Hassan Rehani Bitchuka: Fundi wa muziki wa dansi, sauti ya kinanda. Yu wapi huyu mtaalam wakuu?

Hassan Rehani Bitchuka: Fundi wa muziki wa dansi, sauti ya kinanda. Yu wapi huyu mtaalam wakuu?

Ambae ataweza kutupatia mawasiliano yake atakuwa amefanya jambo la maana sana.


Tujitokezeni tumsaidie wakuu,

Karibuni wote kwa suggestions zaidi.
Muhimu kwa mlioko Dar mkamtembelee...ukiwemo wewe, chukua namba yake(Bitchuka mwenyewe) uiweke hapa (kwa ridhaa yake) ili wadau wa mbali na wa karibu waweze kutoa chochote kumsaidia.
 
Nakuonya nakuhaasa wewe zumbukuku, oooo fikiria dunia, inavyokwenda, hapa alishirikiana na kina marehem shaaaban dede.
Gere mnanionea mieeeee!!! Kwa kunifanya hasidi×2

Wajifanya wajuaaaaa !!!jua litakuwakiaaa!
 
Muhimu kwa mlioko Dar mkamtembelee...ukiwemo wewe, chukua namba yake(Bitchuka mwenyewe) uiweke hapa (kwa ridhaa yake) ili wadau wa mbali na wa karibu waweze kutoa chochote kumsaidia.
Kweli mkuu, issue ni namba yake mimi sina connection yoyote ya kuipata ndio mana tunaomba wadau wanaomfaham vzr watusaidie
 
Sasa jaribu kusikiliza wimbo unaitwa "Kipipa Ayubu" akiwa na OSS
nimetoka kuusikiliza mkuu, dah mbona yale mashairi kama,wimbo wajuzi tu. vijana wa siku hizi ndio wanapenda starehe zaidi kuliko future. mwishoni kuna mzigo unakata mauno sana
 
Kwa kupata namba ya simu ni kwa Zomboko wa radio one.
 
Bichu anaumwa kapumzika kwake Sinza. Jicho lake moja limekufa kbs halioni. Na umri umeenda sana tena sana.. tafuta Dunia kuna Mambo ama Clara ndio utamjua Mbembe wa Kigoma.
 
Samahani nje kidogo ya mada. Kuna wimbo wa zamani kuna kijipande kinasema "nilipomaliza masomo nilipata kazi'' naomba jina la wimbo.
Ahaa badilisha hapo nimemaliza chuo sijapata kaziii,wazazi wangu walinihusia jinsi ya kuishi na walimwengu
 
Bichu anaumwa kapumzika kwake Sinza. Jicho lake moja limekufa kbs halioni. Na umri umeenda sana tena sana.. tafuta Dunia kuna Mambo ama Clara ndio utamjua Mbembe wa Kigoma.
Unajua mwenzangu karibuni utatoka hospitalini,utokapo tafadhali..fika mjini ....
 
Unajua mwenzangu karibuni utatoka hospitalini,utokapo tafadhali..fika mjini ....
"umtafute mpaka umuone mchumba wangu Clara.....mchumba wangu Clara..
Nyumbani anapoishi ni Msimbazi kota.... ukimuona mpe salamu nyingi sana...mueleze mchumba wako Kibwana anakusalimuuu......"
Hatari sana, hawa wazee walikuwa wanajua.
 
Nimetoka kusikiliza moja ya ngoma alizoimba kwa weledi mkubwa, huruma kwa wagonjwa aisee jamaa anajua na nyimbo zake ni darasa tosha.
Halafu jamaa nasikia aliishia std 6,
Ni Muha wa Kigoma kwa Kabila,
Binafsi mm ni shabiki wake haswa...
 
Baadhi ya Nyimbo ambazo huwa nazo siku zote nitembeapo ni :
- Mume wangu Jerry,
-Kila siku Kelele,
- Pata Potea,
-Chenga ya Mwili,
-Hapendeki
-Clara,
-Akiambiwa Aangukie...
-NK Nk.
 
Back
Top Bottom