Hali ni tete Mtwara Leo, Sakata la Gesi

Hali ni tete Mtwara Leo, Sakata la Gesi

Hizo picha zinaonesha vijana wa mitaani wakipitapita na sio maandamano. Kitakachokosekana ni wauza mifuko na korosho pale stendi. Shida ya hili vuguvugu ni kwamba limeasisiwa na mtu asiyejua anadai nini.

Mtapigwa, mtawekwa ndani na gesi hii itakuja Dar es Salaam.

Wenzenu wenye akili timamu saa hizi wapo vyuoni wakijiandaa kuchukua fursa za ajira Msimbati kwenye kiwanda cha kuchakata gesi, ujenzi wa bomba na kinu cha kusukuma gesi kuja Kinyerezi kwenye Power Plant.

Kama kuna anayebisha na asubiri aone. Huu unaofanyika Mtwara ni utoto. Tutaibiwa kwa kuwa badala ya kuhoji yaliyo ya muhimu, tunashabikia yasiyo ya msingi.
Umesema kweli mkuu mwenye macho haambiwi tazama.
 
Mbona simple hiyo gas isitoke Mtwara ikae hapo hapo tutaifuata
 
Mtambo wa kuchuja gesi yatajengwa mtwara by muhongo.

sure mkuu na nimemsikia pia akisema kuwa kutajengwa mtambo wa kufua umeme wa megawatt 400 ambao kwa ajili ya mikoa yote ya kusini ya lindi, mtwara na ruvuma
 
pale somanga pia kuna megawatt 250 zitazalishwa hadi 2015
 
Jamani bomba Hili ni kwa manufaa ya Taifa. .wabunge na maofisa ws juu CCM na Chadema pamoja na vyama vyote vya siasa waelimishe Wananchi.
 
Hawa watu wanaowalipa vijana ili wafanye mandamano ni uasi ni vema waadhibiwe.
 
duh na kungekuwa na mbunge wa chadema huko mtwara, majibwa koko yangeisingizia chadema

mkuu, kuna CUF pia. usiignore nguvu za hicho chama. kule kusini ndo chama kikuu cha upinzani maana kina wabunge kama sikosei watatu
 
Uzushi tu huu hamna kitu, wana mtwara kila kona leo ni furaha baada ya hotuba ya waziri iliyojaa neema kwa mikoa ya kusini

sikilza redio EAST Africa sasa hivi wanazungumzia mabomu ya Mtwara au wewe uko Mtwara gani?
 
Wakuu,

leo ntwara tangu asubuhi kila huduma imefungwa watu wapo kimakundi
makundi wanasikiliza bunge hasa bajeti ya wizara ya nishati na madini,ni
magari ya ffu tu ndio yapo barabarani nayo hupata wakati mgumu kupita
kwasababu ya mawe na magogo yaliyowekwa na vijana,baadhi ya watu kadhaa
wamechukuliwa na askari eti kwakuwa walipita jirani na gari yao,askari
wengi waliokuja si wa hapa ntwara wengi wametoka Masasi na Lindi.


Kauli mbiu ya huku kwa sasa - "gesi haitoki hata kwa bomba la peni"

attachment.php


=======

attachment.php

[FONT=arial
black]

[/FONT]

Acha ushamba wewe na thred yako ya kichochezi! hivi nyie mijitu mingine sijui mkoje, kusoma hamtaki,kufanya kazi hamtaki kibaya zaidi,wale wanaotaka kwenda kazini mnawazuia mnaweka mawe na magogo barabarani! wagonjwa na wazee wapite wapi! na hivi mnadhani hiyo gesi mtagawiwa ktk vikombe au vibakuli kila mtu akauze! acheni ujinga! Fanyeni shughuli za kimaendeleo sio huo uchizi wenu! Na kwa taarifa yako gesi itatoka na haiwi chochote!
 
Nahisi kama mapinduzi ya ukombozi wa nchi hii yataanzia Mtwara!

Yes pamoja na Zanzibar to the East, Arusha to the North na Mbeya to west, together they constitute the four cardinal points of the compass that will set us free. Let freedom ring!
 
"Gesi haitoki hata kwa bomba la peni"
mh hili nalo neno!!
 
Nimesikia wamekata matangazo ya Radio na TV huko Ntwara ili wasisikilize kinachoendelea Bungeni.
mlioko huko tupeni habari kamili.
Kama ni kweli wamekata matangazo ya radio na TV basi hii ni Mugabe Style.

Wameishiwa mbinu sasa wapo tayari kuzika watu wakiwa wazima.
kuweni makini ndugu wa Mtwara.
 
Acha ushamba wewe na thred yako ya kichochezi! hivi nyie mijitu mingine sijui mkoje, kusoma hamtaki,kufanya kazi hamtaki kibaya zaidi,wale wanaotaka kwenda kazini mnawazuia mnaweka mawe na magogo barabarani! wagonjwa na wazee wapite wapi! na hivi mnadhani hiyo gesi mtagawiwa ktk vikombe au vibakuli kila mtu akauze! acheni ujinga! Fanyeni shughuli za kimaendeleo sio huo uchizi wenu! Na kwa taarifa yako gesi itatoka na haiwi chochote!
Taratibu angalia usipate Heart Attach.........:heh:
 
Back
Top Bottom