DOKEZO Halmashauri ya manispaa ya Morogoro wekeni lami barabara ya zamani ya Iringa kuanzia SUA, Magadu mpaka Mzumbe

DOKEZO Halmashauri ya manispaa ya Morogoro wekeni lami barabara ya zamani ya Iringa kuanzia SUA, Magadu mpaka Mzumbe

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

Hismastersvoice

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2013
Posts
21,741
Reaction score
26,735
Natoa pendekezo kwa halmashauri ya manispaa ya Morogoro iweke lami kwenye barabara hii muhimu, miaka ya zamani old Iringa Road ilikuwa na lami ambayo baadae iliondolewa kutokana na uchakavu badala ya kutengenezwa! Barabara hii kuanzia njiapanda ya SUA kuelekea Magadu hospitali ya jeshi mpaka Mzumbe na kukutana na new Iringa Road iko kwenye hali mbaya sana baada ya lami iliyochakaa kukwanguliwa.

Kutokana na kukwanguliwa huko imebaki na kokoto zilizojishikilia ardhini na kuvifanya vyombo vinavyoitumia kuchakaza magurudumu vipitapo. Kutokana na tatizo hili kunalazimisha magari yanayotokea upande wa SUA kuelekea upande wa Iringa kuenda Msamvu ili waingie barabara mpya ya Iringa hivyo kuongeza wingi wa magari hapo kwenye mzunguruko wa Msamvu kuelekea Dodoma na Dar es Salaam.

Manispaa hainabudi kuitengeneza barabara itakayopunguza magari yatokayo upande wa Iringa kuingia mjini kwa kupitia Mzumbe, Magadu mpaka SUA

Bahati mbaya mbunge wa Morogoro haijui barabara hii inayotumiwa na wagonjwa waendao hosipitali ya jeshi Mzinga.
 
Bado kuna vumbi ? Maana ile njia ukiwa kwenye boda kama umepiga kiatu chako kiwi basi unafika hautamaniki
 
Afadhqli umesema wewe, yaani nilikuwa natafuta muda niongee hili hili ulilosema, yaani manispaa ya Morogoro inatia aibu. Sasa hivi Kuna muingiliano mkubwa wa watu na shughuli za kiuchumi makazi yanaongezeka, watu wanaongezeka lakini Morogoro iko vilevile kienyeji enyeji sijui kwanini kila kiongozi anayekuja pale anaupuuza ule mji

Sehemu zinaipaswa kuwekwa lami
Sua hadi mzumbe
Baraba ya chamwino
Mazimbu ndani hadi kihonda mazimbu road
Maeneo ya kiegea na Kilimanjaro
Lukobe hadi mguruwandege

Kuna uchafu unapita kuanzia iringa road modecco hadi kupitia ipoipo mzimbu hadi kihonda maghorofani unaitea lami ila ule ni ushubwada mtupu

Moro iko nyuma sana kwenye suala la miundombinu wanazidiwa hadi na bariadi?
 
Afadhqli umesema wewe, yaani nilikuwa natafuta muda niongee hili hili ulilosema, yaani manispaa ya Morogoro inatia aibu. Sasa hivi Kuna muingiliano mkubwa wa watu na shughuli za kiuchumi makazi yanaongezeka, watu wanaongezeka lakini Morogoro iko vilevile kienyeji enyeji sijui kwanini kila kiongozi anayekuja pale anaupuuza ule mji

Sehemu zinaipaswa kuwekwa lami
Sua hadi mzumbe
Baraba ya chamwino
Mazimbu ndani hadi kihonda mazimbu road
Maeneo ya kiegea na Kilimanjaro
Lukobe hadi mguruwandege

Kuna uchafu unapita kuanzia iringa road modecco hadi kupitia ipoipo mzimbu hadi kihonda maghorofani unaitea lami ila ule ni ushubwada mtupu

Moro iko nyuma sana kwenye suala la miundombinu wanazidiwa hadi na bariadi?
Tatizo mbunge anayo mabasi 200+ ya kuyaangalia kila sekunde, kila dakika, kila saa, kila siku, kila wiki, kila mwezi na kila mwaka! Miaka yenyewe mitano tu, hana muda huo vinginevyo hataweza kulipa mkopo wa mabasi hayo.
 
Bado kuna vumbi ? Maana ile njia ukiwa kwenye boda kama umepiga kiatu chako kiwi basi unafika hautamaniki
Wewe unafikiria kiatu! Fikiria mgonjwa anayepelekwa hospitali huku akichekechwa kama vile yuko kwenye mtambo wa kuchekecha kokoto.
 
Tatizo mbunge anayo mabasi 200+ ya kuyaangalia kila sekunde, kila dakika, kila saa, kila siku, kila wiki, kila mwezi na kila mwaka! Miaka yenyewe mitano tu, hana muda huo vinginevyo hataweza kulipa mkopo wa mabasi hayo.
Sasahivi atakuwa anagawa majiko maana ndiyo rushwa nzuri
 
Hiyo sio kazi ya Halmashauri ya manispaa. Ni kazi ya TARURA
Kwahiyo manispaa hazisimamii barabara! Hawa madiwani kwenye vikao vyao wanaongelea nini! TARURA nao wana ingia kwenye vikao vya madiwani? Kwakua si madiwani hwawana sifa ya kuingia kwenye hivyo vikao, sasa wanajuaje matatizo ya barabara za mijini?
 
Kwahiyo manispaa hazisimamii barabara! Hawa madiwani kwenye vikao vyao wanaongelea nini! TARURA nao wana ingia kwenye vikao vya madiwani? Kwakua si madiwani hwawana sifa ya kuingia kwenye hivyo vikao, sasa wanajuaje matatizo ya barabara za mijini?
Usiwe mbishi usione Soo kuonekana hujui. Peleka hiyo TARURA ama TANROAD depends on the level of the roads
 
Hakuna halmashsuri yenye uongozi mbovu kama ya Morogoro Manispaa, jamaa wanatia kichefuchefu barabara nyingi maeneo muhimu ni mbovu kupindukia
 
Afadhqli umesema wewe, yaani nilikuwa natafuta muda niongee hili hili ulilosema, yaani manispaa ya Morogoro inatia aibu. Sasa hivi Kuna muingiliano mkubwa wa watu na shughuli za kiuchumi makazi yanaongezeka, watu wanaongezeka lakini Morogoro iko vilevile kienyeji enyeji sijui kwanini kila kiongozi anayekuja pale anaupuuza ule mji

Sehemu zinaipaswa kuwekwa lami
Sua hadi mzumbe
Baraba ya chamwino
Mazimbu ndani hadi kihonda mazimbu road
Maeneo ya kiegea na Kilimanjaro
Lukobe hadi mguruwandege

Kuna uchafu unapita kuanzia iringa road modecco hadi kupitia ipoipo mzimbu hadi kihonda maghorofani unaitea lami ila ule ni ushubwada mtupu

Moro iko nyuma sana kwenye suala la miundombinu wanazidiwa hadi na bariadi?
Hiyo ndio manispaa yenye wimbi kubwa sana la wizi wa mapato ya ndani.
 
Usiwe mbishi usione Soo kuonekana hujui. Peleka hiyo TARURA ama TANROAD.
Sipendi ujuaji wako, wapi nimebisha? Nimehoji jinsi TARURA wanavyoweza kujua mahitaji ya miundombinu ya barabara za mijini wakati wahusika wakuu ni madiwani.
Sipendi dharau.
 
Nakumbuka kuna wakati alikuwa anakwenda kwenye vijiwe vya bodaboda kujiselfii!
 
Ulilolisema ni kweli ile barabara kwa mgeni hawezi akajua kama ilikuwa lami.
Ila uliposema ukiwa SUA unapita msamvu kuelekea Iringa hiyo sio kweli, ukitoka sua unapita mafiga unaingia barabara ya Iringa.
 
Kwa ujumla, Manispaa ya Morogoro ni upumbavu mtupu
 
Back
Top Bottom