Unamjua mkurugenzi wa LATRA ,au nikuache kuna wakurugenzi zaid ya 10 nawafahamu sipendi kuweka ID za watu.
Reputation ya universities🤣🤣🤣? Uislamu unajitegemea sio sheria za kizungu kama unaona iran hamna vyuo unavyotaka sikulazimishi...**** elimu nyingi nikitaja utatoa macho tu...Pia haubagui elimu ni nyingi.
Kwa hiyo elimu ya watu wa Iran huijui ?
Kozi niliyosom mm na hobby yang ilikuwa inapatikana chuo kimoja tu Tanzania nchi na wala hakipo Top 10 na pia sio cha dini ni cha Serikali....Hivyo vyuo vya dini vyote utopolo havina mzuka vyuo vikubwa bongo vinajulikana
Ungekuwa na akili ungeuliza wameenda kusomea nn ? Yaani uislamu una elimu zake ukisikia vyuo vya kiislamu sawa na mtu kaenda kusoma Vatican ndio namaanisha hapa....Hivyo vikuu nan kakwambia ni vya wakristo?
Ingependeza sana hivyo vyuo vya Iran ungevitaja maana leo hii nikitaja Havard, Oxford, John Hopkins , Yale huwezi kuwa na maswali juu ya hilo.
Pia unaweza kunitajia walikwenda kusomea nini huko kama ulivyosema senstensi ya mwisho uislam una elimu zake basi ingependeza uzitaje.
Sijaomba uweke ID za watu hapa hatukuongelea watu zaidi ya public figures kama Ally Happi na wengineo ndio maana hata mimi sijawataja hao rafiki zangu wa kiislam maana sio public figures na ni kinyume na policies za JF.
Pia mimi possibly sikuuliza ulisoma nini wala hobby yako ni nini kama ulivyosema pia sikuponda vyuo vya dini kama nilifanya hivyo quote sentensi hiyo hapa.
Tukirudi kwenye mada kuu naomba majibu ya maswali yangu muhimu moja kuu likiwa ni ufadhili wa kimasomo uliowahi kutolewa kwenye vyuo vikuu vya nje ambavyo kimsingi ni notable.
Ukiangalia list ya matajiri wengi waislam wapo kwa kiasi kikubwa ikiwa ni jamii ya waarabu je kuna aliyempeleka mwanaye kusoma Iran?
Nitakupa mfano tu mwepesi ili uelewe nilichomaanisha huyu kasomea mambi yake ya biashara Georgetown university akijikita kusomea biashara na theolojia kwa kiasi akiwa ni muislam wa Shia mbona kama tulivyotarajia hakwenda kusomea Iran ambapo Shia wapo 95% na badala yake kaenda Marekani?
Tukija kwa Professor Mussa Assad baada ya kuhitimu shahada yake ya kwanza alijiendeleza katika nchi za Ireland( University of Dublin na Uingereza(University of Southampton) sijaona mahali Professor alikwenda Saudia Arabia au Pakistan kujiendeleza.
Marehemu Ali Mufuruki alisomea Ujerumani , university of Reutlingen.
Kwa rekodi zangu za haraka ni Hussein Mwinyi alisomea shahada ya udaktari wa binadamu nchini Uturuki chuo cha Marmara na shahada ya pili alifanyia Uingereza , Hammersmith.
Kwa jinsi hiyo utakuwa umepata picha fulani sio kuponda bali ni kipaumbele kiukweli waislam miaka hii ndio wameanza kuamka ndio maana unaona hata diversity inaanza taratibu kwa nchi kama Saudia Arabia leo hii ligi yao inakaribisha wageni wa kutosha tuendako sheria zile kali zitaisha na patakuwa kama UAE , ambapo kuna branches za vyuo vya US,CA na UK.
Mimi naona misimamo mikali ya kidini haina tija watu wapate elimu ya kuendana na kasi ya mabadiliko ya ulimwengu huku wakiendelea na dini yao maana sipo hapa kukataza watu wasiamini dini yao nazungumzia kipengele cha kuipa dini kipaumbele kuliko elimu.
Hata wapo waislam humu wanaoponda wakristu lakini miaka hiyo walisoma shule za mission na ndipo walijulia kusoma na kuhesabu na baadae kwenda mbele zaidi hadi kupata elimu ya juu katika nchi hizo kwa hao hao wanaowatukana leo hii kwakuwa hao ni wa humu na ninawafahamu basi si vyema kuwataja na wakiona ujumbe huu watanielewa.