Hapa ndio ninapokuwa na walakini na uwepo wa Mungu

Hapa ndio ninapokuwa na walakini na uwepo wa Mungu

Kama ni hivyo mbona hatuoni duniani dini kuzuiliwa kwa sababu zinaeneza mafundisho yao ya imani waziwazi kwa watu ambao unasema ni kusambaza uongo? Hebu elezea nielewe.
Dini ni uhuru wako wa kikatiba.

Lakini kupewa uhuru wa kikatiba kuamini kwenye dini, sio kigezo cha kufanya imani za kidini ziwe za ukweli.
Huko kumfosi mtu kukubali imani ndio kunafanyikaje hebu toa mifano wewe ushawahi kufosiwa kukubali imani bila kinyume na ridhaa yake au umeona humu JF watu wakifosiwa kukubali imani fulani?
Nyuzi za kumkiri na kumwamini Yesu ni nyingi sana hapa JF. Wakristo wanapiga kampeni za huyo Yesu akubalike na kila mtu.

Nyuzi za kusilimu na kumwamini Allah ni nyingi sana hapa JF . Waislamu wamekuwa wakipiga kampeni Allah wao na mtume Muhammad akubalike na kila mtu.
Unasema msingi wa imani ni kutokuwa na uhakika na uthibitisho halafu hapo hapo unasema imani hiyo hiyo isipokuwa na uthibitisho ni uongo, hivi kweli hata wewe umeelewa kweli mkuu?
Yani msingi wa imani ni kutokuwa na uthibitisho ila hapo hapo unataka kuonyesha kuwa kuna imani zenye uthibitisho na ambazo zimekosa uthibitisho, kwa kweli ni ngumu kuelewa hapo.
Imani ya aina yeyote ile ni kutokuwa na uhakika wala uthibitisho.

Ukishakuwa na uhakika na uthibitisho juu ya jambo fulani, Hiyo sio imani tena.
 
Lete

Lete ushahidi usio na shaka kuhusu uwepo wake.

Kwa hiyo akiamini nyonzo ndio shonvi naye autambue kuwa ukweli?

Ukweli hakuna Mungu hapa duniani.
Ukweli hauwi ukweli kwa sababu wewe umesema tu ni ukweli, nimekutolea mifano kuonyesha huko kusema hakuna Mungu huo ni mtazamo wako tu na wengine nao wana mitazamo yao tofauti, sasa wewe umekazana kusema kutokuwepo kwa Mungu ndio ukweli halafu hauna cha kushawishi watu wakubali kuwa huo ndio ukweli na si mtazamo tu wa baadhi ya watu ambapo umezaliwa umeukuta.

Kama kutokuwepo ushahidi usio na shaka wa uwepo wa Mungu ndio inatoa tafsiri ya moja kwa moja kuwa hakuna Mungu basi hata Agnostics nao wangesema wazi hakuna Mungu kama usemavyo wewe, ila kwa kuwa kukosekana ushahidi hakutoi tafsiri ya moja kwa moja kuwa hakuna Mungu basi ndio maana Agnostics hawadai hakuna Mungu kama unavyodai wewe.

Ambacho wewe huelewi ni kwamba unaposema kwa uhakika kabisa kuwa Mungu hakuna inakuwa umetoa madai, sasa hauwezi tena kusema mimi nithibitishe ili kupinga unachokidai wewe. Unachokidai wewe kithibitishe mwenyewe.
 
Kama ni hivyo basi usingekuwa unajiingiza kwenye mabishano ya kuhusu Mungu,
Huwezi kuniambia kwamba nisijiingize kwenye mabishano kuhusu Mungu, Wakati habari za uwepo wa Mungu zinaletwa hapa JF kwenye public forum ambako pia kuna sisi tusio amini Mungu.

Ukileta imani yako hapa kwenye public forum JF kuhusu uwepo wa Mungu na wakati huohuo unajua kwamba kuna wasio mwamini Mungu, Basi unakuwa umeiweka hiyo imani yako kikaangoni.

Inaweza kufanywa vyovyote na yeyote.

Ukitaka imani yako ya Mungu isiguswe na yeyote, Baki nayo hukohuko moyoni mwako au kwenye nyumba zenu za ibada.

Lakini mkileta hizo imani na dini zenu hapa JF kuhusu Mungu, Tutazikosoa na kuzichambua.
maana ni sawa na kukuta watu wanajadili tuhuma za Kikwete kumfunga Babu Seya kwa sababu za wivu wa mapenzi halafu ukajiingiza katika hayo majadiliano mwenyewe kisha unasema kwanini watu wamtetee Kikwete na sio Kikwete ajitokeze ajitete mwenyewe tuhuma zake.
 
Dini ni uhuru wako wa kikatiba.

Lakini kupewa uhuru wa kikatiba kuamini kwenye dini, sio kigezo cha kufanya imani za kidini ziwe za ukweli.

Nyuzi za kumkiri na kumwamini Yesu ni nyingi sana hapa JF. Wakristo wanapiga kampeni za huyo Yesu akubalike na kila mtu.

Nyuzi za kusilimu na kumwamini Allah ni nyingi sana hapa JF . Watu wamekuwa wakipiga kampeni Allah wao na mtume Muhammad akubalike na kila mtu.

Imani ya aina yeyote ile ni kutokuwa na uhakika wala uthibitisho.

Ukishakuwa na uhakika na uthibitisho juu ya jambo fulani, Hiyo sio imani tena.
Sasa mbona hatuoni dini kuchukuliwa hatua za kisheria kwa kusambaza uongo kwenye jamii?

Sasa watu kuweka nyuzi za mambo ya imani ndio kumfosi mtu mwengine kuamini jambo bila ridhaa ambapo ni kinyume na sheria?

Ndio maana nasema wewe unapinga imani.
 
Ni Mungu gani anaemtoa mwanae kafara? Hiyo kitu ilitungwa na wayahudi na ikaenea karibu dunia nzima. Walitumia uchawi gani? Eti Mungu kagawanyika sehemu tatu, huo sio uhuni?
 
Huwezi kuniambia kwamba nisijiingize kwenye mabishano kuhusu Mungu, Wakati habari za uwepo wa Mungu zinaletwa hapa JF kwenye public forum ambako pia kuna sisi tusio amini Mungu.

Ukileta imani yako hapa kwenye public forum JF kuhusu uwepo wa Mungu na wakati huohuo unajua kwamba kuna wasio mwamini Mungu, Basi unakuwa umeiweka hiyo imani yako kikaangoni.

Inaweza kufanywa vyovyote na yeyote.

Ukitaka imani yako ya Mungu isiguswe na yeyote, Baki nayo hukohuko moyoni mwako au kwenye nyumba zenu za ibada.

Lakini Mkileta hizo imani na dini zenu hapa JF kuhusu Mungu, Tutazikosoa na kuzichambua.
Sasa kama ni hivyo basi usiseme hautaki watu wamtetee Mungu na kutaka Mungu ajitete mwenyewe, unaingia kwenye majadiliano ya watu kuhusu Mungu halafu unataka hao watu wasijadili wao kuhusu Mungu unataka ajitokeze Mungu mwenyewe hiyo ni akili ya wapi?

Yani wewe unakuta watu wanajadili tuhuma ya Rais Samia iliyoandikwa kwenye kutabu kuwa alikoswa kubakwa halafu unawaambia hao watu waache kujadili na kutaka ajitokeze Samia mwenyewe.
 
Sasa mbona hatuoni dini kuchukuliwa hatua za kisheria kwa kusambaza uongo kwenye jamii?
Nimekwambia dini ni uhuru wa mtu kikatiba.

Una uhuru wa kuamini chochote utakacho, Haijalishi ni ukweli au Uongo.

Hata ukiamua kuamini mawe, miti, mapango, milima n.k
Sasa watu kuweka nyuzi za mambo ya imani ndio kumfosi mtu mwengine kuamini jambo bila ridhaa ambapo ni kinyume na sheria?
Ukianza kuhubiria watu kwamba imani yako ni bora sana kuliko ya kwake.

Hapo unaanza kufosi imani yako ionekane bora kuliko ya kwake.
Ndio maana nasema wewe unapinga imani.
Ndio napinga Imani.

Ila naheshimu wenye hizo imani.
 
Sasa kama ni hivyo basi usiseme hautaki watu wamtetee Mungu na kutaka Mungu ajitete mwenyewe, unaingia kwenye majadiliano ya watu kuhusu Mungu halafu unataka hao watu wasijadili wao kuhusu Mungu unataka ajitokeze Mungu mwenyewe hiyo ni akili ya wapi?
Na wewe kwa nini unataka nisijadili hivi ninavyo jadili?

Kila mtu ana uhuru wa kujadili atakavyo.

Sasa wewe unataka mimi nijadili jinsi wewe unavyo fikiri, Badala ya jinsi mimi mwenyewe ninavyo fikiri?

Na wewe hii ni akili ya wapi?
Yani wewe unakuta watu wanajadili tuhuma ya Rais Samia iliyoandikwa kwenye kutabu kuwa alikoswa kubakwa halafu unawaambia hao watu waache kujadili na kutaka ajitokeze Samia mwenyewe.
Vipi kama hicho kitabu ni uongo?

Tutahakikisha vipi hicho kilicho andikwa kwenye kitabu kumhusu Rais samia ni ukweli?
 
Nimekwambia dini ni uhuru wa mtu kikatiba.

Una uhuru wa kuamini chochote utakacho, Haijalishi ni ukweli au Uongo.

Hata ukiamua kuamini mawe, miti, mapango, milima n.k

Ukianza kuhubiria watu kwamba imani yako ni bora sana kuliko ya kwake.

Hapo unaanza kufosi imani yako ionekane bora kuliko ya kwake.

Ndio napinga Imani.

Ila naheshimu wenye hizo imani.
Sasa kama dini ni uhuru na ni ruksa kusambaza imani bila kujali ni ukweli au uongo sasa shida yako wewe hapo ni ipi? Watu wanatumia uhuru wao hata wewe unao uhuru wa kudai Mungu hakuna huvunji sheria.

Kama unaheshimu wenye hizo imani mbona unapinga wasitangaze imani zao?
 
Na wewe kwa nini unataka nisijadili hivi ninavyo jadili?

Kila mtu ana uhuru wa kujadili atakavyo.

Sasa wewe unataka mimi nijadili jinsi wewe unavyo fikiri, Badala ya jinsi mimi mwenyewe ninavyo fikiri?

Na wewe hii ni akili ya wapi?

Vipi kama hicho kitabu ni uongo?

Tutahakikisha vipi hicho kilicho andikwa kwenye kitabu kumhusu Rais samia ni ukweli?
Sio mimi nakukataza kujadili bali wewe ndio hautaki watu kujadili kuhusu Mungu, unataka Mungu mwenyewe ajitokeze hautaki watu kumtetea.
 
Sasa kama dini ni uhuru na ni ruksa kusambaza imani bila kujali ni ukweli au uongo sasa shida yako wewe hapo ni ipi? Watu wanatumia uhuru wao hata wewe unao uhuru wa kudai Mungu hakuna huvunji sheria.

Kama unaheshimu wenye hizo imani mbona unapinga wasitangaze imani zao?
Wapi nimepinga wasitangaze imani zao?

Mimi napingana na imani zao wanazo zitangaza.

Sipingani na wao kutangaza imani zao.

Ndio maana hakuna anaye kuzuia kuanzisha uzi hapa JF kuhusu imani yako.

Lakini ukianzisha uzi hapa JF kutangaza imani yako, Tutapinga hiyo imani yako kwa hoja.

Hatupingi watu kutangaza imani zao, Tunapinga hizo imani zinazo tangazwa.

Una elewa?
 
Sio mimi nakukataza kujadili bali wewe ndio hautaki watu kujadili kuhusu Mungu, unataka Mungu mwenyewe ajitokeze hautaki watu kumtetea.
Mimi sitaki watu wasijadili kuhusu Mungu.

Kujadili ni uhuru wako wa kikatiba.

Mimi napingana na hizo imani kumhusu huyo Mungu anayejadiliwa.
 
Kasome kitabu cha Ayubu kina unabii mkubwa sana pale..lakini pia wakati una nafasi ya kuandika haya ukiwa na simu janja yenye network, bundle na chaji wakumbuke pia
Waliojibanza vibarazani wasio na makazi
Wagonjwa mahospitalini
Wafungwa magerezani
Nknk
Hayo nduo yanatia mashaka ya huyu mwenye upendo na uwezo wote
 
Ebu soma hili andiko kwanza then ukae ujifikilie:



Dunia hii imepitia uongo/utapeli/propaganda kubwa sana na zikapita lakini uongo pekee ulio dumu kwa muda mrefu ni huu

Hebu fikiria unaambiwa kuna MUNGU muweza wa yote yupo sahihi na hajawahi kukosea

Ameumba dunia kwaajili yetu na ataiangamiza dunia kwaajili yetu
Alijua ataiangamiza dunia kabla hata hajaiumba lakini aliiumba hivyo hivyo ili aje kuiangamiza,
Ameumba moto wa jehanamu kwakuwa ametuumba tukosee ili atuchome moto japo alikua na UWEZO wakutuumba tusiwe wakosefu ili atuumbie Pepo tu tukale bata

Anajua tunacho hitaji lakini lazima tumuombe ili atupe, lakini hata tukimuomba hatupi tunavyo taka sisi maana tayari amekwisha tupangia kila mtu atampa nini, ataishije na atakufaje

Ndio muumba wa kila kitu(magonjwa, bangi, majini, ulabu nk) na anaweza kudhibiti chochote lakini anamlaumu msaidizi wake muasi(Shetani) kuleta mambo hayo mabaya duniani(magonjwa nk) kwa watu wake aliyewaumba wakati yeye ndiye aliye mtupa msaidizi wake huyo huku duniani
Yaani yeye kashindwana naye huko mbinguni kaja kumtupa kwetu sisi viumbe dhaifu tupambane naye na tukishindwa tutachomwa moto milele, lakini anasisitiza anatupenda sana kama mtu anavyopenda na kujali mboni ya jicho lake

Hebu tafakari hili, kawaumba Adam na Hawa na wakati bado wageni duniani akawatupia Nyoka(Shetani) ili awarubuni, na kwa ugeni wao wakarubunika matokeo yake katupa adhabu ya shuruba watu wote hata ambao tulikua hatupo na hata ambao hawajazaliwa chamoto watakiona...... Not fair

Mungu muweza wa yote hayupo WAZI PASI NA SHAKA kwa watu wote kujua huyu ndio MUNGU badala yake Mungu ndio amekua sehemu kubwa ya mgawanyiko wa watu na kusababisha kuwa na imani za MIUNGU zaidi ya milioni dunia nzima
Na kibaya zaidi unatakiwa to blindly believe him, usihoji wala kuwa na shaka juu ya uwepo wake(ni laana na kufuru) vinginevyo moto wa milele unakuhusu

Yaani kuna Fundi Kapenta mmoja huko Galilaya eti kafa kwaajili ya dhambi za watu wote duniani.... seriously
ADKq_NanOtSrTiofgZ8GKcrlzUppoPN47uaEWRTLnWp5aOLqj1Fw2UVggrKgTMaoQYkbbLqm7AaSh9qlGSTCUjtkL8U=s0-d-e1-ft
?
Akaitwa Mungu lakini Mungu huyu akajaribiwa na shetani
ADKq_NanOtSrTiofgZ8GKcrlzUppoPN47uaEWRTLnWp5aOLqj1Fw2UVggrKgTMaoQYkbbLqm7AaSh9qlGSTCUjtkL8U=s0-d-e1-ft

Fundi kampenta huyu hakuandika kitabu chochote ila wahuni walio kuwa wanampinga ndio wakaja kuandika vitabu kuhusu fundi huyu na vinaitwa “Bibilia Neno la Mungu takatifu”
Mabilioni ya watu dunia kote wanakesha makanisani wakimlilia na kumuomba awape uponyaji, mali, waume/wake nk

Hebu fikiria huko Arabia kuna Maamuma mmoja hajui kusoma wala kuandika alidai anashushiwa maagizo na Mungu kukata vichwa watu wote watakao pinga na kutokutii maagizo yake, “akashushiwa” aya za vitisho na neema kwa watakao tii, yaani ukifa unampigania Mungu unakwenda kupewa mbikra 72 kazi yako ni kuzagamua tu
ADKq_Nbuw1UIZCqE5Y9pLRPZlhZlI-SOFRzVgM7CzwW1Eqs44ilAgX075S52J_2AK051Ru4F1ybI2CJ3ABIuxUe5vxc=s0-d-e1-ft
ADKq_Nbuw1UIZCqE5Y9pLRPZlhZlI-SOFRzVgM7CzwW1Eqs44ilAgX075S52J_2AK051Ru4F1ybI2CJ3ABIuxUe5vxc=s0-d-e1-ft
ADKq_Nbuw1UIZCqE5Y9pLRPZlhZlI-SOFRzVgM7CzwW1Eqs44ilAgX075S52J_2AK051Ru4F1ybI2CJ3ABIuxUe5vxc=s0-d-e1-ft

Mabilioni ya watu duniani wanasujudu mara 5 kwa siku na kushinda njaa mwezi kila mwaka ili wakale naye bata Peponi

Kwamba maisha yako hapa duniani ni ya mpito tu maisha yako yapo baada ya kufa
Unachotakiwa kufanya ni kumuamini na kufanya aliyoa agiza ili ukale bata sana baada ya kufa
🤣🤣 problem of Evil..
Mungu Yupo Sema Tunatakiwa Kuchunguza zaidi Kumjua
 
Wapi nimepinga wasitangaze imani zao?

Mimi napingana na imani zao wanazo zitangaza.

Sipingani na wao kutangaza imani zao.

Ndio maana hakuna anaye kuzuia kuanzisha uzi hapa JF kuhusu imani yako.

Lakini ukianzisha uzi hapa JF kutangaza imani yako, Tutapinga hiyo imani yako kwa hoja.

Hatupingi watu kutangaza imani zao, Tunapinga hizo imani zinazo tangazwa.

Una elewa?
Mtu kutangaza imani yake unaita ni kuforce na kwamba ni kosa.
 
Back
Top Bottom