Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kwa upendo ulitaka nimuachie Mil 8 aondoke nazo?Nguvu zote zinatoka kwa Mungu. Ndio kwa Wakristo tukaambiwa upendo ndio amri kuu. Hii amri ikiandamana na upendo nguvu itaelekezwa kwa mambo mema.
Wachache wataelewa hili. Ila mpaka hapo kuna jambo umejifunza.
Mbingu iko wapi? Huu ujinga hadi lini? Ukifa ukaonekana utazikwa, ukifia majini au au kuliwa na wanayama pori ndo basi. Huko mbinguni wanaendaje?Ukusaidie kwenda mbinguni kwa Mungu maana duniani hutozidi miaka 100
(From matai , Rukwa ? ) Liverpool VPN imetosha mkuu hongera sanaNi pisi moja Mfipa (From Matai, Rukwa).
Tulikula bata la asante pamoja..!!!
#YNWA
Mkuu vp huko matai kuna wataalam konki sana sio?(From matai , Rukwa ? ) Liverpool VPN imetosha mkuu hongera sana
Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
A.K.A Sumbawanga.(From matai , Rukwa ? ) Liverpool VPN imetosha mkuu hongera sana
Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
Wataalamu wamehama Sumbawanga mjini (MC), wamehamia Kalambo DC ndani ndani hukoo..!!!!Mkuu vp huko matai kuna wataalam konki sana sio?
Kalambo ni rukwa.mkuu?Wataalamu wamehama Sumbawanga mjini (MC), wamehamia Kalambo DC ndani ndani hukoo..!!!!
#YNWA
Yap.Kalambo ni rukwa.mkuu?
Duh hii ramani nitaihitaji kwa matumizi ya keshoYap.
Ni wilaya ya Rukwa.
Imemegwa kutoka wilaya ya Sumbawanga kipindi kile cha kuanzisha Wilaya ya mikoa mipya.
Kama sijakosea ilianza 2014 na makao makuu yalikuwa Sumbawanga mjini.
Magu alivyopiga biti kila halmashauri iende kwake ndio Kalambo ikaenda Matai, hivyo makao makuu ya Wilaya/Halmashauri yapo Matai.
Na inapakana na Wilaya ya Momba (Mkoa wa Songwe).
Kufika Matai Kuna boda unapitia Momba (Kasinde, mpakani na Zambia - Gari unapandia Tunduma) na Kuna boda la kawaida unapitia Sumbawanga mjini (gari unapandia Sumbawanga mjini).
#YNWA
Ndio maana mkuu nikasema wachache wataelewa na bahati mbaya sana mhusika pia hujaelewa. Nani kakwambia kumwachia mtu haki yako ni upendo? Upendo ni kupambania kile unachokipenda. Ukiachia utakuwa punguani na una-set precedence (cookies) za kupigwa mara kwa mara kwani huthamini mali zako. Hicho ulichofanya kupigania mali yako ni kwa kuwa unaipenda.Kwa upendo ulitaka nimuachie Mil 8 aondoke nazo?
Siwezi kuhubiri upuuzi ambao mimi mwenyewe sijaujaribu na kuuhakiki unafanya kazi. Hiyo nguvu niloisema unatakiwa uitumie kwa upendo sio kuumiza watu. Ukiwa na upendo ambayo ndio amri kuu hauwezi kuitumia hiyo nguvu kukandamiza haki za wengine. Mfano huyo mdeni wako angeingia kwa mganga kutafuta nguvu ya wewe ushindwe kumdai.Usiwe kama motivational speaker anayekuhubiria ujiajiri kupitia platform iliyomuajiri yeye..!!!
Sijawahi kuwa na sipendi kuwa speeker kuhamasisha watu. Labda siku nikiamua nitakuwa naita watu wa karibu kuwafanyia demo ya kile nakijua, kuamini na kufanyaKwa upendo ulitaka nimuachie Mil 8 aondoke nazo?
Hivi kama wewe ni mtumishi wa Umma unajua muda unaotakiwa mtumishi kusave ili afikishe Mil 8?
Mchukulie Mtu mwenye mshahara wa Kati ya TGS A mpaka TGS E.
Huyu ana majukumu na mambo mengine, ila aliamua kukomaa na kusave mil 8, halafu Leo jinga moja linaondoka na saving yotee kirahisiii...
Usiwe kama motivational speaker anayekuhubiria ujiajiri kupitia platform iliyomuajiri yeye..!!!
#YNWA
Hakimu hutoa nafasi ya Mshtakiwa kujitetea akihukumiwa, somasoma kesi magezetini utajua.Sawa ,, lakini naomba kujua ,, baada ya kusomwa hukumu kuna kujitetea na kupunguzi a adhabu? Maana wewe umesema alihukumiwa miez 3 jela na 6 nje Ila katika kujitetea akapunguziwa.
Mzee baba kauli mbiu yangu "USICHEZE NA HELA ZANGU"Sijawahi kuwa na sipendi kuwa speeker kuhamasisha watu. Labda siku nikiamua nitakuwa naita watu wa karibu kuwafanyia demo ya kile nakijua, kuamini na kufanya
Amen.Ndio maana mkuu nikasema wachache wataelewa na bahati mbaya sana mhusika pia hujaelewa. Nani kakwambia kumwachia mtu haki yako ni upendo? Upendo ni kupambania kile unachokipenda. Ukiachia utakuwa punguani na una-set precedence (cookies) za kupigwa mara kwa mara kwani huthamini mali zako. Hicho ulichofanya kupigania mali yako ni kwa kuwa unaipenda.
Siwezi kuhubiri upuuzi ambao mimi mwenyewe sijaujaribu na kuuhakiki unafanya kazi. Hiyo nguvu niloisema unatakiwa uitumie kwa upendo sio kuumiza watu. Ukiwa na upendo ambayo ndio amri kuu hauwezi kuitumia hiyo nguvu kukandamiza haki za wengine. Mfano huyo mdeni wako angeingia kwa mganga kutafuta nguvu ya wewe ushindwe kumdai.
Ndio hapo amri ya upendo ilipo. Upendo sio kuwa zoba unapigwa unaangalia tu kisa Mungu ni upendo. Basi utakuwa mjinga na sio upendo tena. Mungu mwenyewe aliye upendo alimtimua shetani baada ya kuingia kwenye anga zake.
Hii nguvu ni moja, na ipo inafanya kazi. Tunatakiwa kuitumia kwa upendo na sio chuki na uonevu.
Ok mkuu Mimi nilikuwa najua kwamba nafasi ya kujitetea hutangulia kabla ya kusomwa hukumu.Hakimu hutoa nafasi ya Mshtakiwa kujitetea akihukumiwa, somasoma kesi magezetini utajua.
Kwenye yangu nilimsikia hakimu anasema ""Mshtakiwa una lolote la kujitetea?""
Alijitetea; ana mke kajifungua hivi karibuni watoto mapacha, ana maana ake anaumwa, anaendesha biashara hivyo analipa kodi na kaajiri wengi.
Ndio nikaona hakimu akafuta miezi ya jela akamuachia ya nje.
Ina maana hakimu alishawishika na ushawishi/sababu za mshtakiwa.
#YNWA
Unajitetea kabla ya hukumu kupitia ushahidi tunaita hearing stage, ukihukumiwa pia unapewa fursa ya kujitetea upunguziwe adhabu tunaita mitigation.Ok mkuu Mimi nilikuwa najua kwamba nafasi ya kujitetea hutangulia kabla ya kusomwa hukumu.