Hakuna kitu kinaleta Stress kama kuota Mvi au upara halafu bado hujajipata

Hakuna kitu kinaleta Stress kama kuota Mvi au upara halafu bado hujajipata

Mimi kila siku huwa nasema wewe ni kilaza. Unajua mtu aliyeanzisha KFC? Unajua alikuwa na miaka mingapi wakati anaanza? Wacha kukatisha vijana wa Tanzania tamaa. Kufanikiwa hakuna umri, kuna watu wanapiga mpaka miaka 80 ndiyo kinaeleweka.

Kilaza ni wewe ambaye upeo wako upo chini.
Unapotaja miaka 80 unajua Life Expectancy ya Watanzania?
Kwenye ukoo wenu ni wazee wangapi wamefikisha miaka 80?

Ukijadili hoja na mimi hakikisha wiki nzima umekunywa maziwa Fresh ili akili iwe active.

Wéwe unazungumzia Exceptional ndio únashikilia bango
 
mie nilanza kuota mvi nyingi nikiwa mwaka wa3 chuo na hazikua zinaonekana vizuri nilipomaliza na hivyo nilionekana bado mdogo nikashindwa kuaminiwa na wananchi nikapigwa chini...
Awamu ilofata mvi zilikua zimekomaa vizur kuanzia kidevuni na kushoto na kulia mwa kichwa...

Mvi zimenisaidia sana mpaka apa nilipo kwakweli ...

saivi nazipenda nahisi zinanipendeza pia nikijichek halafu,

ila kaupara kanawasha hatar 🐒
Hongera sana mkuu
H
 
Kilaza ni wewe ambaye upeo wako upo chini.
Unapotaja miaka 80 unajua Life Expectancy ya Watanzania?
Kwenye ukoo wenu ni wazee wangapi wamefikisha miaka 80?

Ukijadili hoja na mimi hakikisha wiki nzima umekunywa maziwa Fresh ili akili iwe active.

Wéwe unazungumzia Exceptional ndio únashikilia bango
Kwani hakuna watanzania wanapitisha miaka 80? Na hata kama hakuna hivi ulichoandika huoni ni ujinga mtupu na unafanya watu wakate tamaa baada ya umri fulani?
 
Ila kuna raha yake umri ukiendana na mipango yako, mfano ulipanga ukifika miaka 30 uwe na Kiota chako, Mke na Mtoto alafu unafikisha miaka 30 hivyo vyote unavyo hapo upara, Mvi, Mikunjo Usoni na ije tu... ila sio ulivyopanga vyote umefanikiwa kufikisha miaka 30 tu hapo Utosi lazima upate moto kimtindo
 
Kwani hakuna watanzania wanapitisha miaka 80? Na hata kama hakuna hivi ulichoandika huoni ni ujinga mtupu na unafanya watu wakate tamaa baada ya umri fulani?

Ñimekuuliza unajua life expectancy ya Tanzania NI ngapi?
Pili nikakuuliza kwenye ukoo wenu ni wangapi wametoboa hiyo miaka 80?

Tatu unajua nguvu kazi ya nchi ipo katika umri upi na upi?

Nne, unajua ni kwa nini kwenye kipengele cha kuomba kazi kuna kipengele cha umri?
Tano, unajua ni kwa nini mtu anatakiwa kustaafu akiwa na miaka 60?

Sikatishi mtu tamaa kwa sababu hata mimi naweza kuwa mhanga, kinachojadiliwa hapa ni uhalisia, ukweli uliowazi.

Sasa wewe unataka maneno matamu ya uongo ili kudanganya Watu wasichukue hatua?

Mimi ni Kilaza Mkuu.
 
Yaani ukiwajali na chochote ukipatacho raha sana.
Kwenye haya maisha hakuna chochote utakachokifanya au kukiacha cha thamani kuliko kuacha watoto(uzao).
Kuzaa ndio mafanikio makubwa kwa kiumbe yeyote kuliko kuwa na majumba, magari na viwanda.

Kuzaa ni kufanya maisha na uhai uendelee.

Jumba utakalojenga sasa hivi ni old fasheni kwa miaka 100 ijayo.
Gari utakalonunua hivi leo ni old fasheni kwa miaka 10 tuu ijayo.
Lakini watoto ulionao hivi leo hata ipite miaka 1000 hawawezi kuwa old fasheni kwani ni endless circle
L
Kuna case nyingi nimekutana nazo kuhusu vijana wanaokufa mapema huku wameacha mali .

Wazazi wao hupenda kuhoji huyu mtu Hana mtoto , hamumjui mwanamke aliyezaa nae kwenye pita pita zenu .

Kulikuwa na case Moja 18 yrs old tunduma huko alikufa kijana Kwa ajali ya boda boda , tulifika msibani mama mtu alikiwa akilia sana , huku akilalamika umeniacha peke yangu , hujaniachia mtoto /mjukuu all of sudden akaja Binti ni mjamzito akasema alikuwa na mahusiano na kijana wao , somehow alirelieve That momma's pain . Mpaka naondoka Binti alipokea malezi ya hadhi ya kifalme .. Mpaka anajifungua ..

Nikaconclude kama Taikon /namesake ulivyosema mafanikio makubwa ni kuwa na familia
 
Kwema Wakuu!

Ni Stress hapa!
Ni sonona hapa! Kihoro kinakaba kama pumu huku. Yaani hapa mambo sio mambo.

Kuna Watu wanakuambia umri ni number tuu lakini huko ni kufarijiana tuu!
Hakuna kitu kinauma na kuleta mfadhaiko na mtagusano kulinafsi kama kuona jua lile linazama halafu wewe mambo bilabila.

Nywele kunyonyoka kama mbwakoko mzee. Alafu ukicheki huna mbele wala nyuma sio Pouwa Washikaji.
Mvi kukuota wakati unaishi chumba kimoja sio lelemama ndugu zangu.

Fikiria mvi hizi hapa alafu huna hata mke wala mtoto. Kiumri ni miaka labda 35 hivi. Shida ni kuwa mpaka muda moja na mbili haikai.
Kila ukikumbuka ile kauli ya kusema nikiwa mkubwa nitafanya bla! Blah! Blah! Unapiga ngumi ukutani.
Nani akutake na mvi zako Budah! Yaani huna pesa alafu umejaza mvi kichwani. Ni binti gani yupo tayari kukubali kuwa nawe?
Binti gani atakubali kuwa na wewe na kipara chako na hauna Maisha.

wanasema vijana ndio huona maono bwashee! Wazee wenye mvi na vipara huota ndoto tuu. Yaani kila unaloliwaza kuna asilimia 70 kuwa ni ndoto uotayo ya alinacha.

Kipara sio shida. Shida ni pale huna mbele wala nyuma. Nyie ni mateso bila chuki. Hujui tawi gani ushike.
Yaani Upara na mvi vinakukuta ni Jobless mamaaaa! Hujui ufanye nini unafikiri Daah!

Unakipara chako kinamea polepole, au unamvi zako alafu huna pesa mbona lazima uwe introvert tuu. Yaani ndio ile unajikita mkimya maana nini sasa utaongea. Na hawa vijana wa 2000 hawana salia mtume, hawajui la muhazini wala mnadi Swala. Watakuona Babu yao ilhali hata miaka 40 huijui.
Utani utani wa kijinga na maneno ya kukutania vitazidi kushamiri.
Automatically kijiweni utaanza kupotea na utakuwa mtu wa kuwa bize for nothing.

Usiombe hiyo hali ikukute mazee! Kwanza hata ukienda vibaruani lazima uzinguliwe na matajiri kwa sababu wanajua huna chaguo, alafu mbaya zaidi lazima wakuzungushe kwenye malipo. Alafu ukijaribu kuwa mshari wanakuambia hayo mambo waachiw vijana ilhali wewe mwenyewe ndio kwanza upo miaka 35. Kudadadeki! Innalilah wainalilah Rajuun!

Chochote ukitaka kukifanya ukiwa kipara au mvi tena kwa mtaji mdogo lazima kikutie unyonge, Watu watakuwa wanakuona kama Budah fulani hivi.

Napendekeza, ukiwa below miaka 30 na umetoka familia maskini, kisha bado hauna ramani kivile.
Miaka 20- 30 ndio umri wako wa kujaribu kufanya kazi zózote na kujiweka sawa. Ndio umri wa kutafuta Pisikali moja uzae nayo yaani uanzishe familia ukiwa bado unamuonekano mzuri.

Usibeti kuwa ngoja utafute pesa Kwanza, huko ni kubet Ndugu yangu. Unaweza ukapata pesa au usipate. Lakini kwa umri wa miaka 20-30 huwezi kukosa Mwanamke mzuri wa kuanza naye familia akuzalie watoto angalàu mmoja au wawili.

Ili hata mambo yakibuma na mkeo akakuzingua uwe unafaida ya mtoto au watoto.
Lakini umechelewa kuanzisha familia kwa kubet kuwa unatafuta pesa Kwanza. Alafu umri umesogea, kipara na mvi zile alafu pesa hujapata. Ndugu yangu umekwisha!

This is Africa. Kanuni za huku ni za kipekee. Fanya kile ambacho unauhakika nacho kwa sasa na sio kubet kuwa unatafuta pesa kwanza kama vile uko Ulaya.

Elewa, huku Afrika unaweza ukawa na Juhudi, bidii na akili lakini bado maisha yakakupasua tuu. Lakini kwa Ulaya hilo haliwezekani.
Usijidanganye hapo na vishughuli vyako vya kujitafutia ambavyo vinakuingizia mia mbili mia tatu na kujipa moyo kuwa mambo yakikaa vizuri ndio utaanzisha familia. My friend, unajidanganya. Kwa Afrika labda uwe umeajiriwa tena serikalini ndio unaweza kufikiri kwa namna hiyo.

Biashara inabadilika muda wowote. Ni bora ibadilike ulishapata watoto tena na mke mzuri ambaye hata mkiachana haitalalia upande wako.

Uzee unatísha wazee! Uzee ambao haujajipata sio pouwa ndugu zanguni. Wanaosema Fainali uzeeni wanajua wanasema nini ndugu zanguni.

Tuombe Mungu atupe akili ya kutumia baraka zake lakini pia atupe uwezo wa kufanya mambo kwa wakati ili tusijetaabika.

Mwenye mvi nimemaliza.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Hapa dawa inakuwa double kiki na visungira tu baasi.haha
 
Kuna case nyingi nimekutana nazo kuhusu vijana wanaokufa mapema huku wameacha mali .

Wazazi wao hupenda kuhoji huyu mtu Hana mtoto , hamumjui mwanamke aliyezaa nae kwenye pita pita zenu .

Kulikuwa na case Moja 18 yrs old tunduma huko alikufa kijana Kwa ajali ya boda boda , tulifika msibani mama mtu alikiwa akilia sana , huku akilalamika umeniacha peke yangu , hujaniachia mtoto /mjukuu all of sudden akaja Binti ni mjamzito akasema alikuwa na mahusiano na kijana wao , somehow alirelieve That momma's pain . Mpaka naondoka Binti alipokea malezi ya hadhi ya kifalme .. Mpaka anajifungua ..

Nikaconclude kama Taikon /namesake ulivyosema mafanikio makubwa ni kuwa na familia

Case study ni Kanumba
 
Ñimekuuliza unajua life expectancy ya Tanzania NI ngapi?
Pili nikakuuliza kwenye ukoo wenu ni wangapi wametoboa hiyo miaka 80?

Tatu unajua nguvu kazi ya nchi ipo katika umri upi na upi?

Nne, unajua ni kwa nini kwenye kipengele cha kuomba kazi kuna kipengele cha umri?
Tano, unajua ni kwa nini mtu anatakiwa kustaafu akiwa na miaka 60?

Sikatishi mtu tamaa kwa sababu hata mimi naweza kuwa mhanga, kinachojadiliwa hapa ni uhalisia, ukweli uliowazi.

Sasa wewe unataka maneno matamu ya uongo ili kudanganya Watu wasichukue hatua?

Mimi ni Kilaza Mkuu.
Sijui kama anaelewa Life expectancy ya Tanzania ni ngapi, wazee wanaofikisha miaka zaidi ya 80 ni wachache sana.

Yeye anataka maneno yakutiwa Moyo, atoke kwenye Comfort Zone apambane aache ujinga ashukuru Mungu anapata sehemu yakukumbushwa na kutiwa hasira ya kujipanga na kupambana upya. Jamaa huyo ni kihiyo.
 
Ñimekuuliza unajua life expectancy ya Tanzania NI ngapi?
Pili nikakuuliza kwenye ukoo wenu ni wangapi wametoboa hiyo miaka 80?

Tatu unajua nguvu kazi ya nchi ipo katika umri upi na upi?

Nne, unajua ni kwa nini kwenye kipengele cha kuomba kazi kuna kipengele cha umri?
Tano, unajua ni kwa nini mtu anatakiwa kustaafu akiwa na miaka 60?

Sikatishi mtu tamaa kwa sababu hata mimi naweza kuwa mhanga, kinachojadiliwa hapa ni uhalisia, ukweli uliowazi.

Sasa wewe unataka maneno matamu ya uongo ili kudanganya Watu wasichukue hatua?

Mimi ni Kilaza Mkuu.
Hili bandiko lako linafanya vijana wakate tamaa, find something else to lift them up.
 
Kwani hakuna watanzania wanapitisha miaka 80? Na hata kama hakuna hivi ulichoandika huoni ni ujinga mtupu na unafanya watu wakate tamaa baada ya umri fulani?
Ukate tamaa, embu toka kwenye hiyo Comfort Zone unayo ikumbatia, Watanzania tunapenda kuwa polished sana ukweli hamtaki kuambiwa.

Wewe unaona ni sawa kijana ana miaka 35 yupo kwa baba na mama kula ugali wa shikamoo, ataweza kuwa na familia, mtoto na maendeleo.
 
Hili bandiko lako linafanya vijana wakate tamaa, find something else to lift them up.
Hakuna watu watoke kwenye Comfort Zone wapambane kama unakata tamaa ni wewe. Mtibeli katoa andiko bora la kufunga mwezi Januari.
 
Hakuna watu watoke kwenye Comfort Zone wapambane kama unakata tamaa ni wewe. Mtibeli katoa andiko bora la kufunga mwezi Januari.
Mvi na upara vs maendeleo mkuu. Havina uhusiano wowote, kuna wanaanza kuwa na hizo vitu at 25, vipi nao wakate tamaa kuwa tayari mvi/upara umeota huku hawana kitu.

Be logical mkuu.
 
Mvi na upara vs maendeleo mkuu. Havina uhusiano wowote, kuna wanaanza kuwa na hizo vitu at 25, vipi nao wakate tamaa kuwa tayari mvi/upara umeota huku hawana kitu.

Be logical mkuu.
Sasa kama havina uhusiano iyo habari ya kukata tamaa inakuja wapi

Stress ni predisposition factor ya ku Lower body immunity na hormonal change hivyo inapelekea nywele kunyonyoka na kupata upara mapema na pia kama huna maisha mazuri lishe mbovu na mvi zitakuja pia. Kwa hiyo vina mahusiano na kukosa maendeleo/ ajira kwa vijana inayosababisha persistent stress mtu anaingia kwenye pombe kali and staffs like that body immunity inakuwa shaked, hormonal imbalance n.k

Genetic mnapenda kuisingizia sana, wenye familia za namna hiyo ni chache sana haziendani na ongezeko la sasa la mvi na vipara vya mapema.

Mimi ninakubali sio kwamba nimefanikiwa kwa kila kitu ila nakubaliana na jambo, najipanga vizuri ili nisizidi kupoteza muda kwenye ujana uzee uwe worse zaidi.

Elimu ya sasa hivi imetengeneza watu wenye uwezo mdogo wa kufikiri (reasoning) au ndio extended high school kama Jeneral Ulimwengu alivyosema.
 
Back
Top Bottom