Hapa ni wapi? Trafiki wadakwa kwenye video wakichukua Rushwa mara kadhaa

Hapa ni wapi? Trafiki wadakwa kwenye video wakichukua Rushwa mara kadhaa

Acheni u snitch mnataka wenzenu wakale wapi?
Hahahaaa hata angekuwa mtoa post lazima angepokea ya maji, ila wengine wanaboa unakuta lengo ni pesa ya maji ila ataanza kuwachelewesha wee
 
Hii ndo kula kwa urefu wa kamba au ndo mwongozo wa kazi?
 

Attachments

  • VID-20250115-WA0030.mp4
    19.9 MB
Samaki anaanza kuoza kichwani

Askari anashinda juani analipwa laki 7 na akitaka kununua kagari anaingia mkopo mgumu na kodi anakatwa

Alafu Mh Tumbotumbo ameunga unga shule watoto wanasomeshwa na serikali bills analipiwa na serikali hakatwi kodi na anaiba

maisha sio fair
Rushwa ni adui wa haki
 
Ila watanzania kwa unafiki hamjambo, kweli mtu anashupaza shingo unaishabikia na kuitetea rushwa? Tuna safari ndefu sana na hii Tanzania.

Rushwa haijalishi ni ndogo au ni kubwa, zote ni rushwa. Kosa ni kosa na hakuna uhalali wa kulifanya kosa hili ni zuri na hili ni baya.

Tulikemea hapa Magufuli aliposema ni ya kufutia viatu, tukaja kukemea tena Samia aliposema wa Serikalini wale urefu wa kamba zao.

Tuna viongozi wanaohamasisha rushwa na vitendo vya kifisadi. Tunaangalia nasisi tunakuwa mashabiki wao, tunatengeneza kizazi gani?

Unajua hiyo rushwa usemayo ndogo, ndiyo inapoteza maisha, kwa kutokagua vyombo vya barabarani, ajali zikitoa mnakimbilia kulaumu.
Tuihalalishe rushwa iwe kisheria kama mmeishabikia hivi, ni aibu sana.
 
Aliyeoa/Aliyepokea Wote Watatiwa Msukosuko
By Mwalim JK Nyerere
 
kawaida sana kuna michezo yao ya vikoba kila siku laki moja unadhani watatoa wapi kama sio mambo hayo? na kuna kijitaasiisi kinajiita taakokuru na chenyewe kipo tu na kinaona, kuna kipindi wanakula rushwa hadi mbele ya hao takokuru na wala hawaogopi, wenzetu kenya ila ya kuzuia rushwa yakwao nimoto wanakula nao sahani moja mpaka utaona huruma Polisi anatoka nduki akipiga nduru maamaae , kwetu hukom kawaida sanaa sijui kwakua wote mwalimu wao mmoja.
 
Unaweza kisheria kuprove huyo dada kapokea rushwa au, upigwe kesi ya defamation?
 
Kuna majizi yanatetea majizi humu
Halafu mnaulizana kwanini nchi haimalizi Rushwa
Kweli mnatetea vibaka?
Halafu ajali zikitokea mnaanza mama weee mama wee
Gari linapita halina hata breki na matairi kipara wakifa huko
Kweli mtu anasema kabisa wakale wapi? Seriously
Hao wana mishahara halafu unasema wakale wapi
Yaani wameweka kitega uchumi kabisaa

Haya ya hivi kenya wanapambana nayo sana tena wanawafukuza haswa na wanapunguzwa vizuri tu
Waende wakawe vibaka kuliko kuidhalilisha ngao na uniform hizo
 
Back
Top Bottom