Hapa jirani yangu pana nyumba haijawahi kukaliwa na watu tokea ikamilike kujengwa. Ni mwaka wa 10 huu, mpaka geti linaanza kuoza. Nijitwalie?

Wewe ni mwizi
 
Mkuu hii ni mkoa gani?
 
Unaweza kuichukua,lkn ukajikuta kwenye matatizo makubwa.Ukute nyumba hiyo ina Mazingaombwe mengi yaani full vibwengo na mauzauza.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Una low mind San ukafamie nyumba ya watu kiss ujamuona mmiliki kwa muda mrefu [emoji848]

Sasa naungana na bibie [emoji1663] kuwa shuleni mlikwenda kusomea ujinga ????
 
Nyumba za namna hiyo zipo nyingi mno hasa jijini Dar es salaam.

Mahali ninapoishi,kuna nyumba zimejengwa kwa mfuatano zikiwa 3,inasemekana Mzee anao watoto 3 aliamua kuwajengea hizo nyumba,mzee alifariki ila madogo wapo wanaishi nje ya nchi!

Walikuja kipindi fulani( Zaidi ya mika 10 iliyopita) wakaangalia zile nyumba na mahali zilipo wakasema hawazihitaji!.

Kuna Sheikh mmoja ameamua kujimegea moja anaishi na familia yake,zile nyingine 2 zinazidi kuota nyasi tu na nyoka kujazana huko ndani!.

Nyumba ni nzuri na naza kisasa mno!,lakini madogo walisema hawawezi kuja kuishi Tanzania.

Sasa wenyeji kila mmoja anaogopa na kusema wanaweza kushitakiwa,lakini ukweli ni kwamba hakuna mtu wa kukushitaki wala nini!.

Ngoja nivute muda,mwakani nasafisha moja naingia,mdogo mdogo hadi inakuwa yangu!

Maana kwa dalili zilizopo hakuna wa kuhoji zaidi ya kuendelea kuchakaa!,Siku watu wa Ardhi wakishituka zitakwenda na maji!.

Mwakani najimilikisha moja!
 
Mimi ubavuni kwangu kuna viwanja 2 double sijui vya mtu mmoja au la.
Tangu 2020 nianze kuja huku mara kwa mara na 2021 nilipohamia sijamwona mwenyewe.
Nalima mbogamboga na mihogo.
Nawaza sijui nipige ukuta kote au nitulie kwanza.
Wanadamu tuache ubinafsi, mali zako mtu hutaki hata kumeonyesha mke ukifa je!
 
Safi. Kuitwaa nyumba siyo lazima ufanye vitu vikubwa sana.

Unaweza ukuwa unaenda kuwasha taa na kuzima, kama umeme upo

Mwagilia maua

Panda miti

Kaa kibarazani😀

Fungua na kufunga milango

Washa moto upike

Fanya vikao vya familia

Lima majani huko nje

Panda ukoka

Safisha dari ondoa bui bui

Nenda msalani

Fukuza watoto wanaocheza kibarazani

Fanya jambo lolote ambalo litakupa hadhi ya umiliki.
 

Mkuu haya yote nitayafanya,Ahsante kwa mbinu 🤣
 
Dadeki🙆

Ndiyo maana nikinunua kiwanja au shamba, kama sina hela ya kujenga nitachimba mashimo, au ninakilima nusu, kama kuna miti ninapruni.

Nikishindwa yote hayo ninaenda hapo ninakaa nakula muwa naacha maganda.

Yote hayo ni kuonyesha uhai kwamba hili eneo lina mwenyewe na huenda alitoka hapa siku 1 au 2 zilizopita.
 
Kisheria hii inatwa 'bad means for good motive'.

Umezulumu kwa malengo mema.

Sasa je, umezulumu kweli? Na je lengo lako ni jema?

Majibu hapo yanategemeana na mawazo yako na ya mtu anayepata huu mkasa.

Vipi, rafiki yako alikuwa anaendesha boda au gari? Kwa sababu hujasema aligongana na lori akiwa na usafiri gani
 
Inategemea na Nyumba iko wapi..
Kama Nyumba iko Sumbawanga,Tanga,Zanzibar,Pemba,Shinyanga....
Mkuu Iogope kama Ukoma!

Ila kama iko Dodoma ,Singida, Morogoro ,Arusha mzee we ingia safisha Kabisa iyo mali yako...

Ila hiyo mikoa nilokukataza unaweza geuka Chakula cha Majini au Misukule..

Usiseme hukuambiwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…