Hakuna faida ya kumpeleka mtoto English Medium (mabasi ya njano)



Mleta mada hana uwezo wala ufahamu wa kujenga hoja kwa mtililiko wenye staha na kueleweka.

Unamuonea.
 
Uko sahihi mkuu hawa wa English medium japokuwa wanatumia pesa kubwa kusoma lakini mwisho wa siku tunakutana nao chuo kimoja na maisha yanaendelea, kwahyo tofauti haipo


Kukutana nao chuoni sio ajabu maana mnaishi nao mitaani na wengine ni ndugu zenu kabisa.


Tukitambua role ya Mazingira na vilivyomo ndani ya mazingira hayo katika kumjenga mtu ama kumbomoa mtu tutaelewa utofauti wa Elimu katika shule za Kiswahili na English Mediums.


Mfumo wa maisha haupo bahati mbaya, chagua kesho ya kizazi chako iliyo sahihi. Majuto ni Mjukuu.
 
Ila viwango vya ujinga na upumbavu vilivyo athiriwa na mfumo takataka wa elimu ya Tanzania wote vipo sawa baina ya anaesoma English medium na anaesoma Changamkeni.
Mkuu.. Em tafuta glass ya maji kwanza unywe.!! Hehh!!🤔🤔🤔
🤣🤣🤣

Povu kali Mnoo.
 
Uko sahihi !ila unavowasilisha hoja Yako ni kama una majuto flani ambayo yanafanya wewe pia uwe kwenye kundi la wanaohitaji msaada wa haraka,any way pole sana kaka, hii ndio TZ ,tukiyaangalia matatizo kwa jazba jua hatutaweza kuyatatua,maana walio juu hawashuguliki na hoja zenye jazba ndani yake,,,,uelevu unahitajika ,ili uwe mwelevu unatakiwa usiwe na hasira
 
Yani mi nawazumuu hawa akina LIKUD
nakosa majibu...

Sijui wanashindwa tembelea tu hizi kayumba wakajionee.
 
Uko sahihi mkuu hawa wa English medium japokuwa wanatumia pesa kubwa kusoma lakini mwisho wa siku tunakutana nao chuo kimoja na maisha yanaendelea, kwahyo tofauti haipo
😔😔🤭🤭🤭
 
Baada ya kuona amejua kuziandika one -twenty (kwa maneno) kwa usahihi nikamwambia aandike kwa kiswahili (moja-ishirini) haikumchukua dakika 20 aliunga herufi akapata zote. Mwambie huyo wa mchepuo wa kiswahili kama atakupa English na Kiswahili.
Kamwe usije msikiliza masikini wa akili.
Elimu bure ni umasikini wa miaka ijayo
 
Hongera mkuu kwa kufanya vizuri kwenye kozi ya mipasho.
 
Kibaya kwako ni kipi kati ya mfumo wa elimu na tabia ya baadhi yetu kupeleka watoto huko uliko taja kwenye heading yako?
 
Kamwe usije msikiliza masikini wa akili.
Elimu bure ni umasikini wa miaka ijayo
Wewe umuelewa km mimi nilivyo muelewa.
Mara nyingi mwenye uwezo mdogo wa kipato ama akili huwa ana tamani wanaomzidi waporomoke ili walingane ama wawe chini yake.
 
Mkuu wewe huna pesa acha kujifariji mimi siwezi kumpitisha mwanangu nilipopitia kama nina kipato.

1. 0SHIDA YA NAFASI
Darasa moja watoto 100 ufanisi uko wapi sasa.

2. Mazingira mabovu
Mazingira ni bovu mno mfano vyoo, majengo na mazingira ya kusomea

3. Shida ya usafiri.
Km za kutosha na changamoto za usafiri

Mengine watamalizia mkuu kama huna hela tujipe moyo.
 
Nilichogundua humu watu wengi wanatak mtu aish aonavyo yeye.......

Binafsi kwa dunia ya leo mtoto wako anahitaj kujua lugha kwa ufasaha hasa English...... Nina ndoto na wanangu lzm wasome academy nzurii waelewe lugha masomo, confident, wakutanee na watu tofaut ........

Nii kwelii hakuna ajira..... Ila km mzaz ukatoa hio negativity na kutafuta ela na kuwekeza kwa mwanao mshaur asome course marketable na applicable km BUSNESS ADMINISTRATION, ACCOUNTANT, ECONOMY, FINANCE, hata akifungua biashara ana uwezo wa kuiendesha anajua risks, how to overcome, anajua kuandaa portfolio zAke, profits en loss, tax n.k lkn km mzaz huna mawazo km haya unatak mtt asisome akae kweny duka moja miaka 20?

Ila km una ndoto na mwanao invest, physically, spiritually, mentally en financially
 
Watoto wako hao wakisha balehe na kuvunja ungo utajua kumbe kweli ulikuwa unaota ndoto.
 

Mnavyokuja na lawama mje pia na suluhisho sio maelezo mengi bila njia mbadala. Mi nawaunga mkono wanaopeleka watoto privet otherwise uniambie wanampeleka mtoto shule ili akaajiriwe na sio kupata elimu.
 
Mnavyokuja na lawama mje pia na suluhisho sio maelezo mengi bila njia mbadala. Mi nawaunga mkono wanaopeleka watoto privet otherwise uniambie wanampeleka mtoto shule ili akaajiriwe na sio kupata elimu.
Kupata elimu gani au makapi kwa kingereza ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…