DR HAYA LAND
JF-Expert Member
- Dec 26, 2017
- 23,928
- 63,499
Upo sahihi Ila serikali inauwezo wa kupiga marufuku pombe zote .Hapana, visungura vinatangazwa kwenye radio na tv tena wakati wa taarifa za habari wakati wengi wanatizama. Hakuna sheria inayokataza pombe ila kuna muda wa kufungua bar. Sasa visungura ni portable. Mtu ananunua anaweka mfukoni anaenda kijiweni. Wengine wanauza hapohapo vijiweni. Kudhibiti ni ngumu kama watumiaji hawatajielewa.
Serikali haiwezi kupiga marufuku kwani vinatumiwa na chawa wa CCM wanaotumiwa kushangilia kwenye mikutano.Wapo watakaosema kwamba hakuna anaelezimishwa kunywa hivyo visungura, fine, ila imetosha sasa. Vipigwe marufuku, pombe kali za kiwango hiki hazipaswi kuwa readily available kiasi hiki kama bigijii.
Waweke either kwa packaging ya ujazo mkubwa zaidi ili isizagae na kununuliwa hovyo kama karanga mitaani, au waweke kwenye packaging ghali zaidi ya chupa za kioo, sio hivi viplastiki wanapima kama mkojo na kuuza buku buku.., huu ni uuwaji kabisa..
Serikali ingieni mitaani muone kinachotokea kwa vijana hujo Arusha na kwingineko, hivi mmafurahi watoto wa wenzenu wanavyogeuka mazombi?!
Sisi huku tunaandika tu 'hairuhusiwi chini ya miaka 18.Dah, noma.
Umenikumbusha huku majuzi nimeshangaa tumekwenda kusherehekea kumaliza mwaka, kwenye Italian restaurant ya kishua, sasa kuna kijana mmoja mdogo kaja na mke wake.
Tumeanza kuagiza vinywaji, yule dada akaagiza some sort of martini drink, yule waiter akamuuliza atoe kitambulisho cha kiserikali kuhakikisha kuwa amefikisha umri wa kunywa pombe.
Yani hata restaurant ikiuza glasi ya wine kwa mtu ambaye hajafikia umri inapigwa faini ndefu. Madukani hupati pombe mpaka kwenye duka maalum lenye kibali cha kuuza pombe, na ukija kununua mtu unaonekana mdogo wanakuuliza kitambulisho wahakiki umri wako.
Inaonekana huko Tanzania watu hawajali mambo kama haya.
Lile dude limesababisha had madogo hawasomi shule aloo sijui serikali haiangalii haya madude wengi wanaoenda pale miaka 12-17 sasa si umri wakuwa shule huo aisee hili swala wangeliangalia kinamna nyingineMimi mpaka kutishiwa mkuu.
Niliongea na jamaa mmoja mmiliki wa hilo dude nikamwambia kwanini usiweke jioni na upige marufuku watoto wa shule, akamiambia acha ujinga na ufanye yako.
Nikamwambia mamlaka husika sikizilliona ili utakuwa matatizoni, alichonijibu jamaa nilichoka, akaniambia mamlaka zote ni pesa, na hakuna wakunizuia.
Serikali haina uwezo wa kupiga marufuku pombe zote.Upo sahihi Ila serikali inauwezo wa kupiga marufuku pombe zote .
Visungura ukinywa wiki tu mashavu yanakua kama ya paka shume.Kuna wimbo mmoja wa Singeli jamaa anasema siku hizi wameacha viloba mambo ni Safari na Savanna, nikajua tumepiga hatua.
Kumbe kuna visungura?
Sasa visungura vikoje hivyoo?
Inashangaza serikali kufumbia machoVisungura ukinywa wiki tu mashavu yanakua kama ya paka shume.
😂😂😂😂😂😂😂Visungura ukinywa wiki tu mashavu yanakua kama ya paka shume.
Siri kaliInashangaza serikali kufumbia macho
🤣🤣🤣🤣🤣🤣Wanadondoka tu kama kuku wenye videli😢
Serikali imekosa utu kabisa, wanaangalia kodi tu!!Hii kitu ni hatari sana,wafanya biashara wanachojali ni pesa tu sio afya ya mtumiaji....
Hatari kubwa sanaMfumo ndiyo unataka hivyo
Watu walewe wawe walevi,watu wawe concerntrate tu na starehe na mamiziki
Mapiraaa
Huku wao na familia zao zinasonga
Za kuambiwa changanya na zako
Ova