Hapa jirani yangu pana nyumba haijawahi kukaliwa na watu tokea ikamilike kujengwa. Ni mwaka wa 10 huu, mpaka geti linaanza kuoza. Nijitwalie?

Hapa jirani yangu pana nyumba haijawahi kukaliwa na watu tokea ikamilike kujengwa. Ni mwaka wa 10 huu, mpaka geti linaanza kuoza. Nijitwalie?

Kuna nadharia mbili hapa.

1. Yawezekana mmiliki alikuwa anamjengea mchepuko. Ili siku moja aje amfanyie surprise. Lkn kabla ya surprise jamaa akapata ugonjwa ama ajali na kufariki. Kwahiyo si mchepuko wala familia waijuao nyumba hii.

2. Mmiliki alipoikamilisha alipiga kifungo cha miaka 30 au zaidi jela.

Je, nijitwale hii nyumba? Vipi kama nadhria ya 2 ndiyo sahihi? Akitoka jela na kurudi uraiani itakuwaje? Ingawa kuna usemi wa kiswahili unanipa moyo "cha kuokota siyo cha kuiba, mwenye mali mpumbavu".

😄😄, pole sana SELEMAN, nakushauri kazana kutafuta hela.
 
Kuna nadharia mbili hapa.

1. Yawezekana mmiliki alikuwa anamjengea mchepuko. Ili siku moja aje amfanyie surprise. Lkn kabla ya surprise jamaa akapata ugonjwa ama ajali na kufariki. Kwahiyo si mchepuko wala familia waijuao nyumba hii.

2. Mmiliki alipoikamilisha alipiga kifungo cha miaka 30 au zaidi jela.

Je, nijitwale hii nyumba? Vipi kama nadhria ya 2 ndiyo sahihi? Akitoka jela na kurudi uraiani itakuwaje? Ingawa kuna usemi wa kiswahili unanipa moyo "cha kuokota siyo cha kuiba, mwenye mali mpumbavu".
Acha ufala pangisha hiyo nyumba
 
Kwa nyumba sijui ipoje ila kwa kiwanja afadhali
Mi nilijipatia kiwanja kwa namna hiyo
Kilikuwa ubavuni kwangu na mwenyewe hakuwahi kuonekana
Nikaenda ardhi nikawaeleza wakaniambia kasafishe kwanza ukiona kimya weka msingi tulia

Nilifanya hivyo na hakutokea mtu lakini palikuwa ma tofali 12 pale chini
Baada ya mwaka nikaenda ardhi nikawaeleza wakanipa offer/hati na hadi leo napamiliki
 
Kwa nyumba sijui ipoje ila kwa kiwanja afadhali
Mi nilijipatia kiwanja kwa namna hiyo
Kilikuwa ubavuni kwangu na mwenyewe hakuwahi kuonekana
Nikaenda ardhi nikawaeleza wakaniambia kasafishe kwanza ukiona kimya weka msingi tulia

Nilifanya hivyo na hakutokea mtu lakini palikuwa ma tofali 12 pale chini
Baada ya mwaka nikaenda ardhi nikawaeleza wakanipa offer/hati na hadi leo napamiliki
We ni mwizi
 
kuna ndugu yangu alikiwa mfanyabiashara mkubwa wa mazao, kuna mkoa alienda katika shughuli zake sehemu ya faida alinunua kiwanja ambacho kilikuwa na msingi teyari.

Kwa bahati mbaya makabidhiano ya nyaraka muhimu hayakukamilika ila kwakuwa alikuwa na uhakika akawa amefuata mzigo mwingine.

Aliporudi mkoai ilipo familia yake akawapa hiyo taarifa kuwa kuna kiwanja kanunua mkoa fulani wilaya flani na jinsi kilivyo,

Wakati anajipanga ili kupeleka mzigo tena kwenye ule mkoa akapatwa na maradhi na hayakumchukua siku nyingi akawa amefariki na story ya hicho kiwanja ikaisha kwa namna hiyo.
 
Ngoja niwape kisa kimoja

Kuna jamaa zangu Mzee wao alifariki akawa amewaachia nyumba za urithi, sasa baada ya miaka mingi kupita Kuna nyumba walikua wanaiuza. Katika kupekua mafaili wakampa mnunuzi document ili ajiridhishe. Yule mnunuzi kaenda ardhi anakuta ile document ni ya nyumba nyingine kabisa tofauti na ile aliyopanga kununua

Akajulisha jamaa wakamtaftia document sahihi wakafanya biashara. Sasa jamaa wakaanza kujiuliza hii document ya mara ya kwanza ni ya wapi mbona hii nyumba hatuijui. Wakafatilia kushirikiana na ardhi mpaka kwenye Hio nyumba, wakamkuta Mzee mmoja anaishi hapo baada ya kumhoji Mzee akadai alipewa Hio nyumba Aishi na Mzee mmoja ila ana miaka mingi hawajawasiliana na hajui hata yupo wapi.

Jamaa wakawa wamepata nyumba nyingine kilaini kabisa na hakuna aliyekua anaijua.
Mkuu unajaribu kumshauri nini mdau😅😅
 
Kwa nyumba sijui ipoje ila kwa kiwanja afadhali
Mi nilijipatia kiwanja kwa namna hiyo
Kilikuwa ubavuni kwangu na mwenyewe hakuwahi kuonekana
Nikaenda ardhi nikawaeleza wakaniambia kasafishe kwanza ukiona kimya weka msingi tulia

Nilifanya hivyo na hakutokea mtu lakini palikuwa ma tofali 12 pale chini
Baada ya mwaka nikaenda ardhi nikawaeleza wakanipa offer/hati na hadi leo napamiliki
Acha wizi mkuu
 
Back
Top Bottom