Hakuna mwanasiasa/Rais aliweza kupambana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na akashinda!

Hakuna mwanasiasa/Rais aliweza kupambana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) na akashinda!

Aliye mshauri Mh Rais akae kimya huyo ndio asiyemtakia mema. Unakaje kimya wakati baadhi ya vipengele vya makubaliano ya awali vina ukakasi wa wazi kwa kila mwenye akili timamu kuelewa?

Unaweza kuupotezea waraka wa Maaskofu zaidi ya 30 unao elekezwa kwa namilioni ya wafuasi wao waliokatika kila nyanja ya maisha uijuayo wewe khalafu uwe bado na amani moyoni???, Mungu anahitaji mwenye haki wake mmoja tu kufanya naye kazi. Eliya mmoja aliangamiza makuhani 450 wa mungu baal chini ya Jezeebel???!! CCM na viongozi wenu someni maneno haya ya Biblia, Zaburi 33:16.
 
Kwa wajuzi wa historia ya Tanzania wameishajua kuwa Tamko la Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) la kuhusu mkataba baina ya serikali ya Tanganyika AKA Tanzania na DP World ni kaa la moto mkali ambao unazidi kumchoma vikali muhusika mkuu na chama chake mpaka watakapokufa kisiasa mapema kama wataendelea kushupaza shingo.

Katika historia ya Tanzania hakuna mwanasiasa au Rais aliwahi kupambana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) halafu akashinda. Haijawahi kutokea na haitawahi kutokea katika miaka hii ya karibuni. Kufanya hivyo ni kujiangamiza kisiasa(political suicide).

Unaweza kuukataa huu ukweli lakini kuukataa kwako hakuwezi kuubadilisha kuwa uongo.

Mwl. Nyerere pamoja na nguvu zote za kikatiba alizokuwa nazo katika utawala wake lakini hakuwahi kutumia nguvu katika kupitisha ajenda zake za kisiasa pale ambapo maaskofu walikuwa na shaka au kumpinga. Alitumia nguvu ya ushawishi wa hoja kwa kujadiliana nao mpaka wakamwelewa na kukubali.

Nguvu za Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) zimeendelea hivyo katika tawala zote nchini. Hakuna mwanasiasa mwenye uelewa wa Tanzania na akili timamu aliweza kupuuza sauti ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).

Muhusika mkuu wa mkataba wa DP World hakutegemea kama TEC wanaweza kutoa waraka mkali kama waliotoa kwa sababu sehemu ya 17 ya waraka imepigilia msumari wa mwisho wa jeneza la mkataba.

TEC IMEITAKA SERIKALI IACHANE NA MKATABA HUU.

Sehemu ya 17 ya waraka wa TEC inasema, “Hivyo tukiwajibika kimaadili, tunaona ni jukumu la serikali kusikiliza wananchi wanaotaka mkataba huu ufutwe. Kwa kuwa tumeonesha kuwa Tanzania tumeshawekeza na kuendeleza bandari, reli na bandari za nchi kavu; niwajibu miradi hii tuiendeshe Watanzania wenyewe huku tukikaribisha ubia tunaoudhibiti wenyewe. Hiki ndicho wananchi wanachokililia kusudi tujenge uwezo wetu wenyewe. Kwa vile tumegundua mapungufu yetu ya uendeshaji wa bandari, tunaweza kujizatiti kurekebisha mapungufu hayo wakati njia za kiuchumi zikibaki mikononi mwetu. Kwa sababu hizo na maelezo yote ya hapo juu, sisi Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania hatuungi mkono Mkataba huu”.

Baada ta waraka kutolewa, muhusika mkuu na genge lake akaanza kuhaha akitafuta jinsi ya kukabiliana nao. Amemtuma kiongozi mkuu wa nchi mstaafu ili ajibu hoja lakini hakufanikiwa kuzima moto, amejaribu kutumia mbinu za kidini kwa kuwatuma baadhi ya mashekhe ili wawajibu TEC katika misingi ya kidini lakini pamoja na juhudi zote, moto wa waraka wa TEC ndio unashika kasi ya kumchoma kisiasa. Ametuma “wajinga” fulani washambulie haiba ya maaskofu badala ya kujibu hoja hawajafanikiwa.

Alichofanya kwa sasa ni kuwatuma baadhi ya viongozi ndani ya serikali kwenda Dubai ili kuwaeleza wenye DP World kuhusu moto unavyowaka nchini ili waangalie namna ya kufanya ili kuondokana na moto mkali kisiasa ili kuepuka maafa ya kisiasa. Kwa hivi karibuni ndege ya Rais imekuwa na safari nyingi za kwenda Uarabuni na kurudi.

Katika hali hiyo ya kutapatapa ametangaza eti tenda ya kukaribisha wawekezaji kwenye bandari Terminal 2 ili ionekane hakutaka kugawa bandari zote kwa DP World wakati mkataba(IGA) unabainisha ni bandari zote na maziwa yote ya Tanganyika AKA Tanzania bara. Mjinga gani atakuja kuwekeza kwenye terminal 2 wakati kuna IGA inasema uwekezaji wowote katika bandari na maziwa nchini lazima kwanza uridhiwe na DP World.
Tumeona pia amemuondoa waziri wa katiba na sheria ili eti ionekane kama ndiye aliyesababisha hili sakata la DP World wakati kwenye IGA kuna saini ya Rais! Huku ni kutapatapa.

Kama isingekuwa waraka wa TEC, mchakato wa kuzifuta Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa Rasilimali na Maliasili na Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu Masharti Hasi katika Mikataba inayohousu Rasilimali na Maliasili za Nchi za mwaka 2017 ungefanyika bungeni na hili tangazo lingine la tenda ya kukaribisha wawekezaji lisingetolewa! Hii yote ni imefanyika katika hali ya kutapatapa!
hawa jamaa wameletwa na Mungu, wametufumbua macho, pamoja na kwamba bado kuna watu wapo gizani na wengine macho wanayo ila hawataki kuona.
 
Punguza hasira na siku zote TEC hawajawahi kuishinikiza au kuitaka serikali juu ya mambo yasiyokua ya manufaa kitaifa in favor ya mambo ya kanisa. Siku zote wamekua wakiadress national issues. na hata katika waraka wao hakuna jambo lolote au statement yoyote iwe kwa uficho au kwa uwazi imejielekeza kwenye maslahi au mahitaji ya kanisa.
Sasa hapo shida ipo wapi ? Ukipigania haki na jambo lenye manufaa ya wengi eventually uta-prevail no matter wewe ni nani..., Lakini ukienda vinginevyo mwisho wa siku utaporomoka hata ukiwa nani....; There was a time Theocracy was an order of the day (ila ikafika wakati sehemu nyingi wakaona kinachosimamiwa ni cha wachache na sio kwa faida ya wengi) hivyo uongozi kama huo ulikufa kifo cha kawaida...

Ila Point nayosema na ya maana, kuleta mashindano yasiyo na tija na ubabe wa kitoto ni kupunguza uungwaji mkono....; tuzungumze ni nini kinachopiganiwa kwa wakati husika sababu hii nchi kuna vitu vinavyowagusa wote no matter Imani zao (Kwahio hata Shetani akigombania Haki ya wengi atashinda tu mwisho wa siku)

Post kama hii/ Maneno kama haya wala hayajengi zaidi ya kubomoa
 
hawa jamaa wameletwa na Mungu, wametufumbua macho, pamoja na kwamba bado kuna watu wapo gizani na wengine macho wanayo ila hawataki kuona.
Toa upupu wako mungu gani na ni wachoyo na wabinafsi yote hayo hawajapata mgao hawana lolote safari hii imekula kwao , raisi wetu kanyaga twende tumechelewa sana u know
 
Fafanua mkuu,Covid 19 Magufuli alikinzana na TEC kwenye upande upi wa Corona?
Alisema Corona hakuna Tanzania na akapiga marufuku kuvaa barakoa.Wakatoliki chini ya Fr.Kitima wakasisitiza kuwa Corona ipo na imewaua baadhi ya waumini,mapadre,maaskofu,masista hata mabruda na kuwasihi kuvaa barakoa hata kwenye mikutano ya Magufuri jambo ambalo hakupenda kabisa.Badala yake yeye aligeuka kuwa Papa wa kuwafokea viongozi hao na kuwaambia hawana imani.Unaona kilichotokea?Wakatoliki wanathamini afya na uhai wa waumini wao na ndio maana hata kwenye mkataba huu wa DP World wamejitahidi kuonya ila sisi bado tunawaona kama wanaingilia mambo ya serikali.Uzuri ni kuwa majibu ni hapa hapa duniani.
 
Toa upupu wako mungu gani na ni wachoyo na wabinafsi yote hayo hawajapata mgao hawana lolote safari hii imekula kwao , raisi wetu kanyaga twende tumechelewa sana u know
wachoyo wa nini sasa, wamekunyima ubwabwa? na mgao gani mliodanganywa kwamba maaskofu wa katoliki huwa wanapewa? ukitaka kuwapa hao rushwa nenda kaanze na papa. zote hizo ni propaganda mnadanganyana kwenye tv iman huko baada ya kushiba kalmati.
 
Kama Chifu Hangaya siyo?
Wewe mfano una elimu gani hata ya kumpita mkenya?🤣🤣

Mtu mzima halafu hujielewi !?


Ujinga na ukatoliki wenu ndo umemaliza elimu ya Tz ,kilichobaki ni kusambaza tamaduni zao ila hao maprofessor kama wote hawana kitu kichwani.
 
Hao jamaa wana siri zenu kibao na huwa mnarekodiwa pale mnapo ungama kwaiyo wale pedophiles kwa akili zako wako juu ya serikali na waislamu wote na walutheri

Kama hujui kuwa TEC inaongoza watu na serikali ni watu hao hao ambao wanaongozwa na TEC, basi huwezi pia kujua nguvu ya TEC ndani ya serikali inayotokana na watu ambao wanaongozwa na TEC!
 
Kwa wajuzi wa historia ya Tanzania wameishajua kuwa Tamko la Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) la kuhusu mkataba baina ya serikali ya Tanganyika AKA Tanzania na DP World ni kaa la moto mkali ambao unazidi kumchoma vikali muhusika mkuu na chama chake mpaka watakapokufa kisiasa mapema kama wataendelea kushupaza shingo.

Katika historia ya Tanzania hakuna mwanasiasa au Rais aliwahi kupambana na Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) halafu akashinda. Haijawahi kutokea na haitawahi kutokea katika miaka hii ya karibuni. Kufanya hivyo ni kujiangamiza kisiasa(political suicide).

Unaweza kuukataa huu ukweli lakini kuukataa kwako hakuwezi kuubadilisha kuwa uongo.

Mwl. Nyerere pamoja na nguvu zote za kikatiba alizokuwa nazo katika utawala wake lakini hakuwahi kutumia nguvu katika kupitisha ajenda zake za kisiasa pale ambapo maaskofu walikuwa na shaka au kumpinga. Alitumia nguvu ya ushawishi wa hoja kwa kujadiliana nao mpaka wakamwelewa na kukubali.

Nguvu za Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC) zimeendelea hivyo katika tawala zote nchini. Hakuna mwanasiasa mwenye uelewa wa Tanzania na akili timamu aliweza kupuuza sauti ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC).

Muhusika mkuu wa mkataba wa DP World hakutegemea kama TEC wanaweza kutoa waraka mkali kama waliotoa kwa sababu sehemu ya 17 ya waraka imepigilia msumari wa mwisho wa jeneza la mkataba.

TEC IMEITAKA SERIKALI IACHANE NA MKATABA HUU.

Sehemu ya 17 ya waraka wa TEC inasema, “Hivyo tukiwajibika kimaadili, tunaona ni jukumu la serikali kusikiliza wananchi wanaotaka mkataba huu ufutwe. Kwa kuwa tumeonesha kuwa Tanzania tumeshawekeza na kuendeleza bandari, reli na bandari za nchi kavu; niwajibu miradi hii tuiendeshe Watanzania wenyewe huku tukikaribisha ubia tunaoudhibiti wenyewe. Hiki ndicho wananchi wanachokililia kusudi tujenge uwezo wetu wenyewe. Kwa vile tumegundua mapungufu yetu ya uendeshaji wa bandari, tunaweza kujizatiti kurekebisha mapungufu hayo wakati njia za kiuchumi zikibaki mikononi mwetu. Kwa sababu hizo na maelezo yote ya hapo juu, sisi Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania hatuungi mkono Mkataba huu”.

Baada ta waraka kutolewa, muhusika mkuu na genge lake akaanza kuhaha akitafuta jinsi ya kukabiliana nao. Amemtuma kiongozi mkuu wa nchi mstaafu ili ajibu hoja lakini hakufanikiwa kuzima moto, amejaribu kutumia mbinu za kidini kwa kuwatuma baadhi ya mashekhe ili wawajibu TEC katika misingi ya kidini lakini pamoja na juhudi zote, moto wa waraka wa TEC ndio unashika kasi ya kumchoma kisiasa. Ametuma “wajinga” fulani washambulie haiba ya maaskofu badala ya kujibu hoja hawajafanikiwa.

Alichofanya kwa sasa ni kuwatuma baadhi ya viongozi ndani ya serikali kwenda Dubai ili kuwaeleza wenye DP World kuhusu moto unavyowaka nchini ili waangalie namna ya kufanya ili kuondokana na moto mkali kisiasa ili kuepuka maafa ya kisiasa. Kwa hivi karibuni ndege ya Rais imekuwa na safari nyingi za kwenda Uarabuni na kurudi.

Katika hali hiyo ya kutapatapa ametangaza eti tenda ya kukaribisha wawekezaji kwenye bandari Terminal 2 ili ionekane hakutaka kugawa bandari zote kwa DP World wakati mkataba(IGA) unabainisha ni bandari zote na maziwa yote ya Tanganyika AKA Tanzania bara. Mjinga gani atakuja kuwekeza kwenye terminal 2 wakati kuna IGA inasema uwekezaji wowote katika bandari na maziwa nchini lazima kwanza uridhiwe na DP World.
Tumeona pia amemuondoa waziri wa katiba na sheria ili eti ionekane kama ndiye aliyesababisha hili sakata la DP World wakati kwenye IGA kuna saini ya Rais! Huku ni kutapatapa.

Kama isingekuwa waraka wa TEC, mchakato wa kuzifuta Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa Rasilimali na Maliasili na Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu Masharti Hasi katika Mikataba inayohousu Rasilimali na Maliasili za Nchi za mwaka 2017 ungefanyika bungeni na hili tangazo lingine la tenda ya kukaribisha wawekezaji lisingetolewa! Hii yote ni imefanyika katika hali ya kutapatapa!
ILIKUWA ZAMANI NA SIO ZAMA HIZI, AMBAZO WATANZANIA WANAJIELEWA NA KUJITAMBUA KWA ASILIMIA 100.
 
Baada ya DG Tiss kuondolewa au kubadilishwa ilifuata kulifumua na kulisuka upya baraza la mawaziri ikiwemo kutolewa cheo kipya cha naibu waziri mkuu ambacho hakiko kikatiba nilijua lengo kuu lilikuwa kuupoteza mjadala wa bandari.

Lakini naona ngoma bado iko palepale na waraka wa TEC unaendelea kusomwa kwenye makanisa yote.

Nadhani ni wakati sasa wa serikali kuachana na hili dubwana la DPW
 
Sasa hapo shida ipo wapi ? Ukipigania haki na jambo lenye manufaa ya wengi eventually uta-prevail no matter wewe ni nani..., Lakini ukienda vinginevyo mwisho wa siku utaporomoka hata ukiwa nani....; There was a time Theocracy was an order of the day (ila ikafika wakati sehemu nyingi wakaona kinachosimamiwa ni cha wachache na sio kwa faida ya wengi) hivyo uongozi kama huo ulikufa kifo cha kawaida...

Ila Point nayosema na ya maana, kuleta mashindano yasiyo na tija na ubabe wa kitoto ni kupunguza uungwaji mkono....; tuzungumze ni nini kinachopiganiwa kwa wakati husika sababu hii nchi kuna vitu vinavyowagusa wote no matter Imani zao (Kwahio hata Shetani akigombania Haki ya wengi atashinda tu mwisho wa siku)

Post kama hii/ Maneno kama haya wala hayajengi zaidi ya kubomoa
Na serikali imesikia na imerudisha mpira kwapani DP na serikali wako mezani kurekebisha kile kinacholalamikiwa
 
Wewe mfano una elimu gani hata ya kumpita mkenya?🤣🤣

Mtu mzima halafu hujielewi !?


Ujinga na ukatoliki wenu ndo umemaliza elimu ya Tz ,kilichobaki ni kusambaza tamaduni zao ila hao maprofessor kama wote hawana kitu kichwani.
Nafanya kazi na Wakenya wananifahamu vizuri na kuniheshimu ila wewe mvivu,mchoyo na mla Rushwa unaona sina elimu na sifai.Nakwambia kwa huu Mkataba wa Hangaya na DP World siwezi kutulia labda kama shuleni nilienda kuhesabu makenchi.Lakini kama nilisoma somo la Historia vizuri na Elimu ya Siasa vizuri nitakuwa mpumbavu wa kiwango cha lami kukubaliana na yasiyokubalika na Watanganyika wenzangu.
 
Baada ya DG Tiss kuondolewa au kubadilishwa ilifuata kulifumua na kulisuka upya baraza la mawaziri ikiwemo kutolewa cheo kipya cha naibu waziri mkuu ambacho hakiko kikatiba nilijua lengo kuu lilikuwa kuupoteza mjadala wa bandari.

Lakini naona ngoma bado iko palepale na waraka wa TEC unaendelea kusomwa kwenye makanisa yote.

Nadhani ni wakati sasa wa serikali kuachana na hili dubwana la DPW
 
watu aina yako ndio mzigo wa ajabu kwa taifa hili, ila watu wanaofikiri watakuona ulivyo zuzu badala ya kujibu hoja unakimbilia nimetumwa as if una ahadi ninakuja kwako kukuletea ujumbe.
Ukiulizwa wapi kanisa limepiga mali za umma huwezi kuleta majibu hata kidogo
ukiulizwa duniani kote wapi Askofu au Padre au Cardinal au Abate wa kanisa katoliki aliwahi kuonesha nia au kuogombea au kuteuliwa katika nafasi ya Kisiasa huwezi kutaja hata mmoja. Maana yake huna Taarifa na hujui chochote.
Sindano imeingia if they can do let them do.
Tulimwita tukakaa nae mara tu alipoingia madarakani, kati yako na yeye nani anajua mambo zaidi?: Rais Samia akutana na Maaskofu wa Kanisa Katoliki – DW – 25.06.2021 anajua nguvu yake ndio maana hujaona hata kiongozi hata mmoja wa chama na serikali amejitokeza kubeza, kuponda au kutukana Baraza kwa Tamko walilotoa, Moja wapo ya hoja zao ni kuhusu Bunge kubadili sheria ya 2017 ya ulinzi wa maliasili. Kafuatilie shughuli za BUNGE kuanzia kamati ya katiba na sheria na Tamko la speaker akifungua Bunge. NDIO MAANA YA PHILOSOPHY elimu ya elimu zote.

Asante sana kwa majibu mujarabu yakiyoenda shule ya filosophia.

Tuendelee kuwaelimisha wale wasiojua nguvu za TEC nchini.
 
Back
Top Bottom