Harmonize: Nilipewa Mkataba wa kuonewa na WCB na nilisingiziwa kumroga Diamond Platnumz

Harmonize: Nilipewa Mkataba wa kuonewa na WCB na nilisingiziwa kumroga Diamond Platnumz

YATASEMWA MENGI ILA ALBUM ISHABUMA NA ZA CHINI CHINI KUNA WASANII WANAMKIMBIA HAWAONI KINACHOENDELEA PALE KONDE GANG

BAADA YA MUDA SIO MREFU ATAANZA KUSHIKA UCHAWI WATU WA KIJIJINI KWAO

Hoki ndicho nachokiona
 
Jikite kwenye hoja za Konde kama una ukomavu wa kujibu, hakuna sehemu amelialia bali amechoka kusakamwa like hana fadhira na hana baraka za Wasafi…. hoja zina ukweli au porojo?
Hoja gani za kulia lia alionewa?
Nakubali alionewa so what?

Na nani ana MSAKAMA mmakonde?
Anajisakama mwenyewe kwa kukubali kuishi chini ya kivuli cha wasafi
Miaka mitatu sasa ngonjera ni hizo hizo tuu

Watu wanataka kuona ngoma zaidi ya kwangwaru na iyola
Watu wanataka kuona akina Ibrah, Cheed Angel wakifika mbali
Watu hatutaki kusikia habari za wasafi walinionea........ inatosha
Mwambieni a move on na maisha sio kukaa miaka yote yeyeni kulialia tu
Hata akipigwa chini na mademu zake lawama ni wasafi
Nyimbo zake ni kulia na wasafi
Huu upuuzi sasa
 
Huyu mziki ushamshinda,album inafanya vibaya.

Sasa Diamond kama angetaka kila siku kuwa yy.

Kaanzisha lebo ambayo imemtoa yy.
Kampeleka nje kufanya video kubwa.
Kamkutanisha na wasanii wakubwa Africa.
Kamtoa Rayvanny mpaka kufikia hatua ya Colabo na Maluma na kuchukua BET,Tz hii Rayvanny ndiye mwenye nyimbo yenye streams nyingi, kapiga show jukwaa la essence, mafanikio ambayo Diamond hajawahi kuya fikia.

Angeamua kuto kuanzisha label tusinge mjua na Diamond ni mfanyabiashara, always ana angalia faida na label zote duniani zina angalia faida, hata yy na JembeniJembe wanaangalia faida.

Yeye mwenyewe kuimba aliambiwa hajui, Diamond kakaa nae zaidi ya miaka mitatu, akimfundisha na kumpika kimuziki na kuna watu walimwambia hajui kuimba ila Mondi hakukata nae tamaa, kula,kuvaa na kulala kwa Diamond.

Anadai WCB walikuwa wana muogopa yy, haya leo zaidi ya miaka miwili nje ya WCB, yupo yy peke yake,free habanwi je kafika wapi,kampita Diamond?Anapata airtime ktk media zote kubwa zilizo kuwa hazipigi nyimbo zake.

Halafu haja tuambia wasanii wake wanapata kiasi gani, mikataba yao miaka mingapi,wana miaka miwili hawa heleweki wanafanya nini.
Sijaelewa aliamua kuongea hayo Ili kutafuta kiki mpya au? Maana sijaona logic yoyote so far na wala hakuna ubaya wowote Kwa akina Diamond walichokifanya ..
 
Hapana sio kiki, amezungumza ukweli ambao hajawahi kuzungumza kwenye media yeyote
Lengo la huo ukweli ni nini kama sio kiki kwa wajinga.Kwa mtu mwenye akili timamu sijaona kosa kwa kina diamond wala yeye alipoonewa as far as business is concerned.
 
Sitaisema kwasababu zangu binafsi. Lakini siku ile nilishangaa kuona domo anaonyesha chuki kiasi kile kwa mtu ambaye nilijua ni tim yake,, baadae nikaambiwa dogo amejitoa huko pengine ndio sababu. So hata baadae nilikuwa nikisikia story zao nilikuwa nakumbuka hiyo issue najua kuwa nani ni tatizo.


Na domo ndo alianza vijembe kama una kumbukumbu vizuri.
Ukiwa huna akili ya mtizamo wa kibiashara unaweza ongea huo utoto wako.

Kama kwa kipindi kile Harmo alikuwa ndio nguzo ya label ya wcb ni wazi haingekuwa rahisi kumuachia.Pili kama kutoka kwake kulikuwa na malengo ya kuharibu label na kuwa mshindani lazima aletewe zengwe maana amekuzwa humo.

Mara ngapi wachezaji wanakataliwa kuvunja mikataba? Lazima utafutwe mda muafaka wa kumuachia asiwe threat kwa label yao ,hizo ni vita za kibiashara..

Unaona sasa katoka lakini hakuna cha maana anafanya kwa sababu za miscalculation.
 
Me mbona sionii mond alichofanya mpaka asemwe hivo nafikiri ni sababu ya ukubwa wake,, ukiwa mkubwa lazima usemwe tuu! Sikilizeni nyimbo nyingi za harmonize huwa zinamsema sana mond lakin mond hajawah jibu
Uncle shamte unauhakika
 
Me mbona sionii mond alichofanya mpaka asemwe hivo nafikiri ni sababu ya ukubwa wake,, ukiwa mkubwa lazima usemwe tuu! Sikilizeni nyimbo nyingi za harmonize huwa zinamsema sana mond lakin mond hajawah jibu

Uncle shamte mwenyewe naona upo
 
Dogo angekausha tu aisee, hii ya kutafuta huruma sio poa.

Na bahati mbaya zaidi sidhani kama wcb watamhibu hizo tuhuma zake dhidi yao.
Jamaa walitumia gharama kumtoa mpaka ajulikane sasa anakatwa analalamika.

Halafu huo ni mkataba aliousaini kabisaa, sasa unalalamikaje wakati mkataba uliusoma na ukauelewa kabisa.
Anaelekea kusema kushindwa kwake karogwa, alifanya miscalculation..ndio maana sio kila mtu anaweza kuwa muajiri au kujiajiri ..Sasa anapanic
 
Diamond ni mwanamziki mkomavu sana, toka ameanza kuhit Huwa tunasikia kwamba amefika mwisho wake lakini mwisho wake haufiki.
Diamond ni mwanamziki mkubwa na mziki unachangamoto zake pia biashara haitaki ushkaji.

Nenda hata Kwa akina Bakhresa ongea na wafanyakazi wa viwandani utajua kwamba biashara haitaki utoto hata siku moja.
Na kama utacheka na wapinzani wako wanakupoteza.

Kwamba Harmo yeye Hana matatizo mwenye matatizo ni Diamond tu basi na mchawi ni Diamond yeye sio mchawi kabisa ni mtu wa Sala sana, inachekesha sana.

Uchawi unapozungumziwa sana na mtu na kuona mafanikio ya watu yanatokana na Uchawi hiyo inakua ndio Imani yake huyu mtu anahisi Uchawi anaofanya unafanywa na kila mtu na kila mwenye mafanikio basi ni mchawi zaidi yake.

Mtu akisema huniwezi kwa Uchawi huenda ananguvu inaoushinda Uchawi.

But mafanikio ni shida sana kuyamaintain na watu wanapambana haswa ukikaa kiboya tu kwenye mziki utapoteza hufiki mbali.

Sasa Hamo kama anataka kuonewa huruma kwenye game na washindani wake atapoteza.
Juma juma lokole naona hela ya posho na urafiki wako na dadayake mondi unakufanya unakuwa mtumwa kwa mwanaume mwenzako
 
Naomba kuweka wazi kabisa kwamba mimi si mpenzi wa Muziki wa Tanzania na wala siwapendi wanamuziki wa Tanzania , hii ni kwa vile wamekuwa mara zote wakitumika na ccm kuwapotosha wananchi , na hasa hawa wanaoitwa Wanamuziki wa kizazi kipya , ambao pia wanatuhumiwa kusafirisha na kusambaza madawa ya kulevya hivyo kuharibu nguvu kazi ya Taifa.

Bali nimesononeshwa sana na yaliyojitokeza kwenye mgogoro wa Harmonize na Diamond , pale huyo Harmonize alipokuwa anaomba kujitoa kwenye lebo ya WASAFI , mengi sana ameongea mwenyewe kila mtu kayasikia wala sina haja ya kuyarudia , bali nitagusia kidogo maeneo mawili tu.

Kwamba Diamond alimwambia Harmonize kwamba anaweza asimkamilishie kile anachotaka na wala hatomfanya chochote na kokote atakakoenda hatofanikiwa , kwa vile HAMUWEZI KISERIKALI , KIFEDHA NA KIUCHAWI , hii ni kauli ya kijinga sana kutolewa na anayeitwa msanii mkubwa , ni kauli ya kishamba sana iliyojaa Utanzania mtupu!

Jambo lingine linalotia aibu ni kitendo cha Harmonize Kuomba msaada kwa Magufuli moja kwa moja baada ya ngazi za chini ikiwemo wizara kumgwaya Diamond , Yaani Rais wa nchi ampigie simu Msela Diamond na kumbembeleza ili akubali kuterminate mkataba wa Harmonize na Wasafi ! hili ni jambo la kutia aibu sana , Yaani inawezekanaje Wizara na BASATA kutiwa mfukoni na msanii mmoja?

Haya mambo yakiachwa iko siku yatakuja kufedhesha mamlaka ya Rais , na sisi kama wananchi hatutakubali.
serikali iache kudili na masuala ya maana ianze kuhangaika na wasanii we jamaa kumbe wakat mwengine una tumia Masabuli kufikiria

ushawahi sikia serikali ya Us kuingilia ugomvi wa eastcoast na west coast?
 
ndugu yetu mtaalam wa sheria umeshindwa kabisa kuiona hoja ya harmonize kwenye interview yake ya zaidi ya dakika 40???

tokea mwanzo anakwambia ni kwa namna gani alihangaika kuweka mambo sawa,aendelee kuishi pale lakini katika hali ya amani.unaweza niambia kufanya kazi chini ya visa na vitimbi ni level ipi ya sheria inayosimamia makampuni inafundisha!!!

kavunja mkataba akakabwa alipe 500mln sawa,ambayo mwisho wa siku imekuwa 600 na majungu juu,hii ni sheria gani inazungumza haya!!!

hata serikali haiamini uchawi wala majungu,ila kuwa ofisa wa serikali ndio utajua wewe ni serikali ama ni ofisa wa serikali,hakuna rangi utaacha kuiona humo serikalini.

wenye kampuni zao hata wanapopata faida kwako kupitia sheria walizoweka,bado huwa wanatamani usipeleke ujuzi kwingine baada ya kuachana nao story yako iishie pale pale.
Sasa unasema suala la kulipa 600M linatokea wapi wakati haujausoma mkataba wake? Sheria ya mikataba ndiyo inaratibu mkataba wake alipokuwa WCB.

Aliingia WCB akiwa hana kitu...kampuni ikawekeza milions of money...akakua na kuwa almost msanii wa pili kwa ukubwa nchi hii.

Anapovunja mkataba..lazima mrudi kwenye ule ule mkataba..unasemaje pale upande mmoja unapotaka kuvunja mkataba?

Yeye msanii pale kwenye label alikuwa anafanyiwa kila kitu..kazi yake ni kurekodi nyimbo na video chini ya gharama za label. Promotions zote inafanya label...

Videos na audio zote, jina lake la kisanii, account za YouTube zote ni mali ya label. So anapotoka na akataka kutumia hivyo vitu..ni lazima anunue rights ziwe zake.

So justification ya 600M inakuja baada ya kupiga hesabu za uwekezaji aliofanyiwa toka ameanza kurekodi wimbo wa kwanza. Pia gharama za kununua haki za kazi zake zote ambazo zilikuwa zinamilikiwa na label. Mwisho ni brand kama brand...aliingia kwenye label akiwa pangu pakavu sasa anatoka jina lake likiwa ni brand kubwa...lina value.

Utagundua kuwa 600M ni kama vile WCB wamemfanyia fair...hasa ukizingatia ameruhusiwa kutumia kazi zake, na social media platform kwa majina yake ya kisanii ambayo bado yanazidi kuingiza pesa. Fikiria kama angekatazwa kutumia jina lake na kazi zake...but those guys walimruhusu.

When a contract comes to an end..parties are restored to their original position as if they have never contracted at first place.

So Harmo alipoondoka..ilikuwa ni sawa kulipa gharama hizo maana the other side wali spend zaidi kwake kumkuza na kum brand...angeondoka bila kulipa ingekuwa ni unjust enrichment.

Sasa hivi anaiona hiyo 40% kuwa ilikuwa ni ndogo na alikuwa ananyonywa...wakati anaingia label alikuja na nini? He was broke na diamond took a leap of faith kwa kuwekeza kwake. Imeanza kuonekana ni ndogo once things turned out better.

Pia awe makini...asijepigwa defamation suit maana ametaja majina ya watu clearly na mambo mengi aliyosema hawezi kuyathibitisha endapo atapelekwa mahakamani......na pia kitendo cha kuvujisha mazungumzo yake na Vanny boy publicly kinaweza kuja kum haunt kama wenzake wakiamua kupita route ya jinai.
 
Diamond anatakiwa ayatolee ufafanuz haya malalamiko , Harmonize anamtuhumu Diamond kwamba kuna watu anawatuma wamchafue notable Baba levo na Juma lokole , ili kumharibu kimziki yes yawezekana ni kweli , Ila harmonize haangalii Kwa upande wake kuwa na yeye ana chawa akina mwijaku , carlmastory, hbaba , jaymaudaku na wengine weng na wao kazi Yao ni kumwandama diamond , lakini pia Wasafi wakiandaa event yeye harmonize na yeye anaandaa ili kudivert attention ... Means na yeye anaishi na kuamini humo humo kwenye Fitina na figisu , anamponda mond kwa madhaifu yake hata hvyo bado anamtegemea mond indirect ili awin, ...... Tatizo linakuja hafikii peak Ile anayotaka sababu mwenzake kaenda mile nyingi mbele na ana nguvu nyingi zaidi ndo chanzo cha malalamiko hayo yote.

Turudi Kwa Maghufuli , mtoa mada kuna kitu umekiruka au umekificha Kwa maksudi ili
ujumbe wako wenye utata na kisiasa ufike , mpak kusema Jiwe alimbembeleza Diamond kitu ambacho Kwa Maelezo ya harmonize sio kweli ...

Harmonize anadai alifanya kila njia kuwaomba watu wenye nguvu ya kimaamuz ili wamsaidie azma yake ya kuvunja mkataba , kwani by that time kwake ilikuwa ni ngumu hata kumfikia Diamond Kwa jinsi mambo yalivyokuwa yana-turn around...

Aliwafikia watu kama kusaga ( sababu ya status yake na ushkaji na mond ), alimfikia mama dangote (nguvu ya mama) alimfikia mwenyekiti sjui ndo katibu wa Basata, na alimfikia mwakiyembe ( by that time Wazir wa Sanaa ) , Kwa Maelezo yake anadai wote hawakuonyesha kumsaidia na inaonekana hawakuwa tayar , huku akiandamwa na pressure toka Kwa wadhamini wake CRDB na Sayona , Kondeboy aliona kete Yake ya mwisho ni Raisi John Pombe Joseph Maghufuli....

Jiwe alifanya sehemu yake Kwa kumpigia simu Wazir wa Sanaa na michezo kuhusu hlo sakata,na nafk Mwakiyembe alikuwa aware na hyo changamoto thus why alifanya maamuz ya haraka , kumzuia diamond kukwea pipa mpak amalize hlo suala ...

Kwa hyo Siyo kwamba Maghufuli alimbembeleza Diamond ...na kama ingekuwa hvyo ingechukua sku mbili au tatu ...

Zaidi ya yote Kongole Kwa Harmonize Kwa upambanaji na roho ya kiume , kuhusu Fitina hata yeye hzo Fitina anazifanya , ushindi wake sio wa haraka kama anavyofkria sababu mwenzake still bado ni ngome imara ...!!
Respect Slowly
 
Anaelekea kusema kushindwa kwake karogwa, alifanya miscalculation..ndio maana sio kila mtu anaweza kuwa muajiri au kujiajiri ..Sasa anapanic
Asitafute mchawi nani ajipambanoe tuu

Yeye ni shahidi kipindi yuko wasafi jinsi walivokua wanabaniwa na media kibao bongo ila boss wake aliminya kimya mpaka alivokuja na hiyo wasafi tv & radio. Aongee kwa vitendo sio hizi bra bra ambazo zitatrend wiki 1 zitafutika vichwani mwa watu na kuanza kujudge kazi.
 
Sasa unasema suala la kulipa 600M linatokea wapi wakati haujausoma mkataba wake? Sheria ya mikataba ndiyo inaratibu mkataba wake alipokuwa WCB.

Aliingia WCB akiwa hana kitu...kampuni ikawekeza milions of money...akakua na kuwa almost msanii wa pili kwa ukubwa nchi hii.

Anapovunja mkataba..lazima mrudi kwenye ule ule mkataba..unasemaje pale upande mmoja unapotaka kuvunja mkataba?

Yeye msanii pale kwenye label alikuwa anafanyiwa kila kitu..kazi yake ni kurekodi nyimbo na video chini ya gharama za label. Promotions zote inafanya label...

Videos na audio zote, jina lake la kisanii, account za YouTube zote ni mali ya label. So anapotoka na akataka kutumia hivyo vitu..ni lazima anunue rights ziwe zake.

So justification ya 600M inakuja baada ya kupiga hesabu za uwekezaji aliofanyiwa toka ameanza kurekodi wimbo wa kwanza. Pia gharama za kununua haki za kazi zake zote ambazo zilikuwa zinamilikiwa na label. Mwisho ni brand kama brand...aliingia kwenye label akiwa pangu pakavu sasa anatoka jina lake likiwa ni brand kubwa...lina value.

Utagundua kuwa 600M ni kama vile WCB wamemfanyia fair...hasa ukizingatia ameruhusiwa kutumia kazi zake, na social media platform kwa majina yake ya kisanii ambayo bado yanazidi kuingiza pesa. Fikiria kama angekatazwa kutumia jina lake na kazi zake...but those guys walimruhusu.

When a contract comes to an end..parties are restored to their original position as if they have never contracted at first place.

So Harmo alipoondoka..ilikuwa ni sawa kulipa gharama hizo maana the other side wali spend zaidi kwake kumkuza na kum brand...angeondoka bila kulipa ingekuwa ni unjust enrichment.

Sasa hivi anaiona hiyo 40% kuwa ilikuwa ni ndogo na alikuwa ananyonywa...wakati anaingia label alikuja na nini? He was broke na diamond took a leap of faith kwa kuwekeza kwake. Imeanza kuonekana ni ndogo once things turned out better.

Pia awe makini...asijepigwa defamation suit maana ametaja majina ya watu clearly na mambo mengi aliyosema hawezi kuyathibitisha endapo atapelekwa mahakamani......na pia kitendo cha kuvujisha mazungumzo yake na Vanny boy publicly kinaweza kuja kum haunt kama wenzake wakiamua kupita route ya jinai.
Mkuu hiki kitu kinakwepwa sana kuongelewa na kufanya WCB waonekane kweli ni wanyonyaji. Yule mwamba tumemjua akiwa wasafi mpaka anakua msanii mkubwa yuko chini yao.

Kila kitu anafanyiwa, achana na hilo si ajabu pia alikua anashirikishwa kwenye maamuzi. Sasa asset kama hii kweli ikitaka kuponyoka eti akulipe pesa ndogo.
 
Back
Top Bottom