Dalton elijah
JF-Expert Member
- Jul 19, 2022
- 373
- 829
Hospitali ya Benjamini Mkapa (BMH) imesema kati ya asilimia 40 hadi 50 ya wanaume wanakabiliwa na tatizo la nguvu za kiume, huku wengi wakifika hospitalini hapo kutafuta huduma ya upandikizaji wa uume.
Mkurugenzi Mkuu wa BMH, Prof. Mabere Makubi, akizungumza leo Machi 4, 2025 jijini Dodoma amesema tayari wanaume watano wamefanyiwa upasuaji huo, lakini changamoto kubwa ni gharama zinazofikia Sh milioni 5 hadi 6. Amesema hospitali hiyo inaendelea kushirikiana na serikali ili kupunguza gharama na kufanya huduma hiyo kupatikana kwa wengi.
Aidha, hospitali hiyo inatarajia kuanza kutumia roboti katika upasuaji ndani ya miaka mitatu ijayo ili kuongeza usahihi wa matibabu. Pia, wanawake wenye umri wa miaka 35-50 wamekuwa wakihudumiwa kwa huduma ya upandikizaji wa mimba.
Prof. Makubi amewahimiza wananchi kujiunga na bima ya afya ili kuepuka changamoto za gharama za matibabu na kusisitiza kuwa serikali inaendelea kusaidia wananchi wasio na uwezo.
Mkurugenzi Mkuu wa BMH, Prof. Mabere Makubi, akizungumza leo Machi 4, 2025 jijini Dodoma amesema tayari wanaume watano wamefanyiwa upasuaji huo, lakini changamoto kubwa ni gharama zinazofikia Sh milioni 5 hadi 6. Amesema hospitali hiyo inaendelea kushirikiana na serikali ili kupunguza gharama na kufanya huduma hiyo kupatikana kwa wengi.
Aidha, hospitali hiyo inatarajia kuanza kutumia roboti katika upasuaji ndani ya miaka mitatu ijayo ili kuongeza usahihi wa matibabu. Pia, wanawake wenye umri wa miaka 35-50 wamekuwa wakihudumiwa kwa huduma ya upandikizaji wa mimba.
Prof. Makubi amewahimiza wananchi kujiunga na bima ya afya ili kuepuka changamoto za gharama za matibabu na kusisitiza kuwa serikali inaendelea kusaidia wananchi wasio na uwezo.