Watano waongezewa nguvu za kiume Hospitali ya Benjamini Mkapa

Watano waongezewa nguvu za kiume Hospitali ya Benjamini Mkapa

Dalton elijah

JF-Expert Member
Joined
Jul 19, 2022
Posts
373
Reaction score
829
Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) imesema kati ya asilimia 40 hadi 50 ya wanaume wanakabiliwa na tatizo la nguvu za kiume, huku wengi wakifika hospitalini hapo kutafuta huduma ya upandikizaji wa uume.

Mkurugenzi Mkuu wa BMH, Prof. Mabere Makubi, akizungumza leo Machi 4, 2025 jijini Dodoma amesema tayari wanaume watano wamefanyiwa upasuaji huo, lakini changamoto kubwa ni gharama zinazofikia Sh milioni 5 hadi 6. Amesema hospitali hiyo inaendelea kushirikiana na serikali ili kupunguza gharama na kufanya huduma hiyo kupatikana kwa wengi.

Aidha, hospitali hiyo inatarajia kuanza kutumia roboti katika upasuaji ndani ya miaka mitatu ijayo ili kuongeza usahihi wa matibabu. Pia, wanawake wenye umri wa miaka 35-50 wamekuwa wakihudumiwa kwa huduma ya upandikizaji wa mimba.

Prof. Makubi amewahimiza wananchi kujiunga na bima ya afya ili kuepuka changamoto za gharama za matibabu na kusisitiza kuwa serikali inaendelea kusaidia wananchi wasio na uwezo.
 
ufala mwingi sana wanaume.hebu chukua asali changanya na tangawizi na ponda ponda alovera mchuzi wake changanya humo! kunywa vijiko viwili sabh, mchana na jioni! sku mbili tu utaona hata mwanamke anaweza kukukimbia
 
Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) imafanikiwa kutoa huduma ya kuwawekea vipandikizi maalumu kwenye uume (Penile Implantation) kwa wanaume watano ambao walikuwa na changamoto za upungufu wa nguvu za kiume.

Hayo yamebainishwa leo Jumanne Machi 04, 2025 Jijini Dodoma na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH), Prof. Abel Makubi, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio na mwelekeo wa hospitali hiyo katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Amesema BMH imekuwa hospitali ya Kwanza kutoa huduma hiyo hapa nchini “

Tarehe 04/01/2023, BMH ilianzisha huduma za upandikizaji Uloto na mpaka sasa watoto 20 waliokuwa na ugonjwa wa Sikoseli walinufaika kwakupandikizwa Uloto na kupona ugonjwa huo ambapo kiasi cha Shilingi Bilioni 1.1 imetumika, fedha hizi zimetolewa kupitia mfuko maalum wa Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kama watoto hawa wangepatiwa huduma hii nje ya nchi ingekuwa shilingi Bilioni 2.1, hivyo Serikali imeokoa billion 1,”

Aidha, Prof. Makubi amesema hospitali hiyo imefanikiwa kupandikiza figo wagonjwa 25 kati ya 50 kwa ndani ya miaka minne kwa gharama ya milioni 875, kati ya hao wagonjwa 10 wamelipiwa matibabu haya kupitiamfuko maalum wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kiasi cha shilingi milioni 350.

“Endapo wagonjwa hao wangekwenda kufanyiwa huduma hiyo nje ya nchi Serikali ingetumia shilingi Bilioni 1.875, hivyo kiasi cha Shilingi Bilioni 1 kimeokolewa, aidha, uvunaji wa figo umeboreshwa kwa teknolojia ya kisasa kwa kutumia matundu madogo (Laparoscopic Nephrectomy) ambao ulianza kutolewa mwezi Novemba, 2024 chini ya Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, tangia kuanza, BMH imechangia kupunguza rufaa nje kwa 99%,”.

Mbali na hayo ameendelea kufafanua kuwa Katika kipindi cha miaka minne BMH imefanya upasuaji wamoyo kwa kufungua kifua kwa wagonjwa 60 kati ya hao watoto 38 na watu wazima 22 kiasi cha fedha kilichotumika ni shilingi milioni 562 kati ya hizo milioni 100 zilitoka mfuko maalum wa Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan, aidha, watalalamu wamefanya uchunguzi wa Mishipa ya Moyo (Cardiac Catheterization) kwa wagonjwa 1173, upandikizaji betri wagonjwa 23, kuweka vizibua njia ya mishipa ya moyo
1741097356391.png
 
Dodoma inakwenda kuwa kitovu cha utalii wa nguvu za kiume 🔥

Anyway, kwamba wagonjwa wa figo kama wangeenda nje ya nchi serikali ingetumia 1.8B, kwan hizo gharama hua zinalipwa na serikali au na hao wagonjwa?
 
ufala mwingi sana wanaume.hebu chukua asali changanya na tangawizi na ponda ponda alovera mchuzi wake changanya humo! kunywa vijiko viwili sabh, mchana na jioni! sku mbili tu utaona hata mwanamke anaweza kukukimbia
Mkuu; Hebu fafanua vizuri esp. hiyo alovera ni alovera ipi? Ninachojua mm na kwa uzoefu ni kwamba alovera kwa kiswahili shubiri mwitu kwa kimasai ni Osukuroi. Ni chungu sana (kuzidi kloroquini ) na Kwa uhakika 100% ukiinywa humalizi dk 30 lazima uvae taulo na uwe karibu sana na choo. Utaharisha mno mpaka uone maruweruwe.
IMG_20250304_180013_319.jpg
 

Attachments

  • IMG_20250304_175743_427.jpg
    IMG_20250304_175743_427.jpg
    1.4 MB · Views: 1
ufala mwingi sana wanaume.hebu chukua asali changanya na tangawizi na ponda ponda alovera mchuzi wake changanya humo! kunywa vijiko viwili sabh, mchana na jioni! sku mbili tu utaona hata mwanamke anaweza kukukimbia
Mkuu; Hebu fafanua vizuri esp. hiyo alovera ni alovera ipi? Ninachojua mm na kwa uzoefu ni kwamba alovera kwa kiswahili shubiri mwitu kwa kimasai ni Osukuroi. Ni chungu sana (kuzidi kloroquini ) na Kwa uhakika 100% ukiinywa humalizi dk 30 lazima uvae taulo na uwe karibu sana na choo. Utaharisha mno mpaka uone maruweruwe.
View attachment 3258683
IMG_20250304_175659_119.jpg
 
Hii mada angekuwa ameanzisha mwanamke malaya ningeelewa
 
Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) imafanikiwa kutoa huduma ya kuwawekea vipandikizi maalumu kwenye uume (Penile Implantation) kwa wanaume watano ambao walikuwa na changamoto za upungufu wa nguvu za kiume.

Hayo yamebainishwa leo Jumanne Machi 04, 2025 Jijini Dodoma na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH), Prof. Abel Makubi, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio na mwelekeo wa hospitali hiyo katika kipindi cha miaka minne ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Amesema BMH imekuwa hospitali ya Kwanza kutoa huduma hiyo hapa nchini “

Tarehe 04/01/2023, BMH ilianzisha huduma za upandikizaji Uloto na mpaka sasa watoto 20 waliokuwa na ugonjwa wa Sikoseli walinufaika kwakupandikizwa Uloto na kupona ugonjwa huo ambapo kiasi cha Shilingi Bilioni 1.1 imetumika, fedha hizi zimetolewa kupitia mfuko maalum wa Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan, na kama watoto hawa wangepatiwa huduma hii nje ya nchi ingekuwa shilingi Bilioni 2.1, hivyo Serikali imeokoa billion 1,”

Aidha, Prof. Makubi amesema hospitali hiyo imefanikiwa kupandikiza figo wagonjwa 25 kati ya 50 kwa ndani ya miaka minne kwa gharama ya milioni 875, kati ya hao wagonjwa 10 wamelipiwa matibabu haya kupitiamfuko maalum wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kiasi cha shilingi milioni 350.

“Endapo wagonjwa hao wangekwenda kufanyiwa huduma hiyo nje ya nchi Serikali ingetumia shilingi Bilioni 1.875, hivyo kiasi cha Shilingi Bilioni 1 kimeokolewa, aidha, uvunaji wa figo umeboreshwa kwa teknolojia ya kisasa kwa kutumia matundu madogo (Laparoscopic Nephrectomy) ambao ulianza kutolewa mwezi Novemba, 2024 chini ya Serikali ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, tangia kuanza, BMH imechangia kupunguza rufaa nje kwa 99%,”.

Mbali na hayo ameendelea kufafanua kuwa Katika kipindi cha miaka minne BMH imefanya upasuaji wamoyo kwa kufungua kifua kwa wagonjwa 60 kati ya hao watoto 38 na watu wazima 22 kiasi cha fedha kilichotumika ni shilingi milioni 562 kati ya hizo milioni 100 zilitoka mfuko maalum wa Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan, aidha, watalalamu wamefanya uchunguzi wa Mishipa ya Moyo (Cardiac Catheterization) kwa wagonjwa 1173, upandikizaji betri wagonjwa 23, kuweka vizibua njia ya mishipa ya moyo
View attachment 3258636
Safi kabisa!
 
Apostle kuna muujiza idodomya...
 
Dodoma inakwenda kuwa kitovu cha utalii wa nguvu za kiume 🔥

Anyway, kwamba wagonjwa wa figo kama wangeenda nje ya nchi serikali ingetumia 1.8B, kwan hizo gharama hua zinalipwa na serikali au na hao wagonjwa?
Ukiwauliza watakuambia mchochezi
 
Back
Top Bottom