Hapa ni wapi? Trafiki wadakwa kwenye video wakichukua Rushwa mara kadhaa

Hapa ni wapi? Trafiki wadakwa kwenye video wakichukua Rushwa mara kadhaa

Hivi trafiki ana safari kweli? Per diem yake sh ngapi?

Kuna dubwasha per diem yake ni mshahara wa mtu na ana safari na marupurupu kibao kila mwezi na bado anapiga hela kwenye miradi unaona mambo hayaendi waziwazi.

Sasa mtakapo anza kuwashughulikia hawa msiwasahau na hao madubwasha/mabwanyenye.
 
Kuna foleni inaanzia pale sokota unakutana na malori yanatoka bandarini upo kwenye daladala hapo unaenda mbezi na huku pembeni service road kuna daladala zinapita wanatoa hela kidogo kwa trafic sasa utachagua ukae kwenye foleni ya malori au ubariki kile anachotoa kondakta kwa trafik ili mpite service road
Kiufupi acheni unoko wenzenu wakale wapi)
 
Ndo yaleyale ya kuwanyooshea vidole wanawake wanaojiuza na kusahau kuwa kuna miamba inawanunua.
Anayetoa rushwa na anayepokea rushwa wote ni walewale but shutuma zinaenda kwa hao ndugu zetu utafikiri hizo pesa walikuwa wameweka tangazo wapelekewe - check watu wanajipeleka wenyewe tena kwa utaalamu wa hali ya juu -
Tusiwanyanyapalie polisi pekee -
 
View attachment 3202420

Hizi rushwa kiroboto( rushwa ndogo ndogo) ndio zinawapa kiburi madereva wa daladala kuvunja sheria za barabarani mchana kweupe.

Dereva huwa anajiambia mtanifanya nini, Traffic polisi Janeti tunakula pamoja.

TAKUKURU, mmeiona hii clip inatembea mitandaonikwa kasi.
Rushwa imefanywa kuwa mfumo rasmi wa polisi
 
Hatimaye Sasa Geshi Limeingia Aibu
Kamanda Wankyo Ramadhan Nyegesa
aliomba Nafasi Ya Kunyoosha Geshi La Police
 
Hakuna utaratibu wala maadili ya kondakta wa daladala kushuka na kwenda kwa 'traffic police' anashikana mkono akiwa amekunja ngumi na kuikunjua wakati bado wameshikana; Hakuna mazungumzo yoyote yanayofanyika hapo ya sababu ya kuisimamisha daladala kisha kondakta kushuka na kwenda kwa askari wanashikana mkono anaondoka halafu trafiki anaweka kitu kwenye pochi ya kuwekea mashine ya EFD.

Madereva na kondakta wanakiri bila kutoa chochote kila tripu anayofanya atakamatwa na kuorodheshewa makosa mengi sana ambayo kuyalipa ni mpaka wamtaarifu tajiri ambaye wanatambua huwa hawataki kusikia zaidi ya kupelekewa marejesho waliyopangiwa..

Hao askari polisi wakichukuliwa hatua na hao makondakta na dereva ya Rumion nao wachukuliwe hatua za kisheria pia.

Mtoaji na mpokeaji rushwa wote kosa lao ni moja.
Watangaze ila usiendeshe gari yako ilionamakosa kibao barabarani na ww usifanye makosa through barabarani sasa ndio mtawajua wao nani
 
hamna lolote
geresha tu hiyo.
ni wapi wahusika wametajwa au ni wa nafasi zipi au wanatoka kituo gani au nao ni wale wasiojulikana?
 
Tukitaka haki anzeni na hao mapapa..

Vidagaa vinakusanya hela ndogo ambazo hata zikihesabiwa mwaka hazifiki robo ya wanazochukua hao mapapa.

Sitetei wafanya hiyo ila tutume na clip za hao mapapa wanavyokwapua hela zetu huko sio kuwaonea hawa tu.
Kosa moja halihalalishi kosa lingine.
Two wrongs don't make it right.
 
Kosa NI kupokea au kutoa au vyote kwa pamoja?
Kama kosa n kupokea basi safari ndefu,na kama n kutoa na kupokea kuna upande bado haujasikilizwa
 
Hao waachwe bana!

Sasa watu wakale wapi ilhali hawalipwi living wage?

Let them be.
 
Take home ya traffic wa Dar kila siku ni laki mbili hadi tatu 😁
 
Mbon
Hapa ni wapi, hawa wanajulikana, Kamanda Mulilo, IGP Wambura hapana naona mtaharakisha kutoa press Release kama vile mwafanyaga kwenye matukio mengine.

Zaidi kongole kwa camera man wa kujitegemea.


Updates: Polisi yachukua hatua juu ya hili
MBona CCM inaiba kura na hastuki.??

Waache maafande na wao wapate pesa ya mboga.
Kila mtu achukue chake mapema
 
Tunahangaika na vidagaa tunawaacha mapapa serikalini waokwapua mabilioni ya hela kwenye miradi .
Tena hela ambazo zimekusanywa tayari.. Si bora huyu ni hela ambayo hata haijaingia serikalini..
Mleta mada amejitahidi kukamata dagaa basi nawe jitahidi leta hata perege
 
Back
Top Bottom