Hakuna Kiingilio!! Kichekesho na utapeli wa mialiko ya mikutano ya injili

Hakuna Kiingilio!! Kichekesho na utapeli wa mialiko ya mikutano ya injili

Ndio maana naiomba serikali yetu ilitupie jicho suala hili. Ni utapeli umekuwapo miaka mingi bila kushughulikiwa. Taifa linafanywa la mazezeta. Ni aibu.
Serikali hizi zisizotimiza wajibu wao kwa wananchi, kwa maana ya kuweka mazingira bora ya huduma za kijamii..na zinazoingia madarakani kwa wizi wa kura usitarajie zikawashughulikia hao matapeli, maana lao ni moja..ndio maana unawaona ma RC kwenye hayo makongamano
 
Kwa nini basi mafundisho yao yamejikita kwenye kutoa tu. Hawafundishi hata elimu ya biblia na hostoria ya ukristo ni KUTOA KUTOA KUTOA basi!!
Ni Kwa sababu wewe unasubiri ifike wakati wa kutoa ili uje upige Umbea hapa...!
Aliyekwambia Mwamposa hafundishi Elimu ya Biblia ama Ukristo ni nani..!?

Acheni Unafiki...! Kama huamini endelea na kutoamini kwako, lakini sio kuongea Uongo...!

Unadhani wale Watu woote walijaa juzi pale zaidi ya 5,000 ni Mazuzu na wewe peke Yako ndo una Akili...!?
 
Huo ni utapeli. Neno kila mtu anaweza kutoa. Hao ni motivational speakers kwenye kichaka cha dini. Hakuna mtume wala nabii hapo upuuzi mtupu
kama wanaweza wafanye ruksa bado wajinga ni wengi sana
 
Utawasikia kwenye mialiko yao redioni, kwenye TV na vipeperushi watangaza mialiko uende kwenye makusanyiko yao wanasema hakuna kiingilio, kiingilio ni bure! Ukifika huko unahubiriwa habari za kutoa sadaka na madhara utakayopata kama hutoi! Unachotoa kinaingia kwenye mfuko wa mhubiri na mke/mume wake. Hivi taifa langu Tanzania nani amewaloga kuingia kwenye ujinga wa wa kuwaamini hawa matapeli? Tuwafundishe kiasi gani mpate kuelewa???

Mwaka 2017 nikiwa Nzuguni dodoma walipita mabinti2 na kijana mmoja wanagawa vipeperushi kuwa watakuwa na mkutano jpili ijayo. Walikuwa wanaenda nyumba kwa nyumba wanakualika then wanaacha vipeperushi vikitoa ratiba kamili kwaya zitakazo kuwepo pamoja na muhibiri ayenadiwa kuwa katoka ughaibuni huko.

Kipeperushi kile kilikuwa kinasema usafiri ni bure na chakula ni bure na kama haitoshi punde unapopanda kwenye gari lao unapewa 10k cash! Niliwaza sana bila kupata majibu nini maana ya hela hii halafu na chakula bure?

Basi siku ikafika wale mabinti wakapita tena mapema saa2 wanawakumbusha na kuwaambia magari yapo tiyari na yamefungwa mabango ya vitambaa. Nikasema wacha leo nami niende nikajionee hasa ile teni ya bure iwapo wasipo nipa nitarudia hapohapo stend nilioga nikavaa kisabato na saspenda zangu huyoo kituoni mkutano ulikuwa unafanyika mtaa jirani jina nimesahau unapita unakata kona pale ilipo shule ya martin luther inakuwa mkono wa kushoto unanyooka na barabara hiyo nayo ni lami pia.

Kweli nilipofika tu nikakuta wadada wengine wakaniribisha vizuri huku mmoja akinipa ile hela 10k mpyaa kabisa nikaichungulia kama ni og ama fake hadi wakacheka. Nikaitunza basi mimi sikuwa wa kwanza au wapili kwa muda ule na gari kama dk 8 ikajaa ikatupeleka mkishuka tu hivi chai ya maana.

Baadae kwaya zikaimba na nyimbo zikaibwa mahubiri ya kaanza hatimae wakuombewa wakaombewa.
ibada ikaisha tukarudi. Ukumbuke walikuwa wamechukua no za simu. na majina yetu mida ya saa1-2 nikapigiwa na mrembo mmoja sauti tamu kama ya watoa huduma wa voda.Nikaulizwa ibada yetu uliionaje uliopendezwa na kipi na ulikerwa na kipi? Nikasifia tukaongea hadi tukatoka kwenye maada ya mkutano tukaanza ulizana makazi yetu ya kudumu ni wapi then tukaagana.


Simu ziliendelea kupigwa kama kawaida na siku ya jmos ijayo walikuja tena vilevile wakihamasisha usafiri upo na chakula kipo na pesa mkononi ipo pia.

Kesho yake jpili nilienda tena kama kawaida sema yule mhubiri wao hakuwepo ila hela na vingine vilikuwepo kama kawaida. hadi nikatoka sikuwahi pata jibu kwanini walikuwa wanafanya hivi? sadaka nilitoa buku1 tu kila ibada ila muhamasishaji alikuwa anasema kadiri unavyotoa sadaka kubwa mungu anazidi kukubariki mara dufu. Kwangu mimi wala sikutishika.


Huwa najiuliza lengo la kanisa hili ilikuwa ni nini? makadirio kwa watu wale kama wote walipeqwa hela muhimu m7 ilisha ama zaidi hapo ni jpili moja tu achana na usafiri na chakula
 
Kama unataka kufuata maandiko peleka fungu la kumi Yerusalemu hekaluni. Kinyume na hapo umejitungia mafundisho yako mwenyewe kwamba kanisa ndio mbadala wa hekalu ambapo Mungu aliagiza sadaka zipelekwe. Wayahudi wenyewe waliopewa hilo agizo hawakupeleka fungu la kumi wala sadaka hata kwenye sinagogi ambayo wanatheolojia uchwara wanalifananisha na makanisa ya leo. Upumbavu tu na umbumbumbu wa kutokuijua imani ya kikristo na misingi yake. Wakimbieni matapeli.
Mie huwa sisali mkuu, ukiamua kwenda kanisani sadaka ni sehemu ya Ibadan, sasa unakwenda kufanya nini kama kwenye hela zinauma kutoa ila mengine unayafuata kanisani, hivyo vipaza sauti na viyoyozi vinavyotumika unadhani hela yake inatoka wapi. Mie sio mdini kihivyo ila nimeeleza kwa yale makanisa yanayosimama kama taasisi na sio haya yanayochipuka kama uyoga ya mitume ambapo mke na mume wote ni wachungaji na akaunti za bank zinasoma majina Yao.
 
Utawasikia kwenye mialiko yao redioni, kwenye TV na vipeperushi watangaza mialiko uende kwenye makusanyiko yao wanasema hakuna kiingilio, kiingilio ni bure! Ukifika huko unahubiriwa habari za kutoa sadaka na madhara utakayopata kama hutoi! Unachotoa kinaingia kwenye mfuko wa mhubiri na mke/mume wake. Hivi taifa langu Tanzania nani amewaloga kuingia kwenye ujinga wa wa kuwaamini hawa matapeli? Tuwafundishe kiasi gani mpate kuelewa???
Kuna dogo anaitwa IPM alianza kimasiala,sasaivi ana mawe dogo
 
Utawasikia kwenye mialiko yao redioni, kwenye TV na vipeperushi watangaza mialiko uende kwenye makusanyiko yao wanasema hakuna kiingilio, kiingilio ni bure! Ukifika huko unahubiriwa habari za kutoa sadaka na madhara utakayopata kama hutoi! Unachotoa kinaingia kwenye mfuko wa mhubiri na mke/mume wake. Hivi taifa langu Tanzania nani amewaloga kuingia kwenye ujinga wa wa kuwaamini hawa matapeli? Tuwafundishe kiasi gani mpate kuelewa???
Msenge wewe, kwenye matamasha ya miziki viingilio watu wanatoa na huo tuite ni utapeli ama
 
Mie huwa sisali mkuu, ukiamua kwenda kanisani sadaka ni sehemu ya Ibadan, sasa unakwenda kufanya nini kama kwenye hela zinauma kutoa ila mengine unayafuata kanisani, hivyo vipaza sauti na viyoyozi vinavyotumika unadhani hela yake inatoka wapi. Mie sio mdini kihivyo ila nimeeleza kwa yale makanisa yanayosimama kama taasisi na sio haya yanayochipuka kama uyoga ya mitume ambapo mke na mume wote ni wachungaji na akaunti za bank zinasoma majina Yao.
Makanisa yaliyokaa kitaasisi wala sina shida nayo japo mengi yana mapungufu ya Kitheolojia. Kule pesa inafanyiwa accounting siyo kutoa namba za kutuma pesa na jina ni la mhubiri na mke wake🤣
 
Ni Kwa sababu wewe unasubiri ifike wakati wa kutoa ili uje upige Umbea hapa...!
Aliyekwambia Mwamposa hafundishi Elimu ya Biblia ama Ukristo ni nani..!?

Acheni Unafiki...! Kama huamini endelea na kutoamini kwako, lakini sio kuongea Uongo...!

Unadhani wale Watu woote walijaa juzi pale zaidi ya 5,000 ni Mazuzu na wewe peke Yako ndo una Akili...!?
Kupindisha maandiko ili kujinufaisha binafsi ndiyo kufundisha elimu ya biblia au ni kuwapumbaza watu??
 
Kupindisha maandiko ili kujinufaisha binafsi ndiyo kufundisha elimu ya biblia au ni kuwapumbaza watu??
Kwa Hiyo kwa miaka yote Ibada zote mafundisho Huwa ni Sadaka tu....!?
Kutoa ni hiyari, Kuna kupokea kwenye kutoa....!

Kama wewe huamini endelea na mambo Yako.
Coz hata yanayowakuta wale wanaoenda Kwa Mwamposa huyajui, wanatoa Sadaka Kwa Imani Yao, huchangii hata 10, ila Maumivu unakuja kuyapata wewe.
 
Makanisa yaliyokaa kitaasisi wala sina shida nayo japo mengi yana mapungufu ya Kitheolojia. Kule pesa inafanyiwa accounting siyo kutoa namba za kutuma pesa na jina ni la mhubiri na mke wake🤣
Tupo pamoja mkuu
 
Kwa Hiyo kwa miaka yote Ibada zote mafundisho Huwa ni Sadaka tu....!?
Kutoa ni hiyari, Kuna kupokea kwenye kutoa....!

Kama wewe huamini endelea na mambo Yako.
Coz hata yanayowakuta wale wanaoenda Kwa Mwamposa huyajui, wanatoa Sadaka Kwa Imani Yao, huchangii hata 10, ila Maumivu unakuja kuyapata wewe.
Wewe huna uzalendo kwa taifa letu na unaona ni sawa tu kuacha wengine wakiangamia kisa ati sikutoa pesa zangu. Hiyo ni roho ya uharibifu wala si ukristo.
 
Wewe huna uzalendo kwa taifa letu na unaona ni sawa tu kuacha wengine wakiangamia kisa ati sikutoa pesa zangu. Hiyo ni roho ya uharibifu wala si ukristo.
Sadaka zenyewe unapigia kelele hapa ni hizi Coins za mia 5 mia 5....!?
 
Utawasikia kwenye mialiko yao redioni, kwenye TV na vipeperushi watangaza mialiko uende kwenye makusanyiko yao wanasema hakuna kiingilio, kiingilio ni bure! Ukifika huko unahubiriwa habari za kutoa sadaka na madhara utakayopata kama hutoi! Unachotoa kinaingia kwenye mfuko wa mhubiri na mke/mume wake. Hivi taifa langu Tanzania nani amewaloga kuingia kwenye ujinga wa wa kuwaamini hawa matapeli? Tuwafundishe kiasi gani mpate kuelewa???
Kwa hiyo tusitoe sadaka au tusiende kabisa makanisani?
 
Mkuu ni business model hiyo tena nzuri.
Business model nzuri ni ile ya kuwafanya watu waamini bidhaa ni bure kutumia kumbe in reality wanalipia.
Kama facebook, youtube, google models
Facebook, Google na YouTube unawalipa au unatumia bure?
 
Gharama zao atagharamia Mungu,au wafanye kama wametoa sadaka tu,


Wao si wanawaombea waumini wao kwa Mungu ili wafanikiwe? kwanini hao wachungaji nao wasisubiri kufanikiwa kupitia Mungu huyo huyo badala ya kuwakamua waumini ambao wengi wao ni masikini?
Wanaombewa wafanikiwe kupitia kazi zao, mchungaji naye atafanikiwa kupitia kazi yake ya uchungaji.
 
Back
Top Bottom