Hassan Mwakinyo ndio bora wa wakati wote hapa Tanzania. Wabongo wanataka kumshusha

Hassan Mwakinyo ndio bora wa wakati wote hapa Tanzania. Wabongo wanataka kumshusha

Mwakinyo hana akili ya biashara ya kuitoa boxing keko kuipeleka masaki.
Yeye ni kipaji na juhudi kwenye ulingo ila kwenye biashara ni akili ya Kelvin Twissa chini ya kampuni yake ya Jackson Group ambayo inajihusisha na sports marketing.

Na hawapo tu kwenye boxing, wameshaingia hadi kwenye soccer.

Unaweza fuatilia kazi zao kuliko kumpa mwakinyo ukubwa ambao hana kibiashara
Tulia hujui lolote ww uyo KT kafukuzwa na abubakar kama mbwa pale azam masaki hataki ata kumuona promota mwizi uliza uelekezwe kiande
 
View attachment 2778189

Wote tunajua kwenye mchezo wa boxing hajawai kutokea bondia mwenye uwezo wa kupigana ngumi hapa bongo kama Mwakinyo.

Dunia nzima inajua Hassan ndio alama ya boxing hapa Tanzania.
Ndio biashara kubwa ya ngumi East Africa ukitaka kufanya biashara ya ngumi na upate hela isiyo na longolongo basi mtumie Mwakinyo.

Mwakinyo kaitoa boxing kwenye fight za kwenye bar za Keko na Manzese mpaka ngumi zinapigwa Masaki.
Huwezi mpandisha Hassan ulingoni eti apiganie gari anaijua thamani yake.

Na tatizo ndio linaanzia hapo watu wanashindwa kumtumia kwa urahisi hivyo wanapigana vita ya kumpoteza.

Mnataka mpoteza Mwakinyo ili mbaki na nani?

Anachopitia Mwakinyo alishawai kukipitia Diamond.

Kuna wakati Diamond alipigwa vita na kila mtu kama sio mashabiki wake kusimama nae leo hii tungekuwa tunaongea mengine na sababu walizotoa ni hizi hizi. Anaringa sana, anajiona mkubwa, anavimba, muda wake umeisha ila aliwaprove wrong na wengine kwa sasa wapo kwenye team yake wanajifanya wanampenda kuliko ndugu zake amebaki kuwachora na kuwagawia riziki.
Mwakinyo awe makini sana na acheze game yake very smart, yupo kwenye nchi iliyojaa watu wenye chuki na roho mbaya zisizo na sababu.

Waswahili ni watu wa kuyakadilia mafanikio, kuna mstari wa mafanikio ukiuvuka hata wale waliokupeñda wanageuka kukupiga vita upotee. Huo ndio uhalisia. Na sasa Mwakinyo ana mtihani wa kupambana na ili kundi ambalo limekuwa kubwa likifanya jitihada apotee kabisa.

Tanzania ni nchi iliyojaa watu wajinga, ujinga ukaleta ugonjwa wa roho mbaya na husda na ikifika wakati wa kumuadabisha mtu mwenye mafanikio uwa wanaungana wanakuwa wamoja.

Kwa sasa asipokuwepo Mwakinyo hakuna mwingine wa kukaribia brand yake ila wenye chuki wanaona bora tubaki na kina Kaoneka. So sad ila ndio taifa letu lilivyo.

Naamini ili suala la Mwakinyo litaisha ila inabidi awe makini sana, na fight yake atayopambana hana option nyingine zaidi ya kushinda. Bila hivyo itakuwa ni sherehe kubwa kwa wenye chuki na roho mbaya.
Nimependa Sana haya maneno...
Waswahili ni watu wa kuyakadilia mafanikio, kuna mstari wa mafanikio ukiuvuka hata wale waliokupeñda wanageuka kukupiga vita upotee
 
Kwa hiyo wewe shida yako ulitaka apatikane mtu wa kumfanya kitu?? [emoji28][emoji28][emoji28]

Roho mbaya!
Ndo yaleyale Tu Roho Mbaya wabongo wanapenda mtu afikwe na mabaya Tu! Yaani mtu anatamani afanywe kitu.. Kwanza kitu gani? [emoji23][emoji23][emoji1787]
 
Naomba mwenye ufahamu aweke hapa rekodi ya mapambano aliyocheza bondia Mwakinyo, mapambano aliyocheza mwaka jana na mwaka huu.
 
Huenda ni kweli mwakinyo anajawa dharau na majivuno lakini ni sehemu ya madhaifu yake kama mwanadamu, Mwakinyo amejitahidi kujijengea brand yake na kwa kiasi fulani ameweza ila kuna viongozi wajanja wajanja wanakwamisha
 
Tulia hujui lolote ww uyo KT kafukuzwa na abubakar kama mbwa pale azam masaki hataki ata kumuona promota mwizi uliza uelekezwe kiande

Sijui ndio ila kuzinguana kibiashara ipo ila kitu ambacho huwezi kukitoa kwa Twissa ni ule ubongo.
Kaulize jamaa ni nani kwenye telecommunications Tz hii na hata wakati anarudi bongo kuanzisha kampuni yake, alitokea sportpesa Kenya kwa hiyo, sio choka mbaya au promota chawa kama unavyotaka kumuonesha.

He is a genius na ndio maana Jackson group imeupa thamani mchezo wa ndodi kwa kuupa promotion kubwa lakini pia kuandaa matamasha ya hadhi. Sio huyo mwakinyo maana akili hiyo hana
 
Umenena kweli
Wabongo wanamhukumu kijana eti anaringa kwani kuringa kosa kama anaringa na kipaji ni chake kuna shida gani?

Wanamtafutia sababu wamshushe waharibu kipaji cha kijana

Mwakinyo ni brand ameajiri watu

Ana connection za kimataifa

Anaweza kuwasaidia vijana wengine

Wanaleta ubabaishaji kijana ana exposure na international flights anakataa huo uhuni wanasema eti anaringa

Sio vizuri Mwakinyo muacheni kijana apigania ugali wake hicho chama kiwepo kusaidia vipaji na sio kukomoa na kuharibu Tallent za boxers


Sent using Jamii Forums mobile app
Nyie ndio mnaomharibu mwakinyo kwa uchawa wenu ....mwambieni ukweli

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Mwakinyo hana management? Kama hana basi sio proffesional kama ulivyo muainisha hapo, kama ana mgt walikua wapi kusawazisha haya yasifike huku?

Kwa nini Mwakinyo anajieleza sana kwenye media? Poster moja yenye mfumo wa barua wawe(Mwakinyo mgt) wamemaliza mchezo.
Management anayo ila ni mjuaji sana na mtu wa kujiskia sana ndyo maana anaenda front mwenyewe.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Huenda ni kweli mwakinyo anajawa dharau na majivuno lakini ni sehemu ya madhaifu yake kama mwanadamu, Mwakinyo amejitahidi kujijengea brand yake na kwa kiasi fulani ameweza ila kuna viongozi wajanja wajanja wanakwamisha
Viongozi janja janja wa wapi ilhali ni yeye mwenyewe alikiuka makubaliano ya mkataba aliosaini yeye mwenyewe?

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Nimependa Sana haya maneno...
Waswahili ni watu wa kuyakadilia mafanikio, kuna mstari wa mafanikio ukiuvuka hata wale waliokupeñda wanageuka kukupiga vita upotee
Hayo maneno ni sawa ila kwenye ukweli tuseme ukweli mwakinyo kwenye pambano la juzi kazingua kwa kukiuka mkataba aliosaini yeye mwenyewe kwa io kufungiwa ilikuwa ni halali yake

Hilo la roho mbaya za waswahili sidhani kama ni sehemu yake hapa

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Siku ambayo angepigana na Dullah Mbabe au yule jamaa mjeda ndio siku ambayo angechezea kichapo kama mtoto mdogo.

Wabongo wamekomaa sana miili yao na wanaweza tofauti na wote ambao amewahi kupigana nao Nje ya Nchi na ndio maana hua anaogopa na hataki kupigana na Mbongo kwa sababu anajua atavyochakazwa.
 
Back
Top Bottom