Hakuna Pro-CCM mwenye uwezo wa kujadili mambo ya maana hadi sasa

Hakuna Pro-CCM mwenye uwezo wa kujadili mambo ya maana hadi sasa

Hili liko wazi kabisa, CCM wote ni low minded pakubwa sana, huwezi kusikia wanakuja na mijadala makini yenye maslahi kwa Taifa, huwezi kamwe kuwasikia wakijadili kuhusu hatma ya Taifa, huwezi kuwasikia wakizungumzia mapungufu ya Katiba, huwezi kuwasikia wakizungumzia kwa mfano kuhusu Ujinga wa Tozo, kupanda kwa ruzuku ya mbolea etc.

Leo hii baada ya kupinga Covid 19 Vaccination kwa nguvu, ndio wa kkwanza kupanga foleni ili wachanjwe. Leo hii hawaimbi tena kuhusu kuwekeza Chato, huwasikii tena wakizungumzia kuhusu Elimu bure!

Wao ni CHADEMA kucha kuchwa, CHADEMA na Mbowe yaani utadhani hao ndio Taifa, ndio serikali au ndio Katiba ya nchi.

Natambua uwepo wa Wana-CCM wenye akili wachache ambao kila wakijaribu kufukurukuta wanabinywa.

CCM ni chama cha wapiga soga wasiojua wanachokitaka.
Kiranja wao ni Pascal Mayala
 
Tuko wengi tu mkuu....

Si wachache kama usemavyo KIPROPAGANDA 🤣🤣

CCM ni sawa na bahari......
Aagh wapi, nimezunguka Tanzania nzima, naifahamu Tz kwa 95% pamoja na wilaya zake, na huwa nikifika huko nafuatilia pia mambo ya siasa
 
Aagh wapi, nimezunguka Tanzania nzima, naifahamu Tz kwa 95% pamoja na wilaya zake, na huwa nikifika huko nafuatilia pia mambo ya siasa
Hongera kuifahamu vyema TZ....

Katika kuzunguka huko umefahamu kuwa wanaCDM wana uelewa mpana wa mambo na wanajitambua kuliko wengine.....mimi nimetambua kuwa wana VIPAWA vya KUPANDISHWA JAZBA NA KUWA MAKAMANDA walioko tayari kufanya lolote tu....

Nikiwaangalia CHADEMA ninawaona wale CUF wa jino kwa jino......tofauti tu wengi wa "makamanda" hawavai BALAGHASHIA na MAKOBAZI....
 
Hongera kuifahamu vyema TZ....

Katika kuzunguka huko umefahamu kuwa wanaCDM wana uelewa mpana wa mambo na wanajitambua kuliko wengine.....mimi nimetambua kuwa wana VIPAWA vya KUPANDISHWA JAZBA NA KUWA MAKAMANDA walioko tayari kufanya lolote tu....

Nikiwaangalia CHADEMA ninawaona wale CUF wa jino kwa jino......tofauti tu wengi wa "makamanda" hawavai BALAGHASHIA na MAKOBAZI....
Hahahaa hakuna watu wenye uwezo wa kuchambua mambo kama Wapinzani, weka siasa kando, tuache siasa kwanza, sema ukweli wako, ukimchukua RAIA wa kawaida sana (exposure na hats kiuchumi) ambao mmoja ni ccm na mwingine ni chadema kati ya hawa wawili nani atakua na uwezo wa kufafanua jambo kwa umakini zaidi? Kuwa mkweli.

Mwana CCM yeye ni kusifia tu na ameaminishwa kuwa MTU mwenye mawazo tofauti na wewe Hugo ni adui.

Rejea taarifa ya ile Asasi kuhusu uelewa wa mambo kati ya wana CCM vs Upinzani, ile report ya Aidan Yakuze wa Twaweza.....

Kwa kifupi huo ndio uhalisia, CCM wamejeruhi na wanatuhumiwa kuwa Alphonse Mawazo alifia mikononi mwake, kuna cases nyingi sana za CCM kuwafanyia vurugu wapinzani, kuna hadi makundi mabaya ambayo yamewahi kuwa linked na CCM.

Rejea kauli zisizo za staha za Makonda, Sabaya, Kihongosi, Ex RC Iringa, RPCs etc imagine hata "viongozi wa serikali" wanatake sides ......wacha niende ibadani. Kama hujanielewa basi
 
CHADEMA hakuna hoja wala vision. Wao wenyewe katiba yao hawaifuati yaani hawana moral authority ya kuleta hoja yoyote ya katiba.
Wadanganyifu sana hawatambui wabunge wanawake 19 ila ruzuku yao wana chukua narudia wana chukua.
Mna legitimacy gani ya kutoa amri kwa serikali.
Zaidi ya uanaharakati hakuna chochote walicho nacho ndio maana wakiwa maarufu kidogo wanakimbilia CCM.
 
Back
Top Bottom