Harakati za Ben Saanane kupambana na Rais Magufuli, ni njia sahihi ya kuwaridhisha wafadhili wake?

Harakati za Ben Saanane kupambana na Rais Magufuli, ni njia sahihi ya kuwaridhisha wafadhili wake?

Rais ni muacheni afanye yake huyo kijana apewe tu pesa akajaze choi lakn ninaiman kwa uwezo wa mungu Rais hawez kuchafuka hata kidogo....
Lowassa Alipokuwa akitukanwa Ni Mfu Mtarajiwa, Kajinyea Mwenye Umahututi, Magufuli alisema Mwacheni? Si alikenyua Meno na Kuwapigia makofi? Mtu mzima angewapiga hawa Makofi. Hii Ni Trailer tu, Malipo ya Uovu yako duniani, Magufuli hajaona hata 1/8 ya Kusemwa na Kupingwa Bado, Atamaliza Muda wake kama akijaliwa, amekonda kama Kijiti kwa Kuwa na Ngozi laini Kama ya Konokono, Lakini Kusema na Kusingizia Wenzake Uwongo hajali. Be able to eat what you dish to others other wise 12417 away
 
ccm katika rangi yake, Nyerere alikua mtukufu, Mkapa mtukufu, Mwinyi mtukufu, Kikwete mtukufu, Magufuli nae ni mtukufu.

Tume huru ya uchaguzi kule Kenya wao tayari wamejielewa na viongozi wake wamejiuzulu.

Wewe bado unatetea wakati ndugu zako hawana ajira
 
Rais wangu Magufuli usiwe dhaifu kwa sababu ya demokrasia. Fanya mambo na dunia itakuelewa
 
Anyway lakini kumjadili mtu kama Ben Saa Nane ni kupoteza muda tu.
Muda mwingine kaa kimya maana unafanya majibizano na mtu ambaye akili yake inaendeshwa kwa remote control sio rahisi kuelewana nae.
Ben ni kibaka kila siku nasema ni cheap material kwa wenye pesa.Hana uwezo wa kusimamia akili yake wala kujitawala.
Achana nae jenga nchi yako.Sisi ni matendo tu.
 
ccm katika rangi yake, Nyerere alikua mtukufu, Mkapa mtukufu, Mwinyi mtukufu, Kikwete mtukufu, Magufuli nae ni mtukufu.

Tume huru ya uchaguzi kule Kenya wao tayari wamejielewa na viongozi wake wamejiuzulu.

Wewe bado unatetea wakati ndugu zako hawana ajira
Tatizo CHADEMA mnapendaga sana ujinga
 
Tunapata taabu sana kukuelewa unapoishia kulalamika kua Magufuli ni muovu bila kuuweka wazi huo uovu wenyewe sasa.
1) Kutaka Mtu Kama Jecha apewe Tuzo Ni Unafiki na Uovu
2) Kutupa Vitu vya Mwanasiasa Mwenzako Nje kwa Kisingizio cha Deni halafu Baadaye Unajifanya wote watupiwe, Zimepita siku saba hakuna aliyetupiwa ni Uovu.
3) Kusema Seif akiumwa aachwe afe ni Uovu
4)Kuzuia Mikutano na shughuli za Kisiasa za Vyama Vingine wakati wewe Unafanya Siasa kwa nyimbo Bendera na Uniform pamoja na Hotuba za Uwongo na Majitaka Ni Uovu.
5)Kuzuia Mahafali za wanavyuo wa Chadema Wakati wa CCM wanafanya Maafali hayohayo kwa Uniform, Kwa Nyimbo za siasa Ni Uovu
6) Kuwatuma Polisi wamlinde na Wasimguse Lipumbavu huku akivunja Ofisi za CUF na Kupiga Mlinzi Ni Uovu
7)Kumtumia Mtungi Kuvuruga Demokrasia Ni Uovu
8)Kuzuia Mawazo Kuzikwa mpaka Mahakama ikaingilia Ni Uovu
9) Kupeleka FFU na Mbwa Bungeni Kupiga Wabunge ni Uovu
10) Kufukuzia watoto wa Masikini 7000 Mitaani kwa Makosa yasiyo yao Na Kisha Kuwatukana Vilaza (ingawa wao wanajua Kiingereza) Ni Uovu sana
11) Kukamata Wanasiasa Kwa Kesi za Kuwasingizia Uchochezi ati tu kwa Kukupinga ni Uovu
12) Kukamata Vijana Wadogo Mitandaoni kuwapiga Kuwaweka Rumande zaidi ya Miezi Bila kesi ati walikutukana Mtu Uliyeshangilia Lowassa akitukanwa Matusi ya Nguoni na Ukashangilia, Ni Uovu.
13) Kutuma Wakuu wa Wilaya na Mikoa Wavuruge Upinzania Majiji ambayo Wapinzani Ni Mameya Ni Uovu.
14) Kujifanya Huendi UN, kwa Kisingizio cha Tetemeko, huku Ukigoma kabisa kwenda kutembelea Wahanga uone hali halisi Ni Ujinga na Uovu
15) Kuweka Wakurugenzi wa Wilaya Makada wa CCM huku ukijua wao ndio wanaosimamia Chaguzi na Maendeleo Ni Uovu, Hila na Ujinga.
16) Kutokuchunguza Mauaji ya Polisi wanne waliouawa ili wasingiziwe CHADEMA na UKUTA Ni Uovu Mkubwa sana, Hata tu Kuchunguza? nani anaamini wale Polisi waliuawa na Majambazi?


Nimechoka Mwingine aendelee na List
 
Wewe kama Lizabon ni wapi ulifanya utafiti hata kuja na hitimisho kwamba wabongo karibu wote wanakubaliana na JPM? Watu tunaisoma na hatuna raha halafu unakuja na ngonjera?

Ni hivi, mimi sio shabiki wa Ben lakini pia huyo Ben anaandika sana kiasi kwamba nashindwa kuelewa nini hasa mantiki au theme ya maandiko yake. Ila panapo ukweli lazima aseme maana ndio kazi yake. Sasa ulitaka upinzani ufanye nini rais anapokuwa kimya, ni dhahiri watakaa kimya pia, ika akisema na wao wanasema kwa kupinga tena. Wakiunga mkono sasa nini maana ya upinzani kwa perspective yako? Acha mahaba!

Pangu Pakavu.
 
Anyway lakinu kumjadili mtu kama Ben Saa Nane ni kupoteza muda tu.
Mudamwingine kaa kimya maana unafanya majibizano na mtu ambaye akili yake inaendeshwa kwa remote control sio rahisi kuelewana nae.
Ben ni kibaka kila siku nasema ni cheap material kwa wenye pesa.Hana uwezo wa kusimamia akili yake wala kujitawala.
Achana nae jenga nchi yako.Sisi ni matendo tu.
Ila pia kukaa kimya ni kumpa umaarufu Ben. Wacha kaka Lizaboni aendelee kutudadavulia
 
Ni kweli mh Rais ana fanya kazi nzuri za kimaendeleo tatizo lake mh Rais na wapambe wake mnashindwa kutofautisha kuwa kazi za kimaendeleo ni zipi na kazi ambazo siyo za kimaendeleo ni zipi.

Kwa mtazamo wenu hata kupiga mikutano ya siasa kwenu ni maendeleo,kupiga marufuku bunge live kwenu ni maendeleo,kuwafunga watu wanao mkosoa mh Rais kulingana na mtazamo wao kwenu ni maendeleo.

Mungu mwenyewe utendaji wake unakosolewa na kulaumiwa na binadamu hawahawa waliojifanya kuwa wao ni zaidi ya Mungu wasioweza kukosolewa,wakati hakuna binadamu ambaye ana weza akafanya kazi kwa ukamilifu bila kukosolewaUnapokosolewa ndipo unapoweza ukajua mahali ulipo kosea ni wapi,ulipofanya vizuri ni wapi na wapi ambapo unatakiwa urekebishe.

Pia mazingira ya kutokupenda kukosolewa yanasabisha chuki kati ya asiyependa kukosolewa kwa kuwa ana amini kuwa mwenzake ambaye ana jaribu kumkosoa hana nia njema naye wakati kumbe siyo kweli kwani anayekukosowa ndiye mwenye nia nzuri na wewe kwa kuwa ana taka ufanye vizuri zaidi ya pale.

Ni tofauti na mtu yule ambaye kila unachokifanya kwake ni kupiga makofi tu pwaapwaapwaa,uwe umefanya makosa yeye ni makofi tu pwaapwaapwaa,uwe umefanya vizuri yeye ni wa makofi tu pwaapwaapwaa,kiasi ambacho inakuwa ni vigumu kuelewa,wapu umefanya vizuri,wapi umefanya makosa na wapi pa kurekebisha.

Watu wa aina hii wa kupigia makofi na kuunga mkono kila jambo mara nyingi siyo kwamba wanakuwa wanampenda kwa dhati mtu ambaye kila anapofanya jambo lolote kwao ni zuri tu,mara nyingi huwa wanafanya hivyo kwa kujipendekeza ili kulinda maslahi yao au kuna kitu wanakuwa wanakihitaji kutoka kwake,ndiyo maana watu wajanja wasiotaka kuuziwa mbuzi kwenye gunia kama Nyerere aliwaambia wana CCM wenzake kuwa kila siku mnasema zidum fikra sahihi za mwenyekiti wa CCM leo niambieni fikra sahihi ni zipi na fikra zisizo sahihi ni zipi.
 
Lizaboni Hivi yule Mwenyekiti wa kampeni wa Lowasa yupo wapi? Yule bosi wa UWT wa kipindi cha B
en. Naona kimyaaa tu.m
 
Mwanzoni mwa mwaka huu, niliweka taarifa kwenye mitandao ya kijamii hususan hapa Jamiiforums juu ya Mkuu wa Sera na Utafiti CHADEMA, Ben Saanane kununuliwa vitendea kazi kama simu, kompyuta mpakato, ipad, tablets na zana nyingine. Nilieleza kuwa aliyemnunulia vitu hivyo ni Edward Lowasa. Nilitoa sababu za Lowasa kufanya hivyo ni kutaka Mkuu huyo wa Sera na Utafiti afanye kazi ya kumsafisha Lowasa kwenye mitandao ya kijamii lakini pia amshambulie Rais Magufuli ili tunapoingia 2020, asiaminike tena. Nilieleza kuwa Ben na Lowasa wamekubaliana kuwa malipo ya kazi hiyo ni milioni 4 kwa mwezi.

Kwenye uzi ule, nilieleza bayana kuwa Ben Saanane amepangiwa ofisi ya kufanyia kazi hiyo katika sehemu ambapo sikubainisha kwenye mtandao kutokana na sababu za kimkakati.

Hata hivyo, baada ya uzi ule kuwekwa, Ben Saanane alikosa uvumilivu. Aliishia kuporomosha lugha zilizokosa staha kwa lengo la kushinikiza mods waufute. Alifanikiwa. Uzi ule ukaenda na maji. Leo mdogo wangu Ben namuomba awe mvumilivu ili tujadili kwa staha.

Miezi 5 imepita sasa tangu Ben Saanane anunuliwe. Matunda ya uwekezaji ule yameanza kuonekana. Ben Saanane na genge lake wameanza mashambulizi dhidi ya Rais kwa hoja ambazo kimsingi hazina mashiko.

Ben Saanane na genge lake wameshindwa kabisa kuona udhaifu wa Rais Magufuli kiutendaji na badala yake wanaegemea kwenye mipasho na mapambio. Wanafanya siasa za kuvizia. Niliwahi kuanzisha mada humu kwamba, ikitokea Rais akawa bubu, je CHADEMA watakuwa na ajenda zipi?

Tathmini yangu ya muda mfupi imebaini kwamba, hoja zinazojengwa na Ben Saanane na genge lake zinategemea nini Rais anaongea. Kwa maana utendaji wa Rais uliotukuka unasababisha Ben Saanane na Genge lake wakose hoja za kumkosoa. Hata kama wanapojaribu kukosoa utendaji, wanakosoa kwa hoja dhaifu. Mathalan, ziliponunuliwa ndege mpya mbili aina ya Bombadier Q400, walijenga hoja za kitoto eti ndege hizo hazina mwendo. Mara wanasema ni mapangaboi. Mara wanasema eti water salute haikufanyika kisawasawa. Almradi wanawaonesha wafadhili wao kuwa wametimiza wajibu wao. Utoto.

Uwezo wa vijana wa CHADEMA katika kujenga hoja ni mdogo. Kuna wakati Lusinde aliwahi kuwaambia kuwa akili zao zimeshikiliwa na Mbowe na ndio maana wanawaza kimbowembowe tu.

Hata hivyo, najaribu kuwaza, je kazi anayofanya Ben Saanane na genge lake inatosheleza matakwa ya wafadhili wake? Je watafanikiwa kushusha morali ya Rais Magufuli katika kuwatumikia wananchi? Je watakwamisha juhudi kubwa zinazofanywa na Rais Magufuli katika kutekeleza ilani ya CCM? Thubutu! Rais ameapa kuwa hakuna atakayekwamisha utekelezaji wa Ilani ya CCM. Ben Saanane na Genge lake wataishia kujadili water salute, kuomba Salary Slip ya Rais na kujipongeza kutokana na kauli ya Rais kuwa anatamani malaika afungie mitandao ya kijamii kwa mwaka mmoja ili itakapofunguliwa wakute Tanzania imepaa.

Nimhakikishie Rais wangu kuwa, hawa wapiga kelele mitandaoni hawatafanikiwa kukwamisha harakati zako za kuwaletea maendeleo wananchi. Waache wapige kelele. Wewe piga kazi. Mwisho wa siku kelele zao zitageuka kuwa kicheko kwako. Watanzania tuna imani kubwa kwako. Kazi unayofanya inapokelewa kwa mikono miwili na Watanzania. Utafiti wa Twaweza unabainisha kuwa 96% ya Watanzania wanakulibali. Endelea kupiga kazi ili ifikapo 2020, wapinzani waone aibu kumsimamisha mgombea Urais kupambana na wewe.
Usiseme watanzania tuna imani na rais zungumzia nafsi yako peke yako
 
Nitajie kijana makini wa ccm aneweza kujenga hoja ata upande wa pili wakasoma na kumuelewa
Tupo wengi Mkuu. Muulize Dr Slaa na timu yake akina Marehemu Mohamed Mtoi, John Mnyika, Michael Aweda, Hodbless Lema, Mungi, Crashwise, Maskini Mkulima, Zitto Kabwe na wengine tulivyokuwa tunawachachafya mitandaoni mpaka wakaomba pooo
 
Maybe.. Kiukweli mi sijawahi kusoma makala yoyote ya kijana wa ccm iliokuwa haina ushabiki uliopitiliza,majivuno,dharau na propaganda mfano mzuri ni post yako hii unaandika Vitu ambavyo hauna uhakika simply because hakuna wa kukukamata.... Natumaini unamfaham malissa Godlisten
 
Lizaboni yaani wewe una mawazo finyu mno mbona umeongea pumba tupu hivi huoni JPM anavyofeli? Msaidieni kuanzisha viwanda huku akiua sekta ya kilimo
 
Hawa vijana wa CHADEMA wanatoa Thread ambazo zinawagusa

Asubuhi niliweka UZI WA UKUTA baada ya muda sikuiona tena Uzi wangu

Wanahofu ya nn???
 
Back
Top Bottom