Haikutokea enzi za Nyerere, Mwinyi, Mkapa wala Kikwete, bali enzi za Magufuli na Samia, wananchi kushangilia vifo na kujeruhiwa viongozi na waandamizi

Haikutokea enzi za Nyerere, Mwinyi, Mkapa wala Kikwete, bali enzi za Magufuli na Samia, wananchi kushangilia vifo na kujeruhiwa viongozi na waandamizi

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Katika siku za mwisho za uhai wake, akiwa hospitali Uingereza na alipotembelewa na Mkapa, Nyerere alimwambia hivi Mkapa, "Benjamin, najua Watanzania watalia sana watakaposikia nimekufa"

Na Nyerere alipokufa ni kweli Watanzania tulilia sana. Tulilia pia alipokufa Waziri Mkuu wa enzi hizo, Edward Sokoine.

Watanzania tulilia sana pia alipokufa Dr. Omar Juma chini ya Raisi Mkapa, na tayari tulikuwa katika mfumo wa vyama vingi. Tulilia pia alipokufa Deo Filikunjombe wa CCM. Tulilia bila kujali itikadi zetu za siasa. Tumelia kifo cha Mkapa na Mwinyi, na tukijua hawakuhusikika na mambo ya sasa.

Katika uhai wake, akigusia uwezekano wa kifo chake, Magufuli hakusema Watanzania watalia sana, alisema mtanikumbuka. Naona alijitambua. Hapo ndipo mambo yalipoanza kubadilika. Magufuli alipokufa kuna Watanzania walilia sana, lakini pia wapo wengine walishangilia sana!

Na sasa imekuwa mtindo unaoendelea chini ya Raisi Samia. Kiongozi wa serikali au waandamizi wanapopoteza maisha au kujeruhiwa, tunashuhudia wananchi wengi wakishangilia sana!

Sasa ni bora serikali ya sasa chini ya Raisi Samia ijiulize sana, kwa nini imekuwa hivi? Kwa nini leo wananchi wakisikia polisi amepigwa au amekufa wanashangilia? Kwa nini wakisikia maofisa wa TRA wamepigwa na wengine kufa wanashangilia? Kwa nini wananchi wakisikia basi lililobeba wabunge limepata ajali na wabunge kuumia wanashangilia? Kwa nini wananchi wanatoa maoni kama kutamani kifo cha baadhi ya viongozi na waandamizi? Kwa nini hali hazikuwa hivi wakati wa Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete?

Kuanzia Raisi wetu, tuje Makamu wa Raisi, Waziri mkuu, Mawaziri wote, Spika wa Bunge na wabunge wote, IGP, Polisi kiongozi wa kanda ya DSM, Ma RPC na askari Polisi wote kwa ujumla, TISS, TRA; juilizeni, hivi leo Watanzania wakisikia nimepoteza maisha, watashangilia au kulia sana? Kwa nini? Ndugu zenu mtakaowaacha watajisikiaje kuona watu watajisikiaje wakati wa msiba kuona watu wanashangilia kufa kwenu?

Karibu wote nyie, mtapata jibu kuwa mkifa watanzania wengi tu watashangilia sana! Si jambo jema lakini huo ndio ukweli. Jitafakarini na kutambua kuna kitu mnafanya hakipo sawa, mnapaswa kubadilika! Mnapaswa kuwarudisha wananchi wa Tanzania mahali ambapo wakisikia mmepoteza maisha basi walie sana, bila kujali itikadi zao za kisiasa! Huo ndio Utanzania halisi, na kama umetokweka wenye makosa ni nyie!
 
Nasisistiza: kuanzia Raisi wetu, tuje makamu wa Raisi, waziri mkuu, mawaziri wote, spika wa Bunge na wabunge wote, IGP, Polisi kiongozi wa kanda ya DSM, Ma RPC na askari polisi wote kwa ujumla, TISS, TRA; juilizeni, hivi leo Watanzania wakisikia nimepoteza maisha, nimekufa, watashangilia au kulia sana? Kwa nini? Ndugu zenu mtakaowaacha watajisikiaje wakati wa msiba kuona watu wanashangilia kufa kwenu?

Halafu nyie TRA mnaingizwa tu kwenye bifu msilohusika kwa kimbelembele chenu na kwa kuwa watu hawampendi waziri wenu. Mjue hilo. Hizi ni nyakati za hatari, kaeni upande sahihi.
 
Hakuna Raisi muuaji nchi hii kama Nyerere
Alimuua nani? Kambona, Chipaka na Kamaliza?

Kumbuka, hata wanajeshi wa kesi ya uhaini waliotaka kumpindua na kumuua, Nyerere aliwapuuza tu. Sijui kama unajua mmojawapo alikuwa huyu mfadhili wa Simba aliekufa juzijuzi, Hans Pope? Nchi nyingine angeishia six feet under kwa kupanga kumuua raisi.

Angalia wakati wa Rais Samia Mbowe karibu aozee mahabusu kwa kesi ya kutunga tu ya uhaini, na Samia akaridhia Mbowe kukaa ndani muda wote ule, wala moyo haumuumi kwamba kuna mtu katengwa na familia yake kwa ufitini tu usio na mshiko, halafu watu tunaona ni sawa tu.
 
Alimuua nani? Kambona, Chipaka na Kamaliza?

Kumbuka, hata wanajeshi wa kesi ya uhaini waliotaka kumpindua na kumuua, Nyerere aliwapuuza tu. Sijui kama unajua mmojawapo alikuwa huyu mfadhili wa Simba aliekufa juzijuzi?
Cap. Hans Pope
 
Ubongo wako unamaji mengi,huna kumbukumbu wewe hata kidogo na ndio tatizo la watanzania wengi hasa wana chadema

USSR
 
Kuna viongozi wakifa lazima watu wafungue champagne kufurahia. Ndiyo tulipofikia
 
Ubongo wako unamaji mengi,huna kumbukumbu wewe hata kidogo na ndio tatizo la watanzania wengi hasa wana chadema

USSR
Jibu kwa hoja zenye point. Acha kuropoka kuthibitisha wewe ni mmojawapo wa wenye tatizo la afya ya akili. Kila ubongo lazima uwe na maji, la sivyo utakufa. Kwani wa kwako hauna maji?
 
Kuna viongozi wakifa lazima watu wafungue champagne kufurahia. Ndiyo tulipofikia
Hasa katika kipindi hiki cha Raisi Samia, unfortunately! Na waziri fulani namuona, watu wakisikia amekufa siku hiyo bia zitaadimika! Maana wanaonyesha kuchukia hadi watoto wake wanasema wananuka dola😀
 
Katika siku za mwisho za uhai wake, akiwa hospitali Uingereza na alipotembelewa na Mkapa, Nyerere alimwambia hivi Mkapa, "Benjamin, najua Watanzania watalia sana watakaposikia nimekufa"

Na Nyerere alipokufa ni kweli Watanzania tulilia sana. Tulilia pia alipokufa Waziri Mkuu wa enzi hizo, Edward Sokoine.

Watanzania tulilia sana pia alipokufa Dr. Omar Juma chini ya Raisi Mkapa, na tayari tulikuwa katika mfumo wa vyama vingi. Tulilia pia alipokufa Deo Filikunjombe wa CCM. Tulilia bila kujali itikadi zetu za siasa. Tumelia kifo cha Mkapa na Mwinyi, na tukijua hawakuhusikika na mambo ya sasa.

Katika uhai wake, akigusia uwezekano wa kifo chake, Magufuli hakusema Watanzania watalia sana, alisema mtanikumbuka. Naona alijitambua. Hapo ndipo mambo yalipoanza kubadilika. Magufuli alipokufa kuna Watanzania walilia sana, lakini pia wapo wengine walishangilia sana!

Na sasa imekuwa mtindo unaoendelea chini ya Raisi Samia. Kiongozi wa serikali au waandamizi wanapopoteza maisha au kujeruhiwa, tunashuhudia wananchi wengi wakishangilia sana!

Sasa ni bora serikali ya sasa chini ya Raisi Samia ijiulize sana, kwa nini imekuwa hivi? Kwa nini leo wananchi wakisikia polisi amepigwa au amekufa wanashangilia? Kwa nini wakisikia maofisa wa TRA wamepigwa na wengine kufa wanashangilia? Kwa nini wananchi wakisikia basi lililobeba wabunge limepata ajali na wabunge kuumia wanashangilia? Kwa nini wananchi wanatoa maoni kama kutamani kifo cha baadhi ya viongozi na waandamizi? Kwa nini hali hazikuwa hivi wakati wa Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete?

Kuanzia Raisi wetu, tuje Makamu wa Raisi, Waziri mkuu, Mawaziri wote, Spika wa Bunge na wabunge wote, IGP, Polisi kiongozi wa kanda ya DSM, Ma RPC na askari Polisi wote kwa ujumla, TISS, TRA; juilizeni, hivi leo Watanzania wakisikia nimepoteza maisha, watashangilia au kulia sana? Kwa nini? Ndugu zenu mtakaowaacha watajisikiaje kuona watu watajisikiaje wakati wa msiba kuona watu wanashangilia kufa kwenu?

Karibu wote nyie, mtapata jibu kuwa mkifa watanzania wengi tu watashangilia sana! Si jambo jema lakini huo ndio ukweli. Jitafakarini na kutambua kuna kitu mnafanya hakipo sawa, mnapaswa kubadilika! Mnapaswa kuwarudisha wananchi wa Tanzania mahali ambapo wakisikia mmepoteza maisha basi walie sana, bila kujali itikadi zao za kisiasa! Huo ndio Utanzania halisi, na kama umetokweka wenye makosa ni nyie!
Short memories
 
Hakuna Raisi muuaji nchi hii kama Nyerere
Nyerere hakuua mna kalilishwa. Katika kipindi chake cha uongozi robo karne alimtia sahihi ya kunyongwa mtu mmoja tu aliyeitwa Abdalah Mwamwindi. Huyu jamaa Alimuua aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Wilbert Kreluu. Miaka ya 70 huko. Kama akina Mkemia Pius Mutakubwa Rugangila, uncle Tom, Mcghee Capt. Kadege na Capt. Tamim (huyu aliuwawa alikataa kukamata 'Kiboya' kwani alikuwa commando. Wengine wote kwenye kesi ya uhaini hawakunyongwa. Acha hao hata akina Chipaka na Bibi Titi Nyerere hakuwauwa. Nyerere was a a man of integrity and humour.
 
Viongozi wa siku hizi wengi ni waonevu na dhulumati wa haki za raia.
 
Nyerere hakuua mna kalilishwa. Katika kipindi chake cha uongozi robo karne alimtia sahihi ya kunyongwa mtu mmoja tu aliyeitwa Abdalah Mwamwindi. Huyu jamaa Alimuua aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Iringa Dr Wilbert Kreluu. Miaka ya 70 huko. Kama akina Mkemia Pius Mutakubwa Rugangila, uncle Tom, Mcghee Capt. Kadege na Capt. Tamim (huyu aliuwawa alikataa kukamata 'Kiboya' kwani alikuwa commando. Wengine wote kwenye kesi ya uhaini hawakunyongwa. Acha hao hata akina Chipaka na Bibi Titi Nyerere hakuwauwa. Nyerere was a a man of integrity and humour.
Hawawezi kukuelewa. Na mbaya zaidi hata hawakuwapo enzi za Nyerere, walikuwa hawajazaliwa
 
Viongozi wa siku hizi wengi ni waonevu na dhulumati wa haki za raia.
Ukishajiwekea mazingira ya kufanya ufisadi, inabidi ulinde himaya yako kwa kufanya dhulumati na kunyima watu haki zao, hata pamoja na haki ya kuishi!
 
Kwa akili kama hizi utaacha kushangilia hata kama ungekuwa wewe?!
download.jpeg
 
Back
Top Bottom