Harmonize: Nilipewa Mkataba wa kuonewa na WCB na nilisingiziwa kumroga Diamond Platnumz

Harmonize: Nilipewa Mkataba wa kuonewa na WCB na nilisingiziwa kumroga Diamond Platnumz

Kwa maelezo ya mmakonde ana point kadhaa..

Diamond ana shida mahala, kuna kitu mjomba nchumali kakisema kuwa "diamond ana fanbase kubwa hivyo ukiwa na kaugomvi nae akichukua mashabiki wake we unabaki na kidunchu"

Komenti za wengi humu zinamkandia mmakonde kwa utimu sio kwa kike alichosema.

Inaonekana mondi hakufurahishwa na ujaji wa juu wa kijana, hii kauli ya mmakonde alipomwambia mondi "bro ya nini uumize kichwa, hata nifanye vipi we yako 60, mie nakula 40.. kisha mondi kusema unataka kushindana nami, huniwezi kiserikali,kiuchawi sijui na nini.

Sijajua kabla hajaondoka wcb ni nani alikuwa anaingiza fedha ndefu baada ya mondi nahisi ni mmakonde, kifupi hili jambo mondi hakufurahi.
Na hii ipo, kibinadamu mondi alikuwa anategemea kula pale kwa mjomba nchumali.
Ni kama vile ujenge hotel, kisha serikali waje kuvunja inauma.

Hata pac alipotaka kutoka kwa suge, suge hakifurahia kabisa...
Ile kauli nimesalitiwa na jeshi, inao esha kiasi gani mondi ilimuuma.

Kikubwa mmakonde akaze msuli aendelee na game ndio maisha hayo.

Na shida ni wale kina Salaam wale ndo mambwa kabisa wale tena wale hata Diamond wenyewe hawampendi baasi tu wanaishi nae kinaafk...walimtoa ruge kwenye ramani ili wabaki nae wao tu kimaslahi zaid,wanataka atawale milele peke yake kimziki kitu ambacho hakiwezekani.

Hizi kelele ndo zinazidi hizi sio kua zinaanza zitafika mwisho siku si nyingi hata kama miaka5 ijayo.

Ingawa kwa sasa team Mondi hawataelewa, watakuja kuelewa siku akitoka msanii mwingine pale WCB kinachofanya wengineo wakae kimya wanaogopa kupoteza ushosti na kualikwa kwenye Ep za wasafi tu ila LA kuvunda halina ubani!
 
diamond ni mwizi na ana roho ya kinafki
kama mlivyo mashabiki wake

kama hutaki basi rafiki zake wa mwanzo alishagombana nao kina ommy sheta

akili za kitandale zinamsumbua
Roho ya kinafiki ipi 40/60,unasema unaibiwa haya yy mwenye roho anawapa wasanii wake ngapi.
 
Huyu mziki ushamshinda,album inafanya vibaya.

Sasa Diamond kama angetaka kila siku kuwa yy.

Kaanzisha lebo ambayo imemtoa yy.
Kampeleka nje kufanya video kubwa.
Kamkutanisha na wasanii wakubwa Africa.
Kamtoa Rayvanny mpaka kufikia hatua ya Colabo na Maluma na kuchukua BET,Tz hii Rayvanny ndiye mwenye nyimbo yenye streams nyingi, kapiga show jukwaa la essence, mafanikio ambayo Diamond hajawahi kuya fikia.

Angeamua kuto kuanzisha label tusinge mjua na Diamond ni mfanyabiashara, always ana angalia faida na label zote duniani zina angalia faida, hata yy na JembeniJembe wanaangalia faida.

Yeye mwenyewe kuimba aliambiwa hajui, Diamond kakaa nae zaidi ya miaka mitatu, akimfundisha na kumpika kimuziki na kuna watu walimwambia hajui kuimba ila Mondi hakukata nae tamaa, kula,kuvaa na kulala kwa Diamond.

Anadai WCB walikuwa wana muogopa yy, haya leo zaidi ya miaka miwili nje ya WCB, yupo yy peke yake,free habanwi je kafika wapi,kampita Diamond?Anapata airtime ktk media zote kubwa zilizo kuwa hazipigi nyimbo zake.

Halafu haja tuambia wasanii wake wanapata kiasi gani, mikataba yao miaka mingapi,wana miaka miwili hawa heleweki wanafanya nini.
Humjui diamond vizuri endelea kumtetea ila yule jamaa ni mafia kweli kweli
 
Hao mashabiki wana chukuliwa vp na bastola, saa nyingine kauli nyingine ni kukubali kushindwa tu.

Ina maana Diamond anawashikia bastola watu wasi sikilize na kustreams nyimbo za Harmo.

Yy ana amini bora kuliko Mond its basi aprove hilo kupitia numbers sio maneno,kwani sasa hivi yupo free hayupo chini ya label, Clouds, EA,EFM wanampa airtimes ni wakati wake wa kuprove.
nimechoka kubishana ujinga
mbona basi alipokosa tuzo za kili je kina mange hao waliwashikia.kura mashabiki wasimpigie kura diamond nchi nzima?

unachoongea ni nonsense
 
Kaongeza misamiati siku hizi kuna matusi , huu ndio wimbo wake wa kwanza kwenye album katoa video juzi juzi, haueleweki anaimba nini, hapo kwenye sleep sleep nafikiri alimaanisha halali lali, hiyo outside sijui ndio ametoka😆

"Yeah hustle everyday I never sleep sleep coz am outside
When am falling love I go deep deep coz am outsidee
Time for the money two for the show enzi za kuuza maji na wanangu wa kariakoo
That was before long time ago I wish you know I wish you know yeaah
"

Chorus:
"We are outside outside outside outside
B*tch am outside outside outside outside
Am outside outside outside (Eeeh)
Kondegang we are outside outside outside (Yah yah yah)
"
Ila watanzania tuna shida sana, unamshangaa harmonize kwa lipi English sio first language kwake, hatakama anaimba broken ameonyesha uthubutu

Kukosoa kila kitu ndo kunawapa uoga hata watoto wetu kujaribu wakijua wakikose watakutana na mashambulizi ya kukoselewa tuna jamii ya ajabu sana
 
Pesa ni mwanaharamu, pesa kagombanisha wengi, makundi kibao yamevunjika kisa pesa..

Alichoongea mmakonde kinaashiria vitu fulani.. ofcz mondi sio malaika nae lazima awe na mabaya yake tofauti na watu wanavyomuona.

Wote sio wakamilifu, wote wana mapungufu maisha yasonge, mmakonde apige kazi tu, shida anapaniki atapoteza vita na kujitoa kwenye game mwenyewe, mondi alipofikia ni pakubwa mnoo kimafanikio.

Ili mmakonde atoboe afute kabisa mabaya ya mondi akumbuke yale mazuri tu basi, kisha apige kazi.

Umeongea vitu vya msingi haswaa...afute ubaya wa Mondi aangalie mazuri yake tu!

Ila harmonize nae kachoka jamani kupigwa vijembe kila siku Mara kibonge, Mara ukuti ukuti, Mara njomba nchumali n.k Mara anakula mihadarati.

Mondi ni mswahili sana ingawa kimziki yuko juuu haswaa hatukatai na amefanikiwa mnoo!!!
 
Shida nadhani gharama kubwa za bando,hawajapata kumsikiliza harmo.
[emoji23][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji16][emoji23][emoji23]daah!!!na hatusikilizi ng'oo u tube mb200 natoa wapii....!!!
 
Je mtu kusema yake ya moyoni ndio kigezo cha mziki kumshinda?

Sidhani kama uwezo wako wa kufikiri ndio umefikia kikomo na kufikia hilo hitimisho eti muziki umemshinda.
Nakuhakikishia personal harmonize ana maisha mazuri kuliko watu wengi walioko jamiiforum

Alafu yeye mziki kumshinda mziki ni sehemu ya maisha sababu sio wa kwanza mziki kumshinda
 
Umeongea vitu vya msingi haswaa...afute ubaya wa Mondi aangalie mazuri yake tu...!!!
Ila harmonize nae kachoka jamani kupigwa vijembe kila siku Mara kibonge,Mara ukuti ukuti,Mara njomba nchumali n.k...!!!Mara anakula mihadarati...!!!
Mondi ni mswahili sana ingawa kimziki yuko juuu haswaa hatukatai na amefanikiwa mnoo!!!
Mondi ni mswahili haswaa, kwani yeye hamjui, kipindi yuko wcb si aliona kilichokuwa kinamsibu ali kibakuli.

Mmakonde ni msanii mzuri, wasiwasi wangu ni kama anaweza kujiendesha kibiashara na kama pia anaiweza vita ya kibiashara. Diamond yuko smart katika vitu hivi, mmakonde anasafari mdefu kidogo, lakini anajitahidi anatoa ngoma tamu ni vile watu wako kwenye masuala ya utimu.
 
Mimi Lava lava nakatwa asilimia tatu na hata sjalalamika.
Sasa kama unakatwa 3% Ina maana we unachukua 97%?

Lavalava hata akikatwa 99% asilalamike maana ni sawa tu na msanii anayepambana kutoka
 
Watu hawajui tu kwa sababu hii sanaa labda ni wageni kiasi, Mondi ndo tabia zake anakunja sana ukianza kumzidi hata kwa kile kidogo.. sema anachokosea Harmonize ni njia anazotumia japo nao wanamzingua ona anachofanya Baba Level ila akifanya Harmonize hana nidhamu [emoji3]
Kile kipindi ambacho Mo aliongea shit kwenye video conference ya chama, mimi sikukubaliana na ishu hiyo eti kwakua yeye ni tajiri basi ugomvi wake yeye na manara anataka iwe hivyo hivyo na kwa wachezaji eti kwakua yeye ndio anawalipa mishahara

Na ndio maana magufuli alisema kwenye utawala wake tajiri anaweza kufanywa chochote, na jamii ilishangazwa kwasababu haikua kawaida kuona tajiri akiwajibishwa

We must stop being asskissers, mtu asemwe madhaifu yake bila kujali wadhfa wake, hii tabia ya kuona watu waliosaidiwa na matajiri wao kua ndio wenye wajibu wa kuwa wanyonge hata pale ambapo wanaonewa dhana hii ina mentality ya kitumwa
 
Roho ya kinafiki ipi 40/60,unasema unaibiwa haya yy mwenye roho anawapa wasanii wake ngapi.

Ndio tatizo la wabongo unakomment kitu wakat undani wake hujui ,Ni wapi harmo kasema anaibiwa?

Yeye alikubal kiroho Safi hiyo 40 na kapambana Sana awe sawa na mond Ila mondi akawa kiburi ,issue ya harmo Wala sio hiyo 40, nenda kasikilize interview alafu uje kukoment upya, ushabik utawaua nyie wanaume wa dar .
 
Back
Top Bottom