Hakuna watu wajinga kama watu wanaoamini habari za kichawi

Hakuna watu wajinga kama watu wanaoamini habari za kichawi

Umeeleza vizuri sana, watu wengi wamekua wakiamini hiyo dhana ya uchawi kwa kuihusisha na vitabu vya Mungu.

Tukiangalia kwa upande wa dini kilichoanza kuwepo ni dunia na mazingira yake na viumbe wengine na kisha binadamu. Dhana hii ya uchawi ilikuja kwa mwanadamu wakati alipokosa majibu yanayotokana na mazingira aliyonayo kwahiyo fikra ya uchawi ndio ilianza kabla ya dini.

Dini zilipokuja zilikuta tayari wanadamu wana dhana hii ya kuamini hicho kinachoitwa uchawi ambacho kimsingi ni kukosa majibu ya yale unayoyaona katika mazingira yako, ndipo dini zikazungumzia hilo kwa maana ya kwamba watu wasiamini dhana hizo na badala yake wamuamini Mungu.

Hakuna dini iliyohalalisha uchawi kwamba upo na ufuatwe badala yake dini zinataka watu wasiamini na wasijihusishe na uchawi.

Kama nilivyoeleza hapo mwanzo uchawi ni dhana inayotokana na kukosa majibu ya yale unayopambana nayo katika maisha yako,kwa mfano, hupati ajira, timu yako inafungwa, kifo cha ghafla kwa mtu aliyekua mzima kabisa, umeona paka mweusi, hela zinapotea hovyo, umeona kuna mtu mbele yako ghafla akapotea, umeugua muda mrefu na huponi na hospitali hawaoni tatizo

Katika imani ya dini ukiona tukio lisilo na majibu unatakiwa uamini ni kwa uwezo wa Mungu, na wakati mwingine matukio mengi yana majibu ila huyaoni kwa sababu umeshiba imani ya uchawi.
Hili ndilo lililopo. Hata zile magic tricks usipoelewa utasema mwanamazingaraombwe anatumia uchawi.
 
Unaamini nyuki huwa wanatumwa na wachawi wakaume watu?
We Jamaa bange zimekuharibu hakika mtu mwenye akili zilizosimama hawezi akamezeshwa mentality km hizo for the matter of fact you're so useless shame on you, yaan unaanzisha uzi alafu unatoa ushahidi wa kipuuzi, unatuletea story za kusadikika hapa
 
Wewe sema hizo mentality umemezeshwa na watoto wenzio kwenye kijiwe chenu cha bange baaasi ueleweke, haujakua kijana bado una akili ndogo sana bange zinakuharibu
Unaamini kuwa unaweza kupata dhahabu kwa kutumia uchawi? Unaamini unaweza fanywa mgonjwa kichawi? una mawazo ya kitoto kama hayo?
 
Chuma ulete ipo ila ni uchawi wa kimasikini sana chuma ulete inakusaidia kupata pesa ndogo ndogo tu ambazo huwezi kununua chochote cha maana zaidi ya chakula tena cha kawaida kabisa
Kama ukisoma maandiko vizuri kuna makumi ya aya yanayozungumzia uchawi kama hii kwenye matendo 8: 9-11
Lakini katika mji huo alikuwepo mtu mmoja aitwaye Simoni, ambaye alikuwa mchawi. Kwa muda mrefu alikuwa amewapumbaza na kuwashangaza watu kwa mazingaombwe, akawa anajigamba kuwa yeye ni mtu maarufu. 10 Watu wa tabaka zote, wakubwa kwa wadogo, walivu tiwa sana naye, wakawa wanasema, “Bila shaka mtu huyu ndiye ile nguvu ya Mungu iitwayo ‘Uwezo Mkuu.’ ” 11 Wakamsikiliza kwa makini kwa sababu aliwastaajabisha kwa mazingaombwe yake...
Ukiona neno "uchawi" au "mchawi" katika biblia ujue tu haina maana ya huu uchawi na wachawi tunaoufahamu sisi huku sijui wa kuambiwa kuna watu wameruka na ungo, au chuma ulete au wa kugeuzana misukule nk.

Mkuu Fuatilia lugha za asili za biblia na tafsiri zake kuja lugha zetu izi utanielewa.
 
Una vituko wewe nawe, kwa hiyo mjadala hapa wao nini wanaweza na siyo kwamba wachawi wapo na wanafanya uchawi.

Kujibu swali lako wanaweza hata kukugeuza kuwa mwanamke.
Hapana mkuu. Mjadala ni kuamini uchawi unafanya kazi na unaamini mambo yanayodaiwa unafanya. Kama kutuma mamba, kutuma nyuki, kuleta magonjwa ya kuhara, kuingilia watu kimwili nk
 
Basi ndio maana hauamini kuhusu uchawi, siku ukipigwa tukio ndio utaanza kuamini kwa hio subiri kwanza upigwe tukio ingawa wachawi unawajua
Duh basi itakuwa maajabu ya dunia mtu kuibiwa Instagram account kwa uchawi huu wa kiswahili.
Hii nitabisha hadi mwisho..

Nikutajie account yangu ukawaambie wachawi waiibe.
 
Ingekuwa uwezekano huo upo sidhani kama wale wanaozamia Meli kwenda ulaya na nchi nyingine wangepata shida.
Maana lengo Lao ni kufika huko kwa njia yoyote ile.
Hawajataka tu kutumia njia hizo ni ghali sana kuliko njia za kawaida
 
Hebu nipe habari. Uchawi unaoamini wewe kama hautumi nyuki kudhuru watu unafanya kazi namna gani?
Wewe nani aliekuelezea hizo habari, yaan mnakaa huko kwenye vijiwe mnajazana ujinga alafu unaleta hapa ujinga wako alafu unaanza kusema wanaoamini ujinga wako ni wajinga na unatoa ushahidi wa kijinga, dude you're so bogus yaan umekosa ushahidi wa maana unaleta ushahidi wa kijinga km huo huo si utoto huo sasa
 
Back
Top Bottom