Hali ya maisha imekuwa tete sana. Mawaziri mnakula vizuri, sisi hali mbaya

Nchi zilizoendelea hicho kilimo kinafanywa na wawekezaji 20 tu nchi nzima sasa we unataka kila kijana ashike jembe wakati ulimwengu huu umebadilika sana kutokana na maendeleo ya technolojia mawazo yako ya kijima sana
 
Hao uliowataja unataka wakakulimie au? Hii tabia ya utegemezi na kudhani watu Fulani ndio wekusababishia Ugumu wa Maisha ni mbaya sana.
Maisha magumu yanasababishwa na sera, na maamuzi ya Serikali ambapo wafanyaaamuzi ni hao Mawaziri na Rais.
Mfano mzuri ni kuruhusu Ku export mahindi ghafi huku chakula katika Nchi sio toshelezi huko ni kudababisha bei za nafaka kupanda na kufanya maisha kuwa magumu.
 
Aisee siku hizi kula wali nyama ni anasa!? Aiseeee daa nyama kilo 10000/, mchele kilo 3400/!! Weka mzagazaga!? Nyanya,kitunguu,howo !! Daa
 
Kwa hiyo Tanzania nzima watu wanabeti au unamanisha nini?,na kama Taifa watu wengine wanashiriki upatu jua hayo ni matatizo yanayotokana na Serikali.
Ili watu walime na Ku produce ni swala LA Serikali kuweka mazingira wezeshi.
 
Kwa hiyo hao uliowataja ndio wanesababisha gharama za Afya kuwa Juu?
CAG ametaja jina la mtu kwenye ripoti yake?
Kwani wewe unadhani anayesababisha gharama za Afya kuwa juu ni nani!,Mipango hovyo ya Serikali.

Sio lazima CAG ataje jina LA MTU kwenye report,kama ni madudu yanafanyika huko anayetakiwa kutekeleza majukumu yake hayo madudu yasifanyike ni Rais-ndio maana report inapelekwa kwake.
 
Hivi wewe unajua unachokiandika aununatete pasipo uelewa.
 
Mama asipoamka mambo yatamharibikia vibaya!

Mama asipoamka mambo yatamharibikia vibaya!
Mkuu Kwamba mama ndo alete mvua,ndo awahimize watu waende mashambani!?,hebu tuweni siriazi japo kidogo
 
Sasa Rais hashinikizwi bali anafanya kazi Kwa mujibu wa Sheria ,so lazima utaratibu ufuatwe sio tuu kama mihemko Yako inavyotaka..

Mwisho gharama za Afya ziko ghali all over the World sio Tanzania pekee na Serikali inajitahidi mbona.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…