Hapa jirani yangu pana nyumba haijawahi kukaliwa na watu tokea ikamilike kujengwa. Ni mwaka wa 10 huu, mpaka geti linaanza kuoza. Nijitwalie?

Majirani wananilindia na mawasiliano yapo
 
Mwaka 2009 tulienda na rafiki yangu Bunju kununua Viwanja,tukaanza kujenga mdogomdogo lakini rafiki yangu (RIP)alijenga fasta ikabaki kupaua tu(kumbuka wote tulikuwa mabachela). Siku moja anatoka site akapata ajali Tegeta(aligongana na Lori),alifariki palepale. Huyu rafiki yangu tulikuwa tumepanga nyumba moja Sinza(yeye Chumba chake,mimi changu lakini sebule,jiko nk tunashea. Tangu tunanunua Viwanja mpaka anafariki hakuna aliyewahi kumpeleka site ndugu,rafiki wala jamaa. Hivyo nyumba niliiokota kwa style hiyo,niliipaua,nikaifanyia finishing na sasa nakula Kodi. Lakini kwa kuwa tulikuwa tumeshibana sana hivyo huwa najitajidi kuwatumia Pesa Wazazi wake Moshi kila mwezi,na wamekuwa kama Wazazi wangu na wananiita mwanao.
SWALI KWA NINI SIKUIPA TAARIFA FAMILIA HIYO?huyu Marehemu rafiki yangu ndie aliyekuwa amesoma kwao,Kaka na Dada zake wote ni wale waleviwalevi waliojichokea tu,hivyo kama ningetoa taarifa naamini wangeshauri nyumba iuzwe tu wapate Pesa ya kunywea pombe. Tangu niikamilishe mwaka 2011 mpaka leo nakula Kodi tu,Hati nilishaipata kwa jina langu na maisha yanasonga.
 
Kama unataka kuishi na majini, twaa jengo hilo.
 
Kuna mtu atakuja kusema ni dhulma!Mungu kakupa hiyo nyumba utunze hao wazee.
 
Abandoned house itiazame nyumba vizuri je imechakaa kama haijachakaa basi juwa kuna roho umo zinaishi, ukitaka kuiokota anza kuibadili rangi paka rangi mpya alafu tulia ila umo akukosi majini na kuwaamisha hivi hivi sio rahis mpka mwenye mji aje
Kwani majini hayana nyumba zao huko ujinini?yaache kuzingua
 
Jini gani hilo ambalo haliogopi jina la Yesu?. Kwa nini kujitia hofu wakati Yesu yupo?. Au unadhani Yesu alikuja duniani kuzurura?.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…