Hanspaul: Mshahara wa Laki 5 usikatwe Kodi

Hanspaul: Mshahara wa Laki 5 usikatwe Kodi

Tatizo hao wanaolipwa laki tano na chini ninwengi sana kiasi wasipokatwa kodi serikaki itapunguza mapato sana.

Hivyo, hiyo kodi ama itafutwe kwa wanaoliowa zaidi, ama serikaki ipunguze matumizi.

Hapa panatakiwa uchakataji wa namba kuangalia quantitative analysis.

Anachomaanisha ni ukiongeza uwezo wa manunuzi wa raia wako wigo wa kodi unatanuka mno, unachohitaji ni mifumo ya urasimishaji na ukusanyaji. Amewaza vizuri.
 
Sio kwamba jamaa anajitetea yeye? Mfano alikuwa akikulipa 500,000 wewe unachukua 400,000 halafu 100,000 inakuwa kodi. Wakisema chini ya 500,000 haina kodi anaanza kuwalipa watu wake 400,000 tu.
Wewe unapata 400,000 yako ile ile na yeye anaokoa 100,000 akiwa na wafanyakazi 100 hio ni 10m kwa mwezi savings.
Itazame kwa jicho la macro siyo micro.
 
Kinyume chake pia ni sawa.
Kinyume chake hata akiitumia kama ulivyosema, still kwa kuongeza uwezo wa spending wa raia wako utatanua mno wigo wa kodi sababu kodi inatokana na biashara, na kwenye kila biashara kuna matumizi na wasababisha matumizi ni waajiriwa na waajiriwa wengi wanalipwa laki saba mpaka tano kabla ya kodi.

YAANI KWA UFUPI, HUYU ANASHAURI WAAJIRIWA WALIO WENGI WAWE NA PESA ILI WAKASPEND KWA WAFANYABIASHARA, WAJENZI N.K MAANA NDIO KUNDI KUBWA.
 
Kinyume chake hata akiitumia kama ulivyosema, still kwa kuongeza uwezo wa spending wa raia wako utatanua mno wigo wa kodi sababu kodi inatokana na biashara, na kwenye kila biashara kuna matumizi na wasababisha matumizi ni waajiriwa na waajiriwa wengi wanalipwa laki saba mpaka tano kabla ya kodi.

YAANI KWA UFUPI, HUYU ANASHAURI WAAJIRIWA WALIO WENGI WAWE NA PESA ILI WAKASPEND KWA WAFANYABIASHARA, WAJENZI N.K MAANA NDIO KUNDI KUBWA.
Angeshauri kuwa kima cha chini kiwe 500,000/- ambayo haikatwi kodi. Hapo angeongeza hio spending power.
Ila ya kusema tu chini ya 500,000 isikatwe kodi hawatamuingezea mwananchi chochote ila wao matajiri wataokoa hela zao maana wataendelea kulipa watu wengi 270,000 bila kulipa PAYE.
Point yako nimeielewa vizuri pia.
 
Angeshauri kuwa kima cha chini kiwe 500,000/- ambayo haikatwi kodi. Hapo angeongeza hio spending power.
Ila ya kusema tu chini ya 500,000 isikatwe kodi hawatamuingezea mwananchi chochote ila wao matajiri wataokoa hela zao maana wataendelea kulipa watu wengi 270,000 bila kulipa PAYE.
Point yako nimeielewa vizuri pia.
Upo sawa Mkuu RRONDO
 
Means serikali pia pia ipunguze unnecessary spending.
Magari ya 500b kila mwaka ilhali tunaagiza mafuta ya kupikia yenye thamani ya 500b..kwanni tusiwekeze kwa watu wetu kwenye kilimo cha kisasa kupungiza umasikini,kuongeza ajira na kupandisha thamani ya sh?
Kuna baadhi ya vitu unaona kabisa ni ubinafsi!
 
Wakuu

Mbele ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uwekezaji), Prof. Kitila Mkumbo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Hanspaul Group, Satbir Singh Hanspaul amependekeza mwananchi anayepokea mshahara wa laki tano kushuka chini asikatwe kodi.

Hanspaul ameyasema hayo siku ya Jumatano, Januari 08, 2025 katika Mkutano wa Wafanyabiashara na Wamiliki wa kampuni wa Kuhakiki Rasimu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 uliofanyika katika Serena Hotel, Dar es Salaam.
View attachment 3195925
 
Wakuu

Mbele ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Uwekezaji), Prof. Kitila Mkumbo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Hanspaul Group, Satbir Singh Hanspaul amependekeza mwananchi anayepokea mshahara wa laki tano kushuka chini asikatwe kodi.

Hanspaul ameyasema hayo siku ya Jumatano, Januari 08, 2025 katika Mkutano wa Wafanyabiashara na Wamiliki wa kampuni wa Kuhakiki Rasimu ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050 uliofanyika katika Serena Hotel, Dar es Salaam.
View attachment 3195925
Na kwa serikalini mshahara chini ya laki nane kodi ipunguzwe
 
Sio kwamba jamaa anajitetea yeye? Mfano alikuwa akikulipa 500,000 wewe unachukua 400,000 halafu 100,000 inakuwa kodi. Wakisema chini ya 500,000 haina kodi anaanza kuwalipa watu wake 400,000 tu.
Wewe unapata 400,000 yako ile ile na yeye anaokoa 100,000 akiwa na wafanyakazi 100 hio ni 10m kwa mwezi savings.
nimewaza kama wewe ulivyowaza!
 
Back
Top Bottom