Huruma siyo malezi
JF-Expert Member
- Jul 18, 2020
- 1,433
- 3,210
Maisha hayana formula, wewe pambana tu huenda kesho ikawa zamu yako
Japo siyo kazi rahisi coz Kila njia ina miiba
Japo siyo kazi rahisi coz Kila njia ina miiba
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu umesahau kuwa dunia ni njia?.. waache wao wajenge njiani,Mimi najua kuwa hapa tunapita tu[emoji16][emoji16]Wale wa kupumua tu tunacomment wapi? [emoji16][emoji16]
[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]Ila tupambane aghalau tuache chumba kimoja na sebule.Mkuu umesahau kuwa dunia ni njia?.. waache wao wajenge njiani,Mimi najua kuwa hapa tunapita tu[emoji16][emoji16]
Kiranga!!!Hawa wengine hawana nyimbo wanasingizia nyumba.
Mtu anayetumia nyumba kupata demu siku akitetereka kiuchumi na demu anamkimbia.
He has no game. Not even Playstation.
Mjengo wa maana sanaNikiwa zangu nakimbia jogging nikifika kwenye huu mjengo huwa nautazama sn..kijichi kuna watu Wana hela banaView attachment 1815319
Kawaida ya binadamu tuna hulka ya kutamani tusichokuwa nacho.Kuna Mzee mmoja alikuwa anafanya kazi serikalini. Alikuwa mtu mkubwa kicheo.
Akawa kapandishwa cheo kikubwa kabisa kazini kwake.
Akapewa nyumba nzuri sana Oysterbay.
Karibu kabisa na ubalozi wa Marekani.
Watoto wake wakafurahi sana. Wakaona wanaenda kuhamia Oysterbay, tena karibu kabisa na Ubalozi wa Marekani.
Lakini, yule Mzee hakuwa mtu wa kupenda makuu.
Alisema anapapenda pale alipokuwa anaishi, maana pana sehemu kubwa, tena amezoeana sana na majirani. Wanaishi vizuri.
Zaidi, hakuona sababu za kuhamahama nyumba za serikali kwani alikuwa anakaribia kustaafu.
Watoto wake wakakasirika sana.
Wakasema Baba unaacha nafasi ya kuhamia Oysterbay, tena mtaa wa Laibon ukae jirani na rais Mwinyi na ubalozi wa Marekani?
Baba yao akasema ameshaamua.
Basi muda kidogo tu, ubalozi wa Marekani ukapigwa bomu. Ile nyumba ikapasukapasuka vibaya sana kwa sababu ilikuwa karibu sana na ubalozi wa Marekani.
Kama yule Mzee angehamia pale, familia yake ingeweza kuumia vibaya sana.
Watoto wale wakamuona yule mzee kama alikuwa na uwezo wa kuona yajayo.
Unaweza kutamani kitu kizuri, ukasononeka kukikosa.
Kumbe, usalama wako unakuja unapokikosa hicho kitu.
Ukikipata unapata balaa.
Zamani miaka ya themanini nakumbuka Upanga magari ya Halmashauri ya Jiji Dar es salaam yalikuwa yanazunguka kuzoa uchafu. Kila wiki gari la jiji linakuja mara moja.Niliwahi kusikia kwamba ilikuwepo hata miaka ya karibuni inayofanywa na watu binafsi. Magari yao yako wazi kabisa kule nyuma ni Malori ya kawaida tu. Sasa kama kuna upepo uchafu wote hupeperushwa mitaani na kufanya uchafuzi mkubwa sana.
Umenikumbusha story ya demu wa Uswahilini aliyeenda ushuani akasononeka kwa kuwa mitaa iko kimya sana, hakuna ngoma, hakuna kusutana.Kawaida ya binadamu tuna hulka ya kutamani tusichokuwa nacho.
Umasikini ni kitu kibaya sana kakini kwenye maisha Amani ya Nafsi ni bora kuliko chochote.
Magufuli alikuwa anapenda kwenda kwake CHATO mara kibao ingawa angeweza kuishi Osterbay, Ikulu.
Prod Mwandosya kaamua kukaa kwake huko Mbeya ingawa anaweza kuishi Masaki.
Jambo la msingi ni kuishi sehemu inayokupa Amani.
Na watu wengine pia wanapenda kuishi na watu wanaofahamiana nao ( kijamaa ) maana wanasema zimwi likujualo halikuli likakwisha, siyo kama Osterbay kila mtu ndani ya geti zito lenye umeme.
Leo kina Akon wametafuta pesa US lakini wamerudi Senegal ambako wanaheshimika zaidi.
Wacha wajenge wenye pesa zao kakaMjengo wa maana sana
Zamani miaka ya themanini nakumbuka Upanga magaribya Halmashauri ya Jiji Dar es salaamnyalikuwa yanazunguka kuzoa uchafu. Kila wiki gari la jiji linakuja mara moja.
Bula malipo ya ziada. Kwa kutumia bajeti ya jiji inayotokana na kodi tu.
Kama mji hauna huduma hii, tusijishebedue kufananisha maisha ya Dar na Ulaya.
Mimi nakumbuka wakati niko O-level mwanzoni nilikuwa nakaa na masela, msosi wa kugombania fujo nyingiii.Umenikumbusha story ya demu wa Uswahilini aliyeenda ushuani akasononeka kwa kuwa mitaa iko kimya sana, hakuna ngoma, hakuna kusutana.
Buza ushuani aende mbagalaNjoo kwangu Buza huku ujionee tunaosindikiza wenzetu!!
Huku tukijipa raha wenyewe!!!
Sent using Jamii Forums mobile app
Kama nakuona vile mapigo Haile Selassie fulani hivi, mpaka bustani zinahudumiwa na wafungwa!Mimi nakumbuka wakati niko O-level mwanzoni nilikuwa nakaa na masela, msosi wa kugombania fujo nyingiii.
Sasa, kuna Mkuu mmoja wa Magereza akapenda sana nikaishi kwake: Kwanza kuna kuku wa mayai, mayai kila muda, baiskeli za gia kibao nikapewa za kuendea shule.
Lakini imagine, nilikuwa sina amani moyoni just from within ( for no reason) kabisa ikabidi nirudi kwa masela🤣
Ist ipoo kwenye izo gariSas mm ndio nakupasha mkuu nmekutana nayo tena mbili katika road mbili tofaut maeneo hayo kelele zinazosikika ni za ndege tu na magar
Unafikiri shida nyumba.Nataman kuwa na nyumba kali.
Demu wangu asingeniacha kirahisi vile.
Kuanzia kijichi mpaka njia panda ya neluka shuka mpaka baharini daah ni next level kuleWiki jana nilienda kwa aunt yangu Kijichi kuna mitaa fulani ya ushuani flani. Sasa nikasahau namba ya nyumba na jina la mtaa maana wana vimitaa vidogo vingi. Akawa hapatikani kwa simu, yeye alijua napakumbuka. Nilikuwa nakumbuka njia mbili, ya kutokea kwa Zombe yule askari au ya kutokea kwa Filikunjombe.
Kilichonichanganya katikati mitaani nilikutana na mbwa koko wengi kuliko watu. Yani Kijichi kuna mijibwa mingi njiani. Nikakumbuka hata kwetu pale sisi ndio wa kishua, mapaka hayakomi kuzalia kwetu ila sijawahi ona yanazaliana kwa majirani.
Conclusion niliyopata: hata mbwa koko na mapaka yanajua wapi kuna makombo yakushibisha. Wanapokula miguu ya kuku na kutafuna mifupa yote hawawezi tembelewa na mbwa koko hata siku moja.
Jamani tutafute hela hata wanyama watuheshimu.
Masikini kashaamka sasa tujiandae na porojoMkuu maisha ya huko oysterbay nimeishi sana tena ktk hiyo mijumba ya kifahari ila asikwambie mtu mkuu mambo yanayotokea usiku ni hatari sana yaani hao wenye hiyo mijumba wanafuga viumbe vyakutisha
Amini mkuu hao watu wanamaagano yakishirikina
Shukuru Mungu kwa kila jambo,saa nyingine Muumba anajua kuwa ungekuwa na hela saa hizi ungeshakuwa umekufa,kwahiyo ili kukunusuru ni bora uishi hivyo hivyo kiugumu...
Weka na mjengo wa meliNikiwa zangu nakimbia jogging nikifika kwenye huu mjengo huwa nautazama sn..kijichi kuna watu Wana hela banaView attachment 1815319
Usiumie sana ukasahau "Kuishi" endelea kufurahia maisha yako huku ukitafuta,
Usihuzunike sana coz humo ndani ya hizo nyumba hujui nao pia kuna matatizo yao wanayoyapitia,inaweza kua ni matatizo ya kiafya,kifamilia au matatizo mengine yeyote yale,
Usisubiri mpaka utimize jambo fulani ndio uwe na furaha,unaweza kutimiza jambo hilo kisha ukawa na furaha ila baadae ukaja kuona kua jambo hilo ni la kawaida tu,Siku zote omba afya njema na uzima huku ukiendelea kutafuta.