilichovikwa manyoya marefu, akamtazama Ignosi kwa jicho moja lake, likang’aa kama ile almasi iliyofungwa katika kipaji chake cha uso, akasema kwa sauti yenye uchungu na dharau, ‘Hujambo, Ewe mfalme, wewe uliyekula chakula changu, na sasa kwa msaada wa uchawi wa watu weupe umewashawishi askari wangu kuniasi!

Niambie, ajali yangu ni nini, Ewe mfalme?’

Ignosi akajibu kwa ukali, ‘Ajali yako ni ile ile uliyompa baba yangu, ambaye kiti chake umekikalia kwa miaka hii yote.’ Twala akasema, ‘Vema, nimekubali. Nitakuonyesha njia ya kufia, ili nawe ukumbuke wakati wako utakapowadia.

Tazama, jua linazama, ni vizuri na jua langu lizame pamoja nalo. Na sasa, ewe mfalme, mimi tayari kufa, lakini nataka haki ya mfalme wa Wakukuana, yaani nife nikipigana. Huwezi kunikatalia; ukikataa hata wale waoga waliokimbia leo, hata na wao watakwita mwoga.’

Ignosi akajibu , ‘Nimekubali. Chagua, utapigana na nani? Mimi mwenyewe siwezi kupigana nawe, maana mfalme hupigana katika vita tu.’


Jicho la Twala likatutazama, na kwa dakika moja nilimwona ananitaza mimi tu, na baadaye akasema, ‘Ndovu, wasemaje, tumalize yale tuliyoanza leo, au nikwite kwa jina la mwoga?’

Ignosi akasema kwa haraka, ‘La, huna ruhusa kupigana na Ndovu.’ Twala akajibu, ‘Vema, kama anaogopa, sipigani naye.’ Basi Bwana Henry alifahamu maneno hayo, na uso ulimwiiva akasema, ‘Nitapigana naye, naye ataona kuwa siogopi.’


Nikamsihi, ‘Nakuomba usipigane naye, usijitie katika hatari ya bure, maana huyu anajua lazima afe. Kila mtu aliyekuona leo anajua kuwa wewe ni shujaa, si muoga.’

Akajibu, ‘Lazima nipigane naye. Hapana mtu atakayeniita muoga na kuishi. Sasa mimi ni tayari.’ Akashika shoka lake akasimama mbele. Nilipoona kuwa amekwisha azimia, wasiwasi uliniingia, lakini sikuweza kumzuia asipigane.

Ignosi akaweka mkono juu ya bega lake kwa upole, akamwambia, ‘Rafiki, ndugu yangu mweupe, usipigane naye. Vita uliyopigana leo inatosha kabisa, na ukidhurika, moyo wangu utakuwa mzito sana.’

Bwana Henry akasema, ‘Ignosi, lazima nitapigana naye .’ Akaijibu, ‘vema, Ndovu, wewe ni shujaa kweli kweli. Tazama, Twala, Ndovu yu tayari kupigana nawe.’

Twala akacheka kicheko kikubwa, akasimama akamtazama Bwana Henry. Kwa muda kidogo wakasimama hivi na mwangaza wa jua lililokuwa likishuka ukawaangaza ukaonyesha maungo yao namna yalivyokuwa mazuri.

Kisha wakaangaza kuzungukiana, na mashoka yao juu.

Mara Bwana Henry akaruka mbele akajaribu kumpiga Twala kwa nguvu zake zote, lakini Twala aliepa.

Nguvu za pigo zilikuwa nyingi hata alitaka kuanguka, basi adui yake akawa tayari akapungu shoka lake kichwani, akapiga kwa nguvu nyingi kabisa. Moyo wangu ulisita, nikafikiri kuwa yamekwisha. Lakini sivyo;

Bwana Henry akaweka mkono wake juu kwa upesi akalikinga shoka. Mara Bwana Henry akapata nafasi kupiga mara ya pili, lakini Twala akakinga kwa ngao yake.

Basi ikaendelea hivyo, pigo kwa pigo, na kila pigo lilikingwa. Sasa watu wote waliokuwako wakaanza kusongana katika mshangao wao, wakapiga kelele au kuguna kwa kila pigo.

Hapo Bwana Good aliye kuwa amezimia, akapata fahamu tena, na mara akasimama akaanza kurukaruka huku akimtia moyo Bwana Henry.

Basi hivyo hivyo wakapigana, hata kwa bahati mbaya Twala akapata nafasi ya kulipiga shoga la Bwana Henry likamtoka mkononi, likaanguka chini.

Sasa wote waliugua kwa mashaka na huzuni, na Twala akainua shoka lake juu akamrukia huku akipiga kelele. Nikafumba macho.

Nilipofumbua macho tena, niliona ngao ya Bwana Henry imelala chini, naye amemkumbatia Twala kiunoni.

Huku na huku waliminyana, huku wamekamatana kwa nguvu zao zote. Twala akajitahidi sana, akamwinua Bwana Henry juu, wakaanguka chini wote pamoja, na Twala alijaribu kumpiga shoka la kichwa, na Bwana Henry akajaribu kumpiga Twala kisu.


Ikawa shindano kuu kabisa, na hapo Bwana Good alipiga ukulele, ‘Shika shoka lake!’ Na labda Bwana Henry alisikia, maana alitupa kisu chake akashika shoka la Twala wakaanza kupinduana chini wakipigana kama paka wa mwitu wanavyopigana, huku wakitweta kwa nguvu.

Mara tuliona kuwa ngozi iliyofungiwa shoka kwenye mkono wa Twala imekatika, na Bwana Henry ametengwa naye na amepata shoka hilo. Mara akaruka juu, na damu inamtoka usoni pale alipojeruhiwa na Twala, na mara ile Twala naye akaruka juu.


Basi sasa ikawa kupigana tena, mpaka Bwana Henry akajitahidi akapiga shoka kwa nguvu zote, akampiga la shingo.

Hapo watu waliokuwapo waliguna kwa pamoja maana kichwa cha Twala kikaanguka kikabiringika mpaka kikafika kwenye mguu wa Ignosi kikasita.


Kwa dakika hivi kiwiliwili chake kilisimama wima, kisha kikaanguka kwa kishindo, na pale pale Bwana Henry alizimia, naye akaanguka juu ya maiti ya Twala.


Basi tulimwinua tukammwagia maji akafumbua macho yake. Hakufa, nami, jua lilipokuwa likishuka, nikasimama mbele, nikafungua ile almasi iliyofungwa juu ya kipaji cha uso wa Twala, nikampa Ignosi, nikasema, ‘Itwae Ignosi, mfalme wa haki wa Wakukuana, mfalme kwa ‘kuzaliwa, na mfalme kwa kushinda.’

Ignosi akaifunga juu ya kipaji chake, akaja mbele akaweka mguu wake juu ya kiwiliwili cha Twala, akaanza kuimba wimbo wa ushindi, hivi:

Sasa uasi wetu umemezwa katika ushindi, na vitendo vyetu viovu vimegeuka kuwa haki kwa nguvu. Asubuhi wadhalimu waliamka wakajitikisa; walijifungia manyoya wakajiweka tayari kwa vita. Waliamka wakashika mikuki yao: askari waliwaita wakubwa wao, ‘Njooni mtuongoze.’

Na wakubwa walimwita mfalme, ‘Utuongoze vitani.’ Wakaondoka na kiburi chao, watu ishirini elfu na tena ishirini elfu.

Manyoya yao yalifunika nchi kama manyoya ya ndege yanavyofunika tundu lake; walitikisa mikuki yao kwa vigelegele.

Ndiyo, walirusha mikuki yao katika mwangaza wa jua; wakatamani vita wakafurahi.
Wakanishambulia; wenye nguvu wao eakanijia mbio waniue, wakipiga kelele,’ Hal Ha! Ni kama aliyekwisha kufa.’ Ndipo nilipovuma juu yao, na pumzi zangu zikawa kama upepo wa tufani, na tazama! Wakatawanyika .



Umeme wangu uliwachoma; nililamba nguvu zao kwa umeme wa mikuki yangu; niliwapeperusha kwa ngurumo ya kulia kwangu.

Walivunjika, walitawanyika, walitoweka kama ukungu wa asubuhi.
Sasa wamekuwa chakula cha kunguru na fisi, na mahali pa vita pamenona kwa damu yao.


Wa wapi wale walioamka asubuhi na nguvu zao?
Wa wapi wale wenye kiburi waliotikisa manyoya yao wakasema ‘Ni kama aliyekwisha kufa:’


Wameinamisha vichwa lakini si katika kusinzia; wamejinyosha, lakini si katika usingizi.
Wamesahauliwa; wametoweka gizani nao hawatarudi; ndiyo, watu wengine watawachukua wake zao, na watoto wao hawatawakumbuka tena.



Na mimi, mimi? Mimi ni mfalme. Kama tai nimeona tundu langu.

Tazama! Nilitembea mbali wakati wa usiku, lakini nimewarudika makinda yangu wakati wa mapambazuko.

Ingieni nyinyi kwenye kivuli cha mabawa yangu, ee nyinyi watu, nami nitawafariji, nanyi hamtafadhaika tena.

Huu ndiyo wakati wa neema, huu ndio wakati wa kuteka. Ng’ombe walio bondeni ni wangu, wanawali pia walio mjumbani ni wangu.

Taabu imepita, neema imefika. Sasa uovo utafunikwa uso wake, na Huruma na Furaha watakaa katika nchi.

Furahini, furahini, watu wangu!

Dunia yote ifurahi kwa kuwa jeuri imekanyagwa, na mimi ndiye mfalme.

Ignosi akanyamaza, na kutoka katika giza lililokuwa limeingia, jibu likaja kama ngurumo kutoka milimani, ‘Wewe ndiye mfalme!’

Hivyo yale niliyombashiria Yule tarishi yalitimia, na katika muda wa saa arubaini na nane, kiwiliwili cha Twala kimelala kikavu mbele ya mlango wa jumba lake.
Pamoja sana mkuu blackstarline

Kitu ni kali mpaka ninatetemeka
 
SURA YA KUMI NA TANO

Baada ya mapigano kuisha, Bwana Henry na Bwana Good walichukuliwa na kuwekwa katika jumba la Twala, nami nilikwenda pamoja nao.

Wote walikuwa dhaifu kabisa kwa kuchoka na kwa kutokwa na damu, na hata mimi hali yangu ilikuwa hivyo hivyo.

Lakini mimi ni mwembamba kama uzi wa simu, yaani sichoki upesi: lakini usiku ule kwa kweli nilikuwa nimechoka kabisa.

Kwa hakika sote tulikuwa katika hali dhaifu, tukawa tukijifariji kwa kukumbuka kuwa tu hai wala si kama wale waliolala wakavu katika uwanda ule wa vita.

Kwa msaada wa Foulata aliyejifanya kuwa mtumishi wetu, tulizivua nguo zile za chuma ambazo kwa yakini zimetuokoa hivi leo. Lakini tulipozivua tuliona kama tumechubuka sana, maana ingawa zilitulinda tusichomwe na silaha hazikuzuia tusipate machubuko.

Foulata akaleta majani ya dawa yalionukia vizuri na ambayo yalipunguza maumivu yetu. Lakini maumivu yangu hayakuwa kama yale ya Bwana Henry na Bwana Good.

Bwana Good alikuwa amejeruhiwa mguuni maana mkuki ulipenya hata upande wa pili akatokwa na damu nyingi; na Bwana Henry alikuwa na majeraha mengi, na hasa moja kubwa usoni pale alipopigwa shoka na Twala.

Lakini kwa bahati Bwana Good alikuwa mganga wa kutosha akatuganga sote kwa dawa zilizokuwa katika kasha lake. Huku nyuma Foulata alitupikia mchuzi wa kututia nguvu, maana tulikuwa tumechoka hata hatukuweza kula.


Kisha baada ya kunywa mchuzi tukajitupa juu ya ngozi zilizokuwa katika jumba la Twala tukalala. Lakini ilikuwa vigumu kupata usingizi vizuri baada ya kazi za mchana, kwa sababu sauti za kuagana za wale wanaokufa, na vilio vya wale.

Waliofiwa zilizagaa kote. Kutoka kila upande tulisikia vilio vya wanawake waliofiwa na wanaume, wana na ndugu katika vile vita vikali.

Na kwa hakika walikuwa na haki ya kulia, maana katika jeshi la Wakukuana, karibu elfu kumi na mbili waliangamia katika vita vile.

Ilituathiri sana kusikia vilio vile vya huzuni walivyowalilia wale ambao hawarudi tena; vikanikumbusha sana kazi ya kutisha iliyotendeka siku ile kwa ajili ya kutekeleza tamaa za wanadamu.

Lakini ilipofika kiasi cha saa sita, vilio vilipungua, na baadaye kidogo ikawa kimya ila kwa sauti tuliyosikia ikitoka kwa nyuma ya jumba, tukafahamu baadaye kuwa alikuwa Gagula akimlilia mfalme Twala.



Baada ya saa sita nililala kidogo, lakini mara kwa mara nilishtuka nikafikiri kuwa nimo katika vita tena, na katika ndoto zangu nilipigana vita vyote tangu mwanzo.

Basi usiku ulipita, kukapambazuka; nikaona kuwa hata na wenzangu vile vile hawakulala vizuri.

Bwana Good alikuwa na homa kali sana, na akili zilimruka; pia akaanza kutema damu, maana nadhani Yule Mkukuana aliyejaribu kumchoma mkuki alimuumiza vibaya kwa ndani. Lakini Bwana Henry alipata nafuu ingawa alijimudu kwa shida bado kwa namna alivyokuwa ameumia.


Ilipofika kama saa mbili Infadus akaja kutuamkia, naye alikuwa kama hakuwamo katika vile vita vya jana, jinsi alivyokuwa mzima. Alifurahi sana kutuona tena, akatupa mikono na kututikisa kwa nguvu sana, lakini akamsikitikia sana Bwana Good.
 
Lakini niliona kuwa siha zake kwa Bwana Henry zilikithiri, baadaye tulikuja kujua kuwa askari hawakumfananisha Bwana Henry na mwanadamu wa kawaida.

Walisema kuwa hapana mwanadamu aliyeweza kupigana na Twala kama yeye alivyopigana naye, na hasa baada ya siku ya vita kama vile, maana Twala alisifiwa kuwa si mfalme tu lakini ni askari shujaa kupita wote.

Na pigo lile alilompiga hata kumkata kichwa likawa kama methali, yaani pigo lolote lililozidi nguvu likiitwa, Pigo la Ndovu.


Infadus akatuarifu kuwa askari wote wa Twala wamejiweka chini ya amri ya Ignosi, na wale waliokaa mbali wanafika sasa kujitoa. Kufa kwake Twala kwa mkono wa Bwana Henry kumemaliza kabisa vita katika nchi, maana Skraga aliyekua mrithi hata yeye amekufa.


Baadaye Ignosi akaja kutuamkia amevaa ile almasi ya kifalme juu ya kipaji cha uso. Nikamtazama alipokuwa akija, nikajaribu kumfananisha na Yule aliyekuja kwetu, akiomba tumpe kazi miezi michache nyuma.


Basi alipokaribia nikanyanyuka nikasema, ‘Hujambo, Ewe mfalme!’
Akajibu, ‘Sijambo, Makumazahn, mimi ni mfalme kwa nguvu za mikono yenu.’ Akatuarifu kuwa mambo yote yanaendelea vizuri, naye alitumaini kufanya karamu baada ya juma mbili apate kuonekana mbele ya watu wake.


Nikamuuliza atamfanya nini Yule Gagula, akajibu, ‘Yeye ni kama waziri mwovu katika nchi, na lazima nimuue, pamoja na wachawi wote.


Ameishi sana duniani, hata hapana anayejua miaka mingapi, naye ndiye aliyewafundisha wachawi wote na kufanya nchi iwe mbaya mbele ya Mungu.’
Nikajibu, ‘Kweli, lakini anayo maarifa mengi, na ni rahisi kuharibu maarifa kuliko ‘kuyapata!’


Akajibu, ‘Kweli, ni yeye peke yake ajuaye siri ya Wale Watatu Walio Kimya, na palipozikwa wafalme.’ Nikasema, ‘Ndiyo, na usisahau kuwa almasi zipo. Usisahau, Ignosi, yale uliyoahidi kuwa utatuongoza mpaka mashimo ya almasi, hata kama itakulazimu umwache Gagula aishi.’ Akajibu, ‘Mimi siwezi kusahau, Makumazahn, nami nita yafikiri maneno uliyosema.’


Ignosi alipoondoka nilikwenda kumtazama Bwana Good, nikamkuta ameshikwa na homa kali sana. Kwa siku mbili tulifikiri kuwa lazima atakufa, tukawa na mioyo mizito sana, lakini Foulata hakukubali, akasema kuwa lazima atapona.


Usiku wa tano wa ugonjwa wake nilikwenda kumtazama usiku kabla ya kwenda kulala, nikaingia chumbani pole pole sana, na kwa mwangaza wa taa nilimwona Bwana Good, lakini hakuwa akigaagaa kama siku zote, alilala kimya kabisa. Basi nilifikiri huu ndio mwisho, na nilikaribia kulia kwa uchungu.


Mara nilisikia sauti, ‘Sh! Sh!’ Nikatambua nikaenda karibu nikaona kuwa amelala usingizi wala hakufa, Alilala hivyo kwa muda wa saa kumi na nane, na wakati huo wote ameshika mkono wa Foulata, naye hakuweza kuondoka kwa sababu aliogopa atamwamsha.

Akakaa hivi bila kujinyosha na bila kula; lakini kwa kweli alipoamka ikawa lazima kumchukua, maana hakuweza kwenda kwa sababu viungo vyake vilikufa ganzi.
 
Baada ya hivi, hakukawia kupona, lakini Bwana Henry hakumwambia habari za vitendo vya Foulata mpaka alipokuwa karibu ya kupona. Bwana Good akasema, ‘Mwambie kuwa ameniokoa, nami sitasahau kabisa wema wake.’


Nikamwambia Foulata maneno aliyosema Bwana Good na Foulata akafurahi sana, akamtazama kwa macho ya mapenzi akasema, ‘Sivyo, bwana, labda bwana wangu amesahau kuwa yeye ndiye aliyeokoa maisha yangu, na mimi ni kijakazi wa Bwana.’


Baada ya siku chache Ignosi akafanya baraza kuu akakubaliwa na wakubwa wote wa nchi. Ikawa sherehe kubwa sana, na askari wale waliobaki katika jeshi lile la Wajivu waliwekwa mbele wakapewa shukrani za mfalme kwa kazi nzuri na ushujaa waliofanya katika vita.

Kila mtu alipewa zawadi ya ng’ombe na wote wakapandishwa kuwa wakubwa katika jeshi jipya ambalo vile vile liliitwa kwa jina la Wajivu.


Tena Ignosi alithibitisha maneno yale aliyotuahidi, mbele ya watu wote, yaani, watu hawatauawa tena bila ya kuhukumiwa, naya kuwa desturi ile ya kuwafichua wachawi itakoma mara moja.


Baraza ilipovunjika tulimsuburi Ignosi tukamwambia kuwa sasa tuna hamu ya kuzifichua siri zile za Mashimo yale ya Sulemani ambayo yalikuwepo mwisho wa Njia Kuu ya Sulemani; tukamuuliza kama amekwisha pata habari yoyote, akajibu, ‘Rafiki zangu, nimepata habari kuwa ni pale wanapokaa Wale Watatu Walio Kimya, ambao Twala alitaka kumuua Foulata awe ndiye mhanga wao.


Tena ni pale katika shimo kubwa wafalme wanapozikwa; ndipo mtakapoona maiti ya Twala amekaa pamoja na wale waliomtangulia. Na hapo lipo shimo lililokwenda chini sana lililochimbuliwa na watu wa zamani sana, labda kwa makusudio ya kutafuta mawe ya thamani uliyotaja.


Hapo ndipo Mahali pa Mauti, na humo kuna chumba ambacho hakijulikani. Ila na mfalme na Gagula. Twala alikijua lakini sasa amekufa, nami sikijui, wala sijui nini kilichomo.

Lakini imesimuliwa kuwa zamani mtu mweupe alivuka milima, akaongozwa na mwanamke mmoja, akaonyeshwa chumba kile cha siri, akaonyeshwa hazina.


Lakini kabla hawajaweza kuzichukua, akampitia kinyume na kuwaambia adui zake, akafukuzwa na mfalme wa wakati ule, na tangu siku ile hapana mtu aliyeingia katika mahali hapo.’


Nikasema, ‘Hadithi hiyo ni ya kweli Ignosi, maana tuliona maiti ya huyo mtu katika milima.’ Akajibu, ‘Ndiyo, tulimwona, na sasa nimeahidi kuwa kama mnaweza kukifikia chumba hicho, mna ruhusa kuchukua mawe yale ikiwa yapo.’

Nikasema, ‘Hicho kito unachovaa juu ya kipaji cha uso kila siku chathibitisa kuwa yapo.’ Akasema, ‘Labda, kama yapo mnayo ruhusa kuchukua kadiri mnayotaka, yaani ikiwa ni lazima mniache, ndugu zangu.

’Nikasema, ‘Lazima, lazima tukitafute hicho chumba .’ Akajibu, ‘Yupo mtu mmoja tu anayeweza kutuonyesha, naye ni Gagula.’

Nikasema, ‘Na kama hatakubali kutuonyesha itakuwaje?’
Akasema, ‘Basi atakufa. Nimemwacha hai kwa kusudio hilo tu. Tumwite tuone kama atakubali.’

Akatuma mtu kumwita. Baada ya kitambo akaletwa na askari huku akiwatukana. Mfalme akamwambia askari wamwache, na mara alipoachiliwa akakaa chini, na macho yake yakang’aa kama kito, akasema, ‘Wataka nini kwangu, Ignosi? Huthubutu kunigusa, ukinigusa nitakuua papo hapo ulipokaa. Jihadhari na uchawi wangu.’

Ignosi akajibu, ‘We mbwa jike, uchawi wako haukumwokoa Twala, wala hauwezi kunidhuru mimi.

Sikiliza, nataka utwambie habari za siri za mawe yale yanayong’aa’.
Gagula akacheka, akasema, ‘Ha!Ha! Hapana ajuaye ila mimi nijuaye siri hizo, nami sitakwambia kamwe.

Mashetani weupe hawa watakwenda zao mikono mitupu.’
Ignosi akasema, ‘Lazima utaniambia. Nitakushurutisha.’ Akajibu, ‘Kwa namna gani, Ewe mfalme? Wewe kweli ni mkubwa mwenye nguvu lakini nguvu zako zinawezaje kuukamua ukweli kutoka kwa mwanamke?’


Ignosi akajibu, ‘Najua ni vigumu, lakini nitafanya.’ Gagula akasema, ‘Ndiyo, lakini kwa namna gani?’ Ignosi akasema, ‘Hivi, ikiwa huniambii, utakufa kwa mateso ya pole pole.’
Gagula akalia, akasema, ‘Kufa? Hutothubutu kunigusa; wewe hujui mimi ni nani.


Umri wangu wadhani ni miaka mingapi? Mimi niliwajua baba za baba za baba zako. Nchi ilipokuwa mpya, mimi nilikuwapo; nchi itakapokuwa imechakaa mimi nitakuwapo. Siwezi kufa ila kuuawa kwa ajali, maana hapana anayethubutu kuniua.’


Ignosi akajibu, ‘Ndiyo, lakini nakwambia kuwa mimi nitakuua.’ Akashika mkuki wake akamsimamia juu tayari. Yule kizee akasema, ‘Sitakuonyesha kabisa; huwezi kuthubutu kuniua, huwezi kabisa. Atakayeniua mimi atalaaniwa milele.’


Pole pole Ignosi akashusha mkuki hata ncha yake ilimchoma kidogo, na mara Gagula akaruka juu kwa sauti kali, kisha akaanguka chini akagaagaa, huku akisema, ‘Basi, basi, niachilie niishi nami nitakuonyesha.’


Ignosi akasema, ‘Vema. Nilihisi’ kuwa nitapata njia ya kukufanya ukubali. Kesho utafuatana na Infadus na ndugu zangu weupe, kuwaonyesha hapo mahali, na uangalie sana usifanye makosa, maana usipowaonyesha, hakika utakufa.’


Yule kizee akajibu, ‘Sitakosa, Ignosi. Ni desturi yangu kutimiza niliyoahidi. Ha!Ha!Ha! Zamani mwanamke mmoja alimwonyesha mtu mweupe kile chumba na tazama! Alipatikana na maovu. Jina lake lilikuwa Gagula vile vile.


Labda mimi na huyo mwanamke ni mmoja.’ Na mcho yake maovu yalizidi kung’aa.
Nikasema, ‘Mwongo, hayo yalitokea zamani vizazi kumi nyuma.’


Akasema, ‘Labda, labda; mtu akiishi miaka mingi pengine husahau. Labda lilikuwa jina la mama yangu nayeye aliniambia, kwa hakika jina lake lilikuwa Gagula vie vile. Lakini, angalieni, nawaambia ya kuwa katika chumba kile yalipo hayo mawe, mtaona kifuko cha ngozi kimejaa mawe meupe.


Huyo mtu alijaza kifuko hicho, lakini hakuwahi kukichukua. Alipatikana na maovu , nasema alipatikana na maovu! Labda aliyeniambia alikuwa mama wa mama yangu! Itakuwa safari ya furaha.


Tutapita katika mahali walipopigana askari juzi, tutaona maiti waliokufa katika vita. Macho yao yatakuwa yamekwisha pofuka sasa, na mbavu zao zitakuwa zimekwisha bonyeka. Ha! Ha!Ha!’
 
Baada ya hivi, hakukawia kupona, lakini Bwana Henry hakumwambia habari za vitendo vya Foulata mpaka alipokuwa karibu ya kupona. Bwana Good akasema, ‘Mwambie kuwa ameniokoa, nami sitasahau kabisa wema wake.’


Nikamwambia Foulata maneno aliyosema Bwana Good na Foulata akafurahi sana, akamtazama kwa macho ya mapenzi akasema, ‘Sivyo, bwana, labda bwana wangu amesahau kuwa yeye ndiye aliyeokoa maisha yangu, na mimi ni kijakazi wa Bwana.’


Baada ya siku chache Ignosi akafanya baraza kuu akakubaliwa na wakubwa wote wa nchi. Ikawa sherehe kubwa sana, na askari wale waliobaki katika jeshi lile la Wajivu waliwekwa mbele wakapewa shukrani za mfalme kwa kazi nzuri na ushujaa waliofanya katika vita.

Kila mtu alipewa zawadi ya ng’ombe na wote wakapandishwa kuwa wakubwa katika jeshi jipya ambalo vile vile liliitwa kwa jina la Wajivu.


Tena Ignosi alithibitisha maneno yale aliyotuahidi, mbele ya watu wote, yaani, watu hawatauawa tena bila ya kuhukumiwa, naya kuwa desturi ile ya kuwafichua wachawi itakoma mara moja.


Baraza ilipovunjika tulimsuburi Ignosi tukamwambia kuwa sasa tuna hamu ya kuzifichua siri zile za Mashimo yale ya Sulemani ambayo yalikuwepo mwisho wa Njia Kuu ya Sulemani; tukamuuliza kama amekwisha pata habari yoyote, akajibu, ‘Rafiki zangu, nimepata habari kuwa ni pale wanapokaa Wale Watatu Walio Kimya, ambao Twala alitaka kumuua Foulata awe ndiye mhanga wao.


Tena ni pale katika shimo kubwa wafalme wanapozikwa; ndipo mtakapoona maiti ya Twala amekaa pamoja na wale waliomtangulia. Na hapo lipo shimo lililokwenda chini sana lililochimbuliwa na watu wa zamani sana, labda kwa makusudio ya kutafuta mawe ya thamani uliyotaja.


Hapo ndipo Mahali pa Mauti, na humo kuna chumba ambacho hakijulikani. Ila na mfalme na Gagula. Twala alikijua lakini sasa amekufa, nami sikijui, wala sijui nini kilichomo.

Lakini imesimuliwa kuwa zamani mtu mweupe alivuka milima, akaongozwa na mwanamke mmoja, akaonyeshwa chumba kile cha siri, akaonyeshwa hazina.


Lakini kabla hawajaweza kuzichukua, akampitia kinyume na kuwaambia adui zake, akafukuzwa na mfalme wa wakati ule, na tangu siku ile hapana mtu aliyeingia katika mahali hapo.’


Nikasema, ‘Hadithi hiyo ni ya kweli Ignosi, maana tuliona maiti ya huyo mtu katika milima.’ Akajibu, ‘Ndiyo, tulimwona, na sasa nimeahidi kuwa kama mnaweza kukifikia chumba hicho, mna ruhusa kuchukua mawe yale ikiwa yapo.’

Nikasema, ‘Hicho kito unachovaa juu ya kipaji cha uso kila siku chathibitisa kuwa yapo.’ Akasema, ‘Labda, kama yapo mnayo ruhusa kuchukua kadiri mnayotaka, yaani ikiwa ni lazima mniache, ndugu zangu.

’Nikasema, ‘Lazima, lazima tukitafute hicho chumba .’ Akajibu, ‘Yupo mtu mmoja tu anayeweza kutuonyesha, naye ni Gagula.’

Nikasema, ‘Na kama hatakubali kutuonyesha itakuwaje?’
Akasema, ‘Basi atakufa. Nimemwacha hai kwa kusudio hilo tu. Tumwite tuone kama atakubali.’

Akatuma mtu kumwita. Baada ya kitambo akaletwa na askari huku akiwatukana. Mfalme akamwambia askari wamwache, na mara alipoachiliwa akakaa chini, na macho yake yakang’aa kama kito, akasema, ‘Wataka nini kwangu, Ignosi? Huthubutu kunigusa, ukinigusa nitakuua papo hapo ulipokaa. Jihadhari na uchawi wangu.’

Ignosi akajibu, ‘We mbwa jike, uchawi wako haukumwokoa Twala, wala hauwezi kunidhuru mimi.

Sikiliza, nataka utwambie habari za siri za mawe yale yanayong’aa’.
Gagula akacheka, akasema, ‘Ha!Ha! Hapana ajuaye ila mimi nijuaye siri hizo, nami sitakwambia kamwe.

Mashetani weupe hawa watakwenda zao mikono mitupu.’
Ignosi akasema, ‘Lazima utaniambia. Nitakushurutisha.’ Akajibu, ‘Kwa namna gani, Ewe mfalme? Wewe kweli ni mkubwa mwenye nguvu lakini nguvu zako zinawezaje kuukamua ukweli kutoka kwa mwanamke?’


Ignosi akajibu, ‘Najua ni vigumu, lakini nitafanya.’ Gagula akasema, ‘Ndiyo, lakini kwa namna gani?’ Ignosi akasema, ‘Hivi, ikiwa huniambii, utakufa kwa mateso ya pole pole.’
Gagula akalia, akasema, ‘Kufa? Hutothubutu kunigusa; wewe hujui mimi ni nani.


Umri wangu wadhani ni miaka mingapi? Mimi niliwajua baba za baba za baba zako. Nchi ilipokuwa mpya, mimi nilikuwapo; nchi itakapokuwa imechakaa mimi nitakuwapo. Siwezi kufa ila kuuawa kwa ajali, maana hapana anayethubutu kuniua.’


Ignosi akajibu, ‘Ndiyo, lakini nakwambia kuwa mimi nitakuua.’ Akashika mkuki wake akamsimamia juu tayari. Yule kizee akasema, ‘Sitakuonyesha kabisa; huwezi kuthubutu kuniua, huwezi kabisa. Atakayeniua mimi atalaaniwa milele.’


Pole pole Ignosi akashusha mkuki hata ncha yake ilimchoma kidogo, na mara Gagula akaruka juu kwa sauti kali, kisha akaanguka chini akagaagaa, huku akisema, ‘Basi, basi, niachilie niishi nami nitakuonyesha.’


Ignosi akasema, ‘Vema. Nilihisi’ kuwa nitapata njia ya kukufanya ukubali. Kesho utafuatana na Infadus na ndugu zangu weupe, kuwaonyesha hapo mahali, na uangalie sana usifanye makosa, maana usipowaonyesha, hakika utakufa.’


Yule kizee akajibu, ‘Sitakosa, Ignosi. Ni desturi yangu kutimiza niliyoahidi. Ha!Ha!Ha! Zamani mwanamke mmoja alimwonyesha mtu mweupe kile chumba na tazama! Alipatikana na maovu. Jina lake lilikuwa Gagula vile vile.


Labda mimi na huyo mwanamke ni mmoja.’ Na mcho yake maovu yalizidi kung’aa.
Nikasema, ‘Mwongo, hayo yalitokea zamani vizazi kumi nyuma.’


Akasema, ‘Labda, labda; mtu akiishi miaka mingi pengine husahau. Labda lilikuwa jina la mama yangu nayeye aliniambia, kwa hakika jina lake lilikuwa Gagula vie vile. Lakini, angalieni, nawaambia ya kuwa katika chumba kile yalipo hayo mawe, mtaona kifuko cha ngozi kimejaa mawe meupe.


Huyo mtu alijaza kifuko hicho, lakini hakuwahi kukichukua. Alipatikana na maovu , nasema alipatikana na maovu! Labda aliyeniambia alikuwa mama wa mama yangu! Itakuwa safari ya furaha.


Tutapita katika mahali walipopigana askari juzi, tutaona maiti waliokufa katika vita. Macho yao yatakuwa yamekwisha pofuka sasa, na mbavu zao zitakuwa zimekwisha bonyeka. Ha! Ha!Ha!’
Pamoja sana mkuu
 
mzee baba ...imeishiaa patamuu daa ..fanya mambo yako basiii ..ovaa tunafuatiliaa tamthiliaa za startv ......
 
Baada ya hivi, hakukawia kupona, lakini Bwana Henry hakumwambia habari za vitendo vya Foulata mpaka alipokuwa karibu ya kupona. Bwana Good akasema, ‘Mwambie kuwa ameniokoa, nami sitasahau kabisa wema wake.’


Nikamwambia Foulata maneno aliyosema Bwana Good na Foulata akafurahi sana, akamtazama kwa macho ya mapenzi akasema, ‘Sivyo, bwana, labda bwana wangu amesahau kuwa yeye ndiye aliyeokoa maisha yangu, na mimi ni kijakazi wa Bwana.’


Baada ya siku chache Ignosi akafanya baraza kuu akakubaliwa na wakubwa wote wa nchi. Ikawa sherehe kubwa sana, na askari wale waliobaki katika jeshi lile la Wajivu waliwekwa mbele wakapewa shukrani za mfalme kwa kazi nzuri na ushujaa waliofanya katika vita.

Kila mtu alipewa zawadi ya ng’ombe na wote wakapandishwa kuwa wakubwa katika jeshi jipya ambalo vile vile liliitwa kwa jina la Wajivu.


Tena Ignosi alithibitisha maneno yale aliyotuahidi, mbele ya watu wote, yaani, watu hawatauawa tena bila ya kuhukumiwa, naya kuwa desturi ile ya kuwafichua wachawi itakoma mara moja.


Baraza ilipovunjika tulimsuburi Ignosi tukamwambia kuwa sasa tuna hamu ya kuzifichua siri zile za Mashimo yale ya Sulemani ambayo yalikuwepo mwisho wa Njia Kuu ya Sulemani; tukamuuliza kama amekwisha pata habari yoyote, akajibu, ‘Rafiki zangu, nimepata habari kuwa ni pale wanapokaa Wale Watatu Walio Kimya, ambao Twala alitaka kumuua Foulata awe ndiye mhanga wao.


Tena ni pale katika shimo kubwa wafalme wanapozikwa; ndipo mtakapoona maiti ya Twala amekaa pamoja na wale waliomtangulia. Na hapo lipo shimo lililokwenda chini sana lililochimbuliwa na watu wa zamani sana, labda kwa makusudio ya kutafuta mawe ya thamani uliyotaja.


Hapo ndipo Mahali pa Mauti, na humo kuna chumba ambacho hakijulikani. Ila na mfalme na Gagula. Twala alikijua lakini sasa amekufa, nami sikijui, wala sijui nini kilichomo.

Lakini imesimuliwa kuwa zamani mtu mweupe alivuka milima, akaongozwa na mwanamke mmoja, akaonyeshwa chumba kile cha siri, akaonyeshwa hazina.


Lakini kabla hawajaweza kuzichukua, akampitia kinyume na kuwaambia adui zake, akafukuzwa na mfalme wa wakati ule, na tangu siku ile hapana mtu aliyeingia katika mahali hapo.’


Nikasema, ‘Hadithi hiyo ni ya kweli Ignosi, maana tuliona maiti ya huyo mtu katika milima.’ Akajibu, ‘Ndiyo, tulimwona, na sasa nimeahidi kuwa kama mnaweza kukifikia chumba hicho, mna ruhusa kuchukua mawe yale ikiwa yapo.’

Nikasema, ‘Hicho kito unachovaa juu ya kipaji cha uso kila siku chathibitisa kuwa yapo.’ Akasema, ‘Labda, kama yapo mnayo ruhusa kuchukua kadiri mnayotaka, yaani ikiwa ni lazima mniache, ndugu zangu.

’Nikasema, ‘Lazima, lazima tukitafute hicho chumba .’ Akajibu, ‘Yupo mtu mmoja tu anayeweza kutuonyesha, naye ni Gagula.’

Nikasema, ‘Na kama hatakubali kutuonyesha itakuwaje?’
Akasema, ‘Basi atakufa. Nimemwacha hai kwa kusudio hilo tu. Tumwite tuone kama atakubali.’

Akatuma mtu kumwita. Baada ya kitambo akaletwa na askari huku akiwatukana. Mfalme akamwambia askari wamwache, na mara alipoachiliwa akakaa chini, na macho yake yakang’aa kama kito, akasema, ‘Wataka nini kwangu, Ignosi? Huthubutu kunigusa, ukinigusa nitakuua papo hapo ulipokaa. Jihadhari na uchawi wangu.’

Ignosi akajibu, ‘We mbwa jike, uchawi wako haukumwokoa Twala, wala hauwezi kunidhuru mimi.

Sikiliza, nataka utwambie habari za siri za mawe yale yanayong’aa’.
Gagula akacheka, akasema, ‘Ha!Ha! Hapana ajuaye ila mimi nijuaye siri hizo, nami sitakwambia kamwe.

Mashetani weupe hawa watakwenda zao mikono mitupu.’
Ignosi akasema, ‘Lazima utaniambia. Nitakushurutisha.’ Akajibu, ‘Kwa namna gani, Ewe mfalme? Wewe kweli ni mkubwa mwenye nguvu lakini nguvu zako zinawezaje kuukamua ukweli kutoka kwa mwanamke?’


Ignosi akajibu, ‘Najua ni vigumu, lakini nitafanya.’ Gagula akasema, ‘Ndiyo, lakini kwa namna gani?’ Ignosi akasema, ‘Hivi, ikiwa huniambii, utakufa kwa mateso ya pole pole.’
Gagula akalia, akasema, ‘Kufa? Hutothubutu kunigusa; wewe hujui mimi ni nani.


Umri wangu wadhani ni miaka mingapi? Mimi niliwajua baba za baba za baba zako. Nchi ilipokuwa mpya, mimi nilikuwapo; nchi itakapokuwa imechakaa mimi nitakuwapo. Siwezi kufa ila kuuawa kwa ajali, maana hapana anayethubutu kuniua.’


Ignosi akajibu, ‘Ndiyo, lakini nakwambia kuwa mimi nitakuua.’ Akashika mkuki wake akamsimamia juu tayari. Yule kizee akasema, ‘Sitakuonyesha kabisa; huwezi kuthubutu kuniua, huwezi kabisa. Atakayeniua mimi atalaaniwa milele.’


Pole pole Ignosi akashusha mkuki hata ncha yake ilimchoma kidogo, na mara Gagula akaruka juu kwa sauti kali, kisha akaanguka chini akagaagaa, huku akisema, ‘Basi, basi, niachilie niishi nami nitakuonyesha.’


Ignosi akasema, ‘Vema. Nilihisi’ kuwa nitapata njia ya kukufanya ukubali. Kesho utafuatana na Infadus na ndugu zangu weupe, kuwaonyesha hapo mahali, na uangalie sana usifanye makosa, maana usipowaonyesha, hakika utakufa.’


Yule kizee akajibu, ‘Sitakosa, Ignosi. Ni desturi yangu kutimiza niliyoahidi. Ha!Ha!Ha! Zamani mwanamke mmoja alimwonyesha mtu mweupe kile chumba na tazama! Alipatikana na maovu. Jina lake lilikuwa Gagula vile vile.


Labda mimi na huyo mwanamke ni mmoja.’ Na mcho yake maovu yalizidi kung’aa.
Nikasema, ‘Mwongo, hayo yalitokea zamani vizazi kumi nyuma.’


Akasema, ‘Labda, labda; mtu akiishi miaka mingi pengine husahau. Labda lilikuwa jina la mama yangu nayeye aliniambia, kwa hakika jina lake lilikuwa Gagula vie vile. Lakini, angalieni, nawaambia ya kuwa katika chumba kile yalipo hayo mawe, mtaona kifuko cha ngozi kimejaa mawe meupe.


Huyo mtu alijaza kifuko hicho, lakini hakuwahi kukichukua. Alipatikana na maovu , nasema alipatikana na maovu! Labda aliyeniambia alikuwa mama wa mama yangu! Itakuwa safari ya furaha.


Tutapita katika mahali walipopigana askari juzi, tutaona maiti waliokufa katika vita. Macho yao yatakuwa yamekwisha pofuka sasa, na mbavu zao zitakuwa zimekwisha bonyeka. Ha! Ha!Ha!’
Leo Mkuu umetuweka sana shusha mzigo tunausubiri Kwa hamu sanaa
 
Back
Top Bottom