Hali ya Chid Benz Inasikitisha sana

Hali ya Chid Benz Inasikitisha sana

Kuna muda watu wanashindwa kukusaidia kutokana na tabia zako. Kuna Chid benz na T.I.D hawa watu ni wabishi sana, they know everything about life, hawahitaji ushauri wala kuulizwa kuhusu maisha yao, watakushambulia tu.
Leopard 2, tori_ng.jpg
 
Shida ya Chidi habebeki. Mtu kama blue anambeba sana na hujawahi kumtupa ila dk sifuri anaharibu. Kingine u-born town nao unamcost much know, mjanja yeye.
Hana nguvu ila ule ubabe wa Chidi yule Benzino wa miaka Ile ya 1990s mitaa ya Kkoo, ilala bado anauleta kumbe anaharibu
Kuna siku aliingia kitambaa cheupe Ile Tabata akawanyang'anya pombe Na kuwagawia marafiki zake anaowafahamu yeye Na kuondoka zake......ukweli ni kuwa chidbenz hashauliki....
 
Kutoa tuu taarifa inaweza ikawa msaada coz JF ni platform kubwa sana, angalia hii thread sahv ina views zaidi 5k, utajuaje mmoja kati yao akafanya maamuzi ya kwenda kumsaidia?
Hata kama ingekua na views milioni mia,hiyo haikupi uhakika kua Chid amepata msaad,ila msaada wako kwake ingekua ni uhakika,

Wewe hukua na uwezo wa kumsaidia? kwanini unawalaumu wasanii kutomsaidia? unaonaje ukaanza kujilaumu wewe kwanza? Be the change that u want to see in the World,usitegemee wengine wafanya kwa ajili yako.
 
Walienda beach hapo Koko nahisi km sijakosea Kunduchi wakala mitungi sasa Jamaa 'Pancho Latino' akiwa amelewa akawaambia wenzie anataka akaogelee wakamzuia Ila akakomaa basi wakabidi waende kwenye maji Jamaa akaingia vizuri tu kaanza maji ya ugoko akaendelee mbele maji kiunoni akaendelee mbele maji ya SHINGO

Kumbuka hapo amelewa tungi basi vuaaaa mara hawamuoni wakaanza kupagawa Pancho yupo wapi Pancho yupo wapi wakapigwa bumbuwazi Pancho kazama ikabidi wapige kelele ndio wale Beach boys waje kutoa msaada

Beach boys wakazamia huku na huku huku na huku mara Pancho huyu hapa wakamuibua kwenye Maji Pancho hakua amekufa alipoibuliwa alikua kwenye Koma Ila ilibidi apatiwe huduma ya kwanza ya haraka angepona maana Mwili ulikua bado unapapatika wakiwa wamembeba wale beach boys na mapovu yanamtoka mdomoni na puani wakamweka chini kumkamua maji

Steps za kumkamua maji wakakosea wao walikua wanaminya tumbo lake wakati inabidi uminye kifuani na sio tumboni

Kumbe wakati huo maji yashaingia kwenye Mapafu kingine hawakumpuliza Mdomo kumuongezea Hewa kwenye Mapafu ili maji yaweze kutoka mdomoni na puani wala kumminya Pua ili kusudi Hewa ikijaa ndani maji yanamtoka mdomoni na puani wala hawakumpasha Joto Mwili wake maana Mwili unahitaji nguvu alikua kashalegea

Na ilibidi kuminya kifua chake ila wakambeba huku wanalialia kwamba Pancho ameshakufa lakini laiti wangejua pale walipomtoa kwenye Maji hakua amekufa alikua kwenye Koma nahisi ni tungi ndio zilizowazuzua mpaka wanafika hospital too late taarifa inakuja Pancho Latino is dead

Nimekusimulia kwa mujibu wa Clip waliyoirusha wao wenye waliokua nae kipindi cha umauti unamfika kule baharini

RIP Pancho Latino
Walikuwa hawana utaalamu wa huduma ya kwanza.......Hayo ni makosa yake mwenyewe sio masela mavi sijui upumbavu gani, mtu umelewa unashauriwa usiende kuogelea, unalazimisha, unazama unakufa
Wanachoweza kufanya watu ni kukushauri, ila ukishauriwa ukapuuza ni juu yako, hao sio mama zako...
 
Hata kama ingekua na views milioni mia,hiyo haikupi uhakika kua Chid amepata msaad,ila msaada wako kwake ingekua ni uhakika,

Wewe hukua na uwezo wa kumsaidia? kwanini unawalaumu wasanii kutomsaidia? unaonaje ukaanza kujilaumu wewe kwanza? Be the change that u want to see in the World,usitegemee wengine wafanya kwa ajili yako.
Amsaidie kwani yule ni mtoto wake? Hakuna mtu anayewajibika kwa maisha ya mtu mzima mwenzake mzee
 
Amsaidie kwani yule ni mtoto wake? Hakuna mtu anayewajibika kwa maisha ya mtu mzima mwenzake mzee
Kwahiyo lengo la huu uzi wake lilikua ni nini? au huu uzi umewalenga wazazi wa Chid ili wamsaidie? wao hawajui hali aliyonayo mtoto wao?
 
madawa atumie yeye kuumia uumie wewe..chid alikua miyeyusho utoto wa mjini mwingi
hasaidiki. dk 2 mbele anakuchenjia. yeye aishi tu akifa tunazika. ndio maisha.
 
Mkuu Chidibenz angekua kaka ako ,sidhani kama ungemuacha aendelee kuishi maisha anayoishi sasa
Mkuu,

Hata angekuwa kaka yako, usingekua na cha kufanya, trust me.

Chid ameanza madawa arround 2010. Ni miaka 15 karibu sasa ndugu, jamaa, marafiki, wasanii, na kila aliekua na nafasi ya kujaribu kumsaidia wamejaribu, na imeshindikana. Hapo alipofikia naamini hata mama yake mwenyewe hataki kumsikia, achilia mbali kumuona. Ndio maana wamemuacha, aishi maisha aliyoyachagua mpaka hapo atakapoishia.

Kama umewahi kuwa na mtu wa aina hii kwenye familia yenu, utanielewa.
 
Hali ya Msanii wa Hiphop Rashidi Makwilo (Chidibenz) inasikitisha sana sana, Siku za hivi karibuni amekua akiishi Msasani (Maandazi road) maskani moja na mateja, Kinachonisikitisha zaidi jamaa anaonekana hayuko sawa kiafya miguu imevimba, anaonekana aliumia na hajapona vizuri,miguu ameifunga bandage na anatembelea ndala, Nimemuona leo asubuhi nikiwa naelekea kazini atembea kwa msaada wa watu wanampa support (Nahisi alikuwa amelewa sana) Uso wake ni kama hauna matumaini

Nitoe wito kwa wasanii wenzake na Familia yake wamfuate pale msasani coz anaishi maskani na hana mtu wa kumuangalia, Sina uhakika ila kuna uwezekano labda amerudi tena kwenye wimbi la madawa ya kulevya

Kwa inavyoonekana ni kama wasanii wenzake wamemsusa, hawana time naye tena Lakini naona sio sahihi coz ni Msanii mwenzao inabidi wakubali kubeba hili jukumu la kumlinda na kumtunza Chidibenz, Juzi kwenye show ya Serengeti pale K/nyama viwanja vya posta, Chidibenz alipanda kwenye show ya Rosa ree lakini hakuchukua mda akashushwa, na alikua amevaa ndala, Wakiendelea Kumtenga hivi depression inaweza ikam-maliza kabisa, Kwa upande wa Familia yake sijui wao wamejipangaje coz inaumiza sana kumuona Ndugu au mtu wako wa karibu akiwa anapitia kipindi kigumu

Vijana tujitahidini sana kuishi kwa nidhamu, Ujana una mambo mengi bila yakua na nidhamu ni rahisi kuanguka
Siku zote binadamu huwa tunavuna tulichopanda, Chidi Benz kitakachomsaidia kubadilika ni yeye mwenyewe kuamuakuwa anatakiwa kubadilika na niwajibu wake na siyo watu au sisi mashabiki tumsaidie kubadilika maana ni mtu mzima. Kingine aache kudeka na kujiona yeye si mtu special anaehitaji huruma, dunia haipo hivyo. Ila kwa wengine ambao tunaona mbali tatizo kubwa la Chidi limeanza kwenye familia na tatizo hilo "Fatherlessness" , mkubalinau mkatae Baba ninkiungo muhimu sanaa kwenye malezi ya mtoto wa kiume.
 
Mkuu Chidibenz angekua kaka ako ,sidhani kama ungemuacha aendelee kuishi maisha anayoishi sasa
Mkuu usichojua ni kwamba kina chidi benz tunaishi nao hata huku mtaani kwetu, ndugu zetu, watoto wetu, marafiki zetu. Nimesema hivyo kwa sababu nimeshawahi ishi na ndugu mwenye changamoto kama ya chidi, sio kwamba hatuwajali ila kuna muda hawasaidiki kutokana na hali zao.
 
Back
Top Bottom