Haiwezekani Mungu asimuue Shetani halafu aamuru Watu waue wanaofanya mambo ya kishetani; Haiingii akilini

Haiwezekani Mungu asimuue Shetani halafu aamuru Watu waue wanaofanya mambo ya kishetani; Haiingii akilini

Shetani ana vipawa katika level ya juu kama malaika so anacho kipawa kikubwa kikubwa kama daraja la malaika ...Chanzo ni kudharau kumsujudia mwanadamu ambaye kwa kuumbwa kwake na kuona uwezo wa vipawa vya binadamu akadharau akaona hana uwezo wa kumsujudia dongo...Kitu ambacho hajui mwanadamu alipewa kipawa cha "AKILI" na "MATAMANIO" chini ya nafsi ili kujua lip baya na lip xuri...Ndo maana Mtume alilazimishwa kusoma kwa vile alipewa akili kama binadamu wengine.

Binadamu ana kipawa cha akili pamoja kuongoza wanyama na vitu vyote vilivyopo ardhini na majini ila kiakili ndo maana binadamu anajua uwezo wa wanyama wa bahari kwa kufanya utafiti pia anaweza kumvua hata mnyama mkali kama papa hata nyangumi akiamua ,Na wanyama hata simba unakuta kakamatwa kawekwa kweny zoo na binadamu....Angalia tu neema ya ngo'omb wakubwa hata 10 unaweza kukuta wanapelekwa machungani na kijana mdogo mfani jamii za wamasai.


Wanyama hawa hawana akili ndo wlaivyoumbwa hata baadhi yao wengi wanaweza kuzaa na wazazi wao ...wapo wapo tu duniani ndo level ya kipawa cha ila Mungu anawapa uwezo mdogo wa kujitafuria riziki na makazi na pia akatengeneza mtegemeano (Food web) iliw waweze kukizi vyakula vyao kutoka kwa wanyama wenzao , misituni (nyasi)au binadamu ( mazao waolima)
Na hapohapo tunaambiwa hakuna wa kusujudiwa ila Mungu, iweje Mungu amuamuru Shetani kumsujudia Adam? Contradictions juu ya contradictions argghhh 😬😬😬
 
Mtoa mada umejiabisha kwa hiki ulicho kiandika! Nadhani hujui lengo la kuwepo hapa katika hii Dunia ?? That why unaandika Kila kinachokujia katika akili yako bila kuchuja???

Watatokea watu kukupongeza kwa ulicho andika ila na wao ni pia sio watu wanaofikiria sawa sawa

Hapa tatizo lako ni Moja tu .ni kuwa humjui mungu WA mweli uwezo wake upoje ???

Hapa shetan anaepoteza wanadamu ni yule aliekataa kumsujudia NABII adamu na Sio mwengine na huyo baada ya kufukuzwa na Allah aliomba kwamba Allah asimuue Hadi mwisho WA ulimwengu ( kama Kuna kitu nimekosea naomba kurekebishwa)!

Huyu shetan au ibilis alimuapia Allah kuwa atawapoteza Wana adamu ili waingie wote moton siku ya kiyama . Ila Allah alimwambia waja wake hawawezi kupotezwa na ibilisi yaan shetwan

Note
Hadi hapa kama akili yako Ina akili basi utakuwa umeshaelewa SoMo hapa

Kwa mfano

Mwalimu anatoa mtihani labda form six
Kuna watakao Fanya vyema na Kuna watu watafanya average na Kuna watakao fell pia
Na lengo la mtihani watu wafaulu na Sio kufeli


Kwahiyo hapa Duniani ni kama mtihani tu Kuna watu watapatia na Kuna wengine watafeli

Na kufeli kunachagizwa na mambo mengi kama ulaji WA pombe ,kamari,zinaaa,wizi,fitna, ubasha, n.k


Mtoa mada unaposema shetani ndio mungu mwenyewe unakuwa unafeli pakubwa sana
Mungu hawez kuwa shetan na shetan hawezi kuwa mungu na hata ww unalijua Hilo sema tu unajizima data.

Hoja yako nyingine eti unataka watu wote tuwe aina Moja Yani wote tuwe wema ????

Hili hata mtoto wa darasa la kwanza anakuweka kando ! Ukishawai kwenda sokon ukakuta wanauza nyanya tu soko zima.????

Au ukakuta soko zima wanauza Infinix tu.???

Ni lazima utakuta mixer hapa Wala tusimsingizie mungu

Binadamu wote hatuwezi kuwa na fikra Moja kuwa tunawaza kitu kimoja ili tuwe wema wote
Na ndio maana Kuna moto na pepo

Ukifauli pepo ni yako na ukifeli moto ni wako

Maana tayar tulishaletewa manabii na mitume kuja kutuonya usimtaje shetani tu.

Note.

Rejea mfano WA mwalimu anapotoa mtihani lengo sio watu wafeli lengo ni kuwapima wanafunzi wake .kama lengo angetaka wafaulu wote basi huo mtihani angeutunga na kufanya mwenyewe .kama unavyotaka ww eti mungu amuue shetani ambae ndio huo mtihani alio wapa bina adamu ili kuwapima.


Alafu vijana WA siku hizi Wala hamna hamsomi visa vilivyopita kabla hili suala unaloleta ww lilishawai kuulizwa Enzo hizo za manabii na kama sikosei alikuwa NABII Musa.
 
Na hapohapo tunaambiwa hakuna wa kusujudiwa ila Mungu, iweje Mungu amuamuru Shetani kumsujudia Adam? Contradictions juu ya contradictions argghhh 😬😬😬
Hii ni kwamba alitaka kuonyesha malaika kwamba binadamu ni kiumbe bora zidi yao ...Ibilisi ndo alipogoma na kuona huyu kiumbe ana ubora gani sisi Mungu tunakuabudu leo hii tusujudie hili dongo ... Huyo dongo ntamkalia kila pande kama msalaba duniani ili asimuabudu Mungu na kusahau kuhusu Mungu.

Ni kweli binadamu ni mkubwa kwa vile angalia ni khalifah (kiongozi) wa vitu vyote duniani anaatawala
 
HAIWEZEKANI MUNGU ASIMUUE SHETANI ALAFU AAMURU WATU WAUE WANAOFANYA MAMBO YA KISHETANI; HAIINGII AKILINI!

Anaandika, Robert Heriel
Kuhani

Kwenye nyumba za ibada tangu tukiwa Watoto tulifundishwa kuna Wahusika Wawili mahasimu, wakwanza anaitwa MUNGU na wapili anaitwa SHETANI.

Mhusika Mungu huyu tuliambiwa ndiye Muumbaji wa Mbingu na Nchi, na ndiye Baba yetu (Chanzo chetu). Huyu tukaambiwa pia ni Mwema, mwenye upendo, nguvu na uweza. Chanzo chake hatujaelezewa, na hata wanaotuelezea habari zake hawajawahi kumuona. Hii ni kumaanisha hawajui anafananaje.

Mhusika Shetani huyu amepewa uhusika mbaya Kwa kusemekana alimuasi Mhusika MUNGU, asili ya Shetani wapo waliosema ni Jamii ya Malaika waitwao Makerubi, ambaye jina lake ni Lucifer. Wakati wengine wakidai Shetani au Ibilisi asili yake ni Kutoka Koo za majinni. Hii ni kusema Shetani ni kiumbe kilichoumbwa na Mungu. Ingawaje Stori hizi mbili hazijakamilika na zinaacha maswali mengi kuliko kilichoelezwa.

Lusifa kama aliasi, aliasi sheria ipi miongoni MWA sheria za Muumba wake huko Mbinguni?

Kabla hajaasi hiyo sheria ilitamka kuwa adhabu ya kuasi ni ipi?

Stori za Shetani zimeanzia juujuu na kuishia juujuu kama Stori za masela WA vijiweni. Yaani Stori imeanzia Kati na kuishi katikati.

Tukirudi kwenye Hoja.
Wasimulizi WA hizi dini zakuletwa na Waandishi wa vitabu vyao ambavyo vimeandika habari za huyo Mungu na Shetani Kwa uchache Mno, wakaja na sheria, ni kama sheria za biashara ya Market zile za Qnet. Unawekeza Kwa Imani pasipo kuuliza maswali yenye kufikiri, ATI hivyo ndio namna ya Kupata faida kwenye biashara.

Vitabu vya Dini vinaeleza kuwa Shetani ndiye chanzo cha dhambi, inakazia zaidi kuwa kila dhambi ifanywayo na binadamu chanzo chake ni Shetani kwani Shetani ndiye anayeshawishi Watu au viumbe kufanya Uasi.

Ukisoma kwenye Quran au Biblia yapo Makosa MTU akifanya anatakiwa kuuawa kama adhabu.
Mfano WA Makosa hayo ni kama kuua, kuwa Shoga au msagaji, kulala na mnyama, kuzini na mama mzazi au Baba mzazi au mkwe au mtoto wako. Kumkufuru Mungu na kuwa mchawi au mshirikina. Na Makosa mengine mengi yenye kustahili adhabu ya kifo Kwa mujibu wa vitabu vya Dini.

Swali linakuja, Ikiwa mhusika Mungu wa kwenye vitabu hivyo vya Dini, aliamuru Watu kuwaua Watu wenzao wanaofanya Makosa au dhambi nzito kama zilivyotajwa, ni Kwa nini huyu Mungu asingeshughulika na Shetani mwenyewe ambaye ndiye anawafanya Watu WAUE, wawe mashoga, na kufanya zinaa chafu ya kiwango cha juu?

Kwa sababu kama kweli Mungu hakutaka Dunia iwe na uovu kama ni kweli Kabisa basi ni dhahiri angedili na chanzo ambacho vitabu vya Dini vinamtaja ni mhusika Shetani.

Haiingii akilini badala ya kumuua Shetani ambaye ndiye chanzo cha Watu kufanya uovu mkubwa, ATI uwaamuru hao Watu wawaue Watu wenzao wanaofanya Matendo ya kishetani yaani wanaomfuata Shetani ambaye wamezaliwa wamemkuta na watakufa watamuacha. Hakuna mantiki kabisa ya Jambo Hilo.

Nafikiri Vitabu vya Dini vinashindwa kueleza ukweli Kati ya huu;
1. Binadamu ndio Shetani wenyewe. Lakini wametafuta Shetani bandia asiyeonekana ili wamsingizie.
Hoja hii haina nguvu Kwa sababu Mwanadamu hawezi kupambana na Mungu au Shetani yaani hawezi kupambana na matamanio yake yaliyomo katika Akili yake. Kwani matamanio na utashi ndio humuongoza MTU.

2. Mungu na Shetani ni Mhusika mmoja. Yaani Mungu ndiye Shetani na Shetani ndiye huyohuyo Mungu.
Vitabu vya Dini vinashindwa kuelezea ukweli huu labda Kwa kuogopa kuyafanya Maisha yataonekana hayana maana. Jambo ambalo nikweli kuwa Maisha ni ubatili.

Kama Mungu ndiye muumba wa yote na muweza WA yote tafsiri yake Ipo wazi kabisa.
Hii ni kusema, Mungu hawezi kumuua Shetani Wakati yeye ndiye huyohuyo Shetani. Na Shetani hawezi kumuua Mungu Wakati yeye ndiye huyohuyo Mungu.

Hoja hii inanguvu Kwa sababu, hata vitabu vya Dini vinaeleza kuwa Mungu aliumba Mema na Mabaya (ushetani) lakini akamwambia Mwanadamu achague Mema ili aweze kuishi.

Kumaanisha upande mzuri au Mwema wa Muumbaji wetu ndio wanadini waliuita Mungu na upande Mbaya wa Muumbaji wetu wakauita Shetani. Ni kama vile USO na kisogo ambavyo vyote vipo Kwa mhusika mmoja.

Haiwezekani Lusifa Awe Muasi hivihivi, lazima tujiulize huo Uasi ulitoka wapi ikiwa sio Kwa Muumbaji wake? Kwa sababu kiumbe hakina uwezo wa kuumba Jambo lolote liwe zuri au liwe Baya.

Taikon pumzika sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Ujuaji utakuponza
 
HAIWEZEKANI MUNGU ASIMUUE SHETANI ALAFU AAMURU WATU WAUE WANAOFANYA MAMBO YA KISHETANI; HAIINGII AKILINI!

Anaandika, Robert Heriel
Kuhani

Kwenye nyumba za ibada tangu tukiwa Watoto tulifundishwa kuna Wahusika Wawili mahasimu, wakwanza anaitwa MUNGU na wapili anaitwa SHETANI.

Mhusika Mungu huyu tuliambiwa ndiye Muumbaji wa Mbingu na Nchi, na ndiye Baba yetu (Chanzo chetu). Huyu tukaambiwa pia ni Mwema, mwenye upendo, nguvu na uweza. Chanzo chake hatujaelezewa, na hata wanaotuelezea habari zake hawajawahi kumuona. Hii ni kumaanisha hawajui anafananaje.

Mhusika Shetani huyu amepewa uhusika mbaya Kwa kusemekana alimuasi Mhusika MUNGU, asili ya Shetani wapo waliosema ni Jamii ya Malaika waitwao Makerubi, ambaye jina lake ni Lucifer. Wakati wengine wakidai Shetani au Ibilisi asili yake ni Kutoka Koo za majinni. Hii ni kusema Shetani ni kiumbe kilichoumbwa na Mungu. Ingawaje Stori hizi mbili hazijakamilika na zinaacha maswali mengi kuliko kilichoelezwa.

Lusifa kama aliasi, aliasi sheria ipi miongoni MWA sheria za Muumba wake huko Mbinguni?

Kabla hajaasi hiyo sheria ilitamka kuwa adhabu ya kuasi ni ipi?

Stori za Shetani zimeanzia juujuu na kuishia juujuu kama Stori za masela WA vijiweni. Yaani Stori imeanzia Kati na kuishi katikati.

Tukirudi kwenye Hoja.
Wasimulizi WA hizi dini zakuletwa na Waandishi wa vitabu vyao ambavyo vimeandika habari za huyo Mungu na Shetani Kwa uchache Mno, wakaja na sheria, ni kama sheria za biashara ya Market zile za Qnet. Unawekeza Kwa Imani pasipo kuuliza maswali yenye kufikiri, ATI hivyo ndio namna ya Kupata faida kwenye biashara.

Vitabu vya Dini vinaeleza kuwa Shetani ndiye chanzo cha dhambi, inakazia zaidi kuwa kila dhambi ifanywayo na binadamu chanzo chake ni Shetani kwani Shetani ndiye anayeshawishi Watu au viumbe kufanya Uasi.

Ukisoma kwenye Quran au Biblia yapo Makosa MTU akifanya anatakiwa kuuawa kama adhabu.
Mfano WA Makosa hayo ni kama kuua, kuwa Shoga au msagaji, kulala na mnyama, kuzini na mama mzazi au Baba mzazi au mkwe au mtoto wako. Kumkufuru Mungu na kuwa mchawi au mshirikina. Na Makosa mengine mengi yenye kustahili adhabu ya kifo Kwa mujibu wa vitabu vya Dini.

Swali linakuja, Ikiwa mhusika Mungu wa kwenye vitabu hivyo vya Dini, aliamuru Watu kuwaua Watu wenzao wanaofanya Makosa au dhambi nzito kama zilivyotajwa, ni Kwa nini huyu Mungu asingeshughulika na Shetani mwenyewe ambaye ndiye anawafanya Watu WAUE, wawe mashoga, na kufanya zinaa chafu ya kiwango cha juu?

Kwa sababu kama kweli Mungu hakutaka Dunia iwe na uovu kama ni kweli Kabisa basi ni dhahiri angedili na chanzo ambacho vitabu vya Dini vinamtaja ni mhusika Shetani.

Haiingii akilini badala ya kumuua Shetani ambaye ndiye chanzo cha Watu kufanya uovu mkubwa, ATI uwaamuru hao Watu wawaue Watu wenzao wanaofanya Matendo ya kishetani yaani wanaomfuata Shetani ambaye wamezaliwa wamemkuta na watakufa watamuacha. Hakuna mantiki kabisa ya Jambo Hilo.

Nafikiri Vitabu vya Dini vinashindwa kueleza ukweli Kati ya huu;
1. Binadamu ndio Shetani wenyewe. Lakini wametafuta Shetani bandia asiyeonekana ili wamsingizie.
Hoja hii haina nguvu Kwa sababu Mwanadamu hawezi kupambana na Mungu au Shetani yaani hawezi kupambana na matamanio yake yaliyomo katika Akili yake. Kwani matamanio na utashi ndio humuongoza MTU.

2. Mungu na Shetani ni Mhusika mmoja. Yaani Mungu ndiye Shetani na Shetani ndiye huyohuyo Mungu.
Vitabu vya Dini vinashindwa kuelezea ukweli huu labda Kwa kuogopa kuyafanya Maisha yataonekana hayana maana. Jambo ambalo nikweli kuwa Maisha ni ubatili.

Kama Mungu ndiye muumba wa yote na muweza WA yote tafsiri yake Ipo wazi kabisa.
Hii ni kusema, Mungu hawezi kumuua Shetani Wakati yeye ndiye huyohuyo Shetani. Na Shetani hawezi kumuua Mungu Wakati yeye ndiye huyohuyo Mungu.

Hoja hii inanguvu Kwa sababu, hata vitabu vya Dini vinaeleza kuwa Mungu aliumba Mema na Mabaya (ushetani) lakini akamwambia Mwanadamu achague Mema ili aweze kuishi.

Kumaanisha upande mzuri au Mwema wa Muumbaji wetu ndio wanadini waliuita Mungu na upande Mbaya wa Muumbaji wetu wakauita Shetani. Ni kama vile USO na kisogo ambavyo vyote vipo Kwa mhusika mmoja.

Haiwezekani Lusifa Awe Muasi hivihivi, lazima tujiulize huo Uasi ulitoka wapi ikiwa sio Kwa Muumbaji wake? Kwa sababu kiumbe hakina uwezo wa kuumba Jambo lolote liwe zuri au liwe Baya.

Taikon pumzika sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Mkuu huoni ni kipimo cha utii wa mema na mabaya? maana haiwezekani mwalimu wa chekechea akalipwa sawa na mwalimu wa chuo kikuu utalipwa kutokana na uelewa wako na ulivyotenda.
 
Nimesoma vizuri uzi huu changamoto kwamba auna elimu ya koroho ila umesoma sana theory. Watu wengi wanaopinga uwepo wa Mungu mmoja aliyeumba mbingu na nchi(Simaanishi wewe ila ni baadha ya watu) cha hajabu hao watu wengi ni madevil worshiped waabuduMashetani. Wanakataa uwepo wa Mungu lakini wanakubali uwepo wa shetani ambaye ndie baba yao.

Ukisoma Biblia kwa theory hasa Agano la kale utakuja kuona Mungu ni katili sana. Changamoto inakuja pale neno moja limetumika kwa maana tofauti tofauti kwenye biblia za kishwahili na kingeleza Tofauti ukisoma Biblia ya kiebrania utakuja kuona tofauti mkubwa sana hasa neno Mungu. Kwa asilimia kubwa agano la kale liliongozwa na malaika ndio walikuwa wakihitwa nano Mungu au Bwana,Yehofa au elohiym. Hata Musa mwenyewe hakukutana na Mungu bali alikutana na Malaika uso kwa uso.
Agano jipya kwa njia ya Yesu Kristo ndio aliyekuja kumfunua Mungu halisi katika tabia zake. Ndio maana ukisoma Agano jipya unakuja kuona Mungu ambaye siye katili na ni tofauti wa agano la kale katika Tabia ambazo kristo Yesu alivomfunua.
Tunaposema Yesu atumaanishi mwili bali ni roho ya Mungu iliyokuja kuvaa mwili wa kinadamu kwaiyo aijalishi angekuwa mweusi au mweupe lakini utabaki kua ni mwili tu.

Tunaposema Mungu ni Mungu mwenye haki wala yeye sio kigeugeu wala ajipingi wala kubadilika. Sio Mungu aliyluhusu watu wauwane au watu wawauwe wale wanaompinga yeye na kumkubali shetani.

Mungu aliwaumba wanyama na malaika pamoja na mbingu na nchi kwa ajiri ya kumiliki na kutawala binadamu only. Malaika aitwae Lucifer kabla ajawa shetani alikuwa ni malaika mwema tu aliyemfanya Mungu kwa ajiri ya kumtumikia binadamu lakini kwa utashi wa lusifa aliasi yaani alitoka kwenye nafasi yake ya kutumika kwa wanadamu bali yeye ndio alitamani atumikiwe na viumbe vingine kitu ambacho akiwezekani.

Binadamu pekee ndio aliyepewa uwezo mkubwa wa akili kuliko viumbe vyote. Ndiomaana hao malaika walioasi yaani walioacha wajibu wao wa kumlinda binadamu wanatumia hila kumlubuni binadamu lakini kiukweli hata hao waabudu mashetani ni wajinga na wapumbavu sanaaana wanawaabudu wafanya kazi wao.
Shetani anauwezo wa kutoa utajiri isipokuwa anatumia uwezo wa mwanadamu uwo uwo kukutengenezea wewe utajiri.

Kwaiyo ndugu mtoa uzi tafuta biblia na tafsiri za kiebrania, kiyunani na kigiriki ndio utakuja kupata majibu kamili.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Hiyo ya chini sikuungi mkono inakuja unakataa kukaa kichwani.

Kusema Mungu ndiye shetan and vice versa ni kufuru bro.

Mungu hawez kuwa shetan kwasababu wewe mwenyewe umethibitisha Mungu alimuumba shetani... Hivyo haiwezekan mtu kujitengeneza chenyewe mfano.

Mwalimu anatengeneza Daktar ambapo daktar atabaki daktar na mwalimu atabaki mwalimu
Hiyo ya chini sikuungi mkono inakuja unakataa kukaa kichwani.

Kusema Mungu ndiye shetan and vice versa ni kufuru bro.

Mungu hawez kuwa shetan kwasababu wewe mwenyewe umethibitisha Mungu alimuumba shetani... Hivyo haiwezekan mtu kujitengeneza chenyewe mfano.

Mwalimu anatengeneza Daktar ambapo daktar atabaki daktar na mwalimu atabaki mwalimu
Hamna kufuru yoyote hapo sema imani yako ulivyo fundishwa ukiwa mtoto ndio inakupa fikra hizo. Ukweli ni kwamba Mungu na shetani ni pande mbili za sarafu moja. Mfano wake ni kama betri au kifaa cha kutunzia umeme lazima kuwe na positive na negative charge hivo hivyo ni kama mungu hawezi kuwepo bila shetani kwaiyo ni juu yako kuchagua unataka kwenda upande upi.
 
Nimesoma vizuri uzi huu changamoto kwamba auna elimu ya koroho ila umesoma sana theory. Watu wengi wanaopinga uwepo wa Mungu mmoja aliyeumba mbingu na nchi(Simaanishi wewe ila ni baadha ya watu) cha hajabu hao watu wengi ni madevil worshiped waabuduMashetani. Wanakataa uwepo wa Mungu lakini wanakubali uwepo wa shetani ambaye ndie baba yao.

Ukisoma Biblia kwa theory hasa Agano la kale utakuja kuona Mungu ni katili sana. Changamoto inakuja pale neno moja limetumika kwa maana tofauti tofauti kwenye biblia za kishwahili na kingeleza Tofauti ukisoma Biblia ya kiebrania utakuja kuona tofauti mkubwa sana hasa neno Mungu. Kwa asilimia kubwa agano la kale liliongozwa na malaika ndio walikuwa wakihitwa nano Mungu au Bwana,Yehofa au elohiym. Hata Musa mwenyewe hakukutana na Mungu bali alikutana na Malaika uso kwa uso.
Agano jipya kwa njia ya Yesu Kristo ndio aliyekuja kumfunua Mungu halisi katika tabia zake. Ndio maana ukisoma Agano jipya unakuja kuona Mungu ambaye siye katili na ni tofauti wa agano la kale katika Tabia ambazo kristo Yesu alivomfunua.
Tunaposema Yesu atumaanishi mwili bali ni roho ya Mungu iliyokuja kuvaa mwili wa kinadamu kwaiyo aijalishi angekuwa mweusi au mweupe lakini utabaki kua ni mwili tu.

Tunaposema Mungu ni Mungu mwenye haki wala yeye sio kigeugeu wala ajipingi wala kubadilika. Sio Mungu aliyluhusu watu wauwane au watu wawauwe wale wanaompinga yeye na kumkubali shetani.

Mungu aliwaumba wanyama na malaika pamoja na mbingu na nchi kwa ajiri ya kumiliki na kutawala binadamu only. Malaika aitwae Lucifer kabla ajawa shetani alikuwa ni malaika mwema tu aliyemfanya Mungu kwa ajiri ya kumtumikia binadamu lakini kwa utashi wa lusifa aliasi yaani alitoka kwenye nafasi yake ya kutumika kwa wanadamu bali yeye ndio alitamani atumikiwe na viumbe vingine kitu ambacho akiwezekani.

Binadamu pekee ndio aliyepewa uwezo mkubwa wa akili kuliko viumbe vyote. Ndiomaana hao malaika walioasi yaani walioacha wajibu wao wa kumlinda binadamu wanatumia hila kumlubuni binadamu lakini kiukweli hata hao waabudu mashetani ni wajinga na wapumbavu sanaaana wanawaabudu wafanya kazi wao.
Shetani anauwezo wa kutoa utajiri isipokuwa anatumia uwezo wa mwanadamu uwo uwo kukutengenezea wewe utajiri.

Kwaiyo ndugu mtoa uzi tafuta biblia na tafsiri za kiebrania, kiyunani na kigiriki ndio utakuja kupata majibu kamili.

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
Hivi ulisha wahi kujiuliza kwanini wazungu wanagawa biblia bure, siyo tuu kugawa bali pia wametafsiri biblia kwa lugha zote mpaka za makabila yetu? Kwanini waarabu nao wanagawa misahafu au quran bure? Kwanini wasinge gawa na kutafsiri bure vitabu vya biolojia, kemia vitabu vya sayansi na hisabati? Usiamini sana hizo stori kaka wewe una uhakika huyo musa anakujua? Au musa atakusaidia nini ukifa kirefu cha biblia unakijua? Unajua hiyo biblia vitabu vingapi vimeondolewa na kwanini wameviondoa. Kuwa open minded kaka huyu mtu ameweka hii mada ili akukomboe ki fikra, emancipate yourself from mental slavery kaka
 
😂 uwezo ndo asili ya kipawa chake yaani ndo maana hata tukisema material ya uumbaji wao ni asili ya moto wakati binadamu ni udongo.

Shetani wameumbwa kuwa na uwezo mkubwa zaidi ya binadamu na wanaweza kumshawishi binadamu na binadamu ana akili ambaye anaanza kufikiria halafu ndo anatenda na binadamu huyo huyo anaweza kumkataa shetani kwa kutumia akili ...Huu ni uwezo pekee wa kila kiumbe .


Usifikirie hawa viumbe tunawachinja na kuwafuga ni kwamba hawa hawana uwezo dhidi ya binadamu hata wapewe maumbo makubwa kama nyangumi na Mungu amehalalisha wawe chini ya kiumbe mwanadamu na ulimwengu mzima kutumia akili mwanadamu atajua vyote vilivyopo pamoja na kuweza kuvicontrol...

Ndo maana ni haramu kumfananisha binadamu mwenzio kwa kumtusi jina la mnyama hata kumuita shetani kwani ni viumbe tofauti kama Mungu alivyoumba .


Sisi waislamu tuna sikukuu ya kuchinja si unaona hapa wanyama kama haki yao ya kuishi imedhalilishwa ili mwanadamu amle tu ...Hii ni kutokana na kipawa na heshima ya mwanadamu ipo juu dhidi ya wanyama.


The same shetani ana kipawa kikubwa kuliko mwanadamu kweny ushawishi except wanadamu amepewa akili ya kufikiria kabla ya kutenda..
Na sisi inawezekana ni mifugo kwa viumbe wenye mamlaka juu yetu,,,na ndio maana wanachukua roho zetu na uhai kama sisi tunavyofanya kwa hao wanyama tulio na mamlaka juu yao,,,Duniani hapa na sisi ni mifugo kwa hao viumbe walio na mamlaka juu yetu
 
Na sisi inawezekana ni mifugo kwa viumbe wenye mamlaka juu yetu,,,na ndio maana wanachukua roho zetu na uhai kama sisi tunavyofanya kwa hao wanyama tulio na mamlaka juu yao,,,Duniani hapa na sisi ni mifugo kwa hao viumbe walio na mamlaka juu yetu
😂😂
 
Mtoa mada umejiabisha kwa hiki ulicho kiandika! Nadhani hujui lengo la kuwepo hapa katika hii Dunia ?? That why unaandika Kila kinachokujia katika akili yako bila kuchuja???

Watatokea watu kukupongeza kwa ulicho andika ila na wao ni pia sio watu wanaofikiria sawa sawa

Hapa tatizo lako ni Moja tu .ni kuwa humjui mungu WA mweli uwezo wake upoje ???

Hapa shetan anaepoteza wanadamu ni yule aliekataa kumsujudia NABII adamu na Sio mwengine na huyo baada ya kufukuzwa na Allah aliomba kwamba Allah asimuue Hadi mwisho WA ulimwengu ( kama Kuna kitu nimekosea naomba kurekebishwa)!

Huyu shetan au ibilis alimuapia Allah kuwa atawapoteza Wana adamu ili waingie wote moton siku ya kiyama . Ila Allah alimwambia waja wake hawawezi kupotezwa na ibilisi yaan shetwan

Note
Hadi hapa kama akili yako Ina akili basi utakuwa umeshaelewa SoMo hapa

Kwa mfano

Mwalimu anatoa mtihani labda form six
Kuna watakao Fanya vyema na Kuna watu watafanya average na Kuna watakao fell pia
Na lengo la mtihani watu wafaulu na Sio kufeli


Kwahiyo hapa Duniani ni kama mtihani tu Kuna watu watapatia na Kuna wengine watafeli

Na kufeli kunachagizwa na mambo mengi kama ulaji WA pombe ,kamari,zinaaa,wizi,fitna, ubasha, n.k


Mtoa mada unaposema shetani ndio mungu mwenyewe unakuwa unafeli pakubwa sana
Mungu hawez kuwa shetan na shetan hawezi kuwa mungu na hata ww unalijua Hilo sema tu unajizima data.

Hoja yako nyingine eti unataka watu wote tuwe aina Moja Yani wote tuwe wema ????

Hili hata mtoto wa darasa la kwanza anakuweka kando ! Ukishawai kwenda sokon ukakuta wanauza nyanya tu soko zima.????

Au ukakuta soko zima wanauza Infinix tu.???

Ni lazima utakuta mixer hapa Wala tusimsingizie mungu

Binadamu wote hatuwezi kuwa na fikra Moja kuwa tunawaza kitu kimoja ili tuwe wema wote
Na ndio maana Kuna moto na pepo

Ukifauli pepo ni yako na ukifeli moto ni wako

Maana tayar tulishaletewa manabii na mitume kuja kutuonya usimtaje shetani tu.

Note.

Rejea mfano WA mwalimu anapotoa mtihani lengo sio watu wafeli lengo ni kuwapima wanafunzi wake .kama lengo angetaka wafaulu wote basi huo mtihani angeutunga na kufanya mwenyewe .kama unavyotaka ww eti mungu amuue shetani ambae ndio huo mtihani alio wapa bina adamu ili kuwapima.


Alafu vijana WA siku hizi Wala hamna hamsomi visa vilivyopita kabla hili suala unaloleta ww lilishawai kuulizwa Enzo hizo za manabii na kama sikosei alikuwa NABII Musa.

Atamsujudiaje Adamu Wakati sheria inasema wakusujudiwa ni MUNGU pekee?

Nini kilimfanya akatae, je Mungu hakujua atakataa,
Au Mungu ndio aliweka kukataa ndani ya Shetani?
 
Back
Top Bottom