Harmonize: Nilipewa Mkataba wa kuonewa na WCB na nilisingiziwa kumroga Diamond Platnumz

Harmonize: Nilipewa Mkataba wa kuonewa na WCB na nilisingiziwa kumroga Diamond Platnumz

IMG_3239.jpg
 
sema wakati wa Mungu ukifika umefika ndugu zangu.[emoji23][emoji23][emoji23]

nimecheka sana mtu kakubali kulipa 500mln lakini uhakika alio nao ni milioni 100 tu kwa mauzo ya nyumba yake.
halafu ghafla sayona wanampa hela japo kwa mbinde,crdb nao kwa mbinde[emoji38][emoji38].

all in all anastahili pongezi kwa alipofikia.
 
Harmonize ameonesha Akili Ya Waajiriwa Wengi Tanzania Ilivyo. [emoji28][emoji28][emoji28] Tungepata Hata Siku 7 kuwaona wenzetu walioendelea Namna Gani wanaheshimu Kazi, na Kuheshimu Maboss zao, Leo Harmonize asingeongea kama Anavyo ongea.

Kuna Kitu Kinaitwa Kampuni. Ikisha Kuwa Kampuni basi hata muajiriwa Fikra zako inabidi zianze kubadirika. Walio Ajiriwa kwenye Serious Companies Watakuwa naelewa nacho Sema.

Harmonize Alikuwa Msanii wa Kwanza kabisa Kuwa chini Ya WCB, huenda Wakati Diamond Anamchukua Harmonize Hakuwa na Mawazo ya kuja na Wasanii wengi na Kuwaendeleza wengi zaidi. So alimchukua kama Mtu anayetaka kumsaidia, lakini baada ya Kuingia WCB na Diamond anakuwa kiakili anakutaka na watu, Ndipo Mawazo ya kuwa na Kampuni itakayo kuwa Inamamia wasanii ikazidi kunoga, Hapo ni Lazima Diamond Akili ilianza kubadirika na kuanza kufikiria kama CEO na Sio Kama Diamond. Sasa Harmonize Alitakiwa Naye kuanza kubadirisha Fikra kuwa Sasa nipo chini ya Kampuni na Sio nipo Chini ya Mtu fulani. Angekubali hilo haya yote yasingetokea.

Kwanini Harmonize Anashindwa Kujiuliza hata Mh Rais alivyompigia simu Aliagiza Termination contract iwe signed na Sio Millioni 600 zirudi? Ina maana alielewa mikata ya Kampuni inavyo fanya kazi! Leo atalia na hizo millioni 600 lakini no one ambaye atakuja kusema kuwa hizi millioni 600 hukupaswa kulipa.

Harmonize ananikumbusha Aina ya Waajiriwa ambao wanafanyiwa Interview, anauliza Ungependa Tukulipe Sh ngapi kwa Mwezi anasema Mimi hela yoyote tuu mtakayo ona inafaa nitalipwa. Anaulizwa zaidi ya Mara 3 thamani yako ni Tsh ngapi katika kazi hii, Hataki kusema. Akisha Ajiriwa na Kupewa mkataba akaizoea Kampuni Anaanza kusema Huu mshahara ni mdogo sana na Haunitoshi, lakini kumbuka Umesha Sign mkataba. The same na Harmonize leo anakuja Kulia Na asilimia 60% kwa 40% huenda kweli ni ndogo, lakini kama ulikuwa unajiamini kuwa ipo siku utakuwa Juu, kwanini hukusema mwanzo? Kwanini hukuomba Vipengele vya mkataba Viseme kuwa kwasababu wewe ni msanii na unakua kila kitu, basi kuwe na kipengele cha ku review mkataba wako kila baada ya miezi 6 au Mwaka 1. Hakufikiria kwasababu akili yake ilimezwa kuwa BSS wamenikataa, huyu amenichukua. Hapa ndio Dhana ya Kuwa KUSOMA SHULE NI MUHIMU, Angekuwa Alisoma Suala la Mikataba angejua nini cha kufanya.

Sometime CEO anaweza kuwa Rafiki yako, na jana mmekunywa naye Bia ila kesho ukitaka kwenda Kumuona Ofisini anakwambia Nitumie Email au weka Appointment! Walio ajiriwa hili wanalijua sanaa, The same kwa Diamond Kuna Muda atasimama kama Diamond na kuna muda Atasimama kama CEO, Raisi Akiwa Kwenye Shughuli za kichama, basi wanachama ni rahisi kumuona na kumu access lakini akisimama kama Rais wa Nchi utaona kama Mambo yamebadirika.

Diamond Tunasema Alimsaidia Harmonize kwasababu alitake risk, Aliwekeza Pesa Bila Kujua kama Wananchi watampokea msanii au hawata mpokea, Sahizi Tunasema Harmonize alionewa kwasababu tunaona amesha Kuwa Star, Fikiria Hela Alizowekeza Diamond Kwa Hamornize Halafu, Mashabiki wasinge mpokea Diamond angekuwa Ametengeneza Hasara Kiasi gani? Tunarudi kule kule kwenye Kampuni, ukiwa Unaomba Msaada wa kuanzisha Kampuni na Unataka mtu aweke pesa zake, ni lazima Uandike proposal useme utafanya nini? , utapataje faida na Utarudisha Vipi Mtaji! Wakague ndio upate pesa. Lakini Diamond alimchukua jamaa, akawekeza pesa, bila kujari kama itakuwaje mbele. Sasa Tumuulize Harmonize kwa Jinsi vile alivyo imba BSS nani Angemchukua kama Msanii wake? Diamond alithubutu.

Ufike wakati wasanii wa Bongo waache kuvimba, watafute wanasheria wafundishwe sheria, mikataba na Vitu vingine, Shule ni Muhimu. Yule CEO wa Facebook, Whatsapp na Instagram. Kuna Programmer hawalali kuhakikisha Kila kitu kinaenda, kuna IT wanaipambania Kampuni, lakini CEO anaonekana Kawasaidia kuwapa Ajira na Yeye ndie anaye tajwa duaniani kuwa ni Tajiri sio wewe IT ambaye hulali [emoji28]

ndugu yetu mtaalam wa sheria umeshindwa kabisa kuiona hoja ya harmonize kwenye interview yake ya zaidi ya dakika 40???

tokea mwanzo anakwambia ni kwa namna gani alihangaika kuweka mambo sawa,aendelee kuishi pale lakini katika hali ya amani.unaweza niambia kufanya kazi chini ya visa na vitimbi ni level ipi ya sheria inayosimamia makampuni inafundisha!!!

kavunja mkataba akakabwa alipe 500mln sawa,ambayo mwisho wa siku imekuwa 600 na majungu juu,hii ni sheria gani inazungumza haya!!!

hata serikali haiamini uchawi wala majungu,ila kuwa ofisa wa serikali ndio utajua wewe ni serikali ama ni ofisa wa serikali,hakuna rangi utaacha kuiona humo serikalini.

wenye kampuni zao hata wanapopata faida kwako kupitia sheria walizoweka,bado huwa wanatamani usipeleke ujuzi kwingine baada ya kuachana nao story yako iishie pale pale.
 
Hahaha...siku huyo mwanajeshi wenu akimzidi Naseeb kwa chochote kile (hâta kimoja tu) nitawaelewa,ila kwasasa nawaona kama wafa maji tu maana hakuna hâta hoja moja ya maana mnayotoa.

huu ni ujinga umekujaa.

boss wako angekuwa na mentality kama yako hii,angekuwa kabung'aa wala hajishughulishi tena.
lakini anajua binaadam hana limit katika kutafuta,anawezapitwa.
 
Ila lazima tukubali kila kitu kina kushuka, asipojiweka vizuri atakumbuka
Siku ambayo Diamond atakuwa ameshuka, hakutakuwa na mjadala wowote kuhusu DIAMOND tutakuwa busy na mtu mwingine kabisa mwenye wakati wake.
 
  • Thanks
Reactions: Qwy
Diamond mnyonyaji na wale mameneja wake.Unamlipishaje mwenzako 600M?

Anguko Lake lipo tu,asidhani atakuwa vzr milele.Walikuwepo wakina Juma Nature sembuse yeye!

Halafu anaanza kumfitini mwenzake na figisu kibao ili ashuke na kuanguka chini kimziki.
 
wakati wenzako wana hangaika kutoboa kimataifa zaidi na zaidi kwa kufanya collabo na wasanii wakubwa i.e Justine Bieber kuna mwamba yeye yupo bize studio na 20% ana kwambia we are going global
 
Diamond kashinda vita dhidi ya shujaa muongoza njia, kitu gani mmakonde wa Chitoholi?

mmakonde ndiye msanii mwenzie anayevaa cheni za almas,ambazo yeye anaziita mabati.

wakati mwingine njia bora ya kumzibiti jinamizi,jipake mkaa halafu mfate,uone kama atakuzoea zoea kindezi.
 
Wanaomchukia Diamond ni walewale miaka nenda Rudi,Zaid Zaid wanahamishaga kambi tu.
Huyo mange mwenyewe ndo yule yule tu,yani mpaka wanajitoa akili.

Wakati harmonize yupo full beneti na diamond walianzisha vita KWA diamond ilj amteme huyo mmakonde na wakamsifia kinafiki rayvanny Ili aonekane anajua kuimba KUSHINDA harmonize lakini hata wao hawakutegemea haya,hata leo wanamsapot kinafiki Ili kumkomoa mondi.

Ajabu ni kua anayemtukana mondi anapata umaarufu na faida,anayemsifia pia na kumtetea sana the same.

Cc mwijaku,babalevo,jumalkole na page za udaku.
Ama kweli hii kweli ALMASI,mpaka mzee mzima Ostadh Juma naye kaanza na kuanzisha ka online TV chake,anapiga vifedha vya hapa na pale

mpaka sasa konde anaongoza 8:0

mond anaposimama yeye kama yeye kumejaa baraka na ishara ya mafanikio,shida ni chawa wake wanaotaka kula kupitia yeye ndio wanaharibu.
 
Me mbona sionii mond alichofanya mpaka asemwe hivo nafikiri ni sababu ya ukubwa wake,, ukiwa mkubwa lazima usemwe tuu! Sikilizeni nyimbo nyingi za harmonize huwa zinamsema sana mond lakin mond hajawah jibu
 
Me mbona sionii mond alichofanya mpaka asemwe hivo nafikiri ni sababu ya ukubwa wake,, ukiwa mkubwa lazima usemwe tuu! Sikilizeni nyimbo nyingi za harmonize huwa zinamsema sana mond lakin mond hajawah jibu
 
huu ni ujinga umekujaa.

boss wako angekuwa na mentality kama yako hii,angekuwa kabung'aa wala hajishughulishi tena.
lakini anajua binaadam hana limit katika kutafuta,anawezapitwa.
No mimi sijajaa ujinga, ni weeeh tu na akili zako ndo umeshindwa kunielewa.

Unaposema "anaweza pitwa" hiyo ni probability tayari. It's ether going or not going to happen kwa factor yoyote ile.

Nimekuomba unitajie kitu kimoja tu ambacho Harmo anamzidi Naseeb, na kama hakipo kwa nyanja zote ,unaachaje kuonekana mjinga unapojaribu kushindanisha hawa watu wawili?

Supotini kazi za kijana wenu kama kweli mnampenda, maneno kama haya hayataweza kumpandisha wala kumshusha aliyejuu.
 
Mkuu una uhakika hana copyrights mpaka kupewa nafasi ya kurudia ngoma hiyo au unadhani wanaenda enda tu chief? Hizi mambo zipo sana na ni business, nenda kamdiss Whitney Houston kurudia ngoma ya Dolly Parton au Jay Z ngoma ya Pac Me & My girlfriend, Dakika Moja AY na FA feat. Hard Mad wamerudia ya Ngwea dakika moja.. chimbua vitu chief
Sijasema kaiba kazi ,sasa siijui hayo maswala ya copyright yametoa wapi.

Nilichokisema ni swala la yéyé kujiita teacher wa Amapiano ilhali hiyo ngoma yote aliyoimba ni melody ya "Mang'dakiwe" kwa kila kitu.
 
Diamond ni mwanamziki mkomavu sana, toka ameanza kuhit Huwa tunasikia kwamba amefika mwisho wake lakini mwisho wake haufiki.
Diamond ni mwanamziki mkubwa na mziki unachangamoto zake pia biashara haitaki ushkaji.

Nenda hata Kwa akina Bakhresa ongea na wafanyakazi wa viwandani utajua kwamba biashara haitaki utoto hata siku moja.
Na kama utacheka na wapinzani wako wanakupoteza.

Kwamba Harmo yeye Hana matatizo mwenye matatizo ni Diamond tu basi na mchawi ni Diamond yeye sio mchawi kabisa ni mtu wa Sala sana, inachekesha sana.

Uchawi unapozungumziwa sana na mtu na kuona mafanikio ya watu yanatokana na Uchawi hiyo inakua ndio Imani yake huyu mtu anahisi Uchawi anaofanya unafanywa na kila mtu na kila mwenye mafanikio basi ni mchawi zaidi yake.

Mtu akisema huniwezi kwa Uchawi huenda ananguvu inaoushinda Uchawi.

But mafanikio ni shida sana kuyamaintain na watu wanapambana haswa ukikaa kiboya tu kwenye mziki utapoteza hufiki mbali.

Sasa Hamo kama anataka kuonewa huruma kwenye game na washindani wake atapoteza.
 
Back
Top Bottom