Haijawahi tokea, ni kufuru! Yanga yachangiwa zaidi ya tiketi elfu 30 kutoka kwa Rais, Wizara, viongozi, Mabenki, na bado zoezi linaendelea

Waliofanya hivyo wanawafahamu mashabiki wa Yanga vizuri kwa hiyo point yangu iko pale pale.
Hii ni mechi ya fainali, ni zaidi ya kilele cha wiki ya wananchi. Kama wiki ya wananchi tu uwanja kwa kiasi kikubwa sembuse fainali ya CAF ambapo tokea uwanja wa Mkapa umejengwa ndio fainali pekee ndani ya ardhi ya Tanzania. Umetumia kiungo gani kufikiria?
 
Ndiyo point yangu ilipo hapo. Mechi nyingi tu za Yanga mlijaza uwanja hata kama siyo 60K, sasa kwa nini mnaona fahari sana kununuliwa tiketi na kwa nini hawa watu/taasisi wameona njia sahihi ni kuwanunulia tiketi watu ambao wameonyesha uwezo wa kujinunulia? Jibu unalo au kama hauna litafakari utalipata.

Mngekuwa wajanja mngewaambia BMT badala ya kununua tiketi ambazo mlikuwa na uhakika wa kuziuza, wasichukue makato yao katika mechi kubwa 3 mtakazoamua nyie, mngewaambia Wizara au Serikali hivyo hivyo lakini hamna ubavu wala labda kwa bahati mbaya akili hizo.

Kuna mengi zaidi ningekwambia ila ngoja nione kwanza haya utayapokeaje.
 
Dah
 
Najiuliza watatumia vigezo gani kuwapa mashabiki tiketi?
 
Ubavu mngeanza nyie kwanza kuuonesha siku ambayo mnapewa milioni mia plus katika milioni 400 plus. Simba na Yanga hawana uwanja wao hivyo hawana ubavu wa kuwapangia serikali nini cha kufanya kuhusu hilo. Mbona wadau walikuwa wanapiga kelele Simba wamenyonywa kwa yale mapato lakini hatukusikia kiongozi yeyote wa Simba kaleta fyoko fyoko. Usijitoe akili na kujifanya mjuaji kuliko.
 
Ukatae ujinga, nakufunza ujanja dogo, sikiliza ninachokwambia. Sana sana tingisha tu kichwa kuonyesha unanielewa.

Na mimi point yangu toka mwanzo ilihusiana na mashabiki, wewe unaleta habari za viongozi. Umeaminishwa mnaendeshwa sijui kisomi wakati kuna wajanja wachache wanaokula na wanasiasa ndiyo wameteka timu, wengine mmebaki mnasherehekea kununuliwa tiketi. Mfanyabiashara anayejielewa muda wote atajiuliza "hili ndiyo dili bora ninayoweza kufanya na watu hawa?"

Mmebaki tu mnaimba GSM! GSM! kama mmerukwa akili. Umeona wapi mdhamini wa timu anashangiliwa na mashabiki wa timu inapofunga goli?
 
Wenye wivu wajinyonge.
Sio kila hater anakomolewa kwa kumtambia mafanikio yako.

Kuna haters washapita kwenye hatua kubwa zenye ubora wa juu kuliko hiyo level yako ambayo wewe unaona ni prestige kumvimbia
 
we jamaa ndio huna unachokijua...

hiyo fainali, itasemwa si tu na vyombo vya habari vya ndani bali hata vya nje... juzi tu hapa habari zilikuwa ni kuhusu marumo kununua tiketi zote, hayo yametokea huko ila habari zipo afrika yote...

sasa basi hiyo fainali baadhi ya taasisi wanatumia kama marketing, ni kama kulipia tangazo la kutangaza biashara yako kwa gharama hizo... hivyo ni jambo la kawaida sana katika masuala hayo ya soka kuona taasisis inanunua tiketi badala ya mashabiki.... acha uzwazwa na kufikiri kimaskini maskini kwamba watu hawana uwezo wa kununua tiketi hadi wanunuliwe kichwa panzi wewe
 
Fainali imepoooooooza utadhani pilau lisilo tiwa chumvi.
Limepooza kwasababu hawana uhakika.

We hukuona ike siku wamepangwa na Rivers walianza kushangilia?

Hiyo ilimaanisha wamejipima uwezo dhidi ya mpinzani wao wakaona wanammudu na ndio maana wakawa wanafurahi.

Huyu mpinzani wa saizi hakadiriwi kiboya lazima wachukue caution kabisa na kuacha Polimilai
 
Hao wana siasa ndio unawaona leo kwenye mechi za Yanga? Mara ngapi humu mlikuwa mnaleta uzi wa kupinga viongozi wenu kuwaletea viongozi wa kisiasa kama mgeni rasmi kwenye michezo yenu ya kimataifa? Kuna mechi ilichezwa ya Simba huku mabango na T shirt za raisi Samia zikiwa zitalindima uwanjani. Swala la siasa katika soka letu halianzia kwa Yanga na pia halijaanzia leo.

Hizo tiketi zimekuuma sana eeh? Yanga ni taasisi na taasisi yoyote inakuwa na viongozi ndio wanaratibu kila jambo. Viongozi wangekataa kununuliwa kwa tiketi, mashabiki wangejua nini cha kufanya. Hivyo mashabiki ni watu wa kusikiliza viongozi wamebariki jambo fulani au lah. Mbona unajitia aibu kwa mambo madogo hivyo! Ni hizo taasisi wametumia kama fursa kwao kujitangaza kupita mchezo mkubwa wa ngazi za vilabu Africa.
 
Mumshauri muddy wenu achangie japo moextra energy kwa mashabiki au hata Maji tu....aonyeshe uzalendo....

Yeye ni mfanyabiashara na hii ni fursa, hii ni mechi ya kitaifa,

Aweke Kando ushabiki.....achangie hata Maji tu...tutayanywa
Bwana wee mechi ya kitaifa itakuwa hii?

Nyie nendeni hiyo jumapili mkawatie hasara waliotoa hela zao za tickets baadaye mje na maneno ya "mpira una matokeo matatu"
 
Yanga imewafanya muwehuke haswa mashabiki wa Simba. Yaani mpo hatua mbaya sana ya kurukwa na akili, Sasa tiketi 500,000 mashabiki wakakae kwenye uwanja vipi wakati uwezo wa uwanja ni watu 60,000 pekee?
Ukiangalia ni typing errors tu huoni hapo sifuri zipo 4 halafu iyo comma imewekwa eneo lisilo sahihi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…