Halima Mdee bado una nafasi ya kutubu, Heshima na tamaa havikai pamoja

mie nahisi ma ccm yatakuwa yamemloga kamanda mdee sio bure, ktk wanawake huyu ndiye alikuwa kamanda kwelikweli (kivitendo)...anafuatiwa kwa mbali na mama wa morogoro jina nani sijui alikuwa mbunge wa mlimba

Mkuu binafsi nimetafakari sana hata kushauri mlango wa wazi wa kutokea.

"I wish I could speak to her in person.

Useful to note the difference in speaking to, and pleading with, (someone)."

Kazi kwenu mnaoweza kumfikia au, na kusema naye kabla ya Friday 0800, 27th Nov, 2020.
 

Hongera hizi ni tokea chama rafiki kinachoitakia mema CDM kwa dhati kabisa. Zikiwasilishwa na mjumbe kwa niaba ya comrade pole pole.

Zimefika mkuu. Mjumbe hauwawi.

Amazing!
 
# WAKINA HALIMA WANA BARAKA ZOTE ZA MWENYEKITI CHADEMA TAIFA.

FULL STOP.

Bila mwenyekiti kutamka au kina halima kuthibitisha hilo, mengine ni ramli chonganishi tu.

Kwetu sisi tulio wazalendo,

"everyone is presumed innocent unless proven guilty"

Ndo ndo ndo si chururu, na CDM si CCM!
 
Hapa itategemea ni kosa lipi!!

Nakubalina nawe 100% mkuu!

Niseme bila kumung'unya maneno. Ninayasikia maumivu yako. Nikwambie hata yangu ni hivyo hivyo:

 

Mmekurupuka mashimoni?

Huu uzi hauwafai.

Ikumbukwe kuwa hayupo awaye yote anayeombwa kubakia CDM.

Pia uzi umezingatia itifaki vilivyo katika sentensi ya kwanza kabisa:

"Mabibi na mabwana na hasa wale walio wazalendo."

Wewe na wenzako wachumia tumbo mboga mboga - you're not included!

Furthermore:

 
Msingi wa hoja kama chama ni kutokutambua haramu ya uchaguzi 2020 na yote yatokanayo nao. Huu haupingiki aliye na hoja tofauti na atushawishi kwa hoja. Hiyo ndiyo demokrasia.
Ni mwaka gani kati ya chaguzi zilizopita mliwahi kusema kuwa uchaguzi ulikuwa huru na haki?
Chaguzi zote chadema ilikuwa inakataa matokeo, lakini wabunge wanaingia bungeni! Nadhani tunaijua siri: ni kwa kuwa waliokuwa wanashinda ubunge wengi wao walikuwa wanaume!
Sasa imekuja nafasi ya wanawake kuingia bungeni, nyie minjemba ndio mnawafanyia kauzibe: kwa kuwa ni wanawake!
Kubalini tu yaishe, waachwe waingie bungeni kama ilivyokuwa kwa wanaume: haki sawa kwa wote.
 
Mkuu kwa hiyo hao wamechaguliwa na CCM? shida CDM haina msimamo rejea 2015 Slaa vs Lowassa, siamini Kama hao wamama wamejiamulia wenyewe tu, siamini Kama hii inshu mbowe alikuwa haijui mapema
 
Kwa nini mnataka waombe radhi?? Kwa kosa gani.Yaani kutekeleza kwa takwa la maamuzi ya kamati kuu imekuwa taabu
 
Ushauri mujaraab kwa waungwana,kuomba msamaha na kuweka yote hadharani yatosha kumvua Boxer yustino na genge lake.Tutafakari.
 
Ni kweli hawajawahi kuutambua.2010 waligomea matokeo na walitoka wakati JK anahutubia bunge, 2015 same, 2020 galegale
 

Yoyote aliyeungana na shetani ni kumpiga chini watajuana wenyewe. Ni marufuku kuungana na shetani.
 

Kwamba kwa vile miaka yote mnaiba mlikuwa mmezoea matokeo?

Kwa sasa mnasema mbona miaka mingine tuliiba lakini hamkufanya hivi, hivyo mnaomba tutumie misimamo ile ile kwa sababu wizi ni ule ule?

Maajabu ya firauni.

Haya si ndiyo yale ya kuiba tumekwiba lakini kukiri ng'o!

Hukusikia safari hii kuwa:

Ukhanithi basi au Sasa basi?

Ukhanithi basi! Sasa basi! Hayo ndiyo habari kamili.

Uzee mwisho chalinze - Friday, 0800 27th Nov 2020!
 
Hahaha hawajajikwaa wale ni COVID-19 tu.

Huwezi kula matapishi kwa kisingizio kwamba kichefuchefu kimeisha.

Wafukuzwe tu.
 
Ni kweli hawajawahi kuutambua.2010 waligomea matokeo na walitoka wakati JK anahutubia bunge, 2015 same, 2020 galegale

Wataacha vipi kugomea kama pori jipya nyani wale wale?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…